Tuesday, April 4, 2017

MASHABIKI WAJITOKEZA KUWAPOKEA TIMU YA SIMBA MKOANI GEITA

Timu ya Simba imetua Mkoani Geita  ikitokea Kagera  kwaajili ya kuweka kambi ya siku nne kujiandaa na mchezo Dhidi ya Mbao Fc na Toto zote za Jijini Mwanza Mchezo ambayo itapigwa kwenye Dimba la CCM Kirumba.
Ikiwa Mkoani Geita Simba inatarajia kucheza mchezo wa Kirafiki na timu ya Geita Gold Sport Siku ya Jumatano mechi ambayo itachezwa kwenye  uwanja wa shule ya msingi  Waja.
Kwa Mujibu wa Nahodha wa Kikosi cha Simba Jonas Mkude amewataka mashabiki kuendelea kuhishabikia timu hiyo na kwamba wataakikisha wanafanya vizuri kwenye mchezo  ambayo imebakia.
Hata Hivyo kwa upande wake Mussa Hassan Mgosi ameelezea kuwa wamejipanga vizuri kukutana na Mbao Fc siku ya Jumatatu na kwamba hawatawaangusha mashabiki wao na ni vyema wakasahau ambayo yamepita na  mashabiki wakashikamana na timu ili kuweza kutimiza malengo ambayo wamejiwekea.



IMEANDALIWA NA JOEL MADUKA WA MADUKA ONLINE BLOG.

No comments: