Saturday, September 29, 2018

Dkt. Abbasi, TAGCO Watembelea Kituo cha Radio cha Storm Mkoani Geita



Mkurugenzi wa Idara ya Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akiongea na watumishi wa kituo cha Redio cha Storm FM Mkoani Geita ambapo aliwasisitiza umuhimu wa kufanya kazi ya uandishi wa Habari kwa kuzingatia weledi.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akishiriki Kipindi cha Moja kwa moja katika kituo cha Redio cha Storm FM Mkoani Geita ambapo aliongelea masuala mbalimbali ikiwamo miradi mikubwa inayotekelezwa na iliyotekelezwa na Serikali katika kipindi cha Miaka mitatu ya Serikali ya Awamu ya Tano.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi na viongozi wa Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini (TAGCO) wakiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa kituo cha Redio cha Storm FM Mkoani Geita
Mwenyekiti Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini (TAGCO) Bw. Pascal Shelutete akishiriki Kipindi cha Moja kwa moja katika kituo cha Redio cha Storm FM Mkoani Geita ambapo alisistiza kuwa wataendelea kuwajengea uwezo Maafisa Mawasiliano Serikalini na kuendelea kurahisisha uhusiano kati ya waandishi wa habari na Maafisa Habari wa Serikalini.
Katibu wa Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini (TAGCO) Bw. Abdul Njaidi akiongea na watumishi wa kituo cha Redio cha Storm FM Mkoani Geita ambapo ambapo aliwasisitiza kuhusu umuhimu wa kushiriki katika shughuli za maendeleo katika mkoa wa Geita.

Watumishi wa kituo cha Redio cha Storm FM Mkoani Geita wakimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi alipokutana nao.

No comments: