Friday, October 31, 2014

8th NANYUKI SERIES OPENS IN KIGALI

The 8th Inter-Parliamentary Relations Seminar (Nanyuki Series), was officially opened this morning by the President of the Rwanda Senate, Rt. Hon Bernard Makuza.

In his remarks, Rt Hon Makuza called on EALA and the National Assemblies to strengthen their relations and to effectively collaborate to tackle the underlying conditions that give insecurity and terrorism a chance.

“Parliamentarians and all stakeholders must step up real and collective efforts, to enhance mindset, awareness, and contribute to develop policies and legislations to effectively prevent all violent tendencies, negative and destructive ideologies”, Rt Hon Makuza stated.

The President of the Rwanda Senate called on stakeholders to go the extra mile to provide opportunities for the youth as a strategy to combating terrorism. This he noted, includes providing education, employment and real opportunities for the young people.
The Speaker of EALA, Rt. Hon Margaret Nantongo Zziwa makes her remarks
Rt. Hon Makuza noted that Rwandans were today re-building the country and had embraced good governance as a pre-requisite to development. “Twenty years ago, under the visionary leadership of H.E. Paul Kagame, Rwandans commenced on the process of re-building the country after the Genocide against the Tutsi”, Rt Hon Makuza said.

“Drawing from this experience, I would like to emphasize that security and peace must be focused on as a foundation for our achievements and aspirations. That is why I want to stress especially that we the leaders, have the duty to prevent and to fight the root causes of insecurity and terrorism, genocide ideology and its denial in the region, in all their forms of manifestations”, he added.

The seminar themed: “Insecurity and Terrorism as Threats to EAC Integration: How Can EAC Develop a Common Position” is organized by EALA in conjunction with the Association of European Parliamentarians with Africa (AWEPA).
The President of the Rwanda Senate, Rt. Hon Bernard Makuza delivers his speech
It brings together an estimated 250 participants drawn from Partner States National Assemblies, EALA, academicians, high ranking Government officials as well as other regional stakeholders.

In her remarks, the Speaker of EALA, Rt. Hon Margaret Nantongo Zziwa called for concerted efforts to ensure the region is secure.

“The unwarranted attacks in the region should be a wake-up call that as a region we need to be vigilant at all times and that containing terrorism and ensuring peace must assume greater importance and significance in the agenda of Regional Economic Communities,” she said.

Rt Hon Zziwa urged the Partner States to ratify the Protocol on Peace and Security in order to ensure its effective implementation.  So far, only the Republics of Rwanda and Uganda have ratified the Protocol.
Group photo opportunity
The Speaker challenged the region to look inwards and go the extra mile towards enhancing good governance as envisaged under article 23 of the Treaty for the establishment if the EAC.

“I believe that there is clear correlation between security and governance interventions in terms of cause and effect.  Of essence hereunder, are a number of fundamental areas including promoting rule of law and access to justice, adhering to democratic principles and strengthening of electoral processes and protection and promotion of Human Rights,” Speaker Zziwa said.

In his keynote remarks, Prof Pascal Mihyo, Executive Director of the Organisation for Social Science in Eastern and Southern Africa (OSSREA), an Addis based think-tank remarked that terrorism was threatening integration and that it was necessary to efficiently find adequate solutions.

“Let us not tolerate terrorism, you can smell it….you do not need to see it, just confront it”, Prof Mihyo said. Prof Mihyo noted that terrorists continue to use Africa as a launch pad to attack their historical enemies who are largely from the West.

“We need to strengthen security systems and check on our porous borders among other areas”, he said. Prof Mihyo cited Eco-terrorism and bio-terrorism as new emerging forms.   At the same time, radiological weapons including uranium, plutonium and cobalt are been used as dirty bombs in the quest to spread fear.

Dr Godwin Murunga of the African Leadership Centre stated that legislation was vital to contain terrorism.

Other presentations to be delivered during the two day seminar on the Status of Security in the EAC region by Dr. Adams Oloo, of the University of Nairobi, a presentation on the Role of Parliamentarians and stakeholders in ensuring peace and security in the EAC region and statements by leaders of delegations from the Partner States’ Parliaments.

The seminar aims at promoting functional relations between EALA and the National Assemblies as envisaged in Article 49 of the Treaty for the Establishment of the EAC.

It is anticipated that Members of the National Assemblies will be provided with an opportunity to appreciate the progress made so far in the EAC integration process and therefore the issues discussed will subsequently find their way to be agendas for National Assemblies.

WANAHABARI KILIMANJARO WATEMBELEA MAMLAKA YA MAJI SAFI NA USAFI WA MAZINGIRA MOSHI(MUWSA)

Afisa Uhusiano wa Mamlaka ya Maji safi na usafi wa Mazingira(MUWSA),Florah Stanley akifanya utambulisho kwa waandishi wa habari walipotembelea Mamlaka hiyo.
Baadhi ya Wanahabari waliotembelea Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira(MUWSA)
Meneja Fedha wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Moshi(MUWSA) Joyce Msiru akijitambulisha kwa wanahabari.
Mwenyekiti wa TUICO tawi la MUWSA,Maulid Barie,Katibu wa TUICO tawi la MUWSA ,Jacob Olotu wakati wa ziara ya Waaandishi wa habari katika ofisi za Mamlaka hiyo.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira ,Mhandisi Cyprian Luhemeja akizungumza na wanahabari (hawako pichani)walipotembelea ofisi za mamlaka hiyo.
Toka shoto ni Meneja Biashara wa MUWSA,John Ndetiko ,Meneja rasilimali watu ,Michael Konyaki wakati wa kiako na wanahabari kilicho fanyika katika ukumbi wa Bodi ya MUWSA.
Baadhi ya watendaji wa MUWSA.
Meneja Ufundi wa MUWSA ,Patrick Kibasa akizungumza jambo wakati wa kikao hicho.
Meneaja Biashara MUWSA ,John Ndetiko akizungumza jambo wakati wa kikao hicho.
Mkurugenzi wa MUWSA,Mhandisi Cyprian Luhemeja akitoa maelezo kwa wanahabari kuhusu uchimbaji wa visima kwa ajili ya kuongeza uzalishaji wa maji katika vyanzo vyake.
Mkurugenzi MUWSA,Mhandisi Cyprian Luhemeja akiwaonesha wanahabari Moja ya tanki lililopo eneo la CCP ambalo linatumika kuhifadhi maji.
Mhandisi Luhemeja akionesha moja ya kisima kilichochimbwa katika eneo la matanki ya kuhifadhi maji ambacho pia kutasaidia kuongeza maji katika matanki hayo kwa ajili ya matumizi. 
Na Dixon Busagaga wa Globu 
ya Jamii kanda ya Kaskazini.







TABATA FC YAINGIA ROBO FAINALI YA LIGI YA DK. MWAKA SPORTS EXTRA NDONDO CUP BAADA YA KUIFUNGA SIFA POLITAN KWA PENALTI 4-3

 Wachezaji wa timu za Boom FC na Vijana ya Ilala wakisalimiana kabla ya mchezo wao wa hatua ya 16 Bora ya michuano ya Dk. Mwaka Sports Extra Ndondo Cup 2014 uliofanyika katika Uwanja wa Shule ya Sekondari ya Benjamini Mkapa jijini Dar es Salaam. Timu hizo zilitoka sare ya bila kufungana.
 Kikosi cha timu ya Vijana ya Ilala kikiwa katika picha ya pamoja kabla ya mchezo wao na Boom FC katika Uwanja wa Shule ya Sekondari ya Benjamini Mkapa jijini Dar es Salaam.
Kikosi cha timu ya Boom FC kikiwa katika picha ya pamoja.
 Mashabiki wa timu ya Boom FC, wakipiga ngoma wakati timu yao ikicheza na Vijana ya Ilala.
Nahodha wa timu ya Vijana Ilala (kushoto) akisalimiana na mwenzake wa Boom FC, kabla ya kuanza kwa mchezo wao wa Ligi ya Dk. Mwaka Sports Extra Ndondo Cup.
Mshambuliaji wa timu ya Vijana Ilala, Matola Selemani, kushoto akiwania mpira na winga wa timu ya Boom FC, Nambongo Hussein katika mchezo wa Ligi ya Dk. Mwaka Sports Extra Ndondo Cup.
Mshambuliaji wa timu ya Boom FC,Issac Tesha (katikati) akijaribu kufunga  bao katika Ligi ya Dk. Mwaka Sports Extra Ndondo Cup 
Winga wa timu ya Boom FC, akiwatoka mabeki wa timu ya Vijana ya Ilala katika mchezo wa Ligi ya Dk. Mwaka Sports Extra Ndondo Cup. 
Beki wa timu ya Vijana Ilala Ramadhani Yasini, (kushoto) akiwania mpira na mshambuliaji wa timu ya Boom Ally Kondo, katika Ligi ya Dk. Mwaka Sports Extra Ndondo Cup.     
Baadhi ya wadau wa  Soka wakifuatilia mechi kati ya Tabata FC na Sifa Politan kwenye Uwanja wa Bandari.  
Kiungo mshambuliaji wa timu ya Sifa Politan, Mathayo Edward (kulia) akitafuta mbinu za kuwatoka mabeki wa timu ya Tabata FC, katika Ligi ya Dk. Mwaka Sports Extra Ndondo Cup mechi iliyochezwa katika Uwanja wa Bandari Dar es Salaam. Tabata ilishinda kwa Penati 4-3.    
 Mashabiki wa timu ya  Sifa Politan wakishangilia timu yao.
 Mashabiki wa timu ya Tabata FC wakishangilia ushindi wa timu yao baada ya kuifunga Sifa Politan kwa mikwaju ya penalti 4-3.
 Kipa wa Sifa Politan akiruka bila mafanikio kujaribu kuokoa penalti iliyopigwa na Kudura Shaban wa Tabata FC. 
Heka Heka katika lango la timu ya BOOM FC.
 Mashabiki  soka wakifuatilia pambano la Sifa Politan na Tabata FC kwenye Uwanja wa Bandari.
Wadau wa Soka wakifuatilia pambano la Sifa Politan na Tabata FC kwenye Uwanja wa Bandari.
 Mashabiki  soka wakifuatilia pambano la Sifa Politan na Tabata FC kwenye Uwanja wa Bandari.
 Mashabiki wa timu ya Tabata FC wakishangilia ushindi wa timu yao baada ya kuifunga Sifa Politan kwa mikwaju ya penalti 4-3.
Mashabiki wa timu ya Tabata FC wakishangilia ushindi wa timu yao baada ya kuifunga Sifa Politan kwa mikwaju ya penalti 4-3.

Thursday, October 30, 2014

Uelewa juu ya Brand na Product / Huduma na tofauti zake


Katika ulimwengu wa kijasirimali, tumekuwa tukishuhudia biashara zinazoanzishwa kila kukicha, na moja ya malengo makuu ya biashara yoyote ni kuhakikisha inafanikiwa na kupokelewa vyema na watumiaji.Na mapokeleo haya ndiyo yatakayokujenga au kukubomoa,na mapokeo hayo ndiyo yanayotengeneza brandi ya huduma au bidhaa yako.
Biashara nyingi huwa na majina kama ni njia mojawapo wa kujitambulisha au kujitofutisha na wengine wanaotoa / uza huduma au bidhaa inayofanana.
Kitu unachotakiwa kufahamu ni kuwa, bidhaa / huduma inapokuwa maarufu, inaweza kutengeneza brandi moja kwa moja, na brandi inaweza kutumika kama jina la bidhaa ila kuna utofauti kati ya brandi na huduma. Mfano, bia ya kilimanjaro (brand), watu wengi wakienda madukani husema nipe kilimanjaro ya baridi (wakimaanisha bia ya kilimanjaro),ili kuondoa mkanganyiko, hebu tuangalie tofauti kati ya bidhaa / huduma na brandi.


Makampuni yanatengeneza / toa bidhaa/huduma, wateja wanatengeneza brandi

Makampuni yanatengeneza bidhaa au kutoa huduma zenye majina ambazo hununuliwa na wateja, ila brandi huja kutokana na muono, matarajio na hata uzoefu wa wateja.
Mfano, bidhaa za Toyota ni magari, brandi kuu wanayotumia ni Toyota, na kwenye kila bidhaa zao huwa na brandi nyingine zinazotofautiana kulingana na mifumo yake, mfano Toyota Hiece, Toyota Prado nk, hivyo Prado ni brandi ndogo ya brandi kubwa Toyota. Toyota wanatengeneza magari ila Prado ni gari la toyota leye sifa fulanifulani kulingana na uzoefu wa wateja. Uzoefu huu unaotengenezwa na watumiaji ni lazima utoke kwa muuzaji bidhaa (Nini cha kipekee kwenye bidhaa / huduma yako? , nini unataka wateja wakipate kwenye bidhaa / huduma?). Kumbuka, wateja hawanunui bidhaa, bali kitokanacho na bidhaa na hiki ndicho kitatengeneza brandi yako.Hivyo ni lazima ukidhi matakwa / mategemeo ya wateja toka kwako.


Bidhaa zinaweza kubadilishwa na kukopiwa ila brandi lazima iwe ya kipekee.

Chukuli mfano,kampuni ya Bonite ilipotengeneza maji ya chupa na kuyapa jina la Kilimanjaro ambalo baadaye likaja kuwa brandi, baada ya muda kampuni ya Azam nayo ikaja na maji ya chupa wakayaita Uhai. Hivyo Azam hawakuziwa kutengeneza maji ya chupa ila haiwezekani kuja na maji ya chupa wakayaita Kilimanjaro kwakuwa Bonite tayari wanayo maji ya chupa yenye brandi ya Kilimanjaro.(Ila, kumbuka, ili uwe na haki ya watu wengine kutotumia jina la brandi yako kisheria, unatakiwa kuisajili umiliki wake (Copyright) kwenye idara husika, kwa Tanznia brela ndiyo wanahusika na hili).
Kwenye mfano huu, Brandi ya Kilimanjaro inampa mtumiaji matarajio ya kipekee, pia baada ya kuyatumia kwa muda anapata uzoefu nayo na kuyaweka kwenye kundi fulani. Hivyo kwa kila mteja, uzoefu toka brandi moja ni tofauti kabisa na ule wa brandi nyingine ingawa zote ni bidhaa sawa (kwenye mfano wetu, ni maji ya chupa).
Na hizi brandi hujumuishwa na vitu vingine vingi kama gharama, aina ya watu wanayoitumia, mahali zinapouzwa nk. Hivyo jikite kuhakikisha brandi yako kweli ina upekee.

Kutengeneza bidhaa na kukubalika / tumika ni kitendo cha haraka, lakini kutengeneza brandi inatumia muda

Chukulia mfano Google walipokuja na mtambo wa utafutaji (Search Engine) watumiaji waliutumia, ila mtambo huo (product) haukuwa na maana kwa wateja mpaka walipoutumia na kuona fauida zake na kuanza kuuona ni sehemu yao (brand). Na wakaanza kusema, brandi ya google inawawezesha kutafuta na kupata taarifa haraka online.
Na ndiyo maana, leo hii Google wakitoa huduma yoyote mpya, hutumia muda mfupi sana watu kuikubalikwakuwa watu wanaamini brandi kuu ya Google kama si longolongo.
Ndiyo maana kuna watu, wao ukiongelea magari, ni magari ya Toyota, hata kama ana pesa kiasi gani, huwezi kumuhamisha, na kuna wa Benzi, kuna wa Nissan nk, kutegemeana na uzoefu wao juu ya bidhaa.Hivyo, wateja hawa wanakuwa wamejenga uaminifu na brandi na siyo bidhaa.
Vitu vya muhimu kuzingatia ni kuwa, bidhaa / huduma zaidi ya moja inaweza kuwakilishwa na brandi moja, mfano ndani ya brandi ya Dudumizi, kuna huduma nyingi ndani yake kama kutengeneza websitekutengeneza systems nk, pia inawezekana brandi moja ikawa na brandi nyingine nyingi ndogondogo ndani yake, mfano, brandi ya toyota, ndani yake kuna brandi za Prado, Marino nk. Hapo utagundua, Huduma ya magari inawasilishwa na brandi ya Toyota, halafu kwakuwa kila gari lina uzoefu na utofuti wake, basi linawakilishwa na brandi tofauti.

Ni dhahiri makala hii itakuwa imefungua maswali mengi sana juu ya brandi, tembelea kurasa yetu ya Facebook hapa kwa maoni zaidi. Na tuonane kwenye makala ijayo juu ya jinsi ya kutengeneza brandi ya huduma / bidhaa yako.

Spika Makinda apigiwa chapuo Urais Bunge la SADC


Na Owen Mwandumbya, Victoria Falls, Zimbabwe

Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Anne Makinda ameendelea kuungwa mkono na wajumbe wa Mkutano wa 36 ambao ni Maspika na Wabunge kutoka Umoja wa Chama cha Mabunge ambao ni wanachama wa  nchi za kusini wa Jangwa la Sahara (SADC PF) kugombea nafasi ya Urais ya Umoja huo ili aweze kuongoza kwa kipindi cha miaka 2 ijayo katika chama hicho.

Jitihada hizo zimeendelea kujitokeza hapa Victoria Falls ambako mkutano huo unafanyika baada ya baadhi ya Maspika wa Nchi za SADC pamoja na wabunge wao kuomba miada ya kukutana naye na kumwambia dhahiri kuwa nchi zao wanamuunga mkono na wangependa aweze kushiriki uchaguzi huo ili waweze kumchagua awaongoze katika kipindi cha miaka miwili kutimiza malengo waliyojiwekea katika umoja huo.

Mkutano huo wa 36 wa Wabunge wa SADC umeanza tangu tarehe 26 Oktoba 2014 hapa mjini Victoria Falls nchini Zimbabwe na unatarajiwa kumalizika tarehe 3 Novemba, 2014, na mojawapo ya agenda za mkutano huo ni uchaguzi wa rais wa chama hicho baada ya rais anaemaliza muda wake ambaye pia ni Spika wa Mauritius Mhe. Abdool Razack Mahomed Ameen Peeroo,kutakiwa kukabidhi madaraka kwa rais Mwingine atakayepatikana katika Mkutano huu baada ya kipindi chake kumalizika.


Uchaguzi wa rais wa Umoja huu wa mabunge ya SADC utafanyika tarehe 2 Novemba, 2014, ambapo kwa kuwa nafasi hii ni ya mzunguko kwa nchi za ukanda huu, kwa mzunguko uliopo hivi sasa nchi zinazopewa nafasi ya kuleta mgombea ni tatu ambazo ni Tanzania, Msumbuji, na Seychelles ambapo kila Spika kutoka nchi hizi atapigiwa kura ili aweze kupatikana mmoja wapo atakayeongoza Umoja huu kwa miaka miwili ijayo.

Licha ya kwamba wagombea ni watatu, tayari wajumbe wamkutano kutoka nchi mbalimbali za SADC wamekuwa wakifanya jitihada za Makusudi ili Spika Makinda aweze kupewa nafasi hii waweze kutumiza malengo waliyokuwa mamejiwekea.


Akizungumza na Mhe. Makinda mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Bunge hilo la SADC Mhe. Sylvianne Valmont kutoka Ushelisheli  amesema “tunajua kuwa wewe  sio kwamba ni mgeni katika Umoja huu, ushawishi unaojitokeza kutoka kwetu  unataokana na  mafanikio makubwa uliyoyaleta katika chama hiki pindi ulipokuwa Makamu wa rais wa Umoja huu mwaka 2008 hadi 2010”

Akielezea zaidi baadhi ya mafanikio ya uongozi wake akiwa Makamu wa rais Mhe. Valmont anasema ni jitiohada za makusudi  za kuongoza ujumbe wa Wabunge wanawake kutoka nchi za SADC kwenda katika nchi za Botswana,  Malawi, Mozambique na Zambia kwa lengo la kuwashaiwshi viongozi wa Mataifa hayo kuongeza idadi ya uwakilishi wa wanawake katika mabunge yao angalau kwa asilimia 30, zoezi ambalo lilifanikiwa sana.


Nae Mjumbe kutoka Swaziland Mhe. Sikhumbazo Ndlovu anasema Mhe. Makinda anaweza kuongoza umoja huu na kuupeleka kwenye mafanikio zaidi kutokana na ushawishi Mkubwa iliyonayo Nchi ya Tanzania  katika nchi wanachama wa SADC swala ambalo linafanya wajumbe wengi wa Umoja huu kuamini kuwa chini ya uongozi wake atasaidia sana kusukumu baadhi ya maswala ya chama hiki kwa Serikali za nchi wanachama.

 Kwa upande wake Makinda amewahakikishia Wajumbe wa Mkutano huo kuwa atahakikisha anatimiza matarajio ya wanachama wa umoja huu hususani kuufanya umoja huu kuwa bunge madhubuti la SADC cha msingi ni kuhakikisha wanampigia kura kama wanavyo ahidi.

Pamoja na hilo Mhe. Makinda anasema kukubalika kwa Tanzania katika Ukanda  huu wa SADC na kampeni inayofanywa ili aweze kuongoza Bunge hili la SADC unatokana na historia Tanzania iliyojiwekea tangu wakati wa Ukombozi wa Bara la Afrika mwanzoni mwa miaka ya 1960, ambapo Tanzania chini ya Uongozi wa hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, nchi yetu ilijitwalia heshima mbele ya uso wa kimataifa kutokana na mchango wake wa kulikomboa bara la  Afrika kutoka katika uongozi wa kikoloni hususan katika Kutoa mchango wa ukombozi kwa vyama vya ukombozi vya nchi za Kusini mwa Afrikakama vile, Zimbabwe (ZANU), Afrika Kusini (ANC na PAC),Namibia (SWAPO), Angola (MPLA) na Msumbiji (Frelimo).


Uchaguzi wa Rais wa chama hiki mwaka huu, unakuja kukiwa na matarajio makubwa ya kuanzishwa kwa Bunge madhubuti la SADC ambapo Katibu Mkuu wa umoja huu Dk Esau Chiviya, anasema kauli mbiu ya mwaka huu ambayo inasema “Bunge la kikanda la SADC – Wakati ni huu” inazingatia na kuhitimisha matarajio ya waasisi wa umoja huu ya kuwa na Bunge imara la ukanda huu wa SADC ambapo anaamini kuchaguliwa kwa rais wa umoja huo lazima kwende sambamba na uwezo wake kuweza kufanikisha jambo hili haraka iwezekanavyo. 

“ Tunaaamini rais tutakayempata katika mkutano huu unaweza kuharakisha kuweza kushirikiana na wakuu wanchi za SADC kuweza kufanya umoja huu kuwa Bunge kamili la SADC na lenye nguvu kimaamuzi” anasema Dkt. Chiviya

Kwa hivi sasa Rais Robert Mugabe ndiye mwenyekiti wa wakuu wa  nchi za SAD ambapo endapo  spika Makinda atachaguliwa kuwa rais wa chama hiki atasaidia kuendelea kumshawishi Rais Mugabe ili suala la kuanzishwa kwa Bunge hilo la ukanda wa SADC linakuwa moja ya agenda kuu katika Mkutano ujao wa wakuu wa Nchi za SADC unaotarajiwa kufanyika Mwakani 2015 nchini Botswana.

Katika mkutano huo wa mwaka wa umoja wa Mabunge ya SADC Mhe. Makinda anaongoza ujumbe wa Wabunge sita kutoka Tanzania ambao ni Mhe. Seleman Jafo, Mhe. Anna Abdalah, Mhe. Mohamed Mnyaa, Mhe. Goodluck Ole-Medee, na Mhe. Stella Manyanya.

Zaidi ya Wabunge 100 ikiwa ni pamoja na Maspika wa Mabunge ya nchi za SADC wanashiriki Mkutano huu.

WAZIRI WA FEDHA AZINDUZI WA CHAPISHO KUU LA UTAFITI WA MAPATO NA MATUMIZI YA KAYA BINAFSI 2011-2012-TANZANIA BARA


Waziri wa Fedha, Saada Mkuya Salum (Katikati) akionyesha kitabu cha Ripoti ya Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi wa Mwaka 2011/12 wakati akikizindua katika ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam jana Oktoba 29, 2014. Wanaoshuhudia kutoka kulia ni Ofisa kutoka Shirika la Maendeleo la DPG, Sinikka Antila, Mwakilishi wa Benki ya Dunia, Philippe Dongier na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Beno Ndulu.  Picha zote na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.

Waziri wa Fedha, Saada Mkuya Salum akikata utepe kuashiria uzinduzi wa kitabu cha Ripoti ya Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi wa Mwaka 2011/12 wakati akikizindua katika ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam jana Oktoba 29, 2014. Wanaoshuhudia ni Afisa Habari wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Veronika Kazimoto (kulia) na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Beno Ndulu (katikati).

Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dk. Albina Chuwa akimfafanulia jambo Waziri wa Fedha, Saada Mkuya Salum mara baada ya kufanya uzinduzi.

Waziri wa Fedha, Saada Mkuya Salum akimkabidhi chapisho Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Beno Ndulu.

Wawakilishi toka Mashirika mbali mbali ya Kimataifa wakiwa katika picha ya pamoja.
   Waziri wa Fedha, Saada Mkuya Salum, akihutubia wageni waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa kitabu cha Ripoti ya Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi wa Mwaka 2011/12 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam jana Oktoba 29, 2014.

Wageni waalikwa wakifuatilia kwa makini.
Waandishi wa habari nao hawakuwa mstari wa nyuma.
Meza kuu ikifuatilia kwa makini.
Wanafunzi wa Chuo cha Takwimu nao walifika.
Wawakilishi toka mashirika ya kimataifa nao walifika.

Furaha ya kukutana pamoja.
Picha ya Pamoja.