Thursday, August 31, 2017

WANANCHI WAONDOLEWA WASIWASI KUHUSU FIDIA YA MALI ZAO ZITAKAZOPITIWA NA BOMBA LA MAFUTA

Mkuu wa Wilaya ya Singida Elias Tarimo akizungumza katika kikao na wataalamu watakaofanya uthamini wa mali na ardhi kwa ajili ya fidia katika mradi wa bomba la mafuta la Kutoka Uganda hadi Tanga.


Mthamini wa ardhi kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida Chiku Mkina (aliyevaa miwani) na wataalaamu wengine wakisikiliza kwa makini mada katika kikao kilichohusu uthamini wa mali na ardhi kwa ajili ya fidia katika mradi wa bomba la mafuta la Kutoka Uganda hadi Tanga.
Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt Angelina M Lutambi akichangia mada katika kikao kilichohusu uthamini wa mali na ardhi kwa ajili ya fidia katika mradi wa bomba la mafuta la Kutoka Uganda hadi Tanga.
Mkurugenzi wa kampuni ya Dighy Welly Dkt Jan Perold akiwasilisha mada katika kikao kilichohusu uthamini wa mali na ardhi kwa ajili ya fidia katika mradi wa bomba la mafuta la Kutoka Uganda hadi Tanga.


Mwakilishi wa Serikali katika zoezi la Uthamini kutoka Wizara ya Nishati na Madini Linus Kinyondo akizungumza na wataalamu wa mkoa wa Singida katika kikao kilichohusu uthamini wa mali na ardhi kwa ajili ya fidia katika mradi wa bomba la mafuta la Kutoka Uganda hadi Tanga.


Mhandisi wa Ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida Simwela Nuru Martin akifuatilia kwa makini kikao kilichohusu uthamini wa mali na ardhi kwa ajili ya fidia katika mradi wa bomba la mafuta la Kutoka Uganda hadi Tanga.


…………………….


Wananchi Mkoani Singida wameondolewa wasiwasi kuhusu fidia ya mali au ardhi yao ambayo itapitiwa na mradi wa bomba la mafuta kutoka Uganda hadi Tanga kwakuwa hawatapunjwa bali itazingatia vigezo vya kimataifa na kitaifa.

Mkuu wa Wilaya ya Singida Elias Tarimo amesema hayo mapema leo wakati wa kikao na wataalamu wanaofanya uthamini wa mali na ardhi ambayo itapitiwa na mradi huo.


Tarimo amesema wananchi na taasisi zote wanapaswa kutoa ushirikiano kwa kutaja gharama kulingana na thamani halisi ya mali zao na sio kuongeza gharama za juu kwakuwa vigezo vya kitaifa na kimataifa vitazingatiwa.

“wananchi wengine wasio waaminifu wananweza wakataja pesa kubwa au hata kuvamia maeneo ambayo siyo yao ilimradi wapate tu pesa, nawasihi wasifanye hivyo kwakua watakuwa wanakwamisha mradi huu muhimu sana kwa maendeleo ya taifa letu na majirani zetu Uganda”, amesema na kuongeza kuwa

“ Tunampongeza na kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John P Magufuli kwa kuhakikisha nchi yetu inapata mradi huu, tutoe ushirikiano wa kutosha ili mradi ufanikiwe kw kiwango kikubwa hasa kwa maeneo yote utakapopita kwa Mkoa wa Singida”, amesisitiza.

Tarimo ameongeza kuwa serikali ya Mkoa, wilaya, taasisi na wananchi wote wa Singida wamekuwa mstari wa mbele kutoa ushirikiano kwa miradi yote ya kitaifana kimataifa na hivyo basi wataalamu wanaofanya uthamini na wale watakaokuja kujenga wasiwe na wasiwasi wowote.

Ameongeza kuwa wananchina taasisi ziko tayari kunufaika na mradi huo kupita Mkoani Singida kwa kupata ajira za muda mfupi na mrefu, kufanya biashara pamoja na kutoa huduma mbalimbali.

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt Angelina M Lutambi amewataka wataalmau hao kushirikiana na wataalamau wa ngazi zote kuanzia mkoa hadi vijiji ili zoezi la uthamini liende vizuri.

Dkt Lutambi amesema lengo la uthamini ni kuhakikisha wananchi hawapati madhara makubwa kutokana na kupita kwa mradi huo katika maeneo hayo pamoja na kuhakikisha sheria, miongozo na taratibu zote zinafuatwa.


Ameongeza kuwa wataalamu wanapaswa kuwa wazi kwa kushirikisha taasisi na mashirika ambayo kwa namna moja au nyingine yataguswa na mradi huo pamoja na kutoa taarifa sahihi na kwa wakati kwa wote wanaohusika.

Wakichangia mada katika kikao hicho wataalamu kutoka Mkoa wa Singida wamesema uthamini uangalie athari zote ambazo zinaweza kutokea kutokana na mradi huo mfano athari ya kisaikolojia ya usumbufu wa kumhamisha mtu kutoka katika makazi yake pamoja na thari za maeneo kama vyanzo vya maji ambapo bomba litapita.

BANDARI KAVU YA KWALA –VIGWAZA KUANZA KUTUMIKA JANUARI MWAKANI




Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasilino, Profesa Makame Mbarawa (wa pili kushoto), akifafanua jambo wakati akikagua mchoro wa Bandari kavu ya Kwala –Vigwaza Mkoani Pwani.
Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasilino, Profesa Makame Mbarawa (wa pili kulia), akitoa maelekezo kwa Eng. Charles Salu Ogare anayesimamia ujenzi wa bandari kavu ya Kwala-Vigwaza Mkoani Pwani.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) Eng. Deusdedit Kakoko akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasilino, Profesa Makame Mbarawa alipokagua maendeleo ya ujenzi wa bandari kavu ya Kwala –Vigwaza Mkoani Pwani.
Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasilino, Profesa Makame Mbarawa mwenye kofia ya njano akiwa katika majukumu ya ukaguzi wa ujenzi wa bandari kavu ya Kwala-Vigwaza inayojengwa mkoani Pwani.
Muonekano wa bandari kavu inayojengwa na mkandarasi Suma-KJT katika eneo la Kwala-Vigwaza inayotarajiwa kuanza kutumika Januari mwakani ikiwa katika hatua mbalimbali za ujenzi.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini , Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa ameelezea kuridhishwa kwake na kasi ya ujenzi wa bandari kavu katika eneo la Kwala Vigwaza Mkoani Pwani na kumtaka mkandarasi Suma JKT kuongeza kasi na kuzingatia ubora.

Akizungumza mara baada ya kukagua ujenzi huo ameiagiza Mamlaka ya Bandari nchini (TPA), kushirikiana na Shirika la Reli Tanzania (TRL) na Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) kuhakikisha wanaunganisha kwa haraka ili reli na barabara zinazoingia katika bandari kavu hiyo zinakamilika na hivyo kuiwezesha bandari kavu hiyo kuanza kutumika ifikapo Januari mwakani.

“TPA, TRL na TANROADS uzuri wote mko kwenye wizara moja shirikianeni na hakikisheni kilomita 15 za barabara inayoingia kwenye bandari kavu hii na kilomita moja ya reli zinajengwa haraka,” Amesema Profesa Mbarawa.

Profesa Mbarawa amemtaka Mkurugenzi Mkuu wa TPA Eng. Deusdedit Kakoko kuhakikisha ujenzi wa bandari kavu ya Kwala-Vigwaza unazingatia ubora na viwango vilivyopo katika mkataba ili kuiwezesha kuhudumia zaidi ya makontena milioni moja kwa mwaka na hivyo kupunguza msongamano katikati ya Jiji la Dar es Salaam.

“Hakikisheni eneo la bandari kavu linakuwa na maegesho ya kutosha, taa, maji ya uhakika, gari la zimamoto, uzio na mashine ya ukaguzi wa mizigo scanner itakayowezesha kupima kila mzigo unaopandishwa na kushushwa katika eneo hili,” amesisitiza Profesa Mbarawa.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa TPA Eng. Kakoko amesema TPA imejipanga kuhakikisha ujenzi huo unatumia gharama nafuu na mifumo yote ya teknolojia ya habari na mawasiliano TEHAMA inakuwepo katika bandari hiyo ili kuiwezesaha kufanya kazi kisasa na kwa ufanisi zaidi.

“Tukifanikiwa kuhamia hapa mzigo uliokuwa unasafirishwa kwa siku saba sasa utatumia siku tatu kufika Mwanza hali itakayovutia wasafirishaji wengi kutumia bandari ya Dar es Salaam na hivyo kukuza uchumi wa nchi na kuibua fursa za ajira,” amesema Eng. Kakoko.

Bandari Kavu ya Kwala –Vigwaza inayojengwa na Mkandarasi SUMA JKT ambapo takribani kiasi cha shilingi bilioni 9 kinatarajiwa kutumika katika ujenzi huo ili kuboresha huduma za usafirishaji katika bandari ya Dar es Saalaam ambapo zaidi ya hekta 500 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi huo ambapo kwa kuanza hekta 120 sawa asilimia 24 zinajengwa katika awamu ya kwanza.

UJUMBE WA CPC ULIPOKUTANA NA MANGULA DAR NA ULIPOTEMBELEA ENEO LA UJENZI WA CHUO KIKUU CHA SIASA CHA MWALIMU NYERERE, KIBAHA

Makamau Mwenyekiti wa CCM-Bara Philip Mangula (kulia) akiongoza mazungumzo  baina yake na Naibu Waziri za Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC) Xu Luping (kulia) katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam, leo Agosti 31, 2017
 Makamau Mwenyekiti wa CCM-Bara Philip Mangula akimkaribisha Naibu Waziri za Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC) Xu Luping, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam, leo Agosti 31, 2017. Katikati ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Humphrey Polepole.
 Katibu wa NEC, Iikadi na Uenezi Humphrey Polepole akiwa tayari kumpokea Naibu Waziri za Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC) Xu Luping, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam, leo Agosti 31, 2017.
 Katibu wa NEC, Iikadi na Uenezi Humphrey Polepole akimlaki Naibu Waziri za Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC) Xu Luping, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam, leo Agosti 31, 2017. Kulia ni Katibu wa NEC Siasa na Uhuisnao wa Kimataifa kanali Mstaafu Ngemela Lubinga
 TWENDE HUKU, Lubinga akionyesha njia ya kwenda mgeni huyo
Lubinga na Polepole wakimuongoza Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC) Xu Luping, kwenda kukutana na Makamu Mwenyekiti wa CCM-Bara, Philip Mangula, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam, leo Agosti 31, 2017.
 Mgeni akiwa na Polepole
 Polepole akiendelea kumuongoza mgeni huyo
 Makamu Mwenyekiti wa CCM-Bara Philip Mangula akimsubiri kwa hamu mgeni huyo
 Makamau Mwenyekiti wa CCM-Bara Philip Mangula akimkaribisha Naibu Waziri za Mambo ya Nje
wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC) Xu Luping, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya
CCM, Lumumba, Dar es Salaam, leo Agosti 31, 2017. Katikati ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi
Humphrey Polepole.
 Makamau Mwenyekiti wa CCM-Bara Philip Mangula akimkaribisha Naibu Waziri za Mambo ya Nje
wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC) Xu Luping, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya
CCM, Lumumba, Dar es Salaam, leo Agosti 31, 2017. Katikati ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi
Humphrey Polepole
 Mzee Mangula na Mgeni wakiingia ukumbi wa mazungumzo
 Mangula na Lubinga wakiwaonyesha wageni eneo la kuketi kwa ajili ya kuanza mazungumzo
 Karibuni jamani wageni wetu. Mzee Mangula akimwambia mgeni kutoka Ubalozi wa China aliyeambatana na Naibu Waziri huyo wa CPC
 Ujumbe wa CPC kwenye mazungumzo
 Makamau Mwenyekiti wa CCM-Bara Philip Mangula (kulia) akiongoza mazungumzo  baina yake na Naibu Waziri za Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC) Xu Luping (kulia) katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam, leo Agosti 31, 2017

 Makamau Mwenyekiti wa CCM-Bara Philip Mangula (kulia) akiongoza mazungumzo  baina yake na Naibu Waziri za Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC) Xu Luping (kulia) katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam, leo Agosti 31, 2017
 Ujumbe wa CCM kwenye mazungumzo hayo
 Maofisa wa CCM kwenye mazungumzo hayo
 Maofisa wa CCM kwenye mazungumzo hayo 
 Makamau Mwenyekiti wa CCM-Bara Philip Mangula (kulia) akimkabidhi zawadi maalum Naibu Waziri za Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC) Xu Luping (kulia) katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam, leo Agosti 31, 2017
 Makamau Mwenyekiti wa CCM-Bara Philip Mangula (kulia) akizawadiwa na Naibu Waziri za Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC) Xu Luping (kulia) katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam, leo Agosti 31, 2017
 Mangula akizifurahia zawadi hizo
 Akimshuku kwa zawadi



 Mangula akimsindikiza mgeni wake. Kushoto ni Polepole na kulia ni Lubinga 
 Byeee na karibu tena, Mangula akimuaga mgeni kabla ya mgeni huyo kuondoka rasmi kwenye Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam. PICHA NYINGI ZAIDI/>BOFYA HAPA

KAMATI ZA BUNGE ZA HESABU ZA SERIKALI, NISHATI NA MADINI NA MIUNDOMBINU ZAENDELEA NA VIKAO VYAKE MJINI DODOMA.

 Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Selemani Jaffo (aliesimama)akizungumza jambo pale Watendaji wakuu kutoka ofisi hiyo walipokutana na kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali leo Mjini Dodoma.
 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Ndg. Kapulya Musomba akizungumza jambo pale kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini ilipokutana na Watendaji wakuu kutoka Shirika hilo, Wizara ya Nishati na Madini pamoja na REA leo Mjini Dodoma.
 Wajumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini wakifuatilia majadiliano baina yao na Watendaji wakuu kutoka Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Wizara ya Nishati na Madini pamoja na REA leo Mjini Dodoma.
 Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Dkt. Medard Kalemani (aliesimama) akizungumza na kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Watendaji wakuu kutoka Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Wizara ya Nishati na Madini pamoja na REA (hawapo kwenye picha) leo Mjini Dodoma. katikati ni Makamu Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Deo Ngalawa na kulia ni Katibu kamati wa kamati hiyo, Ndg. Felista Mgonja
 Makamu Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Deo Ngalawa (katikati)akizungumza jambo pale kamati hiyo ilipokutana na Watendaji wakuu kutoka Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) na REA wakijadili taarifa kuhusu Mpango wa Utekelezaji wa Matumizi na Usambazaji wa Gesi Asilia nchini pamoja na Utekelezaji wa Miradi ya REA Awamu ya Tatu pamoja na Utatuzi wa Changamoto za Ukamilishaji wa Miradi wa Awamu ya I na II. Kushoto, ni Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Dkt. Medard Kalemani na kulia ni Katibu kamati wa kamati hiyo, Ndg. Felista Mgonja
 Mjumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo Ndg. Salome Makamba akizungumza jambo pale kamati hiyo ikifanya uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa katika Mkutano wa sita, katika kikao kilichofanyika leo Mjini Dodoma. kulia Mjumbe wa kamati hiyo Mhe. Daniel Mtuka
 Mjumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo, Mhe. Tundu Lissu akisisitiza jambo pale kamati hiyo ikifanya uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa katika Mkutano wa sita, katika kikao kilichofanyika leo Mjini Dodoma, kulia ni Mjumbe wa kamati hiyo Mhe. Salome Makamba
 Makamu Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo, Mhe. Leonidas Gama akizungumza na Wajumbe wa kamati wakati kamati hiyo ikifanya uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa katika Mkutano wa sita, katika kikao kilichofanyika leo Mjini Dodoma, kulia ni katibu kamati wa kamati hiyo, Ndg. Yona kirumbi
Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Mhe. Prof. Norman Sigara king akisisitiza jambo pale kamati hiyo ilipofanya majadiliano baina yao na Watendaji Wakuu kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, TCRA, Vodacom, Airtel na Tigo (hawapo kwenye picha) katika kikao kilichofanyika leo Mjini Dodoma. kulia ni Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Edwin Ngonyani.
 Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Miundombinu wakifuatilia Majadiliano baina yao na Watendaji Wakuu kutoka TCRA, Vodacom, Airtel na Tigo katika kikao kilichofanyika leo Mjini Dodoma.

(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

POLEPOLE: TUPO TAYARI KWA UCHAGUZI MDOGO JIMBO LA LONGIDO

Katibu Wa Halmashauri Kuu Ya Chama Cha Mapinduzi (NEC), Itikadi na Uenezi Ndg Humphrey Polepole akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Sekretarieti, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam.
Waandishi wa habari wakimsikiliza kwa makini Katibu Wa Halmashauri Kuu Ya Chama Cha Mapinduzi (NEC), Itikadi na Uenezi Ndg Humphrey Polepole katika Ukumbi wa Sekretarieti, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam.
Aliyekuwa mgombea Ubunge wa Jimbo la Longido kupitia Chama Cha Mapinduzi Dkt Steven Kiruswa akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Sekretarieti, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam. Kushoto kwake ni Katibu Wa Halmashauri Kuu Ya Chama Cha Mapinduzi (NEC), Itikadi na Uenezi Ndg Humphrey Polepole

Na Mathias Canal, Dar es salaam

Chama cha Mapinduzi kimesema kuwa kipo tayari kuingia katika uchaguzi mdogo wa Ubunge Jimbo la Longido Mkoani Arusha mara baada ya kutangazwa kuwa jimbo hilo lipo wazi kutokana na maamuzi ya mahakama ya Rufaa iliyobainisha kuwa uchaguzi wa mwaka 2015 haukuwa huru na haki hivyo kufuta matokeo ya uchaguzi huo.

CCM imeeleza kuwa kulikuwa na matumizi yasiyostahili kutumika kujazwa matokeo ya Ubunge, kwa kutumia fomu namba 21c za kujaza matokeo ya Udiwani na kujaza matokeo ya Ubunge, badala ya kutumia fomu namba 21b jambo lililopelekea kufungua kesi ya kupinga ushindi wa Ubunge katika Jimbo hilo.

Kauli ya CCM imetolewa na Katibu Wa Halmashauri Kuu Ya Chama Cha Mapinduzi (NEC), Itikadi na Uenezi Ndg Humphrey Polepole wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Sekretarieti, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam.

Polepole alisema kuwa vipo vyama vya siasa ambavyo kwa kawaida hulalamika kila vinaposikia kushindwa na mahakama kwa madai kuwa hakuna haki lakini vyama hivyo kila vinaposhinda vyenyewe husema mahakama imetenda haki.

Alisema kuwa kazi ya mahakama ni kutumia sheria zilizopo na kuamua juu ya malalamiko ya wananchi kwa kuhakikisha usawa mbele ya sheria kwa watu wote unatendeka hivyo maamuzi yaliyotolewa juu ya kuwa wazi kwa Jimbo la longido ni sehemu ya maamuzi huru na haki kwa mahakama ya Rufaa nchini.

Polepole alitoa Rai kwa mahakama zote nchini kuendelea kufanya kazi yake vizuri kwa uhuru na haki pasina kusikiliza kelele za watu wanaotaka mahakama kutekeleza matakwa yao kinyume na sheria za nchi.

Kwa upande wake aliyekuwa mgombea Ubunge wa Jimbo la Longido kupitia Chama Cha Mapinduzi Dkt Steven Kiruswa akizungumza katika mkutano huo na waandishi wa habari alisema kuwa pamoja na mapingamizi ya mara kwa mara katika kipindi chote tangu rufaa ilipoanza kusikilizwa aliamua kuwa mtulivu kwa kusubiri maamuzi yatakayotolewa na mahakama kama chombo huru nchini cha maamuzi.

Alisema kuwa kwa mara ya nne mahakama ya Tanzania imethibitisha kuwa inaongozwa kwa mujibu wa sheria na kujali haki ya mwenye haki ili isipotee bure.

Alisema CCM ilifungua kesi mwanzoni mwa mwezi Novemba 2015 ikiwa ni wiki mbili tangu kumalizika uchaguzi mkuu uliofanyika Octoba 25, 2015 ambapo mahakama kuu ya Arusha ilibaini kwamba uchaguzi haukuwa huru na haki na kufikia June 29, 2016 hukumu ikatolewa na ubunge kutenguliwa jambo ambalo liliwafanya Chadema kukata rufaa zaidi ya mara tatu.

Dkt Kiruswa alisema kuwa wananchi wa Longido wamenyanyasika katika kipindi cha miaka miwili pasina kuwa na muwakilishi wa kuwasemea bungeni hivyo maamuzi ya mahakama yataifanya Tume ya Uchaguzi kutangaza rasmi uchaguzi mdogo na hatimaye muwakilishi kupatikana kwa kura za haki.

Aidha, Polepole alisema kuwa Chama Cha Mapinduzi katika muktadha wa CCM mpya Tanzania Mpya kinaendelea kusisitiza siasa safi na kutoa uongozi bora.

Alisema siasa za kutumia lugha isiyofaa, na Siasa za aina yoyote zenye mtazamo wa fitina hazina nafasi ndani ya Chama Cha Mapinduzi katika kipindi hiki ambacho Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM Mhe Dkt John Pombe Magufuli anaongoza kwani amedhamiria CCM kuwa chama cha wananchi wote chenye mtazamo chanya katika uwajibikaji.

Alitoa Rai kwa vyama vingine nchini kufanya siasa za weledi pasina kutumia lugha za kuudhi dhidi ya serikali na wananchi wake huku akiahidi kuwa chama chake hakiwezi kupoteza muda kujibu porojo za hila kwani kitakuwa hakitendi haki katika kuisimamia ilani ya uchaguzi ya mwaka 2015-2020 kwa kuwaletea maendeleo endelevu wananchi.

Polepole alisema kuwa CCM inaamini katika majibizano ya hoja kwani chama hicho kina deni kubwa kwa wananchi la kuwaletea maendeleo hivyo viongozi wote wa chama na wale wenye dhamana katika dola kuendelea kuishi misingi ya CCM Mpya ya Uadilifu, Uaminifu, Uchapakazi, Vita dhidi ya Rushwa, Vita dhidi ya ubadhilifu wa mali za chama na mali za Umma, Unyenyekevu na kusikiliza watu.

MWISHO