Sunday, January 6, 2019

Idadi ya abiria bado kubwa Ubungo.

*Wengi ni wanafuzi katika mikoa ya Tanga,Morogoro na Dodoma

Na Chalila Kibuda , Globu ya Jamii

Idadi ya abiria katika kituo cha mabasi Ubungo imeendelea kuongezeka kwa kwa sehemu kubwa wakiwa wanafunzi.

Akizungumza na Michuzi Blog Mwenyekiti wa Chama cha Kutetea Abiria Hassan Mchanjama amesema kuwa abiria katika kituo cha Ubungo ni kubwa lakini wanasafiri kutoka na baadhi daladala kupata vibali.

Amesema abiria wengi ni mikoa ya Tanga, Dodoma pamoja na Morogoro ikiwa sehemu kubwa abiria hao ni wanafunzi.

Mchanjama amesema abiria wanavyofika katika kituo cha mabasi Ubungo wakate tiketi ndani ya Kutuo.Mmoja wa abiria Hamis Seif amesema kuwa kuna changamoto ya Usafiri katika msimu wa siku kuu na kuomba yaongezwe mabasi hata daladala katika mikoa ya jirani na Dar es Salaam.

Aidha amesema kuwa suala la ukaguzi katika kituo cha mabasi Ubungo ni mzuri na kutaka na mikoa mingine wafanye hivyo kwa ajili ya usalama wa abiria.
 Askari wa usalama barabarani Grant Pawa akiandika makosa ya basi wakati wa ukaguzi wa mabasi katika kituo cha mabasi Ubungo jijini Dar es Salaam.
 Maafisa Polisi wakiwa katika ukaguzi katika kituo cha mabasi Ubungo jijini Dar es Salaam 
 Moja ya tiketi aliyekatiwa msafiri ambaye kampuni ya basi hilo halipo katika kituo cha Ubungo abiria anadai kuwa aliyemkatia na kutia saini ni Rama Tall.
 Abiria wakisubiri Usafiri katika kituo cha mabasi Ubungo jijini Dar es Salaam.
 Abiria wakiwa wamefurika katika katika Kituo cha Mabasi Ubungo jijini Dar es Salaam.
 Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani katika kituo cha mabasi Ubungo wakiwa na fundi wakufanya ukaguzi wa basi katika kituo cha mabasi Ubungo jijini Dar es Salaam.
 Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani Nuru Hussein akifanya Ukaguzi katika basi kuangalia uimara wa Gurudumu pamoja na Brenk katika kituo mabasi Ubungo jijini Dar es Salaam.
Askari wa kituo cha mabasi Ubungo Nuru Hussein akimpa maelezo Dereva  wakati akifanya Ukaguzi ,jijini Dar es Salaam.

No comments: