Barabara ya lami ya Kia-Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, ambayo imeshakabidhiwa kwa Serikali, inaendelea kuwa kwenye kipindi cha matazamio kwa muda wa mwaka mmoja.
Mradi huo wa barabara uliokabidhiwa serikali Mei 31 mwaka huu, mkandarasi wake anaendelea na kazi ndogo ndogo za ujenzi wa mifereji ya maji ya mvua, vivuko na vituo vya basi hasa eneo la Kairo.
Meneja wa wakala wa barabara nchini (Tanroads) mkoa wa Manyara, mhandisi Bashiri Rwesingisa aliyasema hayo wakati akisoma taarifa ya mradi huo kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Ujenzi) mhandisi Joseph Nyamhanga alipotembelea eneo hilo.
Mhandisi Rwesingisa alisema barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 27 iliyojengwa na kampuni ya China Henan International Cooperation Group (Chico) kwa gharama ya sh32.2 milioni, chini ya usimamizi wa ujenzi mhandisi mshauri M/s LEA International Ltd ya India kwa ushirikiano na kampuni ya DOCH Tanzania Ltd.
Alisema kazi zilizotekelezwa ni ujenzi wa kiwango cha lami urefu wa kilometa 27 ikijumuisha Kia hadi Mirerani, Mirerani hadi eneo la uwekezaji la (EPZ), barabara ielekeayo Arusha inayopitia Mbuguni, barabara ya kuingia na kutoka kituo cha mabasi Mirerani na mzunguko kiwanda cha TanzaniteOne.
"Ujenzi wa barabara hii umehusisha pia kujenga mifereji ya pembezoni mwa barabara kwenye maeneo ya mji, sehemu za kuvuka mifugo na sehemu za kuvushia huduma muhimu kama waya za simu na umeme," alisema mhandisi Rwesingisa.
Alisema mradi huo umekuwa na changamoto za migomo ya wafanyakazi, wananchi kugoma kuondoa mali zao ndani ya hifadhi ya barabara.
Alisema mipango ya baadaye ni kujenga kilometa 114 barabara kwa kiwango cha lami itakayounganisha eneo la EPZ na mji mdogo wa Orkesumet, makao makuu ya wilaya ya Simanjiro, kama ilivyoainishwa kwenye ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015.
Akizungumza baada ya kukagua mradi huo, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo anayeshughulikia ujenzi, mhandisi Joseph Nyamhanga alipongeza jitihada zilizofanyika kwa pande zote hadi barabara hiyo ikamalizika.
Mhandisi Nyamhanga alisema wakati wanasubiri barabara hiyo kuzinduliwa wakati inaendelea kutumika, watumiaji wanapaswa kufuata masharti ya matumizi ya barabara hiyo ili waitunze.
Aliitaka jamii ya eneo hilo ambao kwa muda mrefu walikuwa wanalilia utengenezwaji wa barabara na ndiyo wanufaika wa mradi huo, kuutunza vizuri kwani ni kwa ajili ya faida yao na vizazi vijavyo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Ujenzi) mhandisi Joseph Nyamhanga (katikati) akizungumza na viongozi wa wakala wa barabara nchini (Tanroads) Mkoa wa Manyara, alipotembelea eneo la mji mdogo wa Mirerani, (kushoto) ni meneja wa Tanroads Mkoani Manyara, mhandisi Bashiri Rwesingisa

Meneja wa Tanroads Mkoa wa Manyara, mhandisi Bashiri Rwesingisa (aliyevaa shati la maua) akimwelezea Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Ujenzi) Joseph Nyamhanga (kushoto kwake) juu ya barabara ya lami ya Kia - Mirerani, ambayo imemalizika inasubiri kufunguliwa.

1 comment:
PESA AU UTAJIRI MKUBWA WA MAJINI,, NDAGU NA PETE YA BAHATI,,
======= KUTANA NA MGANGA BINGWA WA TIBA ZA ASILI ,,BINGWA WA TIBA ZA MAPENZI ,,BIASHARA NA KUKUPA UTAJIRI MKUBWA WA MAJINI NA NDAGU,, SI MWENGINE NI DR.Mdiro
MAWASILIANO
WHATSAPP +255742162843
KWA WALIO NJE YA NCHI TUMIENI WHAT'S UP KWA MAWASILIANO
Malipo ni baada ya mafanikio
====Natibu magonjwa sugu kisukali presha kifafa nguvu za kiume uzazi chango ngiri busha ganzi miguu,,tumbo gesi,,maumivu ya mwili,,ndoto mbaya,,na kutafasri maana ya ndoto unazo ota ,, nk
===== Nasafisha nyota,,kutoa mikosi,,nuksi,,kutoa majini mabaya,,kutoa chuma ulete kwenye biashara,, kupandishwa nyota,, kupandishwa cheo,, kupata kazi,, kushinda kesi,,kulipa kisasi kwa ulicho fanyiwa nao wajisikie vibaya Kama wewe ilivyo jisikia,,nk
===== Kumrudisha mpenzi mchumba mume mke uliye tengana nae ,,au kakutelekeza,, kumshika mme wako au mpenzi wa mtu awe anakusaidia na kukutimizia mahitaji Kama NI mpenzi wako,, au Kama anakutaka awe anakupa pesa bila kumuomba ,,
===== Kumrudisha mke mme kwenye himaya yako tena kama mmeachana na unahitaji muwe pamoja au muishi wote Kama zamani,,au Kama humuitaji yeye unataka pesa zake tu pia atakusaidia hata bila kumpa pezi lako,,
=====Kumilikishwa Mali au utajiri mkubwa wa majini,, kupata utajiri mkubwa wa ndagu,,kupata utajiri mkubwa wa freemason,, kukupa utajiri mkubwa kuliko wengine utajiri wa Pete ya bahati ambayo itakuvutia mali pesa na itakupa mvuto mkubwa wa kupendwa na watu,,
===== Kukupa chuma ulete,,kukupandisha nyota ya uganga,, kukupa karama ya kumiliki uchawi,, kukupa nyota ya kushinda bahati nasibu au kamali,, kukupa kinga ya kiwaona wabaya ,, kuona matatizo yako,, kukupa mvuto mkubwa wa kuolewa au kuoa Kama unamchumba au huna kabisa yaani ajitokezee mwenyewe aseme anataka kukuoa au umuowe,,
===== NJOO NIKUHUDUMIE,, PIA NATIBU HATA UKIWA MBALI NAMI UWE MKOANI AU NCHI NYINGINE HUDUMA UTAIPATA KWA HARAKA NA UTAFANIKIWA KWA MDA MFUPI TU,,
====KWA UTAJIRI MKUBWA WA MAJINI
====KWA UTAJIRI MKUBWA
Post a Comment