Thursday, December 15, 2016

KIGOGO WA CHADEMA NA ACT-WAZALENDO AHAMIA CCM NA WAFUASI WAKE

Aliyekuwa Mratibu wa Kanda ya Pwani wa Chadema, na Baadaye Mratibu wa Kampeni wa ACT Wazalendo wakati wa uchaguzi Mkuu ulipita, Nixon Tugara akikabidhiwa kadi ya CCM na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana alipoamua kuhamia CCM wakati wa uzinduzi wa jengo la Kitegauchumi la CCM, Upanga jijini Dar es Salaam, leo.
Nixon Tugara akifurahia kadi yake ya CCM baada ya kukabidhiwa na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana wakati wa hafla ya uzinduzi wa jengo la Kitegauchumi la CCM, Upanga jijini Dar es Salaam, leo
Tugara ambaye ni miongozi mwa watu waliosimamia ujenzi wa jengo hilo la Kitegauchumi akizungumza yaliyomsibu hadi kuhamia CCM, kutoka ACT Wazalendo na Chadema.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdultrahman Kinana akimshukuru Tugara kwa kuwa miongoni mwa viongozi waliosaidia katika kufanikisha ujenzi wa jengo la Kitegauchumi la CCM, lililopo Upanga jijini Dar es Salaam, ambalo amelizindua leo. Kulia ni Katibu wa NEC, Uchumi na Fedha, Zakia Meghji.
Tugara akimshukuru Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimpokea mwanachama mpya aliyejiunga na CCM kutokea Chadema, wakati wa hafla hiyo.

No comments: