Friday, September 22, 2017

NJENDANI YA EFM REDIO YAWAFIKIA WAKAZI WA KINONDONI

Efm redio imewafikia wakazi wa Kinondoni siku ya leo ya tarehe 22/09/2017, kwa kupitia tamasha lake la Njendani lililofanyika katika uwanja wa Biafra – Kinondoni, ambapo watangazaji wa Kipindi cha Joto la Asubuhi, sports HQ, Uhondo na Ladha 3600 wakitangaza moja kwa moja katika kiwanja hicho pamoja na burudani mbalimbali za muziki ikiambapata na kampeni ya kuchangia damu ilioongozwa na Mpango wa Damu salama katika kuokoa maisha ya wagonjwa waliofanyiwa upasuaji wa moyo.
Mkuu wa wilaya ya Kinondoni mheshimiwa Ally Hapi (wa kwanza kulia) akiongea live na wakazi wake kupitia kipindi cha Joto la Asubuhi – Uwanja wa Biafra.
Mtangazaji wa Kipindi cha sports HQ, akizungumza na wakazi wa Kinondoni wakichambua michezo kwa pamoja.
Rdj x5 wa kipindi cha Sports Headquarters akifanya yake Biafra.
Sehemu ya mashabiki wakishuhudia matangazo hayo moja kwa moja.
Baadhi ya wakazi wa kinondoni wakichangia damu kwenye banda.
Mtangazaji wa kipindi cha Ladha 3600 pamoja na Yound D.
Msanii wa bongo fleva Yound D akiburudisha wakazi wa Kinondoni

No comments: