Thursday, October 25, 2018

AWAMU YA TANO YA MAZUNGUMZO YA KUSAKA AMANI YA BURUNDI YAANZA LEO



Rais mstaafu wa awamu ya tatu Benjamin mkapa akifungua majada wa mazungumzo ya kusaka amani ya nchi ya Burundi kwenye ukumbi wa mikutano wa Ngurdoto Mountain Lodge leo wilayani Arusha

 Na Ahmed Mahmoud Arusha

Serikali yashindwa kushiriki licha ya juhudi za msulushi, kundi kubwa la viongozi washiriki wakiwemo marais wastaafu, majadala wa mapitio ya kayanza na enteber kutoka na azimio moja

Mchakato wa mazungumzo ya kusaka amani nchini burundi yameanza rasmi leo ambapo Makubaliano ya Kayanza 1 ,2 na ,makubaliano ya Enteber yanaendelea kujadiliwa ili kuweza kupata taarifa moja ambayo msuluhishi ataipeleka kwenye kikao cha wakuu wa nchi za jumuiya ya Afrika mashariki.

Pamoja na jitihada za Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Benjamini Mkapa ambaye ni msimamizi wa msuluhishi wa amani ya Burundi za kuitaka serikali ya nchi hiyo kuja katika meza ya maungumzo hadi sasa hawajtoa majibu yeyote kama waja au la Juhudi hizo zimepelekea wadau wengine katika mazungumzo ya amani kuendelea na mazungumzo hayo ikiwemo kujadiliana kuhusiana na baada ya serikali kutotuma mwakilishi hadi sasa huku wakiwa hawajatoa majibu kama wanakuja au la.

Akifungua mazungumzo hayo mh.Mkapa akiwa anamaanisha kile alichosema kuwa hadi sasa hakupata maelezo sahihi kutoka kwenye serikali ya Burundi kwani hadi muda huu hawajatoa maelekezo yoyote kama watakuja au hawaji katika mazungumzo hayo. Amesema serikali hiyo imekuwa ikitoa maagizo ya kutaka kusijadiliwe baadhi ya vipengele ikiwemo suala la uchaguzi

Amesema kuwa atapeleka maelekezo yake kwa msuluhishi wa mazungumzo hayo pamoja kikao cha viongozi wakuu wan chi za jumuiya ya Afrika mwezi November mwaka huu ili watoe maamuzi kwani wao ndio walimtuma kuifanya kazi hiyo.

“Nimejitahidi kadiri ya uwezo wangu kuita serikali ya burundi lakini imeshindikiana kwa kuwa haya ni mazungumzo ya mwisho nasubiria mazimio haya ya kikao hichi niwasilishe kwenye kikao cha wakuu wa mataifa ya Afrika mashariki november”

Amewataka viongozi hao kutoka makundi mbalimbali ya kijamii wakiwemo Asasi za kiraia,viongozi wa dini na wa kisiasa,vijana ,kinamama na wazee kuja na muongozo kwa kupîtia ,miongozo hiyo ili kusaidia kwenda kwenye uchaguzi 2020 .

Amesema kuwa serikali ya Burundi Hata kama wasiposhiriki haiwezi kuathiri mazungumzo hayo kwani walishatoa msimamo wao tokea awali tunao hivyo wajadili na kupitia miongozo hiyo ilikufikia kwenda katika uchaguzi .

Msimamo wa serikali ya Burundi kuhusu mkataba wa Kayanza unaona ndio dira ya kuelekea kwenye uchaguzi huru ambapo vyama vya upinzani wao wanaona kuwa muda sasa umefika kukaa mezani kujadili kwa pamoja mustakabali wa nchi yao na suala zima la uchaguzi utakao kuwa huru sanjari na makundi yote kuwa huru kushiriki kuijenga nchi yao.

Msuluhishi wa mazungumzo hayo Rais mstaafu Benjamin Mkapa ameona kuwa viongozi hao wazingatie miongozo hiyo miwili ili aweze kuipitia na baadae kuweza kuja na moja ambayo itapelekwa kwenye vikao vya wakuu wa nchi za EAC.

Wapinzani wa nje na ndani ya nchi wameshatoa miongozo yao kakiao chao cha Enteber cham waka 2018 kinaonyesha jinsi miongozo yao waliopitisha hivyo tuapitia tupate muongozo mmoja huu utakuwa ndio yatakuwa mapendekezo yatakayo saidia kusukuma

No comments: