Wednesday, December 12, 2018

RAIS DKT.SHEIN AFUNGUA KONGAMANO LA PILI LA KISWAHILI LA KIMATAIFA ZANZIBAR

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Mwenyekiti wa Baraza la Kiswahili la Taifa Zanzibar (BAKIZA) Dkt. Mohammed Seif Khatib, alipowasili katika viwanja vya Ukumbi wa Sheikh Idrissa Abdulwakil Kikwajuni Zanzibar, kwa ajili ya Ufunguzi wa Kongamano la Pili la Kimataifa la Kiswahili Zanzibar .(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Mwenyekiti wa Baraza la Kiswahili Zanzibar (BAKIZA) Dkt. Mohammed Seif Khatib, (katikati) wakati akitembelea maonesho ya Vitambu mbalimbali katika viwanja vya Ukumbi wa Sheikh Idrissa Abdulwakil , akiwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Iddi, wakiangalia vitabu hivyo.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk.Alim Mohamed Shein, akiangalia Vitambu mbalimbali vya Wachapishaji wa Vitabu kutoka Tanzani na Kenya wakati wa maonesho hayo yaliokwenda sambamba na Ufunguzi wa Kongamano la Pili la Kimataifa la Kiswahili LILILOFANYIKA Zanzibar katika ukumbi wa Sheikh Idrissa Abdulwakil Kikwajuni Zanzibar.
BAADHI ya Washiriki wa Kongamano la Pili la Kimataifa la Kiswahili la BAKIZA Zanzibar wakifuatilia hutuba ya Ufunguzi wa Kongamano hilo, wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akihutubia na kulifungua rasmin leo katika ukumbi wa Sheikh Idrissa Abdulwakil Kikwajuni Zanzibar.
MWAKILISHI wa Wachapishajhi wa Vitabu Ndg. Gabriel Kitua akitowa Salamu za Wachapishaji waVitambu mbalimbali walioshiriki Kongamano la Pili la Kimataifa la Kiswahili Zanzibar , lililofanyika katika ukumbi wa Sheikh Idrissa Abdulwakil Kikwajuni Zanzibar, wakati wa ufunguzi wake uliofanyika leo,12-12-2018.
WAZIRI wa Vijana Utamaduni Sanaa na Michezo Zanzibar Mhe. Balozi Ali Karume akizungumza wakati wa Ufunguzi wa Kongamano la Pili la Kimataifa la Kiswahili lililofanyika katika ukumbi wa Sheikh Idrissa Abdulwakil, kabla ya kumkaribisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, kulifungua leo. 12-12-2018.
BAADHI ya Mawaziri wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, wakifuatilia hutuba ya Ufunguzi wa Kongamano la Pili la Kimataifa ka Kiswahili Zanzibar, lililoandaliwa na (BAKIZA )wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akihutubia na kulifungua leo ,katika ukumbi wa Sheikh Idrissa Abdulwakil Kikwajuni Zanzibar.12-12-2018.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akihutubia katika hafla ya Uzinduzi wa Kongamano la Pili la Kimataifa la Kiswahili Zanzibar,lililoandaliwa na Baraza la Kiswahili Zanzibar BAKIZA katika ukumbi wa Sheikh Idrissa Abdulwakil Kikwajuni Zanzibar na kuwashirikisha Wadau wa Kiswahuli na Watunzi wa Vitambu kutoka Tanzania na Nje ya Tanzania. 
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akimkabidhi Cheti Mtunzi wa Riwaya Mzee Yussuf Masauni kwa utunzi wake wa nyimbo mbalimbali, kulia Waziri wa Vijana Utamaduni Sanaaa na Michezo Zanzibar Mhe. Balozi Ali Karume.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akimkabidhi Cheti Mtunzi wa Vitabu vya Kiu,Nyota ya Rehema , Ndg. Mohammed Suleiman, wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Pili la Kimataifa la Kiswahili Zanzibar, linalofanyika katika ukumbi wa Sheikh Idrissa Abdulwakil Kikwajuni Zanzibar.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akimkabidhi Cheti Mtunzi wa Vitabu vya Kuli, Vuta N’kuvute, Haini, Mbali na Nyumbani , Kasiri ya Mwinyi Fuad na Mtoto wa Mama kilichozinduliwa leo.Ndg. Shafi Adam Shafi na kulia Waziri wa Vijana Utamaduni,Sanaa na Michezo Zanzibar Mhe. Balozui Ali Karume, hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Sheikh Idrissa Abdulwakil Kikwajuni Zanzibar.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akinesha Kitabu cha Mtunzi Shafi Adam Shafi cha Mtoto wa Mama, baada ya kukizinduwa leo wakati wa hafla ya Kongamalo la Pili la Kimataifa la Kiswahili lililoandaliwa na Baraza la Kiswahili Zanzibar (BAKIZA) katika ukumbi wa Sheikh Idrissa Abdulwakil ,kulia Waziri wa Vijana Utamaduni Sanaa na Michezo Zanzibar Mhe. Balozi Ali Karume, Katibu Mtendaji wa BAKIZA Bi. Mwanahija Juma na kushoto Mtunzi wa Kitabu hicho cha Mtoto wa Mama Mzee Shafi Adam Shafi akipiga makofi baada ya uzinduzi huo, uliofanyika katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Zanzibar.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akikabidhiwa Vitabu mbalimbali vya Kiu na Nyota ya Rehema na mtunzi wa Vitabu hivyo Ndg. Mohammed Suleiman, wakati wa hafla ya Uzinduzi wa Kongamano la Pili la Kimataifa la Kiswahili Zanzibar, lililofanyika katika ukumbi wa Sheikh Idirissa Abdulwakil Kikwajuni Zanzibar.

No comments: