Tuesday, February 28, 2017

 Muonekano wa baadhi ya Nyumba zinazojengwa na Wakala wa Majengo Nchini (TBA) Bunju, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam zikiwa katika hatua za mwisho za ujenzi wake.
 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Nchini (TBA), Arch. Elius Mwakalinga, akifafanua hatua iliyofikiwa kwenye ujenzi wa nyumba kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Eng. Edwin Ngonyani, alipokagua maendeleo ya ujenzi wa nyumba hizo jijini Dar es Salaam.
 Muonekano wa moja ya mtungi wa kutengenezea gesi ukaa (Biogas), inayoendelea kujengwa katika Nyumba zinazojengwa na Wakala wa Majengo Nchini (TBA), eneo  la bunju jijini Dar es Salaam. Gesi hiyo itatumika kutoa huduma kwa wakazi wa eneo hilo.
 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Nchini (TBA), Arch. Elius Mwakalinga (wa tatu kulia), akimuonyesha  Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Eng. Edwin Ngonyani, hatua iliyofikiwa kwenye ujenzi wa hosteli za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam zinazojengwa na Wakala huo.
 Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Eng. Edwin Ngonyani wa pili kulia), akitoa maelekezo kwa Uongozi wa Wakala wa Majengo Nchini (TBA), alipokagua maendeleo ya ujenzi wa hosteli za wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar  es Salaam. Kulia ni Meneja Kikosi cha Ujenzi cha TBA, Arch. Hamphrey Killo.
Muonekano wa moja ya jengo la hosteli ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambalo limekamilika na majengo hayo yataanza kutumika wiki ijayo kufuatia ujenzi wake kukamilika.

No comments: