Friday, June 15, 2018

RC GAMBO:WAANDISHI KUWENI WAZALENDO KWA MKOA NA TAIFA LENU

Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akiendesha mazungumzo pamoja na mijadala mbalimbali iliyokuwa ikiendelea katika kikao. Cha siku. Moja cha waandishi wa habari pamoja na wadau wa taasisi za serikali mkoani hapo. Picha na Vero Ignatus. 
 Mkuu wa Wilaya ya Arusha Fabian Gabriel Daqarro akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano wa siku moja ulioitishwa na mkuu wa mkoa huo. Picha na Vero Ignatus
 Katibu Tawala  wa Mkoa wa Arusha Charles Kwitega akizungumza katika mkutano huo katika Kituo cha kimataifa cha mikutano cha AICC Arusha. Picha na Vero Ignatus.
 Mkurugenzi wa Kituo cha Mikutano ya Kimataifa cha AICC Arusha Eliashialia Kaaya.
Meneja wa TRA mkoa wa Arusha Faustine Mdesa, akiwasilisha mafanikio, changamoto na mpango mkakati wa mwaka wa serikali unaomalizika tar 30 june 2018.Picha na Vero Ignatus
Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa mkoa wa Arusha  Cloud Gwandu akizungumza katika mkutano wa siku moja wa mkuu wa mkoa wa Arusha na waandishi wa Habari. Picha na Vero Ignatus
Naibu Muhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi Ngorongoro, Asangye Bangu akijibu maswali yaliyoulizwa na waandishi wa habari. Picha na Vero Ignatus.
Mdau wa utalii kutoka Shirika la Hifadhi la Taifa (TANAPA) Paschal Shelutete ambae akijibu maswali na kutoa ufafanuzi kwenye mkutano wa waandishi wa habari ulioandaliwa na Rc Mrisho Gambo- Arusha. Picha na Vero Ignatus.
Baadhi ya waandishi wa habari walioshiriki katika mkutano ulioitishwa na mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo ukiwa na lengo la kuhakikisha kuboresha mahusiano kati ya serikali na waandishi mkoani hapo. Picha na Vero Ignatus.
Kutoka kushoto ni Katubu tawala wa mkoa wa Arusha Charles Kwitega akiteta jamba na mkuu wa wilaya ya Arusha Fabian Gabriel Daqqaro. Picha na Vero Ignatus.
Meneja wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Nchini (TIRA) Kanda ya Kaskazini Eliezer Rweikiza akiwasilisha kazi na majukumu ya Mamlaka hiyo na umuhimu wa kuwa na Bima haswa kwa vyombo vya moto.Picha na Vero Ignatus.

Na. VERO IGNATUS ARUSHA

Mkuu wa mka wa Arusha Mrisho Ghambo amefanya mkutano wa siku moja na waandishi wa habari ukiwa na lengo la kuimarisha na kuboresha mahusiano kati ya Serikali na wanahabari.

Katika mkutano huo wa siku moja ambao  ni wapili tangia kuingia madarakani  umewajumuisha wadau mbalimbali wa Taasisi za serikali mkoani hapa katika kueleza mafanikio changamoto mbalimbali za maendeleo na namna ya kuzitatua.

Katika ufafanuzi zaidi Gambo amesema kuwa asilimia 80%ya mapato mkoani hapo yanatokana na utalii hivyo amewataka wanahabari kuwa makini  taarifa ambazo wanaandika wazichuje kabla ya kuzipelea katika jamii.

"Mfano habari ya mtalii kutekwa, mwandishi unapoaiandika hiyo habari na kuitoa katika vyombo vya habari, itasomwa na inaweza kuleta madhara, kuwaogopesha wageni kutokuja nchini kwaajili ya utalii, kuweni makini tangulizeni uzalendo kwanza"

Amewataka viongozi mkoani hapa Kuwapa ushirikiano wa kutosha waandishi kwani kuna baadhi ya viongozi wanawakimbia waandishi na kuwalazimisha waandike kadri wanavyoona inafaa,amekemea na kuwataka kutoa ushirikiano. 

RC Gambo amepongeza juu ya jambo la kujiendeleza kielimu kwa waandishi ambapo ameutaka uongozi wa, APC kupeleka data base ili uongozi wa mkoa waone ni namna gani unaweza kuandika andiko kwa wadau mbalimbali kwaajili ya kuwasapoti kielimu. 

Gambo amewataka wanahabari mkoani hapo kutokukubali kurubuniwa au kutumiwa na mtu awae yeyote yule ili kuharibu amani badala yake watangulize Uzalendo kwanza kwaajili ya mkoa na Taifa kwa ujumla. 

No comments: