Thursday, July 13, 2017

TAASISI YA MOYO JAKAYA KIKWETE (JKCI) KWA KUSHIRIKIANA NA TAASISI YA MADAKTARI AFRIKA YA NCHINI MAREKANI WAFANYA MATIBABU YA MOYO KWA WAGONJWA KWA KUWEKA KIFAA MAALUM

  Daktari Bingwa wa magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)  Peter Kisenge akizungumza na waandishi wa Habari kuhusu kambi maalum ya matibabu ya Moyo inayofanywa na Taasisi hiyo kwa kushirikiana na Taasisi ya Madaktari Afrika ya nchini Marekani kwa wagonjwa ambao mapigo yao ya moyo yako chini sana na hivyo kuwekewa kifaa maalum cha kurekebisha mapigo ili yawe sawa (kwa jina la kitaalamu Pacemaker) . Kushoto ni Daktari Bingwa na Magonjwa ya Moyo Mathew Sackett. Tangu kuanza kwa kambi hiyo mwanzoni wa juma hili jumla ya wagonjwa 20 wameshapatiwa matibabu kati ya hao nane wamewekewa Pacemaker na wengine wanne wanatarajia kuwekewa leo na kesho.  
 Daktari Bingwa wa magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Madaktari Afrika  ya Nchini Marekani Mathew Sackett akizungumza na waandishi wa habari  na  kuipongeza Serikali kwa uwekezaji mkubwa ulioufanya katika matibabu ya Moyo wakati wa kambi maalum ya matibabu ya Moyo inayofanywa na Taasisi hiyo kwa kushirikiana na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete kwa wagonjwa ambao mapigo yao ya moyo yako chini sana na hivyo kuwekewa kifaa maalum cha kurekebisha mapigo ili yawe sawa (kwa jina la kitaalamu Pacemaker). Kushoto ni Daktari Bingwa na Magonjwa ya Moyo Peter Kisenge. Tangu kuanza kwa kambi hiyo mwanzoni wa juma hili jumla ya wagonjwa 20 wameshapatiwa matibabu kati ya hao nane wameshawekewa Pacemaker na wengine wanne wanatarajia kuwekewa leo na kesho.  
 Daktari Bingwa wa magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Peter Kisenge akiwaonyesha waandishi wa Habari jina la Dkt.  Mathew Sackett wa  Taasisi ya  Madaktari Afrika  ya Nchini Marekani lilivyoandika katika nguo yake wakati wa mkutano baina yao uliozungumzia kambi maalum ya matibabu ya Moyo inayoendelea katika Taasisi hiyo  kwa wagonjwa ambao mapigo yao ya moyo yako chini sana na hivyo kuwekewa kifaa maalum cha kuyarekebisha ili yawe sawa (kwa jina la kitaalamu Pacemaker) .
 Daktari Bingwa wa magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Tulizo Shemu  na mwenzake kutoka Taasisi ya Madaktari Afrika  ya Nchini Marekani Mathew Sackett wakimwekea mgonjwa kifaa maalum cha kurekebisha  mapigo ya moyo ili yawe sawa (kwa jina la kitaalamu Pacemaker) kifaa hicho huwekewa wagonjwa ambao mapigo yao ya moyo yako chini sana. Tangu kuanza kwa kambi maalum ya matibabu ya moyo jumla ya wagonjwa nane wameshawekewa Pacemaker na wengine wanne wanatarajia kuwekewa leo na kesho.  
 Wataalamu wa Magonjwa ya  Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)  na wenzao wa Taasisi ya Madaktari Afrika  ya Nchini Marekani wakimwekea mgonjwa kifaa maalum cha kurekebisha  mapigo ya moyo ili yawe sawa (kwa jina la kitaalamu Pacemaker) kifaa hicho huwekewa wagonjwa ambao mapigo yao ya moyo yako chini sana.

Picha na JKCI

No comments: