Tuesday, March 31, 2015

MKUU WA WILAYA YA KINONDONI AZINDUA MPANGO WA KUWAINUA VIJANA WENYE VIPAJI VYA SANAA UJULIKANAO KINONDONI TALENT SEARCH

 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda (katikati), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi, wakati akizindua mpango wa kuwainua vijana wenye vipaji vya sanaa mbalimbali ujulikanao kama Kinondoni Talent Search. Kulia ni Mwanamuziki, Peter Msechu na Emanuel Mathias ambaye ni mchekeshaji maarufu 'MC Pilipili ambao watasaidia kuratibu jinsi ya kuwatambua vijana hao katika wilaya hiyo.
DC Makonda akiwa amekaa na wanakamati watakaoshughulikia  mpango huo. Kutoka kulia ni mwanamuziki Peter Msechu, Mchekeshaji maarufu, Emanuel Mathias 'MC Pili pili', Ofisa Uhusiano wa Manispaa ya Kinondoni, Sebastian Mhowera na Ofisa Utamaduni wa Wilaya hiyo, Jumanne Mrimi.
 Mwanamuziki,  Peter Msechu (kulia), akizungumza katika mkutano huo. Kushoto ni DC Makonda.
 Mchekeshaji maarufu, Emanuel Mathias 'MC Pilipili' akizungumza kwenye mkutano huo.
Wanamuziki wakichukua taarifa hiyo.

Dotto Mwaibale

MKUU wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda ameandaa mashindano maalum ya wenye vipaji kupata nafasi ya kutoka kisanii liiitwalo kama
 'Kinondoni Talent Search'.

Akizugumza na waandishi wa habari ofisini kwake Dar es Salaam leo asubuhi, Makonda alisema lengo kubwa la kuinua vipaji kwa vijana na kuwapatia fursa za kimaendeleo kupitia fani zao.
 
Makonda alisema kuwa 'Kinondoni Talent Search' ni mpango wenye lengo kuu la  kuwatambua vijana waishio kwenye wilaya ya Kinondoni wenye vipaji vya kuimba, kucheza na kuchekesha ambao wengi wao wapo katika mazingira magumu kiuchumi.

Alisema mchakato huo unalenga kuwatengenezea nafasi za mafanikio vijana wenye vipaji, kuwapatia mafunzo na kuwaunganisha na wadau muhimu waliopo katika sekta zao, lakini kubwa zaidi ikiwa ni kutoa hamasa kwa vijana wote wa kinondoni.

Makonda alisema mashindano hayo yatawafanya vijana kuepukana na mambo yanayoweza kuharibu malengo yao ya baadae mfano mzuri  ni matumizi ya dawa za kulevya,ngono zembe na vitendo vya uporaji.

"Ukimiliki kipaji unakuwa unamiliki ajira,ni  kujua tu namna ya kukitumia ili kikufae na kukufikisha  utakapo na ndio maana kauli mbiu
ya mpango huu ni kipaji chako ajira yako," alisema Makonda.

Mashindano hayo yatakayosimamiwa na Manispaa ya Wilaya ya Kinondoni yamezinduliwa rasmi jana, Mkuu huyo waWilaya akitangaza kamati maalumu itakayosimamia zoezi hilo, yenye wajumbe watano kutoka ofisi yake pamoja na baadhi ya wasanii.

Aliwataja wajumbe wa kamati hiyo kuwa ni Jumanne Mrimi ambaye ni Ofisa Utamaduni wa wilaya hiyo, Sebastian Mhowera  Ofisa Uhusiano wa Manispaa ya Kinondoni huku  ikiwahusisha wasanii wa muziki Peter Msechu ,mwanamitindo, Jokate Mwengelo na mchekeshaji maarufu Mc-pilipili.

Makonda alisema Kinondoni Talent Search itachukua takribani mwezi mmoja na nusu, huku ukijumuisha shughuli za utafutaji vipaji ambapo utaanzia ngazi ya kata 34 ambapo kutakuwa na mafunzo kwa washiriki, kuwapa nafasi washiriki kukutana na wadau mbalimbali wanaofanya kazi kama zao.

Aliongeza kuwa mwisho wa kufunga zoezi hilo kutafanyika tukio kubwa lenye hadhi ya kimataifa  litakalowapa vijana wote nafasi ya kuonesha vipaji vyao mbele ya mabalozi toka nchi mbalimbali kama sehemu ya mkakati wa kuwasogeza na wasanii kimataifa.
(Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com)

ASKOFU GWAJIMA APEWA DHAMANA LEO MCHANA

Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima akiwa kwenye baiskeli maalum ya wagonjwa Hospitali ya TMJ Dar es Salam leo mchana, wakati akielekea Kituo cha Polisi cha Oyterbay kupewa dhamana.
Hapa Askofu Gwajima akiingia kwenye gari huku akiwa na maumivu makali wakati akielekea kwenye kituo hicho kupewa dhamana
Wanahabari wakitoka kituo cha polisi Oysterbay kufuatilia 
habari hiyo.
Wachungaji wakibadilishana mawazo wakati wakimsubiri Askofu Gwajima apewe dhamana
Waumini wa kanisa hilo wakijiandaa kumpokea Askofu wao 
baada ya kupatiwa dhamana
waumini hao wakiwa kituoni hapo.
Waumini wa Kanisa la Ufufuo na Uzima wakiwa wamelizonga gari lililombena Askofu Mkuu wa Kanisa hilo, Josephat Gwajima, huku wakishangilia kwa kusema yesu yesu baada ya kupewa dhamana  katika Kituo cha Polisi Oysterbay Dar es Salaam leo mchana.
Waumini hao wakilipungia mkono gari lililomchukua 
Askofu Gwajima. 
(Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com)

Waziri wa Fedha afanya ziara kwenye bandari kavu ya kampuni ya THR jijini Dar leo

Waziri wa Fedha Mhe. Saada Mkuya (katikati) akiwasili katika Bandari ya Nchi Kavu ya TRH katika ziara ya wizara hiyo leo jijini Dar es Salaam ambapo kontena mbili zilikamtwa ambapo moja ilikutwa na bidhaa za tv na nyingine biskuti huku nyingine mbili hazikuweza kupatikana mahali zilipofichwa.
Kamishna Msaidizi wa Forodha wa Mamalaka ya Mapato Tanzania (TRA),Bw. Tiagi Kabisi kushoto akipata maelekezo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Tanzania Road Haulage (TRH) Bw. Ali Lilani katika ziara ilifanywa na Waziri wa Fedha leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha Mhe. Saada Mkuya (kushoto) akisikiliza maelekezo kutoka kwa Kamishna Msaidizi wa Forodha wa Mamalaka ya Mapato Tanzania (TRA),Bw. Tiagi Kabisi katika ziara ya wizara hiyo leo jijini Dar es Salaam ambapo kontena mbili zilikamtwa ambapo moja ilikutwa na bidhaa za tv na nyingine biskuti huku nyingine mbili hazikuweza kupatikana mahali zilipofichwa.
Waziri wa Fedha Mhe. Saada Mkuya (katikati) akiangalia mbidhaa za tv zilizokutwa katika mojawapo ya kontena zilizokuwepo katika Bandari ya Nchi Kavu ya TRH katika ziara ya wizara hiyo leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha Mhe. Saada Mkuya (katikati) akijadiliana jambo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha (kulia) Mhe.Dkt.Servacius Likwelile na Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi wa TRA Richard Kayombo(kushoto) wakati wa ziara ya wizara hiyo katika Bandari ya nchi Kavu ya Tanzania Road Haulage(TRH) leo jijini Dar es Salaam.
Kontena mbili zenye bidhaa za Tv na Biskuti zilizokamatwa katika Bandari ya Nchi Kavu ya Tanzania Road Haulage (TRH) wakati wa ziara ya Waziri wa Fedha Mhe.Saada Mkuya leo jijini Dar es Salaam.(Picha na Lorietha Laurence-Maelezo)

Na Lorietha Laurence- Maelezo

Waziri wa Fedha Mhe.Saada Mkuya amesema kuwa serikali itawashughulikia wafanyabiashara wanaokwepa kulipa kodi kwa kuwachukulia hatua stahiki ikiwemo kunyang’anywa leseni ya biashara na kulipa faini. Aliyasema hayo leo jijini Dar es Salaam katika ziara ya kukagua bandari kavu ya kampuni ya THR ambapo ni mjumuisho wa ziara iliyoanza jana jioni kutembelea Bandari za nchi kavu.

“Tumekamata jumla ya kontena nane ambazo katika taarifa za awali zilieleza kuwa zina bidhaa za gypsum powder na gysum plasta lakini tulipozifungua tumekutana na bidhaa tofauti na kile tulichoambiwa” alisema Mhe. Mkuya Aidha aliongeza kuwa bidhaa zilizokutwa katika kontena hizo ni pamoja na spea za pikipiki,vitenge ,Tv na biskuti ambazo zilitakiwa kulipia ushuru tofauti na zile ambazo ziliandikwa katika taarifa ya kupokea mzigo.

Mhe. Mkuya alisema kutokana na udanganyifu huo takribani shilingi milioni mia tatu zimepotea na hiyo ni mojawapo ya vikwazo vinavyokwamisha shughuli za maendeleo kusonga mbele kwa ukosefu wa fedha.

Naye Kamishana Msaidizi wa Forodha wa Mamlaka ya Mapato Tanzania Bw. Tiagi Kabisi ameeleza kuwa wamekuwa wakikutana na changamoto mbalimbali wakati wa utendaji wao wa kazi ikiwemo udanganyifu unaofanywa na wafanyabiashara ikiwemo hili la kutokulipwa kodi.

“Hii ni mojawapo ya changamoto ambazo tunakutana nazo katika kazi zetu ambapo wafanyabiashara wamekuwa wakitumia mbinu mbalimbali za udanyifu ili kukwepa kulipa kodi” alisema Bw.Kabisi Ziara hiyo ni mojawapo ya mikakati ya Wizara ya Fedha katika kuhakikisha kuwa wafanyabiashara wanawajibika katika suala la ulipaji wa kodi nia ni kuhakikisha nchi inaweza kujitegemea kupitia vyanzo mbalimbali vya uchumi ili kukuza na kuendeleza ustawi wa nchi.

Ujumbe kutoka Chuo cha Kijeshi cha Nigeria watembelea Wizara ya Mambo ya Nje

Mwakilishi wa Katibu Mkuu na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw.Elibariki Maleko(katikati) akizungumza kuukaribisha Ujumbe kutoka Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi cha nchini Nigeria (hawapo pichani) ulipokutana na Watendaji wa Wizara kwa ajili ya kujifunza masuala mbalimbali yanayohusu Sera ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Kikanda na Kimataifa. Ujumbe huo unaongozwa na Brigedia Generali Jimoh (wa pili kushoto) na upo nchini kwa ziara ya mafunzo. Wengine katika picha ni Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango, Bw.James Lugaganya ( kushoto), Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Bw. Innocent Shiyo (wa pili kulia) na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Bi.Maulidah Hassan.

Mwenyeji wa Ujumbe huo kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania, Brigedia Jenerali Mwemnjudi (mwenye nguo nyeupe) pamoja na Mwambata wa Jeshi katika Ubalozi wa Nigeria hapa nchini Brigedia Jenerali Erick Angaye wakimsikiliza Bw. Maleko (hayupo pichani)
Sehemu ya Maafisa wa Jeshi kutoka Nigeria wakifuatilia kwa makini maelezo kutoka kwa Bw. Maleko
Maofisa na Wanachuo wa Chuo cha Kijeshi cha Nigeria wakati wa mkutano huo
Mmoja wa wanachuo akiuliza swaliwakati wa mkutano huo
Kiongozi wa msafara wa Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi cha nchini Nigeria, Brigedia Jenerali Jimoh akimkabidhi zawadi ya nembo ya chuo hicho Bw. Maleko
Picha ya pamoja.
Picha na Reuben Mchome

HUMAN DEVELOPMENT INNOVATION FUND (HDIF) LAUNCHES INNOVATION WEEK IN TANZANIA

Faraja Nyalandu - Executive Director of Shule Direct speaking on entrepreneurship and its' challenges in Tanzania and promoting self employment during the Innovation week organised by Human Development innovation Fund (HDIF) in Dar es Salaam earlier this week. From left Benedict Tesha - Founder of Jamaa Technology, Nisha Ligon - CEO of Ubongo Limited, Taha Jiwaji - CEO of Bongo Live and Co Founder of KINU.
Benedict Tesha - Founder of Jamaa Technology speaking on entrepreneurship and its' challenges in Tanzania and promoting self employment during the Innovation week organised by Human Development innovation Fund (HDIF) in Dar es Salaam earlier this week. From left Nisha Ligon - CEO of Ubongo Limited, Taha Jiwaji - CEO of Bongo Live and Co Founder of KINU and Faraja Nyalandu, Executive Director of Shule Direct.
Dr Jacqueline Thomas, senior Scientist at Ifakara Health Institute (IHI) speaks about the Kigamboni sludge treatment plant during the Innovation Week that was organised by Human Development Innovation Fund earlier this week in Dar es Salaam.
Mr. David McGinty, Team Leader of Human Development Innovation Fund ( HDIF) speaks during the innovation week that was held at Nafasi Art Space in Dar es Salaam.
Andrew Mahiga, Managing Director at Maanisha! speaks on Innovation during the Innovation that was held at Nafasi Art Space earlier this week in Dar es Salaam. To the left Gadi Ramadhani ( An artist), Paul Ndunguru ( An artist at Alama) and to the far right is David McGinty, Team Leader at Human Development Innovation Fund ( HDIF)
David McGinty, Team Leader at Human Development Innovation Fund (HDIF) creating an object with match sticks and a match box that was an exercise during the innovation week held at the Nafasi Art Space earlier this week.
---
The Human Development Innovation Fund (HDIF) convenes entrepreneurs, researchers, academics, creatives & development professionals to collaborate and create social impact through innovation.
Last week, HDIFcollaborated with BUNI Innovation Hub, KINU Innovation Hub, DFID, World Bank, Commission for Science and Technology (COSTECH), Deloitte and Nafasi Art Space to curate a series of interactive events, exploring innovation in research, development, entrepreneurship, technology and the arts. Individuals and organizations shared their insights on innovation respective to their field of expertise for audiences and collaborators from across sectors. This inaugural Innovation Week was designed to catalyze on the innovation process in Tanzania and provide inspiration and connections to individuals and organizations on innovation.
HDIF challenges Tanzanians to implement and scale innovative ideas for more positive sustainable development impact and remove barriers to reach innovation.Over 500 Tanzanians participated in the week-long events that offered interactive seminars, workshops and trainings. David McGinty, HDIF Team Leader commented, ‘We wanted to inspire the current and future leaders in Tanzania to take risks on new ideas, collaborate across sectors, and transform Tanzania through the scaling of innovation.’ He explained ‘Strengthening Tanzania in innovation is a way to create growth, raise the global profile of Tanzania, and tackleTanzania’s social and economic challenges.’
Dr. Donath Olomi, Partner of Tanzania Renewable Energy Business Hub was a panelist during the week. He said ‘I have been genuinely surprised at the attendance throughout this innovation week. It is clear that Tanzanians believe they have potential innovative ideas and are looking for partners, be it in the private or public sector, that can nurture and support their ideas as they develop.’ He added ‘Events like these will help stimulate cross-sector collaborationsin Tanzania to innovate and find profitable ways of addressing key issues in Tanzania.’
Tanzania ranks 123 out of 143 countries according to the Global Innovation Index 2014. Despite its many endowments, Tanzania remains a poor country by both local and international standards. A mapping study conducted by Sosthenes Sambua, Executive Director of Tanzania Entrepreneurship and Competiveness Center (TECC)indicated that the lack of competitiveness in Tanzania is attributed to three factors. The first is lack of innovation policy comprehensive enough to catalyze innovation system in the country. The second factor is lack of linkages between industry, academia and government. The third factor is inadequate funding available to commercialize innovative ideas. Mr. Sambuasays‘Platforms like the Innovation Week that bring together policy makers, private sector actors &entrepreneurs from across all sectors, creates dialogue that will help lead to new orimproved policies that will catalyze the innovation system in Tanzania.’
HDIF was launched to fund innovative and sustainable solutions to create social impact in education, health and WASH (water, sanitation and hygiene) across Tanzania. The second funding round is scheduled for mid-2015. Guidelines and important dates will be posted on the HDIF website www.hdif-tz.org.

EAC PARLIAMENT TO START FORUM ON CLIMATE CHANGE

East African Community, Arusha, Tanzania, March 31, 2015:  The East African Legislative Assembly (EALA) has agreed to form a regional Parliamentary Forum on Climate Change.

The proposal was made during a policy dialogue on Climate Change and Gender for members of EALA to identify the role of parliamentarians in implementation of gender sensitive climate change policies.

The dialogue held on 27th and 28th March, 2015 in Bujumbura, Burundi, was organized by the EAC Secretariat in partnership with the EALA Women Forum. It was also attended by the EALA Committee on Agriculture, Tourism and Natural Resources and the General Purpose Committee.

“We need to establish a parliamentary forum on Climate Change for EALA so that it can feed into the global parliamentary forum and also provide leadership in the regional framework on climate change,” said Hon. Abubakar Zein. The resolution on this proposal will be passed during the next EALA sitting in May.

The impact of Climate Change is most severe for the world’s poor and marginalized communities who often live in stressed environments and have fewer means for coping.  Women are especially vulnerable because of their limited access, control and ownership over resources, unequal participation in decision and policy-making, lower incomes and levels of formal education and high workloads.

As such climate change impacts men and women in different ways and interventions aimed at addressing climate change impacts must include a gender perspective.

Hon. Valerie Nyirahabineza, the leader, EALA Women Forum, stressed that Africa is most vulnerable to climate change and noted that the region’s communities and governments are sometimes constrained to handle challenges of climate change. “Women play a critical role in food and nutrition security and are also responsible for growing, buying, selling, and cooking the food.

Majority of food produced in developing countries is by women, yet only 2% of land is owned by women,” she said. She added that there was need for the legislators to address the underlying causes of gender inequality such as unequal land rights and land tenure through legislative reforms.

Hon. Dora Byamukama noted, “Unless women feel secure as users and owners of land, there will always be a problem of climate change.”

Hon. Kessy Nderakindo said that many people are acquiring things that they don’t need. “Human beings are not respecting the earth and we need to ask, what are the little things we can do to stop climate change?”Hon. Zein also said that the EAC Climate Change Fund be capitalized

“It is not acceptable to have an EAC Climate Change Fund that we have not put money into, we are only depending on development partners to do something.”  He added that it is critical to have seed money from Partner States to support climate change related concerns.

The parliamentarians agreed that   climate change be considered in the EAC Partner States budgeting process, and pledged to make individual contributions to the Fund. The Climate Change Fund was established in 2011.

Hon. Leonce Ndarubagiye decried the overdependence on Development Partners and called for home grown solutions to climate change.The EAC Secretariat, in partnership with the East African Development Bank, is in the process of applying to be a Regional Implementing Entity to the Climate Change Adaptation Fund and Green Climate Fund.         

The Members agreed to revive their pledge where each EALA Chapter is to plant 50,000 trees in their Partner States by 2017. The MPs also observed that East Africans need to revive their traditional knowledge that was sensitive to nature. “We need to look into traditional knowledge and revive what worked before that has been abandoned,” said Hon. Mike Sebalu.

They called on Partner States to promote environmental friendly practices such as the use of renewable energy like biogas and solar power, water harvesting, and irrigation. Hon. Mumbi Ng’aru urged national governments to reduce the cost of materials used in the construction of biogas units.

The Members urged for the finalization of the draft EAC Disaster Risk Reduction Bill noting its urgency and the need for administrative and coordination structures for timely response to climate change induced disasters in the region that are increasing in intensity and frequency.

The EALA members conveyed their sympathies to the government and the people of the United Republic of Tanzania for the climate related hailstorm in Kahama and flooding in Dar es Salaam in March which claimed lives and left many people displaced.

MAHAFALI YA PILI YA PROGRAM YA HAKI ZA BINADAMU UKANDA WA AFRIKA MASHARIKI YAFANYIKA DAR

 Rais wa Foundation For Civil Society, Dk. Stigmata Tenga akitoa hotuba yake wakati wa mahafali ya pili ya Program ya Haki za Binadamu Afrika Mashariki yaliyofanyika katika Chuo cha Bagamoyo (UB) jijini Dar es Salaam.
Rais wa Foundation For Civil Society, Dk. Stigmata Tenga (kulia) akimkabidhi cheti muhitimu wa kozi ya haki za binadamu Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati katika  Chuo Kikuu cha Bagamoyo, Comfort Maembe, kozi hiyo iliandaliwa na Chuo Kikuu cha Bagamoyo kwa kushirikiana na Akiba Uhaki Foundation ya Kenya na kufanyika jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki. (Picha na Francis Dande)
Rais wa Foundation For Civil Society, Dk. Stigmata Tenga (kulia) akimkabidhi cheti muhitimu wa kozi ya haki za binadamu katika  kwa Chuo Kikuu cha Bagamoyo, Sophie Ogutu kutoka Kenya  jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki. Kozi hiyo iliandaliwa na Chuo Kikuu cha Bagamoyo kwa kushirikiana na Akiba Uhaki Foundation ya Kenya.