Thursday, December 1, 2016

Mkutano wa ushirikiano kati ya Afrika na Jamhuri ya Korea kufanyika Addis Ababa

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mindi Kasiga akizungumza kwenye mkutano na Waandishi wa Habari. Katika mkutano huo Bi. Kasiga aliwaeleza Waandishi wa Habari kuhusu Mkutano wa Nne wa Mawaziri wa nchi za Afrika na Korea utakaofanyika Mjini Addis Ababa, Ethiopia tarehe 06 na 07 Desemba, 2016. Mkutano huo utajadili masuala mbalimbali ya ushirikiano baina ya Afrika na Korea pamoja na maeneo mapya ya mashirikiano. 
Afisa Mambo ya Nje, Bi. Bertha Makilagi akifuatilia mkutano kati ya Bi. Kasiga na Waandishi wa Habari. Wengine ni Waandishi wa Habari waliohudhuria mkutano huo. 
Sehemu ya Waandishi wa Habari wakisikiliza na kunukuu kwa makini mkutano uliokua ukiendelea 
Mkutano ukiendelea.
-->
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushrikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb) anatarajiwa kuongoza ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano wa Mawaziri wa Afrika na Korea unaotarajiwa kufanyika nchini Ethiopia tarehe 06 na 07 Desemba, 2016 mjini Addis Ababa, Ethiopia.


Mkutano huu ambao umeandaliwa na Serikali ya Korea kwa kushirikiana na Umoja wa Afrika una lenga kukuza ushirikiano pamoja na kuandaa maeneo mapya ya ushirikiano baina ya Korea na mataifa ya Afrika katika miaka mitatu ijayo.


Tanzania ni moja ya nchi nne (4) za Afrika ambazo Korea imezichagua kuanzisha mahusiano ya kimkakati “strategic partnership” yatakayozifanya nchi hizo kupewa kipaumbele katika kupokea misaada na mikopo nafuu kutoka Korea katika kipindi cha miaka mitano ijayo kati ya 2016 hadi 2020.


Katika kipindi hicho Tanzania itapokea kiasi cha dola za Kimarekani milioni 300 ikiwa ni asilimia 17.1 ya msaada utakaotolewa Barani Afrika, hivyo kuifanya Tanzania kuwa nchi inayoongoza Barani humo kupata msaada wa Jamhuri ya Korea.


Pamoja na ushiriki kwenye Mkutano huo, imependekezwa ufanyike mkutano baina ya Tanzania na Serikali ya Korea kuzungumzia masuala ya ushirikiano baina ya nchi zetu mbili. Aidha, ushiriki wa Tanzania kwenye mkutano wa Afrika na Korea ni fursa muhimu ya kukuza mahusiano baina ya nchi zetu mbili hususan katika Nyanja ya uchumi. Serikali ya Korea ilitoa ahadi ya kuongeza uwekezaji Barani Afrika hususan katikasekta za nishati, miundombinu na viwanda.


Itakumbukwa kuwa, tayari Jamhuri ya Korea inashirikiana na Tanzania katika miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo Mradi wa kuendeleza kilimo cha Mwani Zanzibar wenye thamani ya Dola za Kimarekani milioni 3.6 na Awamu ya Pili ya Mradi wa kuboresha Uchunguzi wa Afya ya Uzazi Jijini Dar es Salaam wenye thamani ya Dola za Kimarekani milioni nne (4).


Miradi mingine ambayo Jamhuri ya Korea inashirikiana na Tanzania ni ujenzi wa Daraja la Selander Jijini Dar es Salaam, Mradi wa Daraja la Kikwete kwenye Mto Malagarasi Mkoani Kigoma na Ujenzi wa Hospitali ya Kimataifa iliyopo eneo la Mloganzila Jijini Dar es Salaam.


 Imetolewa na:

Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Dar es Salaam, 01Desemba, 2016.

TBL yazindua muonekano mpya wa Chibuku Super

 Wafanyakazi wa kampuni ya bia ya TBL wakionyesha kwa waandishi wa habari chupa mpya ya Chibuku Super ya Ml 500 wakati wa hfla fupi ya uzinduzi  iliyofanyika jijini Mwanza leo.
 Wafanyakazi wa kampuni ya bia ya TBL wakionja Chibuku super ya Ml 500 wakati wa hfla fupi ya uzinduzi  iliyofanyika jijini Mwanza leo.
Meneja Masoko wa TBL Group Oscar Shelukindo,akizungumza na waandisi wa kuhusiana na  muonekano mpya wa chupa ya Chibuku Super ya Ml 500 wakati wa hafla fupi iliyofanyika jijini Mwanza leo. kulia ni Meneja Kiwanda cha Chibuku Super Mwanza Herbert Ilembo.

Mwanza Desemba 1,2016:Kampuni ya TBL Group, leo imezindua Chibuku Super kwenye chupa ya bia ya ml 500, huku ikitoa wito kwa watanzania kutumia vinywaji vinavyozalishwa hapa nchini ili kujenga uchumi wa taifa kwa ujumla.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo uliofanyika katika ukumbi wa kiwanda kilichopo eneo la Pasiansi Mwanza , Meneja Masoko wa TBL Group, Bw. Oscar Shelukindo alisema uzinduzi wa bia hiyo ya Chibuku Super” kwenye chupa ya glasi inayorudishwa (Returnable) unatarajiwa kuleta mapinduzi makubwa katika soko la Bia hapa nchini.

“Leo ni siku ya furaha kubwa sana kwetu TBL na kwa watumiaji wote wa Bia yetu hi ya asili , kwani tumeweza kuzindua Bia hii imetengenezwa kwa utaalamu wa hali ya juu na kwa kutumia mitambo ya kisasa kabisa, hivyo kuwahakikishia wanywaji Ubora wa hali ya juu, ina ujazo wa nusu lita na itauzwa kwa bei ya shilingi 700/- tu, kwa chupa na 14,000 kwa kreti,’’ alisema.

Akiizungumzia bia hiyo Shelukindo alisema inatengenezwa kwa kutumia malighafi za hapa nyumbani, ikiwemo nafaka ya mahindi na mtama bora toka kwenye ardhi ya Tanzania na hivyo kutoa kila sababu kwa watanzania kujivunia kinywaji chenye asili ya taifa lao.

“Chibuku Super ina kilevi cha asilimia 4, kinachomfanya mtumiaji aweze kuitumia kwa muda mrefu akiwa na marafiki, lakini pia inampa lishe nzuri kutokana na virutubisho vinavyopatikana katika nafaka zinazotumika kutengeneza bia hii,’’ aliongeza

Akizungumzia juu ya usambazaji wa Bia hiyo, meneja mauzo wa TBL Bw. Fred Kazindogo alisema baada ya uzinduzi huo itaanza kupatikana Desemba 2 mwaka huu kwa wasambazaji wakubwa na katika baa mbalimbali na sehemu nyinginezo zinazouza vileo.

Alisema kwa kuanzia Bia hiyo itaanza kupatikana katika mikoa 15 ikiwemo Mwanza, Kagera, Mara, Shinyanga, Geita, Tabora, Singida, Kigoma, Simiyu, manyara , Kilimanjaro, Arusha, Katavi, Mbeya na Rukwa.

“Na kwa wauzaji wa jumla, tunatarajia watahamasika kuuza bia ya Chibuku Super kwani ina faida nzuri na inadumu kwa miezi 4 kwenye soko, muda ambao ni mrefu sana kulinganisha na products zetu nyingine,’’alisema 

Timu ya Taifa ya kuogelea yatamba kutwaa medali mashindano ya dunia

Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Anastazia Wambura akikabidhi bendera kwa nahodha wa timu ya Taifa ya Kuogelea, Hilal Hemed Hilal


Timu ya Taifa ya mchezo wa kuogelea, imetamba kufanya vyema katika mashindano ya Dunia yaliyopangwa kuanza Desemba 6 mjini Windsor, Canada.

Tanzania itawakilishwa na jumla ya wogeleaji sita ambao wamepatikana kutokana na michujo mbalimbali ikiwa pamoja na mashindano ya Taifa yaliyofanyika mwezi Machi mwaka huu kwenye bwawa la kuogelea la Hopac.

Waogeleaji hao ni Hilal Hilal ambaye ni nahodha, Adil Bharma, Denis Mhini na Joseph Sumari ambao ni wanaume ambapo kwa wanawake ni pamoja na muogeleaji namba moja nchini, Sonia Tumiotto na Catherine Mason.

Akizungumza leo, Hilal alisema kuwa wamejiandaa vizuri chini ya kocha wao, John Belela na morali ipo juu kutokana na mafanikio waliyopata hivi karibuni katika mashindano ya kanda ya tatu yaliyofanyika Kigali, Rwanda na Tanzania kushika nafasi ya kwanza.

Hilal alisema kuwa lengo lao ni kupigia taifa lao na wanaamini watafanya vyema na hasa baada ya kuwaongeza wigo wa waogeleaji.

"Tumejiandaa kufanya vizuri, kama mjuavyo kwenye mashindano ya Afrika ya kanda ya tatu Tanzania ndiyo ilikuwa bingwa, tulipata medali 99, ushindani huu tutakwenda kuuendeleza Canada," alisema Hilal.

Waogeleaji hao leo walikabidhiwa Bendera ya Taifa na Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Anastazia Wambura katika hafla fupi iliyofanyika Wizarani na kuhudhuliwa na Balozi wa Italia hapa nchini, Roberto Mengoni sambamba na mwakilishi wa kampuni ya kutengeneza vifaa vya Michezo ya Errea yenye makao makuu nchini Italia.

Akizungumza katika hafla hiyo, Naibu Waziri Wambura aliwataka waogeleaji hao kupambana huku akimuomba Balozi Roberto na kampuni ya Errea kuendelea kuisapoti Tanzania.

"Ushirikiano wenu isiishie kwa timu yetu teule ya kuogelea, tunaomba muendelee kutusapoti hata kwenye miundo mbinu kwa kujenga mabwawa ya kuogelea hapa nchini na ikiwezekana hata kufungua viwanda vya vifaa vya Michezo," alisema Naibu Waziri huku Balozi Roberto akiahidi kushirikiana nao.





BALOZI WA KOREA KUSINI AENDESHA MHADHARA CHUO CHA BANDARI

 Balozi wa Korea Kusini hapa nchini, Mhe. Song Geum-young (kushoto) akijadili jambo na Mkuu wa Chuo cha Bandari, Dk. Joseph Kakeneno wakati wa mhadhara wake na wanachuo cha Bandari hivi karibuni.
 Mkuu wa Chuo cha Bandari, Dk. Joseph Kakeneno akimkaribisha Balozi wa Korea Kusini hapa nchini, Mhe. Song Geum-young kutoa mhadhara wake kwa Wanachuo.
 Balozi wa Korea Kusini hapa nchini, Mhe. Song Geum-young akitoa mhadhara kwa wanachuo. Kulia ni Mkuu wa Chuo cha Bandari, Dk. Joseph Kakeneno.

Baadhi ya Wanachuo cha Bandari wakifuatilia mhadhara uliokuwa ukitolewa na  Balozi wa Korea Kusini.
 Baadhi ya Menejimenti ya Chuo cha Bandari ikifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Balozi wa Korea Kusini. 
Mkuu wa Chuo cha Bandari, Dk. Joseph Kakeneno akimkabidhi zawadi Balozi wa Korea Kusini hapa nchini, Mhe. Song Geum-young mara baada ya kutoa mhadhara kwa wanachuo.



WAJERUMANI WATENGENEZA FILAMU NDANI YA HIFADHI YA TAIFA YA SERENGETI.

Mkurugenzi wa Utalii wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Ibrahim Musa (katikati) akizungumza na Mratibu wa uzalishaji wa filamu wa kampuni ya Polyphon ya nchini Ujerumani,Mona Lessnick alipotembelea eneo la Kogatende jirani na  Mto Mara ambapo kulikuwa kukifanyika shughuli za uchukuaji wa picha za video kwa ajili ya Tamthiliya ya Dream Boat.kulia ni Meneja Mawasiliano wa TANAPA,Pascal Shelutete.
Mkurugenzi wa Utalii wa TANAPA,Ibrahim Musa akizungumza na Mona Lessnick katika eneo la Kogatende ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Mratibu wa uzalishaji wa Filamu wa kampui ya Polyphon Studio,Mona Lessnick (kulia) akiwa na Mpiga picha mkuu wa kampuni hiyo ,Manuel Schroeder na Jorg Gariel  wakati wakizungumza na wanahabari  (hawapo pichani) juu ya tukio la uchukuaji wa picha za video katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Eneo la Kogatende ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ambapo picha za video za sehemu ya Tamthiliya ya Dream Boat zimepigwa hapo.
Moja ya gari lililotumika katika tukio hilo likitoka eneoo la tukio kando ya Mto Mara unopita katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Uchukuaji wa picha za video kando ya Mto Mara ukiendelea.
Magari yakiwa yamebeba sehemu ya vifaa kwa ajili ya uchukuaji wa picha za Video.
Meneja Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Pascal Shelutete akiteta jambo na Mona Lessnick katika eneo la Kogatende ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Mkurugenzi wa Utalii wa TANAPA,Ibrahim Musa( katikati) akisikiliza kwa makini maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Jorg Gabriel walipoktana eneo la Kogatende katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Meneja Mawasiliano wa Tanapa,Pascal Shelutete akisaidia kubeba moja ya Kamera kubwa zilizokuwa zikitumika katika matukio ya uchukuaji wa picha katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Moja ya Kamera kubwa iliyokuwa ikichukua matukio katika upigaji picha wa Tamthiliya ya Dream Boat katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Mkurugenzi wa Utalii akiitizama Kamera ambayo ilikuwa iktumika kupiga picha za matukio mbalimbali wakati wa utengenezaji wa filamu hiyo.
Wataamu wakifunga Kamera katika ndge ndogo ya Shirika la ndege la Costal Airline kwa ajili ya upigaji wa picha za juu . 

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii ,Kanda ya Kaskazini.

SEKTA ya Utalii nchini inatarajia kupiga hatua baada ya wasanii maarufu wa filamu kutoka nchi za nje kuanza kutumia baadhi ya maeneo katika vivutio vya Utalii vilivyoko nchini kuandaa sehemu za tamthiliyaa zao.

Kampuni kubwa ya utengezaji wa filamu ya Polyphon Group  ya Humburg  nchini Ujerumani imekuwa ya kwanza kupiga picha za video za sehemu ya tamthiliya maarufu nchini Ujerumani ya Dream Boat ambayo imekuwa ikiooneshwa katika vituo mbali mbali vya televisheni kwa nchi zinazozugumza lugha ya Kijerumani.

Maeneo ambayo picha za video zimechukuliwa ni pamoja na Kogatende na Lobo ndani ya Hifadhi za Taifa za Serengeti ,huku picha nyingine zikipigwa katika Hifadhi ya taifa ya Arusha pamoja na Pori la akiba Endumeti.

“Tumefanya Sehemu moja ya Tamthiliya yetu Botswana,moja Zambia na nyingine Kenya katika muendelezo wa tamthiliya hii inayooneshwa kwa mika 30 sasa,Sehemu ya mwisho ya muendelezo wa filamu hii iliyochukuliwa Afrika ilikua mwa 2007,ni muda mrefu na tuliangalia wapi tunaweza enda,na tukafanya utafiti ,tukaja Tanzania,Tumeona hii nchi ni nzuri tukaamua kuleta filamu yetu hapa”.alisema Manuel Schroeder mpiga picha wa kampuni ya Polyphon Studio.

Mkurugenzi wa Utalii wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Ibrahim Musa amesema hatua hii ni fursa nyingine muhimu kwa Tanzania  kutangaza vivutio vya utalii kimataifa huku mratibu wa uzalishaji wa filamu wa kampuni ya Polyphon,Mona Lessnick akieleza utalii utaongezeka kupitia tamthiliya hiyo.

“Kutokana na uzoefu ,watu wametuamini sisi , tumefanya hii kazi kwa miaka 30 sasa,hivyo baada ya kurusha sehemu ya tamthiliya ilichukuliwa hapa itaongeza soko la wageni kutoka nchi zinazozungumza kijerumani,kwa sababu wanajua tunafanya utafiti,tmekwisha fka hapa mara mbili na kukutana na mtaalamu na kutuonesha maeneo ,wanajua tunachukua maeneo mazuri,hoteli nzuri,tuna taarifa  na vifaa vya kutosha,hivyo kutakuwa na matokeo makubwa katika Utalii “alisema Lessnick.

Kuhusu Maudhui ya Tamthiliya hiyo ambayo inaoneshwa kwa zaidi ya miaka 30 sasa ,Mona Lessnick amesema imebeba maudhui ya aina tatu ambayo ni Vichekesho,Mahusiano pamoja na Drama.
“Ni Burudani kwa familia,tuna hadithi tatu,katika hadithi kuu watu wanasafiri kwa meli kuizunguka nchi,wakasafiri kuja Tanzania ,kuna hadithi nzuri za mahusiano ambazo vipande vyake vimechukuliwa Tanzania “alisema Lssnick.

“Katika muongozo tuna aina tatu ya hadithi,tuna hadithi ya mapenzi,tuna hadithi ya vichekesho na drama hii tunayofanya leo ni vichekesho,tuna watu wawili ,katika muongozo wa kwanza inaonesha watu haw wamepata tatizo katika gari lao hapa  Serengeti,lakini tulipaa ugumu kupiga picha ndio tukapata mahala hapa pazuri kwa kufanya video,tukafanya Drama hapa ya gari kukwama ndani ya maji na gari nyingine ikaja nyuma kuoka watu hawa wakiw wamekaa juu ya gari lao na kuondolewa katika maji”alisema Schroeder.

Tamthiliya ya Dream Boat imefikisha miaka 35 sasa tangu kuanza kurushwa katika vituo mbalimbali vya Televisheni nchini Ujerumani na kwamba sehemu mbili zenye urefu wa dakika 90 kila moja za tamthiliya hiyo ,picha zake hupigwa katika nchi moja ya kiafrika .

Mwisho.


NAIBU INSPEKTA JENERALI WA POLISI ABDULRAHMANI KANIKI AFUNGA MAFUNZO YA KATIKA CHUO CHA MAAFISA WA POLISI KIDATU.

Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi , Abdulrahmani Kaniki akimkabidhi cheti cha Upelelezi Polisi Konstebo Jonathani Tossi wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya upelelezi kwa askari polisi wa Kinondoni katika chuo cha maafisa wa polisi Kidatu mkoani Morogoro
Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi , Abdulrahmani Kaniki akifafanua (katikati) jambo wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya upelelezi kwa askari polisi wa Kinondoni katika chuo cha maafisa wa polisi Kidatu mkoani Morogoro. Kulia ni Kamishina wa Polisi operesheni na mafunzo, Nsato Marijani 
Kamishina wa Operesheni na Mafunzo ( CP) Nsato Marijani akimsikiliza mwakilishi wa Taasisi ya Hans Sidel Bi Juliana wakati wakimsubili Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi kuwasili katika chuo cha maafisa wa Polisi Kidatu kwa ajili ya kufunga mafunzo ya upelelezi kwa askari Polisi wa mkoa wa kipolisi Kinondoni. ( picha na Tamimu Adam- Jeshi la Polisi).
Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi , Abdulrahmani Kaniki akisalimiana na Kamishina wa Polisi operesheni na mafunzo, Nsato Marijani alipofika kufunga mafunzo ya upelelezi kwa askari polisi wa Kinondoni katika chuo cha maafisa wa polisi Kidatu mkoani Morogoro.
Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi , Abdulrahmani Kaniki akisamilimiana na Mkuu wa Upelelezi wa Kinondoni Mark Njera alipofika kufunga mafunzo ya upelelezi kwa askari polisi wa Kinondoni katika chuo cha maafisa wa polisi Kidatu mkoani Morogoro

KAMISHNA WA TRA AHITIMISHA MAFUNZO YA ‘SCANNER’ MPYA BANDARINI


Kamishna wa Mapato ya ndani wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Elijah Mwandumbya akizungumza na wahitimu wa mafunzo ya usimamizi na uendeshaji wa mashine za ukaguzi wa mizigo ‘scanner’ kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) na TRA. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa TEHAMA, Bw. Abdulrahman Mbamba pamoja na Wakufunzi kutoka Kampuni iliyofunga mashine hizo.


Kamishna wa Mapato ya ndani wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Elijah Mwandumbya akikabidhi vyeti kwa wahitimu mbalimbali kutoka TPA na TRA.



Kamishna wa Mapato ya ndani wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Elijah Mwandumbya akiwa katika picha ya pamoja na Wahitimu na Wakufunzi

MADIWANI MERU WAMKATAA MKURUGENZI

Na Woinde Shizza, Globu ya Jamii - Arusha 

BARAZA la madiwani Halmashauri ya Meru mkoani Arusha wamkaanga Mkurugenzi wao kwa kusema hana uwezo wa kuongoza Halmashauri hiyo.


Akitoa maazimio ya kikao cha baraza kilichokaa siku mbili kwa kuwajumuisha madiwani, wakuu wa idara mbalimbali na wataalam, Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Willy Njau Alisema wametafakari kwa kina utendaji wa Mkurugenzi na kubaini kuwa hafai. "Tumejadili ajenda ya utendaji usioridhisha wa Mkurugenzi wetu na tumeona kuwa haufai kutokana na mambo mengi anayoyafanya yanakiuka kanuni na taratibu za Halmashauri"alisema Njau.

Aidha Njau alisema Mkurugenzi huyo ameonekana kukata mawasiliano na Mwenyekiti wa Halmashauri jambo alilosema siyo sahihi. pia ameweza kukata mawasiliano na madiwani wa Halmashauri hiyo pamoja na kusababisha hata wakuu wa idara kutokuwa na mawasiliano na madiwani jambo linalorudisha maendeleo nyuma.
Aliongeza kuwa Mkurugenzi huyo ameshindwa kukusanya makusanyo ya pesa kiasi cha milioni 150 kilichokusudiwa kukusanywa tangu Julai hadi Septemba mwaka huu jambo alilosema linaweza kusababisha Halmashauri kutopewa ruzuku kutoka serikalini kwasababu ya uzembe.


" Tumejiridhisha kuwa uwezo wa Mkurugenzi kuiongoza Halmashauri yetu kama Mkurugenzi Mtendaji ni mdogo hivyo hafai anadidimiza maendeleo ya Halmashauri ya meru" alisema Njau. Na kuongeza "Tumeamua kuiomba mamlaka yake na Uteuzi ichukue hatua stahiki za kumuwajibisha ili kunusuru maendeleo ya Halmashauri ya Meru".



Vilevile alisema kuwa Mkurugenzi huyo amekuwa akidharau maagizo yanayotolewa na kamati mbalimbali za baraza hilo na Kushindwa kuzitekeleza, ambako ni kuvunja kanuni na taratibu za Halmashauri. Hata hivyo alisema kitendo cha Mkurugenzi kukata posho za madiwani ni kinyume na utaratibu kwani ziliwekwa kisheria ambapo alisema Kama kuna tatizo la kukatwa posho ni lazima sheria hiyo ingebadilishwa kwanza. "Mwenye dhamana ya kutangaza kuwa posho zinabadilika ni Waziri mwenye dhamana hiyo lakini siyo Mkuu wa Mkoa, Wilaya au Mkurugenzi" alisema.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Meru, Christopher Kazer akijibu hoja za Madiwani katika kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo.


Naye Diwani wa Kikatiti Elisa Mungure ambaye ni Mwenyekiti wa madiwani alisema Mkurugenzi huyo amekuwa akiendesha Halmashauri kisiasa jambo ambalo halifai. "Ninasikitishwa na uongo unaoelezwa na Mkurugenzi ambaye kateuliwa na Mheshimiwa Rais hii ni ajabu haiwezekani kuendelea kumuamini mtu wa aina hii" alisema Mungure.

Alisema Mkurugenzi huyo amekuwa akiwahamisha watendaji wa kata bila kufuata taratibu huku akishinikiza ofisi ya kata ya Kikatiti kuwa ni ya CCM huku ikiwa ni ofisi ya wananchi wala siyo ya chama chochote. Kwa upande wake Mkurugenzi Huyo, Christopher Kazer alisema anafuata maagizo ya mkuu wa nchi na hawezi kuwanyima watu kufikiri wanavyofikiri. "Maelekezo ya kupunguza matumizi yasiyolazima kutoka kwa mkuu wa nchi ninayafuata pia ndio maana nimepunguza matumizi mengi" alisema.

Alisema hawezi kuzuia maamuzi yanayotolewa na baraza hilo maana kwa namna moja au nyingine wamekaa wakatengeneza maamuzi hivyo hawezi kuwalazimisha kutofanya maamuzi.
baadhi ya madiwani wakifuatailia.


Aidha pia alibainisha kuwa anaamini kabisa madiwani hawa wanataka halmashauri iendeshwe kisiasa wanataka iendeshwe kama wao wanavyotaka kitu ambacho hatakubali kwani sio hakutumwa kufanya kazi ya siasa bali alitumwa kufanya kazi ya kuwasaidia wananchi na serikali kwa ujumla 

Alisema kuwa anaamini haya yote yanatokea kutokana na madiwani hawa kukatwa fedha za posho na usafiri ambao walikuwa wamejiwekea bila kufuata taratibu


"Hivi jamani ndugu waandishi mtu anatoka hapo Usa River anataka alipwe nauli elfu 80 ni haki kweli wengine wanatoka hapa hapa wakija kikao kikichelewa kuisha wanataka walipwe fedha za kulala laki laki sasa mimi hayo yote nimeyatoa, sasa hivi wanalipwa elfu 40 tu na mshahara wao upo pale pale sasa wao ndio maana wananipiga zegwe. mimi nasema nitasimamia ilani ya chama ambacho kinaongoza serikali pia nitafata sera ya Mheshimiwa Rais ya kubana matumizi sitakubali wafanye vitu ovyo na ninyamaze walifikia hatua wakataka hata kunigombanisha na watendaji wangu ila mimi nimeajiriwa na serikali mimi sio mwanasiasa na nitafanya kazi kama nilivyoaidi siku niliyoapishwa "alisema Mkurugenzi Kazer.