Friday, February 20, 2015

FUTURE STARS KUSHIRIKI MICHUANO JIJINI KAMPALA


Kituo cha kukuza soka la vijana cha Future Stars Academy(FSA) cha jijini Arusha  kinataraji kushiriki  katika  michuano ya Uganda Junior League inayotaraji kutimua vumbi jijini Kampala mnamo Aprili 24 hadi 26 mwaka huu.


Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mkurugenzi na mwanzilishi wa kituo hicho,Alfred  Itaeli alisema kuwa kituo chao kinataraji kupeleka timu ya watoto ya U-15 katika michuano hiyo kwa lengo la kushindana na kisha kunyakua ubingwa.


Alisema kuwa  ushiriki wao umefuatia kupitia mwaliko walioupata kutoka nchini Uganda kutokana na  nchi hiyo kutambua jitihada za kituo chao za kukuza soka la vijana hapa nchini pamoja na ndani ya jumuiya ya Afrika Mashariki.


Hatahivyo,mkurugenzi huyo alisisitiza ya kwamba katika kuhakikisha wanashriki mashindano hayo kituo chao kimeanza mkakati wa kusaka fedha za nauli na matumizi wakiwa nchini wakati wote wa mashindano kwa kusaka udhamini kutoka kwa wadu mbalimbali wa soka mkoani Arusha na nchini kwa ujumla.
Alisema kuwa wameanzisha tamasha la soka liitwalo “Quiz Night” ambalo linataraji kufanyika mnamo febuari 28 mwaka huu katika viwanja vya TGT jijini Arusha ambapo wanataraji kukusanya fedha za ushiriki katika tamasha hilo ili ziweze kuwasaidia katika safari yao nchini Uganda.


Itaeli,aliwataka wadau mbalimbali wa soka mkoani Arusha ana nchini kwa ujumla kuwapa sapoti katika safari yao kwa kuwa hadi sasa wamekusanya kiasi cha sh,2 milioni  ambapo kwa safari yote nchini humo kinahitajika kiasi cha sh,7 milioni.

HABARI kwahisani ya libeneke la kaskazini blog

No comments: