Friday, June 15, 2018

DK.NDUGULILE ASEMA HAIRUHUSIWI DUKA LA DAWA KUWA NA DIRISHA LA USHAURI


Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

NAIBU Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk.Faustine Ndugulile amesema hairuhusiwi katika duka la dawa kuwa na dirisha la ushauri kwani huo si utaratibu huku ikielezea sababu zinazosababisha usugu wa dawa.

Dk.Faustine Ndugulile amesema hayo jana katika kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Famasi yaliyofanyika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.Akizungumzia maduka ya dawa kuwa na dirisha kwa ajili ya kutoa ushauri, Dk.Ndugulile amesema kisheria hairuhusiwi kwani kuna mgawawanyo wa majukumu.

"Kuna baadhi ya maduka ya kuuza dawa wameweke na madirisha kwa ajili ya kutoa ushauri.Hairuhusiwi na hivyo baraza la famasi linatakiwa kusimamia hili kwa kuhakikisha hakuna duka la dawa ambalo limeweka dirisha la ushauri,"amesema Dk.Ndugulile.

Akizungumzia usugu wa dawa kwa mtumiaji, Dk.Ndugulile amefafanua zipo sababu nyingi ikiwamo ya matumizi ya dawa yasiyo sahihi na ulaji holela wa dawa.Amefafanua mbali ya kuwapo kwa sababu hizo kuna tafiti ambayo imebaini kuna vimelea ambavyo ni sugu wa hali ya juu kwa dawa zote zilizopo duniani.

Wakati huohuo Dk.Ndugulile ameliezea baraza la Famasi kuwa anao ushahidi wa baadhi ya watalaam wa famasi si waaminifu kwani wamekuwa wakiiba dawa na hivyo hao wachache kuharibu sifa ya famasi.

Ameliomba baraza la famasi kuhakikisha wanachukua hatua dhidi ya wanaokiuka sheria za famasi kwani kukaa kimya kunatoa nafasi ya baadhi yao kukika sheria zilizopo, hivyo wafuatilie.Hivyo amesema wenye tabia hiyo ya kuiba dawa waache mara moja kwani Wizara yao inafuatilia huku akielezea kwa sasa hakuna tatizo la uhaba wa dawa kwani zipo za kutosha.

Kuhusu kilele cha maadhimisho hayo, Dk.Ndugulile amesema anampongeza Msajili wa Baraza la Famasi pamoja na timu yake kwa kuona umuhimu wa kuadaa maadhimisho hayo.

Amesema kauli mbiu ya maadhimisho hayo inasema hivi "Taaluma ya Famasi kuelekea Tanzania yenye uchumi wa viwanda" ambapo amesisitiza kupitia kauli mbiu hiyo wanataaluma wanaunga mkono nia ya dhati na juhudi za Serikali chini ya Rais Dk.John Magufuli katika kuboresha huduma za afya kwa wananchi ili kufikia uchumi wa kati na Tanzania ya Viwanda.

"Sina shaka kuwa wanataaluma kwa kushirikiana na wadau wa ndani na nje mtaweka mikakati thabiti kupitia viwanda vya dawa ambavyo matokeo yake yataboresha uchumi wa nchi na kuhakikisha Tanzania inakuwa na uchumi imara,"amesema Dk.Ndugulile.

Kwa upande wa Meya wa Jiji la Dar es Salam Isaya Mwita amesema anapongeza na namna ambavyo baraza hilo limejipanga kuhakikisha wanatoa huduma bora za famasi huku akitoa ombi kwa Serikali kuandaa mazingira ambayo yatatoa nafasi kwa kuongezeka kwa viwanda vya dawa na vifaa tiba nchini.

Wakati huo huo Baraza la Famasi limetumia nafasi hiyo kuelezea mafanikio na changamoto huku pia wakielezea mikakati waliyonayo katika kuhakikisha wanaboresha huduma za famasi nchini.
 Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiwakabidhi zawadi baadhi ya wadau wa Famasi kwa mchango wao katika sekta hiyo wakati wa maadhimisho ya wiki ya Famasia yaliyofanyika leo jijini Dar es salaam.
 Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiwakabidhi zawadi baadhi ya wadau wa Famasi kwa mchango wao katika sekta hiyo wakati wa maadhimisho ya wiki ya Famasia yaliyofanyika leo jijini Dar es salaam.
 Picha ya Pamoja
 Baadhi ya Washiriki 
 Meya wa jiji la Dar es salaam Mh. Isaya Mwita akizungumza katika madhimisho ya wiki ya wafamasia Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam.
 Msajili wa Baraza la Famasia Bi. Elizabeth Shekirego  akitoa maelezo kuhusu maadhmisho ya wiki ya wafamasia yaliyofanyika jana Mnazi Mmoja
Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile kushoto akionesha juu Bango Kitita la famasia baada ya kulizindua wakati  wa maadhimisho ya wiki ya Famasia yaliyofanyika leo jijini Dar es salaam. Kulia ni Msajili wa Baraza la Famasia Bi. Elizabeth Shekirego Kushoto ni Mganga Mkuu wa Serikali Profesa Muhamed Bakari

No comments: