Monday, October 24, 2016

SHEREHE YA KUMUAGA ALIEKUWA MKURUGENZI MWENDESHAJI WA SHIRIKA LA BIASHARA LA TAIFA ZANZIBAR (ZSTC)

mkul1
Katibu Muhtasi wa Shirika la Biashara la Taifa Zanzibar (ZSTC) Fatma Saadat akimvisha Koja la Mauwa aliekuwa Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika hilo Bi. Mwanahija Almasi Ali katika sherehe ya kumuaga iliyofanyika eneo tengefu Saateni Mjini Zanzibar. Bi Mwanahija kwa sasa ni Mhasibu Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
mkul2
Wanafunzi wa Madrasa wakisoma Dua maalum ya kumuaga aliekuwa Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika la Biasha la Taifa Zanzibar (ZSTC)Bi. Mwanahija Almasi Ali iliyofanyika eneo tengefu Saateni Mjini Zanzibar.
mkul3
Wafanyakazi  wa Shirika la Biashara la Taifa Zanzibar (ZSTC) na wageni walikwa wakiongozwa na Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika hilo Dkt. Said Seif Mzee (alievaa shati jekundu) wakiitikia Duwa maalum ya kumuaga aliekuwa Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika hilo.
mkul4
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya ZSTC Kassim Maalim Suleiman akimkabidhi Cheti cha utendaji kazi aliyekuwa Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika la (ZSTC) Bi. Mwanahija Almasi Ali katika sherehe iliyofanyika eneo tengefu Saateni Mjini Zanzibar. (Katikati) Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika hilo Dkt. Said Seif Mzee.
mkul5
Mgeni rasmin aliekuwa Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika la Biasha la Taifa Zanzibar (ZSTC)Bi. Mwanahija Almasi Ali akizungumza na wafanyakazi na wageni waalikwa katika sherehe aliyoandaliwa na wafanyakazi wa Shirika hilo.
mkul6

Mgeni rasmin (katikati) waliokaa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa wa Shirika hilo.Picha na Makame Mshenga/Maelezo Zanzibar.

No comments: