Wednesday, February 14, 2018

MAPOKEZI YA VIFAA VYA MATIBABU ZAHANATI YA KOMKONGA

 Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mh. Martine Shigela akizungumza na watumishi na wananchi wa Komkonga juu ya utunzaji wa vifaa hivyo na kupongeza uongozi wa Halmashuri kwa ujenzi wa maabara ndogo.
 Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh.Godwin Gondwe aki shukuru Rais kwa fedha alizozitoa na kufikia hatua ya kupokea Vifaa hivyo kwenye Zahanati ya Komkonga.
 Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Dk. Credeanus Mgimba akisoma taarifa ya vifaa vilivyonunuliwa.
 Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Mh. Ramadhani Diliwa akishukuru kwa kuletewa vifaa vitakavyosaidia kuboresha huduma ya Afya kwa wananchi wa Komkonga na kupunguza adha ya kufata hudduma hizo maeneo ya Mkata na Handeni.
 Baadhi ya Wananchi wa Komkonga waliofika kushuhudia makabidhiano.
 Mkurugenzi Mtendaji Bw. William Makufwe akisaidiana na mganga mkuu katikati na mkuu wa Mkoa kutoa hadubini tayari kwa kuikabidhi kwa viongozi wa Komkonga.
  Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mh. Martine Shigela(kulia) akikabidhi hadubini kwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Komkonga Bw.Omary Mngazija ikiwa ni moja ya kifaa kwaajili ya kuboresha huduma za Zahanati ya Komkonga.
 Mwenyekiti wa Kijiji cha Komkonga Bw.Omary Mngazija akishangilia kupokea hadubini ikiwa ni moja ya kifaa alichokabidhiwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mh. Martine Shigella mwenye suti ya kijivu kwaajili ya kuboresha huduma za Zahanati ya Komkonga.

No comments: