Tuesday, February 6, 2018

wanahabari wapewa somo USIMAMIZI WA MABENKI NA TAASISI ZA FEDHA mkoani Mtwara

1
 Meneja Usimamizi wa Mabenki (BOT), Eliamringi Mandari akiwasilisha mada ya Usimamizi wa shughuli za Mabenki na Taasisi za Fedha katika semina ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali inayofanyika kwenye ukumbi wa (BoT) mkoani Mtwara, ambapo wanahabari wamepata ufafanuzi mbalimbali katika masuala ya ya shughuli zinazofanywa na mabenki katika biashara ya kifedha nchini Tanzania kwa kufuata sheria kanuni na taratibu zinazosimamiwa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT)
2
3
Eliamringi Mandari Meneja Usimamizi wa Mabenki (BoT) akifafanua mambo kadhaa wakati alipokuwa akiwasilisha mada ya Usimamizi wa shughuli za Mabenki.
4
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia mada katika semina hiyo inayoendelea kwa siku ya pili leo mjini Mtwara
5
Kushoto ni Vick Msima Meneja Msaidizi Idara ya Uhusiano wa Umma na Itifaki na Sadiki Nyanzowa Afisa Benki Mwandamizi Idara ya Udhamini wa Mikopo wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri ukumbini humo.
6
Bi. Zalia Mbeo Meneja Idara ya Uhusiano wa Umma na Itifaki (BOT) akitoa mchango wake katika semina hiyo kuhusu mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa.
7
Jonson Myella Mkurugenzi Tafiti za Uchumi (BoT) akichangia mada kuhusu Mabadiliko ya Mfumo mpya wa Kuandaa sera ya Fedha, Mapitio ya Maendeleo ya Uchumi nchini, Kikanda na Kimataifa Duniani iliyotolewa katika semina hiyo.
8
Meneja Msaidizi Idara ya Utafiti Dkt Suleiman Missango  akifafanua baadhi ya mambo kwa waandishi wa habari wakati wa semina hiyo
9
Baadhi ya wanahabari wakifuatilia kwa makini mada zilizokuwa zikitolewa.
10
Bi. Fatma Kimario Meneja Msaidizi Idara ya Udhamini na Mikopo akitoa mada kuhusu Mifuko ya Dhamana kwa Wajasiriamali na Dhamana za Serikali
11
Jonson Myella Mkurugenzi Tafiti za Uchumi (BOT), Bi. Zalia Mbeo Meneja Idara ya Uhusiano wa Umma na Itifaki (BOT) na Eliamringi Mandari Meneja Usimamizi wa Mabenki (BOT) wakifuatilia mambo mbalimbali wakati wa semina hiyo. 

No comments: