Sunday, August 31, 2014

Wabunge Afrika Mashariki watembelea Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSuBa)

 Spika wa Bunge la Jumuiya ya AfrikaMashariki (EALA) Mhe. Margareth Zziwa akipanda mti  katika eneo la Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSuBa) jana wakati wa ziara ya Wabunge wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Upandaji wa mti huo ni katika kutekeleza azimio la Jumuiya ya Afrika Mashariki katika jitihada za kutunza mazingira
 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na  Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara (MB) akipanda mti  katika eneo la Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSuBa) jana wakati wa ziara ya Wabunge wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Upandaji wa mti huo ni katika kutekeleza azimio la Jumuiya ya Afrika Mashariki katika jitihada za kutunza mazingira.
 Spika wa Bunge la Jumuiya ya AfrikaMashariki (EALA) Mhe. Margareth Zziwa (Kulia) akipata maelezo kutoka kwa mmoja wa wajasiriamali waliokuwa wameweka bidhaa zao nje ya ukumbi wa  Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSuBa) tayari kwa kuonyesha na kuuza bidhaa zao wakati wa ziara ya Wabunge wa Jumuiya ya Afrika Mashariki waliotembelea Taasisi hiyo jana mjini Bagamoyo. 
 Mmoja wa wabunge wa Bunge la Jumuiya ya AfrikaMashariki (EALA) Mhe. Susan Nakawuki (mwenye blauzi ya pinki) akinunua bidhaa kutoka kwa mmoja wa wajasiriamali waliokuwa wameweka bidhaa zao nje ya ukumbi wa  Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSuBa) tayari kwa kuonyesha na kuuza bidhaa zao wakati wa ziara ya Wabunge wa Jumuiya ya Afrika Mashariki waliotembelea Taasisi hiyo jana.
 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara (MB) akiweka saini katika daftari la wageni katika moja ya kikundi cha wajasiriamali waliokuwa wameweka bidhaa zao nje ya ukumbi wa  Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSuBa) tayari kwa kuonyesha na kuuza bidhaa zao kwa wakati wa ziara ya Wabunge wa Jumuiya ya Afrika Mashariki waliotembelea Taasisi hiyo jana.
 Baadhi ya Wabunge wa Afrika Mashariki akiwemo Mhe. Shyrose Bhanji anayewakilisha  Tanzania katika bunge hilo wakiangali kazi za sanaa ya uchingaji kutoka kwa mmoja wa wajasiriamali waliokuwa wameweka bidhaa zao nje ya ukumbi wa  Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSuBa) tayari kwa kuonyesha na kuuza bidhaa zao kwa wakati wa ziara ya Wabunge wa Jumuiya ya Afrika Mashariki waliotembelea Taasisi hiyo jana.
 Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki Mhe. Shyrose Bhanji wa Tanzania akimkabidhi zawadi ya sinia lililotokana na kazi za uchongaji Spika wa Bunge la Afrika Mashariki Mhe. Margareth Zziwa mara baada ya kupenda bidhaa hiyo na kuamua kumnunulia spika huyo jana wilayani Bagamoyo wakati wa ziara ya Wabunge wa Afrika Mashariki katika Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSuBa).
 Katikati ni Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki ambaye pia ni mtoto wa Baba wa Taifa Mhe. Makongoro Nyerere (katikati) akifurahia jambo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afika Mashariki wa  Serikali ya Tanzania Bibi. Joyce Mapunjo na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel walipokuta katika viwanja vya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSuBa) wakati wa ziara ya wabunge wa Afrika Mashariki katika Taasisi hiyo.
 Spika wa Bunge la Jumuiya ya AfrikaMashariki (EALA) Mhe. Margareth Zziwa (Kulia) akikabidhi kitabu cha mpango mkakati wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa  Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSuBa) Bw. Michael Kadinde wakati wa ziara ya Wabunge wa Afrika Mashariki. TaSuBa ni taasisi pekee katika ukanda wa Afrika Mashariki uliopewa dhamana ya kuwa Kituo cha Maarifa katika Nyanja za Sanaa na Utamaduni
 Spika wa Bunge la Jumuiya ya AfrikaMashariki (EALA) Mhe. Margareth Zziwa (Kulia) akikabidhi kitabu cha mpango mkakati wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Mhe Ahmed Chipozi jana wilayani Bagamoyo wakati wa ziara ya Wabunge wa Afrika Mashariki katika taasisi ya Sanaa na Utamaduni (TaSuBa). Anayeshuhudia katikati ni Waziriwa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara (MB).
 Spika wa Bunge la Jumuiya ya AfrikaMashariki (EALA) Mhe. Margareth Zziwa (Kushoto)  na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara (MB).wakiwa na baadhi ya Wabunge wa Afrika Mashariki wakipata maelezo kuhusu muelekeo na malengo ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSuBa)  kutoka Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa taasisi hiyo Bw. Michael Kadinde jana wakati wa ziara ya wabunge hao.
 Kikundi cha Sanaa kutoka Taasisi ya Sanaa na Utamaduni (TaSuBa)wakifanaya sanaa za maonyesho kwa mchezo aina ya  Akrobati mbele ya wageni ambao ni wabunge wa Afrika Mashariki wakiongozwa na Spika wa Bunge hilo Mhe. Margareth Zziwa (Hawapo picha) walipotembelea taasisi hiyo jana mjini Bagamoyo.
 Kikundi cha Sanaa kutoka Taasisi ya Sanaa na Utamaduni (TaSuBa)wakichezo ngoma yenye asili ya kabila la Kisukuma ijulikanayo kama Gobogobo mbele ya wageni ambao ni wabunge wa Afrika Mashariki wakiongozwa na Spika wa Bunge hilo Mhe. Margareth Zziwa (Hawapo picha) walipotembelea taasisi hiyo jana mjini Bagamoyo.
 Baadhi ya wageni wakifurahia ngoma wakati wa ziara ya wabunge wa Afrika Mashariki jana mjini Bagamoyo walipotembelea Tasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSuBa).
Kutoka kulia mwenye skafu niNaibu Waziri wa Afrika Mashariki wa Tanzania Dkt.Abdulla Juma Abdulla, Spika wa Bunge la Jumuiya ya AfrikaMashariki (EALA) Mhe. Margareth Zziwa (mwenye miwani), Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara (MB), Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki Mhe. Makongoro Nyerere, Mwenyeki ti wa Bodi wa TaSuBa Bw. Abraham Bafadhili na Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa TaSuBa Bw. Michael Kadind wakiwa katika picha ya pamoja na wasanii wa kikundi cha sanaa kutoka taasisi hiyo wakti wa ziara ya wabiunge wa Afrika Mashariki katika taasisi hiyo jana.

RACHAEL CLAVERY ASHINDA TAJI LA MISS LAKE ZONE 2014. AONDOKA NA MKOKO WA MILIONI 10!

Mshindi wa Miss Lake Zone 2014 Rachael Clavery (katikati) akila pozi katika picha ya ukumbusho na mshindi wa pili Mary Emanuel( kulia) na Mshindi wa tatu Nikole Sarakikya ( kushoto). Rachael amejinyakulia zawadi nono ya Gari la millioni 10 CCM Kirumba Jijini Mwanza. Shindano hilo lililokuwa na Walimbwende 18 wote wakichuana vikali kila mmoja akitaka ashinde hatimaye usiku huu Rachael Clavery amewafunika wenzake na kuibuka na ushindi. Picha zote na Faustine Ruta wabukobasports.com
Kwenye picha ya pamoja
Kwenye picha ya pamoja washindi Mshindi wa Miss Lake Zone 2014, Rachael ClaveryDoreen Robert (kushoto) Aliyeshika nafasi ya nne akipata picha ya pamoja na wenzake.Gari aliloshinda Miss Lake Zone 2014 Rachael Clavery usiku huu...Mshindi wa kwanza alizawadiwa gari ya shilingi mil 10, mshindi wa pili alijibebea bajaji yenye thamani ya sh. mil 4 huku mshindi wa tatu alijipatiapatia pikipiki ya Tsh mil 1.8
Jaji Mkuu wa shindano hilo, Mkurugenzi wa Lino International Agency, Hashim Lundenga ambao ndio waandaaji wa Miss Tanzania akitangaza tano bora.Walioshika nafasi tano boraWakiulizwa maswali.Viongozi mbalimbaliWarembo wakiwa katika Vazi la UfukweniWarembo wakiendelea na Vazi la UfukweniDoreen Robert(kulia) akipita na mwenzake na Vazi la UfukweniWarembo hao walikuwa wamepiga kambi ya siku 10 katika Lenny Hotel ya Mkoani Geita na walichuana kuwania taji lililokuwa linashikiliwa na Ruth Charles.
Dada wakiwaangalia wadogo zaoWadau wakichukua kumbukumbu..Msanii wa Kizazi kipya Barnabas akitumbuiza mashabikiBarnabas akiimba wimbo wake live na kundi la Sky Light Band jukwaani.
Kundi zima la Skylight Band likishusha muziki mkali
Skylight Band wakifanya yao jukwaani..Meneja wa bendi ya Skylight, Anneth Kushaba a.k.a AK 47 akifanya yake jukwaani.Meneja wa bendi ya Skylight, Anneth Kushaba a.k.a AK 47 akizungusha zungusha huku akiweka mbwembwe juu ya jukwaa CCM Kirumba kwenye mashindano ya Miss Lake Zone 2014.
Mgeni rasmi Leonard Bugomola Mkurugenzi wa Lenny Hotel ambaye pia alikuwa mmoja wa wadhamini wa Shindano hilo akizungumza na Wakazi wa Mwanza waliojitokeza katika Uwanja wa CCM Kiumba juu ya swala zima la Miss Lake Zone 2014. 
Mratibu wa shindano la Miss Lake Zone 2014, Flora Lauwo (kushoto) akiwa na Mgeni rasmi Bw. Leonard Bugomola. Pia Mratibu aliongeza kuwa Wakiwa kambini wilayani Geita, warembo hao walifanya shughuli za kijamii ikiwemo kutoa msaada kituo cha Yatima cha Moyo wa Huruma na kutembelea mgodi wa GGM na Hospitali ya Geita na Hifadhi ya Lubondo na kufanya usafi.
Mratibu huyo ametoa pongezi kwa wadhamini wakuu, Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia kinywaji cha Redd’s, Lenny Hotel, Crown Paint, Shule ya Rishor Pre & Primary English Medium na Benki ya CRDB ya Geita. Picha na Faustine Ruta wa bukobasports.com
Warembo wote 18 jukwaani
Vazi la ufunguzi..warembo wote 18 walipanda jukwaani
Warembo waliopanda jukwaani ni Mikoa yao kwenye mabano ni Moshy Shaban: Doreen Robert; Christina Jilulu (Mwanza): Nikole Sarakikya, Mary Emanuel na Rachael Julika (Shinyanga).
Wengine ni Faudhia Haruna, Jackline Kimambo na Christina John (Kagera), huku Nyangi Warioba: Cecilia Kibada na Everlyn Charles (Simiyu). Wamo pia Martina John: Elinaja Nnko, Winfrida Nashon (Mara)huku Rose Msuya, Rachael Clavery na Faridha Ramadhani wakiwakilisha mkoa wa Geita.

MSAMA AKAMATA CD FEKI ZA MIL 200 PAMOJA NA MASHINE YA KISASA YA KURUDUFU CD

Sehemu ya CD Feki zilizokamatwa.
Msama akionesha CD zilizokamatwa katika maeneo ya Kariakoo na Kimara Bonyokwa.
Baadhi ya vifaa vinavyotumika katika kutengeneza CD feki zikiwa Kituo cha Polisi Urafiki.
Hizi ni sehemu ya CD feki zilizokamatwa.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions, Alex Msama akionyesha mashine ya kisasa aina ya LG iliyokamatwa kutoka kwa watuhumiwa wa kurudufu kazi za wasanii (CD FEKI) katika maeneo ya Kariakoo na Kimarta Bonyokwa jijini Dar es Salaam. (Picha na Francis Dande)
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions, Alex Msama akionesha mashine ya kisasa aina ya LG waliyokamatwa nayo watuhumiwa wa kurudufu CD feki za kazi za wasanii katika maeneo ya Kariakoo na Kimara Bonyokwa jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mrakibu Msaidizi wa Polisi ASP, Denis Moyo. (Picha na Francis Dande)  

Msama akionyesha wino na vifaa vingine vinavyotumika katika kutengeneza CD feki za kazi za wasanii.
Msama akionesha mashine ya kuprint Cover za CD.
CD feki zilizokamatwa katika maeneo ya Kariakoo.
Msama akizungumza na waandishi wa habari leo.
Lundo la CD feki zilizokamatwa katika maeneo ya Kimara na Kariakoo.
Kasha la CD iliyokuwa na nyimbo za mwimbaji Bahati Bukuku ikiwa imewekea stika feki ya TRA.
Baadhi ya CD feki zilizokamatwa na Kampuni ya Msama Auoctions Mart.

NA FRANCIS DANDE

OPERESHENI ya kukamata watuhumiwa wa wizi wa kazi za wasanii, imeshika kasi baada ya Kampuni ya Msama Auction Mart kukamata mashine za kisasa za kurudufu kazi za wasanii na CD feki zenye thamani ya shs. milioni 200.
Huo ni mkakati wa kampuni hiyo kwa kushirikiana na Wizara ya Habari Vijana Utamaduni na Michezo pamoja na Jeshi la Polisi katika vita ya kuwapigania wasanii waweze kunufaika na kazi zao.
Mbali ya wasanii, pia harakati hizo zinalenga kuiwezesha serikali kupata mapato yake kutoka kwa wasanii ambao siku zote wamebaki duni huku wajanja wachache wakivuna mamilioni ya fedha.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions, Alex Msama alisema operesheni hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki katika maeneo ya Kariaakoo na Kimara Bonyokwa  jijini Dar es Salaam.
 “ Ttumekamata vijana watano ambao wapo katika kituo cha Polisi cha Urafiki   na taratibu za kuwafikisha mahakamani zinafanyika,” alisema Msama.
Aidha, Msama amesema katika zoezi hilo wanamshikiria mmiliki wa nyumba moja ambayo baadhi ya watuhumiwa walikutwa wakifanya uharamia wa kudurufu kazi za wasanii, hivyo kuikosesha serikali mapato yake halali. 
“Kwa namna hii, serikali haiewezi kupata mapato na pia wasanii wataendelea kuwa ombaomba kutokana na kuibiwa kazi zao,” alisema Msama.
Msama alisema, zoezi hilo ni endelevu na litafanyika nchi nzima ambapo kampuni Msama kwa kushirikiana  na Polisi wa Kituo cha Urafiki, wameweza kuwakamata jumla ya watuhumiwa 20 ambao wanasubiri taratibu za kisheria ili kesi zao ziweze kufikishwa mahakamani.
Msama aliongeza, matunda ya operesheni hiyo, yameanza kuonekana kwani kwa kushirikiana na raia wema, wameweza kukamata mashine moja kubwa ya kisasa aina ya LG ambayo huweza kuzalisha CD feki zaidi ya ishirini kwa dakika tano. 
“Katika kipindi kicha wiki moja tumekamata mzigo mkubwa wa shs mil.200 katika maeneo ya Kimara Bonyokwa na Kariakoo na kazi bado inaenedelea,” alisma Msama.
Msama aliyechangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya muziki wa injili nchini, amejitwika jukumu hilo zito katika kupigania maslahi ya wahusika ambao wameshindwa kupiga hatua kutokana na wiki wa kazi zao.