Tuesday, February 28, 2017

ALLY KIBA APOKEWA KISHUJAA, AISIMAMISHA JIJI LA DAR ES SALAAM NA VIUNGA VYAKE

 Ally Kiba akiwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere  akitokea nchini Afrika Kusini mara baada ya kukabidhiwa tunzo yake ya MTV kama msanii bora wa kiume Afrika
Ally Kiba akiwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere  akitokea nchini Afrika Kusini mara baada ya kukabidhiwa tunzo yake ya MTV kama msanii bora wa kiume Afrika

               

 Mashabiki wa AlyKiba ambao walifika katika uwanja wa ndege wa JNA jijini Dar es Salaam wakiwa na mabango kama wanavyoenekana pichani
 Kiba kielekea kwenye gari maalum aliyoandaliwa mara baada ya kuzngumza na mashabiki wake
 Aly Kiba akiwa na Meneja wake  Seven Mosha mara baa da ya kuingia katika gari hiyo maaalum
 Ally Kiba akiwa katika mitaa ya Kariakoo huku akiwa amezunguskwa na mashabiki mbalimbali ambao walipata fursa ya kuona Tunzo yake ya Mtv base kama msanii bora wa kiume Afrika
 Mashabikiw a Ally Kiba wakiwa wamezunguka gari ya msanii huyo katika mitaa ya Kariakoo
 Ally kiba akiwa katika mtaa wa Mueza eneo alikokokulia akiwa na Tunzo yake

 Ally Kiba akiwa na Ndugu Yake Abdul Kiba juu ya gari la wazi katika mita aya Buguruni
 Ally Kiba akimkabidhi Tunzo yake Mama yake mzazi maarufu kama Mama k
 Mama K ambaye ni mama mzazi wa Ally Kiba akionyesha Tunzo ya msani huyo juu
Baadhi ya Mashabikiwa Ally Kiba wakiwa katika Pikipiki na shangwe ya Alli ya juu

 Muonekano wa baadhi ya Nyumba zinazojengwa na Wakala wa Majengo Nchini (TBA) Bunju, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam zikiwa katika hatua za mwisho za ujenzi wake.
 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Nchini (TBA), Arch. Elius Mwakalinga, akifafanua hatua iliyofikiwa kwenye ujenzi wa nyumba kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Eng. Edwin Ngonyani, alipokagua maendeleo ya ujenzi wa nyumba hizo jijini Dar es Salaam.
 Muonekano wa moja ya mtungi wa kutengenezea gesi ukaa (Biogas), inayoendelea kujengwa katika Nyumba zinazojengwa na Wakala wa Majengo Nchini (TBA), eneo  la bunju jijini Dar es Salaam. Gesi hiyo itatumika kutoa huduma kwa wakazi wa eneo hilo.
 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Nchini (TBA), Arch. Elius Mwakalinga (wa tatu kulia), akimuonyesha  Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Eng. Edwin Ngonyani, hatua iliyofikiwa kwenye ujenzi wa hosteli za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam zinazojengwa na Wakala huo.
 Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Eng. Edwin Ngonyani wa pili kulia), akitoa maelekezo kwa Uongozi wa Wakala wa Majengo Nchini (TBA), alipokagua maendeleo ya ujenzi wa hosteli za wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar  es Salaam. Kulia ni Meneja Kikosi cha Ujenzi cha TBA, Arch. Hamphrey Killo.
Muonekano wa moja ya jengo la hosteli ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambalo limekamilika na majengo hayo yataanza kutumika wiki ijayo kufuatia ujenzi wake kukamilika.

WAZIRI NAPE MGENI RASIMI FAINALI ZA ULEGA CUP ZITAKAZOFANYIKA MACHI 5 MKURANGA

Timu ya kata ya Tengelea, Tengelea FC  imefunzu kuingia katika fainali ya Ulega Cap baada ya kuifunga Timu ya Mwandege FC  bao 1 – 0 katika mcheezo uliochezwa jana katika viwanja vya shule ya Mkuranga jana .

Bao la timu ya Tengelea lilipatikana katika kipindi cha pili kupitia mchezaji  wao Andew Joseph aliyepokea cross ambayo ndio ilipa ushindi timu hiyo.
Timu ya kata ya Tengelea, itaingia fainali kwa kukipiga na timu ya Kisiju na mechi itanguliwa na mechi ya mshindi wa tatu kati ya Mwandege FC na Lukanga FC.

Mgeni rasmi katika fainali za Ulega CUP ni Waziri Habari, Michezo, Utamaduni na Sanaa, Nape Nnauye.

Akizungumza na waandishi wa habari muandaji wa mashindano hayo Mbunge wa  Mkuranga, Abdallah Ulega amesema kuwa mashindano yameibua vipaji ya vipya.

Amesema kuwa inahitaji uwekezaji katika michezo kutokana na vijana kuonyesha vipaji vyao ambavyo vinatakiwa kuendelezwa.
 Mbunge wa Mkuranga , Abdallah Ulega akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa timu ya Tengelea iliyopata ushindi wa kuingia fainali ya Ulega CUP katika mchezo uliochezwa jana katika viwanja vya shule ya Mkuranga jana.
 Mbunge wa Mkuranga , Abdallah Ulega akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa timu ya Mwandege ambao ni washindi wa tatu katika mashindano ya Ulega Cup baada ya kupata kichapo jana na timu ya Tengelea katika mchezo uliochezwa katika uwanja wa shule ya msingi Mkuranga.
  Vijana wakionyesha vipaji vyao katika mashindano ya Ulega CUP katika mchezo uliochezwa katika uwanja wa shule ya msingi Mkuranga.
 Mashabiki  wakiwa juu ya miti wakifatilia mpira kati ya timu ya Tengelea na Mwandege FC katika mchezo uliochezwa katika uwanja wa shule ya msingi Mkuranga.

TNRF yazindua mpango mkakati wa Ardhi

Kamishna wa Ardhi kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mary Makondo(aliyesimama) akizungumza jambo wakati wa uzinduzi wa mpango mkakati wa ardhi hapa nchini Tanzania ambao utajumuisha mradi wa majaribio katika mikoa mbalimbali kuona kama utawezekana maana swala la upatikanaji wa ardhi imekuwa ni changamoto kubwa sana hapa nchini.
Mkurugenzi wa Jumuiko la Maliasili Tanzania( TNRF), Joseph Olila akizungumza wakati wa uzinduzi wa mpango mkakati wa ardhi hapa nchini Tanzania uliodhaminiwa na Jumuiko la Maliasili Tanzania ili kuweza kupatikana kwa ardhi hasa maeneo ya vijijini .
Mkurugenzi Mtendani wa Taasisi ya MVUWATA ya Morogoro, Steven Ruvuga akizungumza jinsi wanavyoweza kuhamasisha watu kwenye matumizi mazuri yaardhi pamoja na kutatua migogoro ya ardhi kwenye mkutano uliofanyika kwneye ukumbi wa Hotel ya Wanyama jijini Dar es Salaam.
Bwana Alain Essimi  Biloa  akitoa mada juu ya matumizi mazuri ya ardhi kwenye jamii hasa kwa wananchi waishio vijijini
Baadhi ya wadau wakichangia mada kwenye kongamano lililofanyika leo katika Hotel ya Wanyama jijini Dar es Salaam leo
Baadhi ya wadau wakiwa kwenye mkutano wa uzinduzi wa mpango mkakati wa ardhi unaoratibiwa na Jumuiko la Maliasili Tanzania( TNRF).
Meneja Program wa Jumuiko la Maliasili Tanzania( TNRF), Zakaria Faustine akizungumza na waandishi wa habari wakati wa ufunguzi wa uzinduzi wa mpango mkakati wa ardhi hapa nchini Tanzania ambao utajumuisha mradi wa majaribio katika mikoa mbalimbali 
Afisa Program za Ardhi Jumuiko la Maliasili Tanzania( TNRF),Godfrey Massay akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mkakati waliojiwekea kama Jumuiko la Maliasili Tanzania(TNRF) ili kufikia malengo  waliyojiwekea.
Kamishna wa Ardhi kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mary Makondo akizungumza na waandishi wa habari leo baada ya kufanya uzinduzi wa mpango mkakati wa ardhi utakaoleta tija kwa wananchi hasa vijijini.
Picha ya Pamoja

EAST AFRICAN NGWASUMA ORINGINAL BAND WAWAPAGAWISHA WAKATI WA MKOANI KILIMANJARO

Kiongozi wa band ya  East African Ngwasuma Original Band Kingombe Blaise  wa pili kulia akiwa anafanya mambo katika ukumbi wa Filomena Bar uliopo Boma Ngo'mbe  mkoani Kilimanjaro  wakati wa onyesho lao walilofanya mwishoni mwa wiki hii
 waimbaji na wanenguaji wa bendi ya East African Ngwasuma Original Band wakiwa wanawapagawisha wakazi wa Bomang'ombe na mitaa yake

 wanenguaji wa band ya  East African Ngwasuma Original Band wakiwa wanaonyesha viuno ikiwa  wanacheza staili yao mpya ya Kampa Kampa tena




 Rappa anaejulikana kwa jina la Papii katalogi akifanya yake ndani ya ukumbi wa Filomena Bar mkoani kilimanjaro
Habari picha na Woinde Shizza,Kilimanjaro

Bendi mpya iliongia mjini kwa kasi inayoongozwa na msanii maarufu Kingombe Blaise imewapagawisha wakati wa mji wa BomaNg'ombe na vitongoji vyake mara baada ya kutoa burudani kali ambayo iliacha historia

Wakiongea na blog hii baadhi ya washabiki wa mziki wa dance walisema kuwa wamefuarahi sana kupewa burudani na bendi hiyo , kwani walikuwa walikuwa na kiu ya mda mrefu kupata burudani kama hii

Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Pendo Petro alisema kuwa bendi hii iko vizuri na imewapa burudani nzuri hivyo wanaiombea iendelee kudumu ili wao kama wananchi wa mkoa wa kilimanjaro waweze kuendelea kupata burudani 

Akiongelea onyesho hilo kiongozi wa bendi hiyo  Kingombe Blaise alisema kuwa wao wamejipanga kuwapa burudani ya kutosha wakazi wa mkoa wa Arusha ,moshi naTanzania kwa ujumla 

"sisi tumejipanga kuwapa burudani wapenzi wa mziki wa dance na kwa sasa tunafanya hizi show ila tunampango wa kuzindua Albamu yetu hivi karibuni na muda ukifika atutaacha kuwaaambia wapenzi wetu wa muziki huu ili nao waweze kutusapoti na tunawaaidi tutawapa burudani ya kweli ambayo kila mmoja ambaye anajua mziki wa dance  ataifaurahia"alisema Kingblez

Aidha alisema kuwa  pamoja kunaushindani mkubwa katika muziki huuu wao hawatetereki maana wanaamini kabisa amna bendi ambayo inawafikia kwa kutoa burudani hivyo wapenzi wa mziki wa dance waendelee kusubiri na waendelee kuwapa ushirikiano ili watimize malengo yao ya kuwapa burudani .


Airtel washirikiana na UCSAF kufikisha mawalisiano vijiji 49 Dodoma

Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Jabir Shekimweri  akizugumza na Wakazi wa kijiji cha Mbori, Kata ya Matomondo Wilayani Mpwapwa wakati wa uzinduzi wa Mnara wa Matomondo. Aidha Airtel pamoja na USCAF ilizindua minara minne wilayani hapo na kuwawezesha wakazi katika vijjiji 49 kupata huduma za mawasiliano ya uhakika.
Meneja wa Kampuni ya Simu ya Airtel, Mkoa wa Dodoma Paschal Bikomagu akizugumza na Wakazi wa kijiji cha Mbori,  Kata ya Matomondo Wilayani Mpwapwa wakati wa uzinduzi wa Mnara wa Matomondo. Aidha Airtel pamoja na USCAF ilizindua minara minne wilayani hapo na kuwawezesha wakazi katika vijjiji 49 kupata huduma za mawasiliano ya uhakika.
Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa, Jabir Shekimweri akisalimiana na mchezaji wa timu ya Manchester United ya Mbori Wilayani Mpwapwa, Juma Athmani katika mchezo wa fainali iliochezwa juzi katika uwanja wa Ikulu kata ya Matomondo Wilayani Mpwapwa. Mchezo huo ulikuwa madhumuni kwa ajili ya uzinduzi wa mnara wa simu wa Matomondo uliojengwa na Kampuni ya simu ya mkononi ya Airtel kwa kushirikiana na USCAF ili kufikisha huduma mawasiliano kwa wananchi waishio maeneo ya pembezoni mwa nchi. Manchester ilishinda kwa mabao 4-3 dhidi ya Liverpool.
Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Jabir Shekimweri akisalimiana na wachezaji wa timu ya Liverpool ya Mbori Wilayani Mpwapwa katika mchezo wa fainali uliochezwa juzi katika uwanja wa Ikulu kata ya Matomondo Wilayani Mpwapwa. mchezo huo ulikuwa na madhumuni kwa ajili ya uzinduzi wa Mnara wa simu wa Matomondo,uliojengwa Kampuni ya simu ya mkononi ya Airtel kwa kushirikiana na USCAF ili kufikisha huduma mawasiliano kwa wananchi waishio maeneo ya pembezoni mwa nchi. Manchester ilishinda kwa mabao 4-3 dhidi ya Liverpool.


Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel katika mpango wake wa kufikisha huduma za mawasiliano kwenye maeneo ya pembezoni imeshirikiana na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF) kwa kujenga na kukamilisha miundombinu ya mawasiliano katika kata 10 zilizoko katika maeneo ya vijijini ili kutoa huduma bora ya mawasiliano.

Katika kufanikisha mkakati huo, Airtel na UCSAF leo imefanya uzinduzi wa kwanza wa minara minne iliyoko katika kata za Matomondo, Mbuga and Ipera wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma ambapo uzinduzi huo utawawezesha wakazi zaidi ya  38,000 katika vijiji 49 kuunganishwa na huduma za mawasiliano toka Airtel na kufurahia huduma na bidhaa mbalimbali ikiwemo huduma za intaneti, kupiga simu pamoja na huduma ya Airtel money ili kutatua changamoto zao

Akiongea wakati wa uzinduzi wa huduma za mawasiliano katika kata ya Matomondo Dodoma,  Meneja wa mauzo wa Airtel Dodoma, Bwn Pascal Bikomagu alisema” Airtel imejipanga katika kuboresha na kupanua upatikanaji wa huduma za mawasilino  ili kuchochea kukua kwa shughuli za kijamii na kiuchumi katika maeneo yaliyo na changamoto hususani vijijini

“Kufatia uzinduzi huu leo tunawashauri wakazi wa kata ya Matomondo na vijiji vya jirani kutumia huduma za Airtel Money katika kufanya miamala ya kifedha. Huduma hii ya Airtel Money itawawezesha kutuma na kupokea pesa, kulipia ankra mbalimbali kwa urahisi na gharama nafuu, na pia kutumiaka kama mfumo rasmi wa huduma za  kifedha kwani upatikanaji wa huduma zingine za kibenki katika maeneo hayo bado ni changamoto.” Aliongeza Bikomagu

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa, Mh. Jabir Shekimweli Alisema “ mawasiliano ya simu ni nyenzo muhimu katika kukuza uchumi wa jamii na nchi kwa ujumla, nachukua fursa hii kuwahimiza wakazi wa kata za Ipera,Matomondo na Mbuga kutumia mawasiliano hayo katika kuboresha shughuli zao za kilimo na biashara ili kuinua kipato.

Naye Mkuu wa Huduma za Ununuzi na Ugavi UCSAF, John Munkondya alisema  “Tunawapongeza Airtel kwakumaliza ujenzi wa minara hii yakutoa mawasiliano bora, leo hii tumeanza kuzindua huduma za mawasilino katika mkoa wa Dodoma. ni matumaini yetu tutaendelea kushirikiana na kuboresha huduma hizi za mawasiliano ili kuwafika watanzania wengi zaidi.

Airtel ilisaini makubaliano na Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote UCSAF kwa lengo la kufikisha mawasilino katika maeneo ya pembezoni mwa nchi. Kupitia mpango huu kata 28 nchini zimeweza kufikiwa na hivyo kuongeza idadi ya minara ya mawasiliano ya Airtel kufikia 2,210 ndani ya miji zaidi 128 na hivyo kuwafikishia huduma za mawasiliano wakazi zaidi ya  asilimia 85 nchini.