Tuesday, June 6, 2017

ZIARA YA BULEMBO YAVUNA WANACHAMA MACHACHARI WA CHADEMA NGARA


Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akipokea kadia kutoka kwa Niniani Bakhari, aliyekuwa Kada machachari wa Chadema, ambaye alitangaza kuhamia CCM wakati wa mkutano wa ndani uliofayika leo katika mji mdogo wa Ngara mkoani Kagera
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akimpongeza Ninian kwa uamuzi wake wa kurejea CCM
Baadhi washiriki wa kikao wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM wilaya ya Ngara, Mabalozi na viongozi kutoka Jumuia zote za CCM wakimpongeza Ninian kwa furaha baada ya kukabidhi kadi yake ya Chadema kwa Bulembo wakati wa kikao hicho
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akisikiliza kwa makini wakati Ninian alipokuwa akieleza yake ya moyoni, alisema, aliamua kwenda Chadema baada ya kuona CCM ya wakati huo ina mambo mengi ya hovyo, lakini sasa ameamua kurejea baada ya kuona kuwa Mwenyekiti wa CCM Rais Dk Magufuli amekisafika Chama
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abadalla akitoa kadi kwa mmoja wa wanachama hao wapya 71 waliohamia CCM wakati wa kikao hicho
Wengine waliamua kumkabidhi Ahaj Bulembo hadi bendera ya Chadema baada ya kulifunga tawi lao
Baadhi ya kadi za Chadema zilizorejeshwa kwa Alhaj Bulembo
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo (kushoto) akishiriki wakati wachama wapya 71waliohamia CCM wakitokea Chadema, walipokuwa wakila kiapocha Mwana CCM, baada ya kukabidhiwa kadi za Chama kwenye kikao hicho,leo
Ukumbi ukilipuka kwa nderemo na vifijo baada ya wanachama hao wapya kulakiapo
Wajumbe wakiwa ukumbini kuendelea na kikao baada ya zoezi hilo la kupokea wanachama wapya 71 wa CCM kutoka Chadema
Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Kagera Oliva Semgurika akisalimia baada ya kutambulishwa kwenye kikao hicho
Mwenyekitiwa CCM wilaya ya Ngara Hudson Bagege akifunguakikao hicho. Kulia ni Alhaj Bulembo
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kagera Constansia Buhiye akimkaribisha Alhaj Bulembo kuzungumza katika kikao hicho
Mzee Said ramadhani Sudi akimkabidhi zawadi Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo kabla ya kuzungumza katika kikao hicho
Mwenyekiti wa Kamati ya mapokezi Jason Bahema akikabidhi zawadi maalum ya kimila kwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaji Abdallah Bulembo kabla ya kuzungumza katika kikao hicho
Mjumbe wa kamati Kuu ya CCM, Alhajj Abdallah Bulembo akizungumz na wajumbe wakati wa kikao hicho cha Wajumbwa wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Ngara, Mabalozi, viongozi wa Jumuia zote za CCM na watendaji wa Serikali, leo
Vijana wa UVCCM wakimvisha skafu mjumbea wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdalla Bulembo wakati wa mapokezi kwenye Ofisi ya CCM Wilaya ya Ngara mkoani Kagera leo
Vijanawa UVCCM wakionyesha ukakamavu wao wakati wa paredi la mapokezi
Vijana wa UVCCM na Skauti wakifanya manjonjo yao ilimradi kunogesha mapokezi ya Mjumbea wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulebo alipowasili Ofis ya CCM Wilaya ya Ngara mkoani Kagera leo
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akiwasalimia baadhi ya viongozi alipowasili kweneye Ofisi ya CCM Wilaya ya Ngara mkoani Kagera,leo. Kushoto ni Katibu wa CCM wa Wilaya hiyo Mwajemi Balagama
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akiwa na viongozi wengine meza kuu alipowasili ukumbini baada ya kutoka Ofisi ya CCM Wilaya ya Ngara mkoani Kagera leo
Mjumbe wa NEC Ngara, Issa Saama akisalimia baada ya kutambulishwa
Wazee maarufu walioalikwa kwenye kikao hicho wakiwa ukumbini. PICHA: BASHIR NKOROMO

No comments: