Monday, May 16, 2016

KAMPUNI YA BIA YA SERENGETI YAZINDUA PROMOSHENI YA MILIONI 100 NA TUSKER - FANYA KWELI UWINI.


MILIONI MIA MOJA (100M) KUSHINDANIWA KUPITIA BIA YA TUSKER LAGER

Dar es Salaam 16 May, 2016; Kwa kutambua thamani ya wateja wake Kampuni ya Bia ya Serengeti imezindua promosheni maalum ya kutoa shukrani kwa wateja wake ambao ni watumiaji wa bia ya Tusker Lager, ambapo watajishindia pesa taslimu Milioni 1 kwa washindi kumi (10) kila wiki kwa muda wa wiki kumi na kufanya jumla ya Milioni mia kushindaniwa na Zawadi za bia kibao. 

Uzinduzi huo uliofanyika kwa aina yake katika mikoa miwili tofauti kwa wakati mmoja, mikoa hiyo ni Dar es Salaam na Kilimanjaro hii ni tofauti na ilivyozoeleka kwani uzinduzi hufanyika Katika sehemu moja tu. Promosheni hii imeanza rasmi leo na itaendeshwa kwa muda wa wiki kumi. Uzinduzi ulipambwa na maonyesho ya barabarani, msafara ulianzia kiwandani Chang’ombe na kuishia Fyatanga Bar Tegeta huku ukipokelewa na shamrashamra za aina mbalimbali.

Hii si mara ya kwanza kwa Kampuni ya Bia ya Serengeti kuendesha promosheni kama hii kwani ni wengi wameshanufaika kupitia promosheni mbalimbali za mfumo huu na hata kubadili maisha ya watumiaji wa bidhaa zake kwa kiasi kikubwa. Kupitia bia ya Tusker Lager Kampuni hiyo inaendeleza kile kilichokuwepo cha kurudisha fadhila na kutoa shukrani kwa watumiaji wa bia ya Tusker Lager. 

Wateja wanaweza kujaribu mara nyingi kadiri wawezavyo. Ili kuwa mshindi wa Tusker milionea, washiriki wataweza kujishindia pesa taslimu kupitia droo zitakazochezeshwa kila wiki. Unapofungua bia ya Tusker Lager (500ml) chini ya kizibo ukapata kizibo cha Tusker Milionea hii inakuingiza Katika droo ya kupata Milioni moja, au unaweza kupata Bia ya Zawadi – hii inampa mteja wa Tusker bia ya bure papo hapo alipohudumiwa na ikiwa utapata jaribu tena utaendelea kuburudika kistaarabu ili kuongeza nafasi yako yako kuibuka mshindi. Promosheni hii itasimamiwa na Bodi ya Michezo ya Kubahatisha nchini ili kuleta ufanisi zaidi.

Akiongea wakati wa uzinduzi huo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Bia ya Serengeti alisema promosheni hii si kwa ajili ya kuongeza mauzo tu bali ni kutoa shukrani kwa wateja wao kwa kuwaunga mkono na kusapoti bidhaa zao.

“Kupitia Bia ya Tusker Lager wateja wetu wanaweza kujishindia shilingi Milioni Moja kwa washindi kumi kila wiki kwa muda wa wiki kumi ambao tutawapata kutoka Katika droo za kila wiki nchi nzima. Lengo kubwa ni kumwezesha mnywaji na mdau wa bia ya Tusker kufanya kweli kupitia bia yetu ya Tusker Lager”aliongeza Bi. Cesear Mloka.

Kwa upande wa Mkoa wa Kilimanjaro uzinduzi ulifanyika katika manispaa ya Moshi huku ukihudhuriwa na wageni mbalimbali wakiwemo wasambazaji na baadhi ya wafanyakazi wa Kampuni ya Bia ya Serengeti na wana habari. Akizungumza katika uzinduzi huo Mkurugenzi wa Mauzo bwana Alain Tsageutayo ambae alisema “Wakati wa kuchagua zawadi za kushindaniwa pesa taslimu ilichukua nafasi ya juu – na kiwango cha Milioni moja kinaweza kusaidia kujikwamua kwa namna moja au nyingine. Wateja wetu ndio wametufikisha hapa tulipo basi nasi hatuna budi kurudisha shukrani kwako mtumiaji wa bia yetu ya Tusker Lager na ndio maana tunatoa kwa washindi 100, milioni 1 kila mmoja katika kipindi cha promosheni.”

Milioni 100 na Tusker Lager - Fanya kweli na Uwini itadumu kwa muda wa wiki kumi nchi nzima. Kwa washiriki wa Tusker milionea wataweza kushuhudia droo zitakazofanyika kila ijumaa na kuonyeshwa kwenye runinga. Washindi watakaopatikana watakabidhiwa pesa zao kila ijumaa inayofuatia kwenye sherehe maalum ya promosheni.

Baadhi ya Wafanyakazi wa Kampuni ya Bia ya Serengeti katika picha ya pamoja wakishangilia uzinduzi wa kampeni ya Tusker Fanya Kweli Uwini kiwandani hapo na baadae kufuatiwa na maonesho ya barabarani jijini Dar es Salaam.
Vijana wa amsha amsha wakiburudisha barabarani katika jiji la Dar es Salaam.
Msafara maalum ukielekea katika Bar ya Fyatanga tayari kwa uzinduzi rasmi kwa wateja wa bia ya Tusker
Mkurugenzi wa Masoko Cesear Mloka (katikati) pamoja na wafanyakazi wengine wa SBL wakishangilia uzinduzi rasmi wa Tusker Fanya Kweli Uwini kwa wateja uliofanyika katika Bar ya Fyatanga nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
Meneja Mauzo wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Kanda ya Kaskazini Amoni Kabagi(kushoto) akieleza jambo kwa wageni waalikwa (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa 'Tusker Fanya Kweli Uwini' mjini Moshi, pamoja nae ni Meneja wa Mauzo wa Kilimanjaro, Godwin Seleli.
Burudani ikiendelea katika uzinduzi jijini Dar tusker UTC Launch dance - Burudani ikiendelea katika bar ya Oriento Mjengo, Mjini Moshi

No comments: