Thursday, February 16, 2017

Shule ya Msingi ya Wavulana ya Almuntazir yawatuza wanafunzi waliofanya vizuri katika mitihani yao

Mkurugenzi wa Habari na Elimu ya Mpiga Kura wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bi. Giveness Aswile (kulia) akisalimiana na Mkuu wa Shule ya Msingi ya Wavulana ya Almuntazir   Bi. Shaimuna Chandro wakati alipowasili shuleni hapo kwenye Sherehe ya Kuwazawadia Wanafunzi wa shule hiyo waliofanya vizuri katika mitihani yao leo jijini Dar es Salaam.Katikati ni Naibu Mkuu wa shule hiyo Bi. Zai Abdi.

 Mkurugenzi wa Habari na Elimu ya Mpiga Kura wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bi. Giveness Aswile akizungumza na Afisa Mtendaji Mkuu wa shule hiyo Bw. Mahmood Ladak.
 Mkuu wa Shule ya Msingi ya Wavulana ya Almuntazir   Bi. Shaimuna Chandro akitoa neno la ukaribisho.
 Mwanafunzi Ali Askher Walji akifurahia zawadi kutoka kwa Mgeni Rasmi, Mkurugenzi wa Habari na Elimu ya Mpiga Kura wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bi. Giveness Aswile baada ya kufanya vizuri katika Mitihani ya Taifa ya Daraja la 7 ya mwaka 2016.
 Mkurugenzi wa Habari na Elimu ya Mpiga Kura wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bi. Giveness Aswile, akiwa kwenye picha ya pamoja na wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Wavulana ya Almuntazir waliofanya katika Mitihani ya Taifa ya Daraja la 7 ya mwaka 2016.
Dokta Faraji Lydenge kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili akiwa kwenye picha ya pamoja na wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Wavulana ya Almuntazir waliofanya katika mitihani ya Taifa ya daraja la 4 ya mwaka 2016.
 Afisa Mtendaji Mkuu wa Shule ya Msingi ya Wavulana ya Almuntazir Bw. Mahmood Ladak akiwa kwenye picha ya pamoja na wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Wavulana ya Almuntazir waliofanya katika Mitihani ya Taifa ya Daraja la 3 ya mwaka 2016.
  Sheikh Ali Azim Shiraz akimbusu mmoja wa wanafunzi wa daraja la awali wa Shule ya Msingi ya Wavulana ya Almuntazir, baada ya kumpatia zawadi.
 Sheikh Ali Azim Shiraz akiwa kwenye picha ya pamoja na wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Wavulana ya Almuntazir waliofanya vizuri katika mitihani ya Taifa ya Daraja la 1 ya mwaka 2016.
 Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Wavulana ya Almuntazir, wakishuhudia utoaji wa zawadi.
 Baadhi ya wazazi wakifuatilia utoaji wa zawadi.
 Afisa Mtendaji Mkuu wa Shule ya Msingi ya Wavulana ya Almuntazir Bw. Mahmood Ladak, akimkabidhi zawadi mgeni rasmi Mkurugenzi wa Habari na Elimu ya Mpiga Kura wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bi. Giveness Aswile.Katikati ni Dokta Faraji Lydenge kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, akishuhudia.
Mgeni rasmi Mkurugenzi wa Habari na Elimu ya Mpiga Kura wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bi. Giveness Aswile, akiangalia moja ya vitabu vilivyoko kwenye Maktaba ya shule ya Msingi ya Wavulana ya Almuntazir wakati alipotembea maeneo mbalimbali ya shule hiyo akiwa na Naibu Mkuu wa shule hiyo Bi. Zai Abdi.

Mkurugenzi wa Habari na Elimu ya Mpiga Kura wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bi. Giveness Aswile (wa pili kushoto) akibadilishana mawazo na viongozi wa Shule ya Msingi ya Wavulana ya Almuntazir hiyo.Kulia ni Afisa Mtendaji Mkuu Bw. Mahmood Ladak, Mkuu wa Shule Bi. Shaimuna Chandro na kushoto ni Naibu Mkuu wa shule hiyo Bi. Zai Abdi.


    Picha na Hussein Makame, NEC

    No comments: