Monday, January 7, 2019

Wahitimu wa chuo cha NDF Waelezwa Fursa za Uwekezaji Zinazopatikana Rukwa

Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amefafanua fursa mbalimbali za uwekezaji zinazopatikana katika Mkoa hasa sekta ya kilimo kwa wahitimu wa mafunzo kwa vitendo kutoka katika Chuo cha Taifa cha Ulinzi waliotembelea mkoani hapa ili kujionea maendeleo ya mkoa.

Wahitimu hao kutoka katika nchi kadhaa barani Afrika wamelenga kutembelea katika viwanda vikubwa vinavypoaptikana katika mkoa, maeneo ya uwekezaji wa kilimo, kufika kwenye vivutio vya utalii, machimbo ya makaa ya mawe pamoja na hifadhi za misitu.

Mh.Wangabo alisema kuwa uwekezaji wa kwenye viwanda unahitajika kwasababu ya uwepo wa mazao ya kulisha viwanda hivyo ikiwemo viwanda vya kuchakata mahindi, maharage na mpunga na kuwaondoa shaka juu ya upatikanaji wa umeme kwani hadi kufikia mwaka 2020 vijiji vyote vya mkoa wa Rukwa vitakuwa na umeme.

“Maeneo mazuri ya uwekezaji upo kwenye viwanda hasa viwanda vya kuchakata mazao ndani ya mkoa wetu, pia mwaka huu tuna zao la alizeti kama zao la Kimkakati ambapo hadi sasa kuna tani za mbegu zaidi ya 11,000 ambazo zimeshanunuliwa na wakulima na kupandwa na hivyo tunategemea uzalishaji mkubwa wa alizeti kwa mwaka huu na hivyo tunawaalika wawekezaji kuweka viwanda vya uchakataji wa alizeti ikiwa ni zao la kimkakati kwenye mkoa wetu.” Alisema.

Aidha, alibainisha kuwa katika kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano, mkoa umejipanga kulima zao la kahawa ambalo ni moja ya mazao matano ya kimkakati kwa serikali, na kusisitiza kuwa upatikanaji wa samaki katika ziwa Tanganyika na ziwa Rukwa bado unahitaji uwekezaji ili kukuza sekta hiyo na hatimae kukuza vipato vya wavuvi wa maeneo ya maziwa hayo, huku akielezea uboreshwaji wa miundombinu ya barabara na kiwanja cha ndege cha mkoa.

Ameyasema hayo wakati akijibu swali la Brigedia Generali Mohamed Montaser muhitimu kutoka nchini Misri aliyetaka kujua maeneo ya vipaumbele katika uwekezaji kwa mkoa wa Rukwa. Halikadhalika, Kiongozi wa wahitimu hao Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Magereza SACP Justine Kaziulaya aliushukuru uongozi wa Mkoa wa Rukwa kwa mapokezi mazuri waliyoyapata na kuomba kupokewa tena endapo watarudi Mkoa wa Rukwa katika miaka inayofuata.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa Benard Makali (kulia) akipokea moja ya zawadi alizopewa na Uongozi wa chuo cha Ulinzi nchini ikiwasilishwa na Kiongozi wa Msafara huo Commodore M. Mumanga
Picha ya apmoja kati ya Wahitimu wa Chuo cha Ulinzi nchini pamoja na Wataalamu wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa wakiongozwa na Mkuu wa mkoa Mh. Joachim Wangabo (wa tatu toka Kulia).
Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo (kulia)akipokea moja ya zawadi alizopewa na uongozi wa chuo cha Ulinzi nchini kama shukrani ya kuwapokea vizuri katika Mkoa, zawadi iliyowasilishwa na Kiongozi wa Msafara huo Commodore M. Mumanga. 

SERIKALI YAZIPA KANDARASI YA THAMANI YA 2.9BN KAMPUNI ZA VIJANA KUTEKELEZA MAFUNZO YA KILIMO CHA KITALU NYUMBA

Serikali kupitia Wizara ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu imezipa Kandarasi ya thamani ya shilingi 2.9 bilioni kampuni tatu za vijana wa Kitanzania ili kutekeleza mafunzo kwa wakufunzi ya kilimo cha Kitalu Nyumba (Green House). 
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Ajira na Vijana Mhe.Anthony Mavunde wakati akizindua mafunzo hayo  Januari 05, 2019 yanayoendelea katika Chuo kikuu cha Kilimo cha Sokoine mkoani Morogoro. 
Programu hiyo ambayo itatumia jumla ya shilingi 2.9bilioni katika utekelezaji wake ambapo kampuni zilizoshinda kandarasi hiyo ni Kampuni za vijana wazalendo wa kitanzania ambao ni wabobezi katika masuala ya kilimo ikiwemo kampuni na Royal Agriculture Ltd, Holly Agriculture  Group Ltd, na SUGECO. 
Mafunzo haya yatafanyika katika Mikoa yote Tanzania Bara na kuhakikisha Halmashauri 84 zinafikiwa kwa awamu hii ya kwanza lengo likiwa ni  kuwajengea vijana ujuzi kupitia kilimo cha kisasa ambapo tayari kwa mwaka huu wa fedha imeanza mafunzo hayo  kwa kutumia teknolojia ya Kitalu Nyumba (greenhouse). 
“Kwa kuanzia tutahakikisha kila Halmashauri tunatoa mafunzo kwa vijana 100 na kati yao vijana 20 watapatiwa mafunzo ya kujenga Vitalu Nyumba ili kwa wale watakaopenda kuendelea na kilimo hiki wasikose wataalamu wa kuwajengea Vitalu hivyo ”alisisitiza Mavunde. 
Aidha, Amewataka vijana kutumia fursa ya kilimo katika kujikwamua na changamoto za ajira na kuelezea umuhimu wa kilimo katika kuongeza pato la Taifa na kuchangia katika uchumi wa viwanda nchini.

“Wote tunatambua kwamba kilimo ni uti wa mgongo wa Taifa letu kwani kwasasa kimeajiri takribani asilimia 65.7 ya nguvu kazi nchini na kinachangia asilimia 29.1 ya pato la taifa, pia sekta ya kilimo ndiyo chanzo kikuu cha chakula, ajira, na malighafi ya viwanda”Alisisitiza Mavunde.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa SUGECO Bw.Revocatus Kimario alieleza kuwa wataendelea kushirikiana na Serikali katika kuhakikisha wanafikia kundi kubwa la vijana nchini na kushukuru mchango wa serikali katika programu za ukujazi ujuzi kwa vijana.

“Kipekee naishukuru Wizara hii kwa kuendelea kuunga mkono jitihada za kuhakikisha inatoa mchango mkubwa kwa vijana na kusaidia kuwakwamua kiuchumi.”alisema Kimario.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Ajira Ofisi ya Waziri Mkuu Bw.Ally Msaki aliwataka vijana kutumia fursa hiyo kwa kujiimarisha kupitia mafunzo hayo watakayoyapata ili kujikwamua na tatizo la ajira nchini.

“Tunataka vijana wawe mstari wa mbele katika kilimo cha kisasa ili kuendana na mazingira ya sasa na kujikwamua katika kundi la wasio na ajira nchini”.alisistiza Msaki.
 Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe.Anthony Mavunde akizungumza na watendaji wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine pamoja na viongozi walioshiriki katika warsha ya uzinduzi wa Mafunzo kwa wakufunzi ya kilimo cha Kitalu Nyumba (Green House) yanayoendelea kwa siku tano katika Chuo hicho mkoani Morogoro.kushoto kwake ni Naibu waziri wa ofisi hiyo, anayeshughulikia wenye ulemavu Mhe.Stella Ikupa
 Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe.Anthony Mavunde akizungumza na mtaalamu wa masuala ya kilimo cha kisasa kwa  kutumia mabwawa ya samaki (Acquculte) alipotembelea kukagua mradi huo, wa kwanza kulia ni Naibu Waziri Ofisi hiyo Mhe Stella Ikupa
 Manaibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu wakiangalia kiazilishe katika moja ya banda la maonesho la vijana walioshiriki mafunzo ya Kilimo cha kisasa cha kitalu nyumba. Katikati ni Mhe.Stella Ikupa anayeshughulikia Wenye Ulemavu na Kushoto ni Mhe.Anthony Mavunde (Kazi, Vijana na Ajira).
 Mkurugenzi wa Ajira Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Bw.Ally Msaki  akizungumza wakati wa uzinduzi huo.
 Baadhi ya viongoizi wakishuhudia Naibu Waziri Ofisi ya Waziri (Wenye Ulemavu) Mhe.Stella Ikupa akikata utepe ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa Muongozo wa masuala ya kilimo cha Kitalu Nyumba wakati wa warsha hiyo.
 Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe.Anthony Mavunde akikagua biskuti zilizotengenezwa kwa kutumia nanasi ikiwa ni moja ya bidhaa zilizotengenezwa na vijana waliopewa mafunzo na SUGECO wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa SUGECO Bw.Revocatus Kimario .
 Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe.Anthony Mavunde akiangalia mapapai yaliyolimwa kwa njia ya kisasa katika mashamba ya SUGECO katika Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine Morogoro.
 Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe.Anthony Mavunde akipewa maelezo na Mtaalamu wa masuala ya lishe (SUGECO) Jolenta Joseph kuhusu ukaushwaji wa viazi lishe wakati akikagua kaushio la jua (solar dryer).
 Manaibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe.Anthony Mavunde na Mhe.Stella Ikupa (Wenye Ulemavu) wakiangalia karatasi inayotumika kama  kifungashio cha unga unaotengenezwa kwa viazi lishe.
 Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Royal Agri.Co.ltd Bw.Jonathan Sangau akitoa maelezo kwa Manaibu Waziri kuhusiana na vifaa vinavyotumika katika  kufungia vitalu nyumba
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe.Anthony Mavunde akimwaga zege kwa ajili ya kutengeneza vitalu nyumba kama ishara ya uzinduzi wa mradi huo. Picha na Nyamagory Omary wa PMO

MAGAZETI YA LEO JUMATATU JANUARI 7,2019

















Sunday, January 6, 2019

RAIS WA ZANZIBAR DKT.SHEIN AWEKA JIWE LA MSINGI JENGO JIPYA OFISI YA ZURA ZANZIBAR



Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk,Ali Mohamed Shein akikunjuwa Kitambaa kuashiria Uwekaji wa Jiwe la msingi Jengo Jipya litakalokuwa na Ghorofa Saba la Ofisi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati Zanzibar(ZURA)Maisara Wilaya ya Mjini Unguja.Ikiwa ni Shamra shamra za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar. 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk,Ali Mohamed Shein akiwa na Viongozi mbalimbali wakilitembelea Jengo Jipya litakalokuwa na Ghorofa Saba la Ofisi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati Zanzibar(ZURA)baada ya kuliwekea jiwe la Msingi Maisara Wilaya ya Mjini Unguja.Ikiwa ni Shamra shamra za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar. 
-Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba Maji na Nishati Ali Khalil Mirza akisoma risala katika hafla ya Uwekaji wa Jiwe la Msingi Jengo Jipya litakalokuwa na Ghorofa Saba la Ofisi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati Zanzibar(ZURA)Maisara Wilaya ya Mjini Unguja.Ikiwa ni Shamra shamra za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar. 
Waziri wa Ardhi Nyumba Maji na Nishati Salama Aboud Talib akitoa hotuba ya makaribisho kwa mgeni Rasmi katika hafla ya Uwekaji wa Jiwe la Msingi Jengo Jipya litakalokuwa na Ghorofa Saba la Ofisi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati Zanzibar(ZURA)Maisara Wilaya ya Mjini Unguja.Ikiwa ni Shamra shamra za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Jengo jipya litakalokuwa na Ghorofa Saba la Ofisi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati Zanzibar(ZURA)lililowekwa jiwe la msingi na  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk,Ali Mohamed Shein Maisara Wilaya ya Mjini Unguja.Ikiwa ni Shamra shamra za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar. 
Baadhi ya Wafanyakazi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati Zanzibar(ZURA)waliohudhuria katika hafla ya Uwekaji wa Jiwe la Msingi Jengo Jipya litakalokuwa na Ghorofa Saba la mamlaka hio Maisara Wilaya ya Mjini Unguja.Ikiwa ni Shamra shamra za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar. PICHA NA YUSSUF SIMAI/MAELEZO ZANZIBAR.

SERIKALI KUENDESHA OPARESHENI KUBWA KUWAONDOA WAVAMIZI WA HIFADHI YA MISITU NA MAPORI YA AKIBA

Serikali kuendesha operesheni kubwa kuwaondoa wavamizi wanaofanya shughuli za kilimo na ufugaji pamoja na watu wengine wanaofanya shughuli zisizo halali katika misitu na mapori yaliyohifadhiwa kisheria zikiwemo hifadhi za misitu ya serikali Kuu na halmashauri za vijiji.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Suleiman Jafo wakati akisoma  maazimio ya kikao cha mawaziri watano kilichofanyika mkoani Kigoma leo kutafuta utatuzi wa mgogoro wa matumizi ya ardhi katika hifadhi na Mapori ya Akiba ya Moyowosi.

Jafo alisema, wale wote  waliovamia hifadhi wanatakiwa kuondoka kwa hiari kabla ya zoezi la kuwaondoa kwa lazima, operesheni hiyo itafanyika wakati wowote ndani ya kipindi cha miezi sita kuanzia Januari 2019.

Na kusisitiza kuwa wale wenye mazao katika hifadhi na mapori ya akiba wanaweza kuomba idhini ya kuvuna mazao yao.

Jafo alisema Serikali imetenga jjmla ya hekta 10,012.61 kutoka kwenye hifadhi ya msitu wa Makere kusini kwa ajili ya kilimo na mipango ya halmashauri ya wilaya ya Kasulu ambapo Hekta 2,174 kwa ajili ya kijiji cha Mvinza, hekta 2,496 kwa kijiji cha Kagerankanda na halmashauri ya wilaya ya Kasulu Jumla ya hekta 5,342.61.

Kwa mujibu wa Jafo uamuzi huo unafuatia kuwepo kwa changamoto katika maeneo ya hifadhi za misitu na mapori ya Akiba ambapo maeneo mengi yamevamiwa kwa shughuli za kilimo na ufugaji  na hivyo kupoteza uoto wa asili katika hifadhi na mapori ya Akiba.

Mapema jana Mawaziri watano wakioongozwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Suleiman Jafo wamekagua hifadhi ya  Msitu  wa Makere Kusini  uliopo wilaya ya Kasulu mkoa wa Kigoma kwa takriban saa tano ili kubaini changamoto mbalimbali za msitu huo na kuzipatia ufumbuzi.

Mawaziri hao ni Waziri wa Maliasili na Utalii Dk Hamis Kigwangala, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina, Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk. Angeline Mabula pamoja na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Musa Sima.

Ziara ya mawaziri hao katika hifadhi ya msitu huo ambao pia unatambulika kama Kagera Nkanda ambayo ni ya kihistoria kutokea hapa nchini ilianza majira ya saa saba mchana jana Mawaziri hao wakitokea wilayani Kigoma ambako walikuwa na kikao cha utatuzi wa mgogoro wa matumizi ya ardhi katika hifadhi ya Msitu na Pori la Akiba Moyowosi mkoani Kigoma na kumaliza ukaguzi majira ya saa kumi na mbili jioni.

Baada ya kumaliza ukaguzi katika Msitu wa Makere Kusini, Mawaziri hao watano walielekea kijiji cha Kabulanzwili na kukagua mpaka baina ya kijiji hicho na hifadhi ya msitu huo kwenye mto Migezibiri na baadaye kukutana na wananchi wa kijiji hicho kwa lengo la kuwaeleza nia ya serikali kunuru hifadhi ya msitu ambapo walizungumza nao hadi saa moja na nusu usiku.

Wakazi wa kijiji cha Kabulanzwili waliwapokea mawaziri hao kwa mabango wakionesha kutoridhishwa na hatua zinazochukuliwa na askari wa wanyama pori kuwaondoa kwa nguvu wananchi wanaoendesha shughuli za kilimo na ufugaji kwenye hifadhi hiyo huku baadhi yao wakidai kutofahamu mipaka halisi baina ya kijiji na hifadhi.

Meneja wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Kanda ya Magharibi Valentine Msusa alisema eneo lote la hifadhi ya Msitu wa Makere Kusini linalopakana na Halmashauri za wilaya za Kasulu na Uvinza lina ukubwa wa hekta 72,000 lakini baada ya hekta 10,000 kutolewa kwa wananchi sasa imebakia na hekta 62,000.

Mmoja wa wakazi wa kijiji cha Kabulanzwili Nolvet Mtana alieleza kuwa awali waliambiwa waendelee na shughuli za kilimo katika maeneo waliyoanza kufanya shughuli hiyo bila kuanzisha maeneo mapaya lakini wameshangazwa na uamuzi wa kuwaondoa katika maeneo hayo kinyume na kauli ya awali jambo walilolieleza linawafanya waishi maisha ya wasiwasi.

Mkazi mwingine Kidaga Tito alisema hata kama wao walivamia eneo la hifadhi basi  ni vyema wakapewa muda kuvuna mazao yaliyopo shambani ili kuepuka hasara na kutaka mipaka kati ya hifadhi na kijiji iwekwe wazi ili ifahamike kuepuka wananchi kuingia ndani ya hifadhi kwa ajili ya shughuli za kilimo na ufugaji.

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk Angeline Mabula aliwaeleza wananchi wa kijiji cha Kabulanzwili kuwa, tatizo lilipo katika kijiji hicho ni kukosekana mpango wa matumizi bora ya ardhi na kubainisha kuwa suala hilo halihitaji wizara bali kijiji chenyewe kupitia watendaji wake kuanza mchakato wa kupanga maeneo kama vile kilimo, ufugaji, makazi na maeneo ya huduma za jamii.

Aliwataka wananchi wa kijiji hicho kukaa pamoja na kupanga maeneo kulingana na mahitaji na kuacha ile dhana ya kutaka baadhi ya wananchi waliohamia kuondoka na kubainisha kuwa cha msingi ni kujua idadi na mahitaji ya wakulima na wafugaji pamoja na maeneo ya huduma za jamii na halmashauri ya wilaya ya Kasulu na serikali ya kijiji zinapaswa kupanga maeneo na kazi ya wizara yake itakuja kuanisha mipaka na hapo hakutakuwa na migogoro tena.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Suleiman Jafo alieleza kuwa ujio wa mawaziri hao watano ni wa kihistoria na unaangalia changamoto zinazokabili hifadhi ya msitu wa Makere sambamba na kuona namna bora ya kutatua tatizo linalowakabili wananchi wa eneo linalozunguka hifadhi ya Msitu huo ambapo aliwataka kukubaliana na maamuzi yoyote ya serikali yatakayofikiwa kwa kuwa maamuzi hayo yatakuwa kwa maslahi ya taifa.

Awali Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Luteni Simon Anange aliwaeleza wananchi wa Kabulanzwili kuwa ujio wa mawaziri watano katika eneo la hifadhi ni kuangalia namna bora ya kuitunza misitu ya Makere na Mvuti iliyopo Kasulu Kigoma ambayo imeanza kuharibika kutokana na uwepo wa shughuli za kilimo na ufugaji na kueleza kuwa kazi ya kushughulikia suala hilo bado haijafika mwisho na kinachofanyika sasa ni kuangalia namna bora ya kunusuru msitu huo.

Hifadhi za Misitu na Mapori ya Akiba ya Moyowosi yamekuwa na mgogoro kwa muda mrefu kutokana na wananchi kuendesha shughuli za ufugaji katika hifadhi za misitu na mapori ya akiba, uchomaji mkaa, uchimbaji haramu wa madini ya chokaa, uwepo silaha za kijeshi, uvunaji haramu mazao ya misitu na uendeshaji kilimo cha mazao ya chakula jambo lililopelekea Katibu Mkuu kiongozi kuandika barua kwa Makatibu Wakuu wa Wizara husika kutafuta ufumbuzi wa mgogoro huo Novemba 2018
 Sehemu ya wananchi wa kijiji cha Kabulanzwili kilichopo Kasulu Kigoma wakiwasikiliza Mawaziri walipofanya ziara katika eneo la hifadhi la Msitu wa Makere lililopo Kasulu Kigoma.
 Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk Angeline Mabula akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kabulanzwili kilichopo Kasulu Kigoma wakati wa ziara ya Mawaziri watano kukagua eneo la hifadhi la Msitu wa Makere.
 Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk Angeline Mabula akikatiza katika moja ya vichaka vilivyopo kwenye hifadhi ya Msitu wa Makere Kasulu Kigoma wakazi wa ziara ya Mawaziri watano kukagua msitu.
 Mawaziri Dk Hamis Kigwangala Waziri wa Maliasili na Utalii, Suleiman Jafo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Musa Sima, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina na Dk Angeline Mabula Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi wakiwasikiliza wananchi wa kijiji cha Kabulanzwili alipofanya ziara katika eneo la hifadhi la Msitu wa Makere Kasulu Kigoma.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Suleiman Jafo (wa kwanza kushoto) , Dk Hamis Kigwangala Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Angeline Mabula Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Musa Sima wakiangalia ndege inayochukua picha angani (Drones) wakati wakikagua hifadhi ya Msitu wa Makere uliopo Kasulu Kigoma.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Suleiman Jafo akiwaongoza Mawaziri wenzake kukagua maeneo mbalimbali katika hifadhi ya Msitu wa Makere Kasulu Kigoma.
 Moja ya eneo ndani ya hifadhi ya Msitu wa Makere uliopo Kasulu Kigoma ambapo Mawaziri watano walibaini uendeshaji shughuli za kilimo ukifanyika ndani ya hifadhi.
 Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Musa Sima (kushoto), Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina na Dk Angeline Mabula Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi wakiwa katika gari wakati wa kukagua hifadhi ya Msitu wa Makere Kasulu Kigoma.
Moja ya eneo ndani ya hifadhi ya Msitu wa Makere uliopo Kasulu Kigoma ambapo Mawaziri watano walibaini uendeshaji shughuli za kilimo ukifanyika ndani ya hifadhi.
Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Luteni Simon Anange akiwaonesha Mawaziri Dk Hamis Kigwangala Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Angeline Mabula Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Suleiman Jafo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Musa Sima pamoja na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina eneo la hifadhi la Msitu wa Makere lililopo Kasulu Kigoma walipofanya ziara katika hifadhi hiyo kujionea changamoto mbalimbali ndani ya Msitu huo.


Idadi ya abiria bado kubwa Ubungo.

*Wengi ni wanafuzi katika mikoa ya Tanga,Morogoro na Dodoma

Na Chalila Kibuda , Globu ya Jamii

Idadi ya abiria katika kituo cha mabasi Ubungo imeendelea kuongezeka kwa kwa sehemu kubwa wakiwa wanafunzi.

Akizungumza na Michuzi Blog Mwenyekiti wa Chama cha Kutetea Abiria Hassan Mchanjama amesema kuwa abiria katika kituo cha Ubungo ni kubwa lakini wanasafiri kutoka na baadhi daladala kupata vibali.

Amesema abiria wengi ni mikoa ya Tanga, Dodoma pamoja na Morogoro ikiwa sehemu kubwa abiria hao ni wanafunzi.

Mchanjama amesema abiria wanavyofika katika kituo cha mabasi Ubungo wakate tiketi ndani ya Kutuo.Mmoja wa abiria Hamis Seif amesema kuwa kuna changamoto ya Usafiri katika msimu wa siku kuu na kuomba yaongezwe mabasi hata daladala katika mikoa ya jirani na Dar es Salaam.

Aidha amesema kuwa suala la ukaguzi katika kituo cha mabasi Ubungo ni mzuri na kutaka na mikoa mingine wafanye hivyo kwa ajili ya usalama wa abiria.
 Askari wa usalama barabarani Grant Pawa akiandika makosa ya basi wakati wa ukaguzi wa mabasi katika kituo cha mabasi Ubungo jijini Dar es Salaam.
 Maafisa Polisi wakiwa katika ukaguzi katika kituo cha mabasi Ubungo jijini Dar es Salaam 
 Moja ya tiketi aliyekatiwa msafiri ambaye kampuni ya basi hilo halipo katika kituo cha Ubungo abiria anadai kuwa aliyemkatia na kutia saini ni Rama Tall.
 Abiria wakisubiri Usafiri katika kituo cha mabasi Ubungo jijini Dar es Salaam.
 Abiria wakiwa wamefurika katika katika Kituo cha Mabasi Ubungo jijini Dar es Salaam.
 Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani katika kituo cha mabasi Ubungo wakiwa na fundi wakufanya ukaguzi wa basi katika kituo cha mabasi Ubungo jijini Dar es Salaam.
 Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani Nuru Hussein akifanya Ukaguzi katika basi kuangalia uimara wa Gurudumu pamoja na Brenk katika kituo mabasi Ubungo jijini Dar es Salaam.
Askari wa kituo cha mabasi Ubungo Nuru Hussein akimpa maelezo Dereva  wakati akifanya Ukaguzi ,jijini Dar es Salaam.