Saturday, September 29, 2018

VODACOM WASAINI MKATABA KUTUMIA MKONGO WA TAIFA WA MAWASILINO









Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Simu za mkononi nchini Vodacom Tanzania, Ndugu Hisham Hendi (wa pili kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL Corporation), Ndugu Waziri Kindamba (wa pili kulia) wakisaini mkataba wa kibiashara leo Makao Makuu ya TTCL jijini Dar es Salaam. Katika makubaliano hayo Vodacom watatumia huduma za Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano katika huduza za data na sauti maeneo mbalimbali kuboresha mawasiliano. Nyuma ni wanasheria wa makampuni hayo wakishuhudia.










Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Simu za mkononi nchini Vodacom Tanzania, Ndugu Hisham Hendi (kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL Corporation), Ndugu Waziri Kindamba (kulia) wakipongezana mara baada ya kubadilishana nakala za mkataba wa kibiashara leo Makao Makuu ya TTCL jijini Dar es Salaam. Katika makubaliano hayo Vodacom watatumia huduma za Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano katika huduza za data na sauti maeneo mbalimbali kuboresha mawasiliano. Wa pili kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Mawasiliano), Jim James Yonazi akishuhudia tukio hilo pamoja na Ofisa Msimamizi wa Mkongo wa Taifa.




Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Mawasiliano), Jim James Yonazi (katikati) akizungumzia tukio hilo kwenye hafla hiyo ya kusaini mkataba wa kibiashara kati ya Vodacom na Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano. Kushoto ni Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Simu za mkononi nchini Vodacom Tanzania, Ndugu Hisham Hendi na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL Corporation), Ndugu Waziri Kindamba (kulia) kabla ya tukio la kusaini mkataba wa biashara na Vodacom ya kutumia huduma za Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano leo jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Simu za mkononi nchini Vodacom Tanzania, Ndugu Hisham Hendi (kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL Corporation), Ndugu Waziri Kindamba wakionesha mikataba hiyo mara baada ya kusainishana.
Mh. Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Mawasiliano), Jim James Yonazi (wa pili kushoto) akimpongeza Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL Corporation), Ndugu Waziri Kindamba (wa pili kulia) mara baada ya kusaini mkataba wa biashara na Vodacom ya kutumia huduma za Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano leo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Simu za mkononi nchini Vodacom Tanzania, Ndugu Hisham Hendi.





Na Joachim Mushi, Dar es Salaam


KAMPUNI ya Simu za mkononi nchini Vodacom Tanzania leo imesaini mkataba wa kibiashara na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL Corporation) wa kutumia Huduma za Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano (NICTBB) utakaowezesha mkongo kusambaza huduma za mawasiliano maeneo ya vijijini.

Hafla ya makubaliano hayo ya kibiashara imefanyika leo jijini Dar es Salaam, ambapo TTCL Corporation imewakilishwa na Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo, Ndugu Waziri Kindamba na Vodacom ikiwakilishwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Ndugu Hisham Hendi.

Akizungumza katika hafla hiyo, Kindamba alisema Vodacom amekuwa mteja wa Mkongo wa Taifa tangu Mei Mosi, 2013 na hadi sasa anatumia huduma za ukubwa wa STM-4 (Jumla 7) na STM-16 (Jumla 9), huku akiongeza kuwa Mkataba mpya uliosainiwa unaongeza viwango vya matumizi ya Mkongo kwa Vodacom kwa STM-16 (Jumla 2) na STM-64 (Jumla 1) wenye thamani ya Shilingi bilioni 25.6 bila VAT.

“..Mkataba wa leo unatufanya sisi NICTBB na TTCL kutambua uzito wa majukumu tuliyokabidhiwa na Serikali ya kuhakikisha kuwa huduma za Mkongo zinaimarishwa ili watoa huduma za Mawasiliano hapa nchini waboreshe huduma zao na kuwafikia wananchi wengi zaidi,” alisema.

“Mkataba wa leo unatufanya sisi NICTBB na TTCL kutambua uzito wa majukumu tuliyokabidhiwa na Serikali ya kuhakikisha kuwa huduma za Mkongo zinaimarishwa ili watoa huduma za Mawasiliano hapa nchini waboreshe huduma zao na kuwafikia wananchi wengi zaidi,” aliongeza Kindamba.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom, Ndugu Hisham Hendi akizungumza katika hafla hiyo alisema unalenga kuboresha huduma za mawasiliano za sauti na data kanda ya ziwa kati kaskazini na mikoa ya kusini ya Tanzania kwa kuwezesha kuleta maendeleo kupitia huduma teknolojia ya mawasiliano.

Alisema Vodacom inatumia mkongo kwa takribani zaidi ya miaka 5 na kwa mwaka huu Vodacom inakodisha mkongo huo ambao miundombinu yake imesambaa kwa urefu wa kilomita zipatazo 7,560 nchini kote kwa kipindi cha miaka 10 kwa thamani ya dola za Kimarekani USD11.2 milioni bila VAT.

“miundombinu ya mkongo wa taifa wa mawasiliano imesambaa katika eneo kubwa kwa urefu na unao uwezo mkubwa wa kuwezesha kurusha mawasiliano ya data kwa ufanisi mkubwa, teknolojia hii itawezesha wateja wa Vodacom kupata mawasiliano mazuri zaidi nchini kote,” alisisitiza Ndugu Hisham Hendi.

Hadi sasa wateja wanaohudumiwa na mkongo wa Taifa wa mawasiliano ni pamoja na kampuni ya TTCL, Vodacom, Tigo, Viettel, Airtel, Simbanet, Zantel, Raha, Smile, Sasakwa, eGA na ISP wengine yanatumia Mkongo wa Taifa kufikisha huduma zao kwa wateja. Mkongo wa Taifa hutumiwa pia na nchi za Afrika Mashariki na eneo la Maziwa makuu yaani Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Malawi na Zambia na hivyo kuufanya Mkongo huu kuwa na umuhimu wa kipekee kwa mawasiliano.

No comments: