Friday, June 29, 2018

BENKI YA CRDB YADHAMINI MKUTANO WA MAKANDARASI JIJINI DODOMA



Meneja Mahusiano wa Benki ya CRDB anayeshughulikia wateja wakubwa na taasisi, Jane Ikira, akimkaribisha Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa, alipotembelea banda la benki hiyo. Katikati ni Meneja Mahusiano wa benki hiyo anayeshughulikia wateja wakubwa na taasisi, Shima Danford.
Meneja Mahusiano wa Benki ya CRDB anayeshughulikia wateja wakubwa na taasisi, Shima Danford (katikati), akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa.
Meneja Mahusiano wa Benki ya CRDB anayeshughulikia wateja wakubwa na taasisi, Shima Danford, akizungumza na waandishi wa habari.
Jane Ikira, akimkabidhi zawadi Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa.
Baadhi ya maofisa wa Benki ya CRDB wakiwa katika banda lao wakati wa mkutano wa mashauriano na wadau na maonyesho ya bidhaa na huduma za ujenzi yanayofanyika mkoani Dodoma.
Meneja wa Benki ya CRDB tawi la LAPF-Dodoma, Martha Ngwenya, akipeana mkono na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa, alipotembelea banda la benki hiyo.
Ofisa Masoko Mwandamizi wa Benki ya CRDB, Nasibu Kalamba (kushoto), akielezea juu ya huduma na bidhaa zinazotolewa na Benki ya CRDB kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa (kulia).

Meneja Mahusiano wa Benki ya CRDB anayeshughulikia wateja wakubwa na taasisi, Shima Danford (katikati), akielezea juu ya dhamana ya mikopo ya makandarasi inayotolewa na Benki ya CRDB kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa, alipotembelea banda la Benki ya CRDB katika mkutano wa mwaka wa makandarasi jijini Dodoma, ulioandaliwa na Bodi ya Makandarasi (CRB) na kudhaminiwa na benki hiyo. Kushoto ni Meneja Mahusiano wa hiyo anayeshughulikia wateja wakubwa na taasisi, Jane Ikira.
Baadhi ya wateja wakiwa katika banda la Benki ya CRDB wakipata huduma mbalimbali ikiwemo ya kufungua akaunti.
Mteja wa Benki ya CRDB akielezwa kuhusu Kampeni ya Shuhudia Kombe la Dunia la Fifa 2018 na TemboCardVisa baada ya kufungua akaunti katika banda la benki hiyo.
Baadhi ya washiriki wa mkutano huo wakiwa kwenye ukumbi wa mkutano.
Meneja Mwandamizi Huduma za Kibiashara wa Benki ya CRDB, Baraka Eusebio, akitoa ufafanuzi juu ya huduma mbalimbali za kibenki wanazotoa.
Maofisa wa Benki ya CRDB wakiwa wamepozi kwa picha ndani ya banda lao kutoka kushoto ni Lucy Kiondo kutoka tawi la Dodoma, Ofisa Maendeleo ya Biashara tawi la Chamwino, Ingrid Nestory, Veronica Komba na Wakala wa Benki hiyo, Upendo Moses.
Ofisa wa Benki ya CRDB, Veronica Komba (kushoto), pamoja na Ofisa Maendeleo ya Biashara tawi la Chamwino, Ingrid Nestory, wakimuhudumia mteja.
Wakala wa Benki ya CRDB tawi la Chamwino, Upendo Moses, akitoa huduma kwa wateja waliokuja kuweka fedha zao kupitia banda la CRDB.
Maofisa wa Benki ya CRDB wakiwa wamepozi kwa picha ndani ya banda lao, kutoka kushoto ni Lucy Kiondo kutoka Dodoma Branch, Veronica Komba na Ofisa Maendeleo ya Biashara tawi la Chamwino, Ingrid Nestory.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa (katikati aliyekaa), akiwa katika picha ya pamoja na wadhamini wa mkutano wa mwaka wa makandarasi unaofanyika jijini Dodoma ambapo Benki ya CRDB ni miongoni mwa wadhamini wa mkutano huo.

No comments: