Saturday, September 29, 2018

NAFASI ART SPACE KUSHEHEREKEA MIAKA 10 TANGU KUANZISHWA KWAKE, WAANDAA TAMASHA MATATA DAR

 *Ni leo Septemba 29 ,kufanyika katika ukumbi wao uliopo Mikocheni B kuanzia saa tisa alasiri
*Wasanii maarufu ndani na nje ya nchi kutoa burudani

Na Said Mwishehe, Globu ya jamii
 NAFASI Art Space katika kusheherekea miaka 10 tangu kuanzisha kwake wanatarajia kufanya tamasha kubwa na la aina yake leo kuanzia saa tisa alasiri ambapo wasanii maarufu katika uchoraji, uimbaji na waimbaji wa muziki wa dansi wafanya show kwa mashabiki na wapenzi wa Sanaa ndani na nje ya nchi.
Tamasha hilo linatafanyika katika Ukumbi wa Nafasi Art Space uliopo Michokeni B jijini Dar es Salaam na kwamba hakutakuwa na kiingilio chochote na lengo la kufanya hivyo ni kutoa nafasi kwa mashabiki na wapenzi wa sanaa kufika kwa wingi.
 Akizungumza na Michuzi Blog jana kuhusu Tamasha hilo ambalo limepewa jina la Sanaa Yetu Festival, Ofisa Maendeleo Biashara na Masoko wa Nafasi Art Space Agnes-Senga Tupper amesema katika kusheherekea miaka 10 ya Nafasi Art Space wanatarajia kufanya show hiyo matata ambayo itagusa sanaa za aina zote nchini Tanzania.
Amesema zaidi ya wasanii 19 wa uchoraji, uimbaji , wanamuziki wa dansi ni miongoni mwa watakaotoa burudani kwa mashabiki wao ambao kwa kipindi cha miaka 10 wamekuwa wakiwaunga mkono.
Tupper amefafanua kwamba “Mwaka 2008 kikundi kidogo cha wasanii wa Tanzania walijikusanya na kuanzisha Nafasi Art Space kwa ajili ya wasanii nchini kuwa na sehemu ya kufanya kazi zao, pamoja na msaada kutoka Denmark Embassy, Nafasi Art Space ilianzishwa.Tangu wakati huo, Nafasi imeweza kusaidia wasanii zaidi ya 100 nchini Tanzania kuendeleza na kukuza vipaji vyao .
 “Hii imewapatia wapenzi wa sanaa fursa ya kuona, kujifunza na kufahamu sanaa na utamaduni jijini Dar es Salaam pamoja na nje ya nchi. Hivyo kwa mwezi huu wa Septemba, Nafasi Art Space imekuwa ikisherehekea miaka 10 kwa kufanya matukio mbalimbali ya kisanaa kwa ajili ya umma,”amesema Senga.
 Ametaja baadhi ya matukio ambayo wameyafanya kama sehemu ya kusheherekea miaka 10 ambayo kesho ndio kilele chake ni pamoja na kufanya mkutano na waandishi wa vyombo vya habari, uzinduzi kwa kuchora live soko la Karume, kutembelea Wodi ya Watoto katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, wameshiriki kwenye kipindi cha Jukwaa la Sanaa pamoja na Baraza la Sanaa Tanzania(BASATA).
Pia wameshiriki Siku ya Usafi Dunaini kwa kusafisha eneo la Coco Beach, kufanya warsha ya sanaa katika Shule ya Mgulani na Chang’ombe za jijini Dar es Salaam pamoja na uchoraji Graffiti Live Nafasi Art Space.
Senga amesisitiza “Kwa kumalizia tunafanya bonge moja la Festival –Sanaa Yetu Festival .Hivyo Septemba 29 (Jumamosi)  wakati wa Festival hiyo ikiendelea kutakuwa na nafasi ya kuchora T-shirt kwa mashabiki watakao hitaji. Pia kutakuwa na maonesho, uuzaji wa sanaa za uchoraji kutoka kwa wasanii mashuhuri dunia nzima ambao ni wanachama wa Nafasi,”amesema Senga.
Pia amesema baada ya hapo itafuata Show ya wasanii kama vile Muda Africa,  Wamwiduka Band, Wahapahapa Band, Bagamoyo Players, Fashion Show ya Makeke International.Kisha watamaliza na Mfalme wa Kisengeli Mfalme Ninja Na DJ Frank.
“Septemba hii ni fursa kwa Nafasi kusherehekea mafanikio ya sanaa ya kisasa nchini Tanzania kwa kutoa shukrani kwa wafadhili na mashabiki wetu, na kuleta jamii pamoja katika ujenzi wa kizazi kijacho cha wasanii na wapenzi wa sanaa.  Nisisitize hakuna kiingilio na watu wa rika zote wanakaribishwa.Lakini Michango ya tunapokea,”amesema Senga.
Kuhusu mgeni rasmi amesema wanatarjia kuwa na mgeni rasmi katika tamasha hilo ambaye atatoka Ubalozi wa Norway nchini Tanzania hasa kwa kuzingatia ndio wafadhili wakuu wa Nafas Art Space.
Baadhi ya matukio ambayo wameyafanya kama sehemu ya kusheherekea miaka 10 ambayo leo ndio kilele chake ni pamoja na kufanya mkutano na waandishi wa vyombo vya habari, uzinduzi kwa kuchora live soko la Karume, kutembelea Wodi ya Watoto katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, wameshiriki kwenye kipindi cha Jukwaa la Sanaa pamoja na Baraza la Sanaa Tanzania(BASATA).
 Michoro mbalimbali ilichorwa na vijana wenye vipaji ikiwa ni sehemu ya maandalizi
 Vikundi mbalimbali vilishiriki kuelekea kilele cha  NAFASI Art Space ambapo leo inatimiza miaka 10 tangu kuanzisha kwake 

No comments: