Sunday, October 29, 2017

UHAMIAJI WAFANYA USAFI NA KUTOA ZAWADI KWA WATOTO HOSPITALI YA TEMEKE

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Tanzania Dkt Anna Peter Makalala ametoa zawadi kwa akina mama na watoto waliokuwa wamelazwa katika hospitali ya Temeke sambamba na kufanya usafi wa mazingira kuzunguka eneo hilo.

Hatua hiyo imekuja ikiwa ni katika kutilia mkazo agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jhn Pombe Magufuli la kufanya usafi kila mwisho wa mwezi.
Kamishna Jenerali Anna alimkabidhi kijarida chenye masuala mbalimbali yanayohusu uhamiaji kwa mganga mkuu wa hospitali ya Temeke na kumtaka kushirikiana nao kwenye kutoa elimu kwa wagonjwa wanaofika hapo pale pindi wapatapo muda.

Mganga Mkuu wa hospitali ya Temeke Dr Amani Malima  amewashukuru sana kwa kuja kufanya usafi kwenye hospitali hiyo na kutoa zawadi kwa wakina mama na watoto huku akiwahakikishia kuwa watatoa elimu kwa wagonjwa wanaofika hapo kuhusiana na masuala ya uhamiaji.
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Tanzania Dkt. Anna Peter Makakala akifanya usafi katika Hosptali ya Temeke ikiwa ni katika kutilia mkazo agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Mafuguli ya kufanya usafi kila mwisho wa mwezi, usafi huo umefanyika kwa pamoja na wafanyakazi wa Uhamiaji Dar es Salaam Oktoba 28, 2017.


 

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Tanzania Dkt. Anna Peter Makakala pamoja na Mkuu wa Wilaya ya emeke Felix Lyaviva wakifanya usafi katika Hosptali ya Temeke ikiwa ni katika kutilia mkazo agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Mafuguli ya kufanya usafi kila mwisho wa mwezi, usafi huo umefanyika kwa pamoja na wafanyakazi wa Uhamiaji Dar es Salaam Oktoba 28, 2017.
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Tanzania Dkt. Anna Peter Makakala akijadiliana jambo na mkuu wa wilaya ya Temeke Felix Lyaviva baada ya kuwasili katika Hospitali ya Temeke kwa ajili ya kufanya usafi wa kila mwisho wa mwezi kutii agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Mafuguli.

Kamishna Jeenerali akitoa zawadi ya pampers na sabuni kwa wakina mama waliojifungua watoto walio chini ya muda wake (njiti) walipowatembelea kwenye Hospitali ya Temeke walipokwenda kufanya usafi wa kila mwisho wa mwezi.
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Tanzania Dkt. Anna Peter Makakala akitoa zawadi kwa wakina mama walipowatembelea kwenye Hospitali ya Temeke walipokwenda kufanya usafi wa kila mwisho wa mwezi.

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Tanzania Dkt. Anna Peter Makakala  akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumaliza kufanya usafi katika hospitali ya Temeke sambamba na kutoa zawadi kwa watoto na wakina mama waliokuwa wamelazwa kwenye hospitali hiyo, hilo ni katika kutilia mkazo agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Mafuguli ya kufanya usafi kila mwisho wa mwezi. Kushoto ni Mganga mKuu wa Hospitali ya Temeke Dr Amani Malima.
Kamishna Jenarali wa Uhamiaji Dkt Anna Peter Makakala akimkabishi jarida la Uhamiaji navifaa vya usafi kwa Mganga Mkuu wa Hospitali ya Temeke Dr Amani Malima  ikiwa ni siku ya usafi wa kila mwisho katika kutilia mkazo agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Mafuguli,  usafi huo umefanyika kwa pamoja na wafanyakazi wa Uhamiaji Dar es Salaam Oktoba 28, 2017.
Kamishna Jenarali wa Uhamiaji Dkt Anna Peter Makakala akisaini katika kitabu cha wageni.

Kamishna Jenarali wa Uhamiaji Dkt Anna Peter Makakala akijadiliana jambo na Mganga Mkuu wa Hospitali ya Temeke Dr Amani Malima pamoja na kufurahi pamoja baada ya kumaliza kufanya usafi,

Wafanyakazi wa uhamiaji wakiwa wanafanya usafi.
Kamishna Jenarali wa Uhamiaji Dkt Anna Peter Makakala na Mganga Mkuu wa Hospitali ya Temeke Dr Amani Malima wakiwa wanaelekea katika wodi za kina mama na watoto baada ya kumalizika kwa usafi.
Kamishna wa Uhamiaji- Pasi na Uraia, Gerald Kihinga akitoa zawadi kwa watoto waliolazwa kwenye Hospitali ya Temeke walipokwenda kufanya usafi wa kila mwisho wa mwezi.
Kamishna wa Usimamizi na Udhibiti wa Mipaka, Samwel Magweiga kitoa zawadi kwa watoto waliolazwa kwenye Hospitali ya Temeke walipokwenda kufanya usafi wa kila mwisho wa mwezi.
Kamishna wa Sheria Hanerole Manyanga akitoa pole na zawadi kwa mama aliyetoka kujifugua walipotembelea  Hospitali ya Temeke walipokwenda kufanya usafi wa kila mwisho wa mwezi.Picha zote na Zainab Nyamka.


No comments: