Tuesday, October 31, 2017

PTA BANK BECOMES TDB - WITH INCREASED COMMITMENT FOR FUNDING IN EASTERN AND SOUTHERN AFRICA

Trade and Development Bank (TDB), Principal Project and Infrastructure Finance Officer, Neema Siwingwa (right), addresses a press conference in Dar es Salaam yesterday to announce the changes of its trade name which were former known as Eastern and Southern Africa Trade and Development Bank (PTA Bank) to TDB. Looking on is Trade and Development Bank (TDB), Director Corporate Affairs & Investor Relations, Mary Kamari. 
 
 The Eastern and Southern African Trade and Development Bank, commonly known as PTA Bank, has changed its official brand name to TDB (Trade and Development Bank).

Since its establishment over three decades ago, the Bank has operated under its legal name ‘’Eastern and Southern African Trade & Development Bank” as well as two trading names in English and in French: PTA Bank / Banque de la ZEP. Through the revitalization of its corporate branding, the Bank will be trading under one trade name (Trade and Development Bank – TDB) and a new logo while its legal name ’Eastern and Southern African Trade & Development Bank” will remain unchanged.

The leading regional multilateral Development Finance Institution (DFI) has also announced that it will continue to increase financing for priority sectors such as infrastructure, manufacturing, industry and agribusiness across the 21 member states it operates in, over the next five years.

“Our rebranding represents our rejuvenation and recommitment to innovate and play a more active role in promoting trade, economic development and regional integration, at a crucial time when the region is looking to more vigorously advance economic transformation and ratchet up the tapering growth ,” said Admassu Tadesse, President and Chief Executive of the Trade and Development Bank.

Mr. Tadesse further stated, “In recent years, we have been giving a big boost to our financing of trade, enterprise and infrastructure, which is evidenced in the tripling of our loan assets in the past five years. We have made substantial contributions to the rising economic growth and infrastructure development in the region, in line with regional and international development strategies, notably those aimed at achieving the Sustainable Development Goals and Africa’s Vision 2063. We have funded several landmark projects such as Kilwa Power in Tanzania, the Fibre Optic Backbone Project in Burundi and renewable energy projects such as Turkana Wind Power in Kenya, Hydromax Minihydro in Uganda, and industrial projects such as cement and steel plants in DR Congo, Djibouti, Zambia, Rwanda, Ethiopia and Zimbabwe. We will continue scaling up, with continued attention to sustainability and good corporate governance.”

The rebranding follows several years of improved asset quality, healthy profitability and innovation, on the back of a series of institutional reforms aimed at strengthening and modernizing the Bank. “We have dramatically increased our capacity to meet the rising demand for the Bank’s products and services, thanks to the strong funding partnerships we have built up with long term funders and investors. Our shareholder base has increased by more than 50% in recent years, with several new institutional investors and Member States. Indeed our equity capital has tripled since we embarked on the current corporate plan in 2012” added Mary Kamari, Director of Corporate Affairs and Investor Relations.

The Trade and Development Bank will continue to support independent power and transport projects, as well as agribusiness, and industry, alongside trade financing of essential commodities such as fertilizer, equipment, agricultural commodities and petroleum. Trade finance is typically provided on a structured basis, with emphasis on self-liquidation mechanisms, term lending is done mostly on a balance sheet, and at times on a project basis, with tenors ranging up to three years for trade related financing, and up to 15 years for infrastructure projects. The Bank has also financed numerous agribusiness projects throughout eastern and southern Africa, notably Malawi and Sudan, and provided important asset finance facilities to the air-transport sector in the region, with Rwanda Air, Kenya Airways and Ethiopian Airlines benefitting.    

RC MAKONDA AOKOA BILLION 1.11 KUFUFUA MAGARI MENGINE YA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA YALIYOKUFA


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akikaribishwa na viongozi wa jeshi wakati alipokwenda kukabidhi Mabasi 10 chakavu ya Vyombo vya Ulinzi na Usalama kwa kampuni ya Dar Coach kwa ajili kufufuliwa upya na kuwa ya kisasa.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda leo amekabidhi Mabasi 10 chakavu ya Vyombo vya Ulinzi na Usalama kwa kampuni ya Dar Coach kwa ajili kufufuliwa upya na kuwa ya kisasa.

Mabasi hayo 10 chakavu yanatoka kwenye Vyombo vya Ulinzi na Usalama ikiwemo Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ Magari 3, Jeshi la Polisi Magari 4 pamoja na Jeshi la Magereza Magari 3 ambapo yote kwa pamoja Matengenezo yake yameokoa kiasi cha Shilingi Billion 1,110,000,000 ya Serikali.

Makonda amesema kuwa Gari hizo zitatengenezwa na kukamilika ndani ya Siku 90 hadi 120 ambapo ameipongeza Kampuni ya Dar Coach kwa kujitolea kukarabati Magari hayo bila kutumia pesa ya Serikali.

Aidha Makonda amesema Magari hayo yatafungwa Vifaa vya Kisasa ikiwemo Kiyoyozi (AC), Mfumo wa Chaji ya Simu kila Seat, Runinga, Radio, Viti vya kisasa, Vyoo vya Ndani, Bodi mpya pamoja na mwonekano mzima wa Gari ili ziwe za kisasa.

Amesema mpango wake wa kuendelea kuongezea nguvu Vyombo vya Ulinzi na Usalama hautokoma kwakuwa lengo lake ni kuwatumikia Wananchi na Askari wajivunie kufanyakazi chini ya Mkuu wa Mkoa mwenye kuwapenda na kuwajali.

Amemuagiza Kamanda wa Polisi kanda maalumu ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa kuhakikisha Ving'ora vya Jeshi la Polisi vinakuwa tofauti na kampuni za Ulinzi na Usalama, Magari ya Wagonjwa ili kupunguza Mkanganyiko kwa wananchi na kujengea heshima Jeshi la Polisi.

Makabidhiano hayo yameshuhudiwa na Viongozi wa Vyombo vya Ulinzi na usalama akiwemo Kamanda wa Polisi Dar es Salaam Lazaro Mambosasa, Mkurugenzi wa usafirishaji JWTZ Kanal RAajab Mwenyumbu, Mnadhimu wa Jeshi la Magereza ACP. Noel James ambapo wote kwa pamoja wamempongeza mkuu wa mkoa kwa hatua kubwa anayoifanya ya kuhakikisha wanafanya kazi katika mazingira mazuri.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda akimkabidhi Mabasi 10 chakavu ya Vyombo vya Ulinzi na Usalama kwa Mkurugenzi wa kampuni ya Dar Coach kwa ajili kufufuliwa upya na kuwa ya kisasa wakishuhudiwa na  Mkuu wa Wilaya ya Temeke Felix Lyaviva,Kamanda wa Polisi Dar es Salaam Lazaro Mambosasa, Mkurugenzi wa usafirishaji JWTZ Kanal RAajab Mwenyumbu, Mnadhimu wa Jeshi la Magereza ACP. Noel James.
Mabasi 10 chakavu yakiwa yanatoka katika Chuo cha Polisi Kilwa Road kuelekea Mkuranga kwenye ofisi za Kampuni ya Dar Coach kwa ajili ya kufanyiwa marekebisho na kuwa ya kisasa zaidi.
Mkuu wa Mkoa Paul Makonda akiwa ndani ya basi la Magereza.


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akiwa sambamba na Mkuu wa Wilaya ya Temeke Felix Lyaviva,Kamanda wa Polisi Dar es Salaam Lazaro Mambosasa, Mkurugenzi wa usafirishaji JWTZ Kanal RAajab Mwenyumbu, Mnadhimu wa Jeshi la Magereza ACP. Noel James wakati wa kukagua mabasi 10 chakavu kabla ya kupelekewa kwenye gereji ya Dar Coach kwa ajili ya matengenezo.Picha zote na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

RC Rukwa aahidi kuimarisha utendaji kazi wa watumishi wa Rukwa katika Sekta zote

​Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joackim Wangabo amewatahadharisha watumishi kutobweteka baada ya aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen kustaafu na kumkabidhi yeye kijiti cha utekelezaji wa shughuli za maendeleo ya mkoa.

Amesema kuwa hatomwangusha Rais Dk. John Pombe Magufuli kwa kumuamini na kumkabidhi madaraka hayo na kuahidi kuwa ataimarisha elimu inayoonekana bado ipo chini kwa ufaulu lakini pia kuendeleza kasi ya uzalishaji katika kilimo.

“Baada ya kusoma kabrasha hili la kukabidhiana ofisi kuna mambo mengi ya kuyazingatia ikiwemo, elimu, kilimo, ulinzi na usalama, utunzaji wa mazingira, uvuvi na uwekezaji katika viwanda. Hasa katika elimu maana mimba ni nyingi, kuna upungufu wa madawati, upungufu wa vyumba vya madarasa lakini pia kiwango cha ufaulu hakijafikia kile kilichopo katika ilani ya Chama cha Mapinduzi ambayo ni asilimia 80 kwa darasa la saba,” Alisisitiza.

Mh. Wangabo ameyasema hayo katika makabidhiano ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa mapema leo hii tarehe 31/10/2017 katika ukumbi wa ofisi hiyo, jambo lililoshuhudiwa na watumishi wa sekretariet ya Mkoa pamoja na baadha ya Halamashauri.

Katika kuhakikisha utendaji kazi unakuwa wa ufanisi Mh. Wangabo amesema kuwa hupemda kusikiliza mipango ya watendaji inayotekelezeka ili waweze kuitekeleza kama walivyoipanga nay eye ataisimamia na kutoa ushauri wa kuongeza kasi ya utekelezaji pale inapobidi ili kuyafikia malengo waliyojiwekea kwa wakati.

Kwa upande wake aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen amewashukuru watumishi wote wa serikali katika Mkoa wa Rukwa pamoja na wananchi wa mkoa kwa kumpa ushirikiano katika kipindi chote alichokuwepo na kuwaomba waendeleze kumpa ushirikiano huo huo Mkuu wa Mkoa mpya ili naye aweze kufanya majukumu yake kwa ufanisi.
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joackim Leonard Wangabo (kushoto) na Mh. Zelote Stephen (Waliokaa) katika picha ya pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, Wakuu wa Wilaya pamoja na baadhi ya Wakurugenzi wa Halmashauri na Mwenyekiti wa CCM Mkoa.
 Mkuu nwa Mkoa wa Rukwa, Mh. Joachim Leonard Wangabo akisalimiana na Meneja wa PS3 Mkoa wa Rukwa Bi. Rose wakati wa kumkaribisha Mh. Wangabo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa tayari kwaajili ya Kuanza kazi.
Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Kamishna Mstaafu Zelote Stephen (kushoto) akimkabidhi nyaraka za ofisi Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joackim Wangabo. katika makabidhiano ya ofisi hiyo yaliyofanyika katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa. 

 Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Kamishna Mstaafu Zelote Stephen (kushoto) akisaini nyaraka za ofisi Mkuu wa Mkoa kwaajili ya Kumkabidhi ofisi hiyo Rukwa Mh. Joackim Wangabo. 

IGP SIRRO ATAKA JESHI LA POLISI KUDUMISHA MICHEZO

Na Jeshi la Polisi.

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro amewataka Maofisa na Askari Polisi kote nchini kushiriki michezo ili kujenga Afya,ukakamavu na urafiki baina ya wenyewe kwa wenyewe na raia.

IGP Sirro ameyasema hayo jijini Dar Es Salaam wakati hafla fupi ya kuwapongeza wachezaji wa TAEKWONDO waliofanya vizuri katika michezo ya Taekwondo Pumsae (kucheza Kata), Taekwondo Gyeokpa ( kuvunja kibao kwa kuruka Juu) na Taekwondo Gyeorugi (Mapigano) iliyomalizika hivi karibuni ambapo timu ya Polisi iliibuka na ushindi wa kwanza  katika timu 17 zilizoshiriki.

Sirro alisema Jeshi la Polisi litaendelea kutilia mkazo michezo ya aina mbalimbali na atahakikisha Askari na Maofisa wanapata fursa ya kushiriki michezo kwakuwa kwakufanya hivyo kutasaidia pia kulitangaza Jeshi la Polisi na kujenga mahusiano na jamii."Hakikisheni hamrudi nyuma,tutawapa sapoti ya kila namna ili tusiwe wasindikizaji bali tuweze kutoa ushindani na kufanya vyema na ni jambo linalowezekana kwa kuwa ari na morali ipo"Alisema Sirro.

Kwa Upande wake Mkuu wa Michezo wa Jeshi la Polisi,Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Philip Kalangi alisema ushindi wa timu hiyo ni chachu katika kujiandaa na michezo ya majeshi ya EAPCCO itakayofanyika hapa nchini mwakani ambapo Tanzania itakuwa mwenyeji.

mashindano hayo yaliyoandaliwa na ubalozi wa Jamhuri ya korea ukishirikiana na Chama cha Walimu wa Taekwondo kutoka korea (Korean Taekwondo Masters Association) ambayo ni mashindano ya Taekwondo ya kitaifa yaliyofanyika tarehe 21/10/2017 ambayo yalishilikisha vilabu 17 vya Taekwondo kutoka  nchi nzima ambavyo ni Makongo Juu, Kariakoo,Shark TKD,Twiga Triple A,HTC DSM, KILI, Vingunguti,Arusha Morden,TCC,AICC,UAUT pamoja na vilabu vya Polisi ambavyo ni DPA, MPA na ZPA.
  Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro, akiwa na viongozi wa Jeshi la Polisi  Sambamba na Askari Polisi walioshiriki na kujinyakulia medali mbalimbali katika mashindano ya mchezo wa Taekwondo iliyo andaliwa na Ubalozi wa Jamuhuri ya Korea ukishirikiana na Chama cha walimu wa Taekwondo kutoka Korea. (Korean Taekwondo Masters Association)
 Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro, akiwa na askari wa jeshi hilo wanaounda timu ya Taekwondo ambao walishiriki na kujinyakulia medali mbalimbali katika mashindano ya Taekwondo yaliyo andaliwa na Ubalozi wa Jamuhuri ya Korea ukishirikiana na Chama cha walimu wa Taekwondo kutoka Korea. (Korean Taekwondo Masters Association) yaliyoshirikisha vilabu 17 vya Taekwondo kutoka nchi nzima.

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simoni Sirro akimvisha medali askari Polisi ambaye ni miongoni mwa askari waliojinyakulia medali katika mashindano taekwondo iliyo andaliwa na Ubalozi wa Jamuhuri ya Korea ukishirikiana na Chama cha walimu wa Taekwondo kutoka Korea. (Korean Taekwondo Masters Association). Picha zote na Jeshi la Polisi

CLINIC YA METHANONE ZANZIBAR YAPATIWA VIFAA VYA KUCHUNGUZA WATEJA WAO

 Mratibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la dawa za Kulevya na Uhalifu  (UNODC) Bi. Immaculate Nyoni  akimkabidhi boksi lenye vifaa vya kupimia mkojo watumiaji dawa ya Methadon ambao wanatumia  aina nyengine ya dawa kinyume na taratibu katika hafla iliyofanyika Kliniki Methadone Kidongochekundu.
 Rais wa watumiaji dawa ya Methadon Zanzibar Hilal Nassor akizungumza na wandishi wa habari baada ya kukabidhiwa vifaa vya kuwatambua watumiaji wa tiba ya Methadone na baadae kutumia dawa aina nyengine.
Baadhi ya watumiaji dawa za Methadone wakisubiri kupatiwa huduma katika Kliniki yao iliyopo Hospitali ya wagonjwa wa akili Kidongo- Chekundu Mjini Zanzibar.Picha na Makame Mshenga.

Na Ramadhani Ali – Maelezo .
          
Wagonjwa wanaotumia dawa aina ya Methadone kama tiba baada ya kuathirika kutokana na dawa za kulevya na wanaoutumia aina nyengine ya dawa  kwa njia za siri wamepatiwa muarubaini baada ya kupatikana vifaa maalumu vya kumgundua mtumiaji kwa kumpima mkojo.

Vifaa hivyo vinavyojulikana kwa jina la DOAKIT vimetolewa na shirika la Umoja wa Mataifa la kupambana na madawa ya kulevya na uhalifu (UNODC).Mratibu wa Mradi wa Taifa wa kupambana na HIV/AIDS kwa wafungwa, Immaculate Nyoni ambae ni afisa wa UNODC Tanzania amemkabidhi vifaa hivyo Mratibu wa huduma za ukimwi kwa watu wa makundi maalum Zanzibar Dkt. Shaaban Hassan katika hafla iliyofanyika Kliniki ya Methadone iliopo ndani ya hospitali ya wagonjwa wa akili Kidongo- chekundu.

Immaculate alisema UNODC itaendelea kuunga mkono juhudi zinazochukuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuwapatia tiba sahihi wagonjwa walioathirika na dawa za kulevya.Alisema kwa kuanzia wameleta DOAKIT 1500 ambazo zinaweza kutumika kwa kipindi cha miezi mitatu kwa mujibu wa idadi ya wagonjwa wanaotumia Methadone waliosajiliwa katika kliniki hiyo.

Daktari dhamana wa hospitali ya Kidogochekundu Dkt. Khamis Othman alilishukuru shirika la UNODC kwa kuwapatia msaada huo ambao kwa kipindi cha mwaka mmoja walikuwa na upungufu mkubwa na kupelekea baadhi ya wagonjwa kutumia aina nyengine ya dawa bila kujulikana.

Alisema kwa mujibu wa taratibu za kutumia tiba ya Methadone mgonjwa hatakiwi kutumia aina nyengine ya dawa za kulevya na akifanya hivyo hupata madhara makubwa kwa kuongeza kiwango cha dawa mwilini.

Alisema DOAKIT ni viifaa vyenye uwezo wa kugundua aina sita ya dawa za kulevya kwa kuchunguza mkojo wa mtumiaji na vinaweza kutumika katika maeneo mbali mbali kuwachunguza watumiaji wa dawa hizo.Dkt. Khamis alieleza kuwa Kliniki ya Methadone ya Kidongochekundu ilianzishwa mwaka 2015 na imesajili wagonjwa 434 ambao wanapatiwa  tiba kamili na imekuwa mkombozi wa vijana wengi waliokubali kujiunga.

Alisema kazi ya Methadone ni kusaidia kuondosha hamu ya kutumia Heroine na dawa nyengine za kulevya hatimae mtumiaji huacha kidogo kidogo kutumia dawa hizo.Hata hivyo amekiri kuwa bado wanakabiliwa na changamoto kubwa kwani baadhi ya wagonjwa wanaotumia Methadone hukosekana baadhi ya siku na wanatumia dawa nyengine za kulevya kwa siri.

Wagonjwa wanaotumia Methadone wamekiri kuwa inawasaidia  kujitambua na imewarejesha katika mfumo bora wa maisha na wanaaminika ndani ya jamii zao.
Amina Omar mkaazi wa Jangombe, alietumia dawa za kulevya kwa miaka 25, alisema wakati anatumia dawa hizo alikuwa hajitambui na alidhoofu kufikia uzito wa chini ya kilo 40 na baada ya kutumia Methadone hivi sasa uzito wake umefikia kilo 80.

ZIARA YA NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII, MHE. JAPHET HASUNGA KATIKA SHAMBA LA MITI SAO HILL NA KITUO CHA MALIKALE CHA ISMILA NA KALENGA MKOANI IRINGA

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kulia) akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Amina Masenza alipotembelea shamba la miti Sao Hill kukakua shughuli mbalimbali zinazofanywa na shamba hilo mkoani Iringa hivi karibuni. Aliagiza uongozi wa shamba hilo kuongeza juhudi za upandaji miti ili kukidhi mahitaji makubwa yaliyopo nchini na hivyo kusisimua ukuaji wa uchumi wa viwanda.
Naibu Waziri wa Maliasili, Mhe. Japhet Hasunga (kulia) akikagua baadhi ya vifungashio vya asali alipotembelea shamba la miti Sao Hill kwa ajili ya kukakua shughuli mbalimbali zinazofanywa na shamba hilo mkoani Iringa hivi karibuni. Asali inayozalishwa na shamba hilo imefanyiwa vipimo nchini Ujerumani na kugundulika kuwa ni bidhaa bora isiyo na viambata vya kemikali ya aina yeyote. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Amina Masenza na Afisa Ufugaji Nyuki wa shamba hilo, Said Abubakar. 
Meneja wa shamba la miti Sao Hill, Salehe Beleko (kushoto) akimueleza Mhe. Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kulia) kuhusu moto uliovamia hekta 77 za shamba hilo na hatua zilizochukuliwa kuudhibiti alipotembelea  kukakua shughuli mbalimbali zinazofanywa na shamba hilo mkoani Iringa hivi karibuni, alisema moto huo uliozuka hivi karibuni ulianzia kwenye mashamba ya wananchi haukuwa na madhara makubwa. 
Meneja wa Shamba la Miti Sao Hill, Salehe Beleko (kulia) akimuelezea Naibu Waziri wa Maliasili, Mhe. Japhet Hasunga kuhusu utafiti unaofanywa na shamba hilo kwa kushirikiana na Kampuni ya Art International kuhusu uvunaji wa utomvu kwa ajili ya kutengeneza madawa mbalimbali, bazooka (chewing gums) na ‘gel’ kwa ajili ya kujiongezea kipato alipotembelea shamba hilo kukagua shughuli mbalimbali hivi karibuni. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Mhe. Jamhuri David. 
Meneja wa Shamba la Miti Sao Hill, Salehe Beleko (kulia) akimuelezea Naibu Waziri wa Maliasili, Mhe. Japhet Hasunga (hayupo pichani) kuhusu njia mpya ya kuzalisha mbegu za miti kwa njia ya vikonyo ili kuongeza zaidi uzalishaji alipotembelea shamba hilo kukagua shughuli mbalimbali hivi karibuni. Aliagiza uongozi wa shamba hilo kuongeza juhudi za upandaji miti ili kukidhi mahitaji makubwa yaliyopo nchini na hivyo kusisimua ukuaji wa uchumi wa viwanda.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kushoto) akimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Amina Masenza (wa pili kulia) alipotembelea Kituo cha Mambo ya Kale cha Ismila kukakua shughuli mbalimbali zinazofanywa na kituo hicho mkoani Iringa hivi karibuni. Wa pili kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Mhe. Richard Kasesela. 
Naibu Waziri wa Maliasili, Mhe. Japhet Hasunga (wa pili kushoto) na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Amina Masenza (kushoto) wakipata maelezo kutoka kwa Mhifadhi wa Mambo ya Kale, Laurent Nampunju (kulia) kuhusu fuvu la Chifu Mkwawa alipotembelea Makumbusho ya chifu huyo kukakua shughuli mbalimbali zinazofanywa na kituo cha Mambo ya Kale cha Kalenga mkoani Iringa hivi karibuni. 
Jengo la Makumbusho ya Mkwawa ambalo lipo ndani ya Kituo cha Mambo ya Kale cha Kalenga Mkoani Iringa.
 Picha ya Chifu Mkwawa ambayo inapatikana katika makumbusho hayo.
Muonekano wa fuvu la Chifu Mkwawa ambalo pia linapatikana katika makumbusho hayo. (Picha na Hamza Temba - WMU)

WAKAZI WA BAGAMOYO WAKUNWA NA TAMASHA LA EFM MZIKI MNENE

 Msanii wa Muziki wa Hip Pop Nchini, Izo Busines akitoa Burudani kwa wakazi wa Wilaya ya Bagamoyo katika Tamasha Maarufu la Mziki Mnene lililofanyika katika Bar ya Dunda Dunda linaloandaliwa na Efm Radio kwa kushirikiana na Tv E
 Mkali wa Muziki wa Bongo Fleva nchini, Prince Dully Sykes akiimba na Mashabiki wakati wa Tamasha la Muziki Mnene linaloandaliwa na Radio ya Efm na Tv E ambalo lilifanyika katika Bar ya Dunda Dunda Wilaya ya Bagamoyo mkoa wa Pwani.
 RDJ Mamy kutoka Efm Radio akitoa burudani kwa wakazi wa Wilaya ya Bagamoyo kwenye Tamasha la Mziki Mnene lililofanyika katika Bar ya Dunda Dunda
  Mkali wa Muziki wa Bongo Fleva nchini, Prince Dully Sykes akiimba na Mashabiki wakati wa Tamasha la Muziki Mnene linaloandaliwa na Raido ya Efm na Tv E ambalo lilifanyika katika Bar ya Dunda Dunda Wilaya ya Bagamoyo mkoa wa Pwani.
 Msanii Mkongwe wa Muziki wa Bongo Fleva nchini, Dudubaya akitoa Burudani kwa Mashabiki wake wa Bagamoyo katika Tamasha la Mziki Mnene lililoandaliwa na Efm Radio.
 Mkali wa Muziki wa Singeli nchini Msaga Sumuakitoa burudani kwa wakazi wa Bagamoyo wakati wa Tamasha la Muziki Mnene lililoandaliwa na Kituo cha Radio cha Efm na Tv E katika Bar ya Dunda Dunda.
  Mkali wa Muziki wa Singeli nchini Msaga Sumuakitoa burudani kwa wakazi wa Bagamoyo wakati wa Tamasha la Muziki Mnene lililoandaliwa na Kituo cha Radio cha Efm na Tv E katika Bar ya Dunda Dunda.
 RDJ Timber Mtu Mbaya akitoa Burudani kwa wakazi wa Bagamoyo wakati wa Tamasha la Mziki Mnene lililoandaliwa na Efm Radio na  Tv E.
 RDJ Black kitoa Burudani kwa wakazi wa Bagamoyo wakati wa Tamasha la Mziki Mnene lililoandaliwa na Efm Radio na  Tv E.
Mashabiki wakishangilia Tamasha la Efm MZIKI MNENE Katika Bar ya Dunda Dunda Bagamoyo.

MAKANDARASI KUKUTANA JIJINI DAR, KUJADILI MAENDELEO YA UKUAJI WA VIWANDA

 Mwenyekiti wa Chama cha Makandarasi Mhandisi Lawrence Mwakyambiki (katikati) akieleza jambo kwa waandishi wa habari(hawapo pichani) katika utambulisho wa mkutano wa chama hicho utakaofanyika Novemba 17, 2017 Diamondi Jubilee Jijini Dar es Salaam,kulia ni Meneja Mauzo wa benki ya cba Bi.Kunenguda Dedede na kushoto ni Mkuu wa Masoko kutoka NMB Bi.Linda Teggisa.
Meneja Mauzo wa benki ya cba Bi.Kunenguda Dedede akieleza jambo kwa waandishi wa habari( hawapo pichani)  kuhusu mkutano wa makandarasi hapo novemba 17, 2017 katika ukumbi wa diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam, wa kwanza kushoto ni Mkuu wa masoko  kutoka NMB Bi.Linda Teggisa na Mwenyekiti wa Chama cha Makandarasi Mhandisi Lawrence Mwakyambiki.(Picha na Paschal Dotto-MAELEZO)

Na.Paschal Dotto-MAELEZO.
Chama cha Makandarasi (CATA) kinachounganisha wakandarasi wote nchini kinatarajia kukutana Novemba 17, 2017 kujadili kuhusu ukuaji wa viwanda nchini mkutano utakaofanyika katika ukumbi wa Diamondi Jubilee Jijini Dar es Salaam.

Akizungumuza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho Mhandisi Lawrence Mwakyambiki alisema kuwa  Serikali ya Aawamu ya Tano chini ya uongozi wa Rais John Pombe Magufuli iko kwenye njia ya ujenzi wa viwanda kwa hiyo sekta ya ujenzi inahitajika kwa kiasi kikubwa kwenye sera hii ya viwanda.

“Lengo la mkutano huu kwa wakandarasi hawa ni kutaka kuleta mchango wao katika ujenzi wa uchumi wa Tanzania na wameona kwamba kama wazawa wanaowajibu wa kutoa mchango katika katika ujenzi wa viwanda nchini”, alisema Mhandisi Mwakyambiki.

Aidha Mhandisi Mwakyambiki aliseka kuwa katika maendeleo ya taifa tasnia ya ujenzi ni muhimu kwani inabeba vitu vingi na kuwawezesha wananchi kupata huduma stahiki kama elimu na afya na kuwataka makandarasi kufanya kazi zo kwa ufanisi mkubwa.

Katika mkutano huu ambapo CATA watakuwa waratibu vyama vingine vya wakandaarasi vikiwemo Tanzania Civil Engineering Contractors Association(TACECA) pamoja na Association of Citizen Contractors(ACCT) na  mabenki  ya cba na NMB ambayo yatatoa ufadhili wa mkutano huo.

Akibainisha miradi itakayochukua nafasi katika majadiliano hayo Mwakyambiki alisema kuwa katika serikali hii ya awanu ya tano miradi inayohitaji  wakandarasi ni Ujenzi wa miundombinu ya reli(SGR), sekta ya maji, bomba la kusafirisha mafuta ghafi(uganda –tanzania) pamoja na ujenzi wa makao makuu ya nchi Dodoma.

Aidha aliongeza kuwa katika mkutano huo ambao unatarajiwa kuhudhuliwa na wakandarasi zaidi ya 200 ambao watatoa mawazo yao kuelekea ujenzi wauchumi wa viwanda kama sera ya awamu ya tano inavyoelekeza  ni muhimu kwa ujenzi wa taifa.



Mhandisi Mwakyambiki alisema kuwa katika kutambua mchango wa wakandarasi ni mara ya kwanza kwa mkutano huo kutokea Tanzania katika tasnia hiyo na mgeni rasmi katika mkutano huo atakuwa katibu mkuu wa sekta ya ujenzi kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe Injinia Joseph Nyamuhanga.

OFISI YA MAKAMU WA RAIS YAANDAA WARSHA YA UZINDUZI WA MRADI WA KUJENGA UWEZO KWA TAASISI KATIKA UDHIBITI WA KEMIKALI NA TAKA SUMU

 Mgeni Rasmi katika warsha ya uzinduzi wa Mradi wa kujenga uwezo kwa Tasisi katika udhibiti wa kemikali na taka sumu , Bwana Richard Muyungi ambaye ni Mkurugenzi idara ya Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais akiongeakatika uzinduzi wa warsha hiyo.
 Mkurugenzi Msaidizi wa Mazingira katika Ofisi ya Makamu wa Rais Bi Magdalena Mtenga akiongea wakati wa warsha hiyo iliyoandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais, Idara ya Mazingira.
 Sehemu ya Washiriki wa warsha hiyo wakifuatilia kwa makini hotuba ya Mgeni Rasmi (hayupo pichani).
Mwakilishi wa UNEP  Bibi Nalimi Sharma akiongea katika warsha hiyo, pembeni yake Mkurugenzi wa Mazingira Ofsis Ya Makamu wa Raisambaye  ni Mgeni Rasmi Bwana Richard Muyungi
 Mkurugenzi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais Bwana Richard Muyungi akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe waliohudhuria warsha hiyo kutoka Taasisi mbalimbali za Serikali.

Nchi zinazoendelea zinakabiliwa na changamoto katika suala zima la usimamizi na udhibiti wa kemikali na taka sumu. Taka sumu nyingi zimekua tishio kwa Wananchi hasa Wanawake na Watoto. 

Hayo yamesemwa na Mgeni Rasmi  ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais,  Bwana Richard Muyungi alipokua akifungua warsha ya uzinduzi wa mradi wa kujenga uelewa kwa Taasisi za Serikali katika udhibiti na usimamizi wa kemikali na taka sumu jijini Dar Es Salaam.

Pia ametoa shukrani kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira (UNEP) kwa msaada wa kifedha katika kuanzishwa kwa mradi huo, ameongeza pia  Wajumbe waliohudhuria warsha hiyo wakaitumie vema elimu watakayoipata katika sehemu zao za kazi ili kuongeza weledi na maarifa.

Akiongea katika warsha hiyo Mwakilishi kutoka UNEP Bi.Nalimi Sharma amesema amefurahi sana kuhushuria uzinduzi wa warsha ya mradi huo na kuona jitihada mbalimbali zinazochukuliwa katika suala zima la usimamizi na udhibiti wa kemikali na taka sumu. Ameongeza kuwa UNEP itaendelea kutoa msaada wa kifedha kwa kwa Ofisi ili kuendelea kuimarisha shughuli za usimamizi na udhibiti wa kemikali na taka sumu. 

TANZANIA YAWA KINARA KATIKA MAPAMBANO YA UKATILI WATOTO BARANI AFRIKA

Na Humphrey Shao Globu ya Jamii

TANZANIA imetajwa kuwa ni nchi ya kwanza barani afrika katika mapambano dhidi ya ukatili watoto kulinganisha na mataifa mengine.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa shirika la Kimataifa linaloshughulikia haki za watoto, Elimu na Ushauri, Michael Gibbons alipokuwa akitoa mada katika mkutano wa kujadili masuala ya ukatili kwa watoto na Wanawake uliofanyika jijini Dar es Salaam Leo.

Gibbons amesema Tanzania ndio nchi pekee Afrika iliyoweka nguvu kubwa katika mapambano ya ukatili wa mtoto pamoja na kuweka mazingira wezeshi ya elimu kutokana na sera yake ya Elimu Bure.

Akizungumza kwa Niaba ya Waziri wa afya jinsia Wanawake na Watoto, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Watoto, Magreth Mussai amesema Serikali inatumia takribani Bilioni 6.7 kutibu naa kushughulikia matokeo ya ukatili.

“katika kulinda watoto baada ya matukio ukatili kutokea Taifa linatumia Bilioni 6.7 kwa ajili ya kushughulikia Mahakamani, Matibabu na hatua zote anazostaili mtoto na Wanawake baada ya ukatili kutokea.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Haki Elimu nchini John Kalaghe amesema asilimia 52.6% ya vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa watoto hutokea mashuleni jambo ambali limekuwa likipigiwa kelele na wazazi wengi.

Kalaghe amesema ukatili wa watoto ni moja ya jambo ambalo linasumbua katika ukanda huu wa Afrika Mashariki ikiwemo Tanzania na kutaja watoto wa kike na wakiume hapa nchini upitia ukatili wa kupigwa mashuleni kwa asilimia 52.6 %.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Haki Elimu,John Kalaghe akizungumza wakati wa mkutano wa kujadili Masuala ya haki za Watoto na Wanawake katika ukanda Afrika Mashariki
Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa linaloshughulikia haki za Watoto, Elimu na Ushauri, Michael Gibbons akizungumza katika Mkutano wa kujadili Masuala ya haki za Watoto na Wanawake katika ukanda Afrika Mashariki
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Watoto na Wanawake , Magreth Mussai akizungumza katika mkutano huo kwa Niaba ya Waziri wa Afya Wanawake jinsia na watoto.
Meneja Maendeleo na utawala wa shirika la kutetea Watoto nchini Uganda , Deogratias Yiga. akizungumza kwenye mkutano wa kujadili Masuala ya haki za Watoto na Wanawake katika ukanda Afrika Mashariki.
baadhi ya wadau walioshiriki katika mkutano wa kujadili Masuala ya haki za Watoto na Wanawake katika ukanda Afrika Mashariki.
baadhi ya wadau walioshiriki katika mkutano wa kujadili Masuala ya haki za Watoto na Wanawake katika ukanda Afrika Mashariki.
baadhi ya wadau walioshiriki katika mkutano wa kujadili Masuala ya haki za Watoto na Wanawake katika ukanda Afrika Mashariki
wadau walioshiriki katika mkutano wa kujadili Masuala ya haki za Watoto na Wanawake katika ukanda Afrika Mashariki wakiwa katika Picha ya pamoja