Wednesday, July 18, 2018

MOJASPESHO YATOA MSHINDI WA SHILINGI MILIONI 204

  Mchezo wa bahati nasibu wa Mojaspesho umetoa kwa mara ya kwanza mshindi wa kiasi kikubwa cha pesa cha shilingi Milioni 204 kwa ROSEMARY ONESMO LUHAMO, mfanyabiashara kutoka MPWAPWA DODOMA mwenye umri wa miaka 26.

Akuzungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam wakati wa kukabidhi pesa kwa mshindi, Meneja biashara wa kampuni ya Lucy Games Patrick Salamouni ambayo ndio inajechezesha mchezo wa Mojaspesho alisema kuwa ushindi wa Rosemary umekuja baada ya kucheza Mojaspesho zaidi ya mara nyingi sana bila kukata tamaa, na hatimaye kulinganisha namba zake za tatu spesho ambazo zilikuwa 873 siku ya Jackpot ya Jumamosi ya tarehe 14 mwezi Julai 2018.

Huu ni mchezo wa bahati nasibu. Unaweza ukacheza mara moja ukashinda lakini pia unaweza isishinde. Ninachoweza kuwaambia ni kuwa kila mtu anayecheza anayo nafasi ya kuwa mshindi. Naomba Watanzania kuwa huu ni mchezo halali na kila anayeshinda anapata zawadi yake, alisema Salamouni. Salamouni aliongeza kuwa huu ni ushindi mkubwa kuwahi kutokea tangu Moja Spesho ianze kuchezesha Droo zake na ni uthibitisho kuwa kila mtu anaweza kushinda Mojaspesho.

‘Unaweza kucheza MOJASPESHO kupitia simu yako ya mkononi kwa kuingia sehemu ya KULIPIA BILI kwa watumiaji wa AIRTEL MONEY, TIGO PESA, MPESA au HALOPESA, kisha ingiza NAMBA YA KAMPUNI/BIASHARA ya MOJASPESHO ambayo ni 123255 - kisha INGIZA NAMBA ZAKO 3 SPESHO ZA USHINDI’ aliongeza Salamouni.

Kwa upande wake, mshindi Rosemary Onesmo alisema kuwa anayo furaha kubwa na kujiona wa bahati kuwa mshindi wa kwanza wa milioni 204. ‘Namshukuru Mungu kwa kunisaidia kuwa mshindi wa MOJASPESHO. Pia nawapongeza MOJASPESHO kwa kuwa wa kweli na kuweza kunipa zawadi yangu hapa leo kila mtu akishuhudia. Napenda kuwahakikishia Watanzania kuwa mchezo wa MOJASPESHO ni wa ukweli na nawaomba wajitokeze kwa wingi kwani hata haujashinda zawadi kubwa kama mimi unaweza kuwa mshindi wa zawadi zingine, alisema Rosemary.

Rosemary aliongeza kuwa atatumia pesa zake kuendeleza biashara yake kwani ameweza kupewa utaalamu wa biashara kabla ya kubabidhiwa zawadi yake. MOJASPESHO wameweza kunipa elimu nzuri jinsi ya kutunza pesa hizi na pia jinsi ya kufanya biashara bila kuteleleka. Ni heshima kubwa mno kwa upande wangu, aliongeza Rosemary.


Mshindi RoseMary Onesmo Luhamo (katikati) akikabidhiwa zawadi ya ushindi wake wa milioni 204 kutoka kwa Meneja wa Lucky Games Ltd, Patrick Salamouni, ambayo ni kampuni inayochezesha mchezo wa MojaSpesho pamoja. Kushoto ni Meneja wa tawi la benki ya CRDB Azikiwe Premier Fabiola Msula. Kwa kucheza mchezo wa MOJASPESHO kupitia simu yako ya mkononi nenda sehemu ya KULIPIA BILI kwa watumiaji wa AIRTEL MONEY, TIGO PESA, MPESA au HALOPESA, kisha ingiza NAMBA YA KAMPUNI/BIASHARA ya MOJASPESHO ambayo ni 123255 - kisha INGIZA NAMBA ZAKO 3 SPESHO ZA USHINDI’09
Mshindi RoseMary Onesmo Luhamo wa kwanza wa droo ya milioni 204 ya MOJASPESHO, akifurahi baada ya kukabidhiwa pesa za ushindi wake leo jijini Dar es Salaam. Kwa kucheza mchezo wa MOJASPESHO kupitia simu yako ya mkononi nenda sehemu ya KULIPIA BILI kwa watumiaji wa AIRTEL MONEY, TIGO PESA, MPESA au HALOPESA, kisha ingiza NAMBA YA KAMPUNI/BIASHARA ya MOJASPESHO ambayo ni 123255 - kisha INGIZA NAMBA ZAKO 3 SPESHO ZA USHINDI’

No comments: