Friday, December 23, 2016

KAPU LA SIKUKUU LA EFM RADIO KWA WASIKILIZAJI WAKE

 Kwa mara nyingine tena EFM redio imegawa makapu ya sikukuu leo tarehe 23/12/2016 kwa wasikilizaji wake ikiwa kama ishara ya kusheherekea kwa pamoja katika msimu huu wa sikukuu. Efm redio hugawa makapu hayo katika msimu wa sikukuu ya Krismasi na Iddi kwa takribani mwaka wa tatu sasa.  
Mwaka huu EFM redio ikishirikiana na wadau wake Dstv wamewakabidhi makapu kwa watu 24  baada ya kuibuka na ushindi kwa kufanikiwa kujibu maswali yaliokuwa yakiulizwa katika vipindi vya redio kuhusiana na maudhui ya redio pamoja na wadhamini hao.
Akiongea Mkurugenzi Mkuu wa EFM redio Francis Siza, “Tunapenda kuwathamini na kuwashukuru  wasikilizaji wetu kwa namna moja au nyingine kwani wao ndio mchango mkubwa sana kwetu hivyo zawadi hizi za makapu ni shukrani yetu kwao”. 
 Makapu ya sikukuu yakiwa yamesheheni mazagazaga kibao pamoja na kingamuzi cha DSTV
 Makapu ya sikukuu yakiwa yamesheheni mazagazaga kibao pamoja na kingamuzi cha DSTV
 Mkuu wa wilaya ya Ilala Sofia Mjema, akipeana mkono na Muigizaji wa Tamthilia Irene Paul katika uzinduzi wa ugawaji wa makapu hayo, wakiwa pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Efm redio Francis Ciza, Kutoka kulia ni Mboto Haji (Muigizaji) Pamoja na Meneja Masoko Dstv Bwana Alpha Mria.
  Meneja Masoko Dstv Bw. Alpha Mria kutoka kushoto  akimkabidhi mshindi wa kapu la sikukuu wengine katika picha ni waigizaji wa tamthiria za Dstv  Haji Salum (mboto) na Irene paul  pamoja na Swebe Santana Mtangazaji wa kipindi cha uhondo, efm redio
 Washindi wakapu wa sikukuu wakifurahi kwa pamoja
 Makapu ya sikukuu kwa wasikilizaji wa EFM
 Zawadi kwa msikilizaji
  Mkuu wa wilaya ya Ilala Sofia Mjema akiwapongeza EFM na DSTV kwa hatua hii ya aina yake
 Makapu ya sikukuu kwa wasikilizaji wa EFM




 Mazagazaga kibao

   Meneja Masoko Dstv Bw. Alpha Mria kutoka kushoto  akimkabidhi mshindi wa kapu la sikukuu wengine katika picha ni waigizaji wa tamthiria za Dstv  Haji Salum (mboto) na Irene paul  pamoja na Swebe Santana Mtangazaji wa kipindi cha uhondo, EFM redio

1 comment:

Anonymous said...

Nivizur ila no: hamtaj natumeandaa majibu,toeni mikoa yote