Tuesday, February 6, 2018

SERIKALI YATOA SIKU SABA WANANCHI WALIOVAMIA JUMUIYA HIFADHI WANYAMAPORI YA JUKUMU KUONDOKA

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga akizungumza waliovamia eneo la Mkesa ndani ya Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori ya JUKUMU iliyopo Morogoro vijijini wakati walipofanya ziara na Naibu Waziri wa Tamisemi, Joseph kakunda kutembelea eneo hilo kwa lengo la kuwasikiliza wananchi hao kwa ajili ya kujionea uharibifu unaoendelea katika eneo hilo . Wengine ni Naibu Waziri wa TAMISEMI, Joseph Kakunda (wa pili kulia) akiwa na Mkuu wa wilaya ya Morogoro,Regina Chonjo (katikati
Naibu Waziri wa TAMISEMI, Joseph Kakunda (katikati) akizungumza na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga ( kulia) pamoja na na Mkuu wa wilaya ya Morogoro,Regina Chonjo (kushoto) ofisis kwa mkuu wa wilaya hiyo kabla ya kuanza kwa ziara iliyofanyika jana ya kutembelea eneo la Mkesa liliopo ndani ya Jumuiya Hifadhi ya Wanyamapori ya JUKUMU kwa lengo la kuwasikiliza wananchi hao na kujionea uharibifu unaoendelea katika eneo hilo.
Naibu Waziri wa TAMISEMI, Joseph Kakunda akizungumza na wananchi waliovamia eneo la Mkesa ndani ya Jumiya Hifadhi ya Wanyamapori ya JUKUMU iliyopo Morogoro vijijini wakati walipofanya ziara na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga kutembelea eneo hilo kwa lengo la kuwasikiliza wananchi hao kwa ajili ya kujionea uharibifu unaoendelea katika eneo hilo . Wengine ni Naibu Waziri wa TAMISEMI, Joseph Kakunda (wa pili kulia) akiwa na Mkuu wa wilaya ya Morogoro,Regina Chonjo (katikatiNaibu Waziri wa TAMISEMI, Joseph Kakunda (wa pili kulia) Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga ( wa kwanza kulia) pamoja na na Mkuu wa wilaya ya Morogoro,Regina Chonjo ( wa pili kushoto) wakiangalia nyaraka feki iliyowasilishwa na miongoni mwa wananachi aliyedai kuwa yeye ni mkazi halali katiaka eneo hilo la Mkesa liliopo ndani ya Jumuiya Hifadhi ya Wanyamapori ya JUKUMU wakatia wa ziara iliyofanyika jana ikiwa na Manaibu wa wawili wa Maliasili na Utalii pamoja na wa TAMISEMI.Mkuu wa wilaya ya Morogoro akizungumza na wananchi waliovamia eneo la Mkesa lililopo ndani ya Jumuiya Hifadhi ya Wanyamapori ya JUKUMU iliyopo Morogoro vijijini wakati walipofanya ziara akiwa ameongozana na Manaibu wawili wa Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga pamoja na Naibu Waziri wa TAMISEMI, Joseph Kakunda wakati walipotembelea eneo hilo kwa lengo la kuwasikiliza wananchi hao na kujionea uharibifu unaoendelea katika .


Naibu Waziri wa TAMISEMI, Joseph Kakunda (wa pili kulia akiwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga ( wa kwanza kulia) pamoja na na Mkuu wa wilaya ya Morogoro,Regina Chonjo ( wa pili kushoto) wakimsikiliza miongoni mwa wananachi aliyedai kuwa yeye ni mkazi halali katika eneo hilo la Mkesa liliopo ndani ya Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori ya JUKUMU wakati wa ziara iliyofanyika jana kwa ajili ya kuwasikiliza wananchi hao na kujionea uharibifu unaoendelea katika .Baadhi wananchi wakiwasilikiliza Manaibu Waziri katika mkutano uliofanyiak jana katika eneo la Mkesa lililopo ndani ya Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori ya JUKUMU iliyopo Morogoro vijijini wakati wakati wa ziara kutembelea eneo hilo kwa lengo la kuwasikiliza wananchi hao na kujionea uharibifu unaoendelea katika .Naye Mwenyekiti wa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori ya JUKUMU, Shaban Kolahili akisalimia na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga wakati Naibu Waziri huyo alipowasili katika kijiji cha Mbwade akiwa ameongozana naNaibu Waziri wa Tamisemi, Joseph Kakunda.
( PICHA ZOTE NA LUSUNGU HELELA- MNRT


Serikali kupitia Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii na wa TAMISEMI imetoa siku saba kwa wananchi waliovamia kwa kuendesha maisha yao na kufanya shughuli za kilimo pamoja na kulisha mifugo ndani ya Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori ya JUKUMU iliyopo katika Halmashuri ya Morogoro vijijini kuondoka katika hifadhi hiyo.

Hali hiyo inafuatia baada ya wananchi hao kwenda mjini Dodoma kuonana na Waziri Mkuu, Kassimu Majaliwa na kumuelezea malalamiko yao kuwa wao ni wakazi halali katika eneo hilo lakini hata hivyo Mkuu wa Wilaya ya hiyo, Regina Chonjo amekuwa akiwalazimisha kuondoka.

Kufuatia hali hiyo , Waziri Mkuu K Majaliwa alimuagiza Waziri wa Maliasili na Utalii pamoja na Waziri wa TAMISEMI kwenda huko kwa ajili ya kushughulikia tatizo hilo ambapo Mawaziri hao kutokana na kubwana na majukumu mengine waliwaagiza Manaibu Waziri wao kutembelea eneo. .

Katika ziara hiyo, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga pamoja na Naibu Waziri wa TAMISEMI, Joseph Kakunda jana walitembelea eneo hilo na kujionea uharibifu unaoendelea.Katika ziarz hiyo Manaibu Waziri hao walizungumza na wananchi hao kwa kumtaka mwananchi yeyote mwenye nyaraka halali za kuishi katika eneo hilo aziwasilishe katika mkutano huo lakini hata hivyo hakuna mwananchi yeyote aliyeziwasilisha

Kutokana na wananchi hao kukiri kuishi kinyume na sheria katika eneo hilo la Hifadhi, Wananchi hao waliowaomba viongozi hao wapewe muda ili waweze kutafuta sehemu ya kuhamia kwa vile hawana sehemu ya kwenda,Kulingana uharibifu mkubwa waliojionea katika eneo hilo hali ya mazingira, Mnaaibu Waziri hao waliweza kuagiza mambo yafuatayo huyo. Kama.

Manaibu Waziri hao waliagiza kuwa materekta yote yatakayoonekana katika eneo hilo la hifadhi baada ya siku saba kupita yataifishwe.Pia, Waliagiza kuwa yakamatwe na hatimaye kupigwa mnada kwa mujibu wa sheria kwa mifugo yote itakayooneka katika eneo hilo la hifadhi.Aidha, Waliagiza kuwa mwananchi yeyote atakayekutwa ndani ya hifadhi hiyo baada ya siku saba kuwa atakamatwa na kufunguliwa mashtaka kwa kosa la kuvamia hifadhi.

Awali, Mkuu wa Wilaya hiyo, Regina Chonjo aliwaeleza Manaibu Waziri hao kuwa wananchi hao wamekuwa wakilima na kuchunga mifugo katika maeneo hayo hali iliyopelekea wanyamapori katika maeneo hayo kuhama.Naye Mwenyekiti wa Jumuiya ya JUKUMU, Shaban Kolahili ameiomba Wizara ya Maliasili na Utalii iwasaidie kuhakikisha kuwa hifadhi hhiyo inalindwa ili kuzuia vitendo vya ujangili na uvamizi unaoendelea ili kuwavutia wawekezaji ili hatimaye iweze kujitegemea.

Wananchi wa eneo hilo mnamo mwaka 2010 walituma maombi kwa Wizara ya Maliasili na Utalii ya kuomba wasaidiwe katika kulihifadhi eneo hilo ambalo hutumiwa na wanyapori kupimzika na kuzaliana

No comments: