Wednesday, May 7, 2014

VIONGOZI WA DINI WAWASILI KUTOKA NCHINI THAILAND

Baadhi ya viongozi wa dini kutoka katika Mikoa ya Lindi na Mtwara wakiwasili katika Uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNIA) kutokea nchini Thailand. Viongozi hao walifanya ziara nchini humo kwa ajili ya kujifunza na kupata uzoefu wa uendelezaji wa sekta ya gesi.
Viongozi wa dini wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuwasili Uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNIA) kutokea nchini Thailand.
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Baraza la Waislamu Tanzania (BAKWATA) Bw. Mohamed Sinani akielezea jinsi nchi ya Thailand ilivyopiga hatua kimaendeleo kutokana na mchango wa sekta ya gesi.
Badhi ya viongozi wa dini wakiwasili katika Uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNIA) kutokea nchini Thailand.
Padri Dkt. Aidan Msafiri ambaye ni Mhadhiri Mwandamizi kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino tawi la Mtwara akizungumza na waandishi wa habari katika Uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNIA) mara baada ya kuwasili kutoka nchini Thailand.
Makamu wa Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana Tanzania kutoka dayosisi ya Newala Bw. Oscar Stephen akizungumza kwa niaba ya viongozi wenzake uzoefu walioupata walipokuwa nchini Thailand hususan katika sekta ya gesi.
Shehe Mkuu kutoka Mkoa wa Mtwara Bw. Nurdin Abdalah akiwaeleza waandishi wa habari jinsi wananchi wa Thailand walivyoweza kutunza vyema rasilimali yao ya gesi ikiwa ni pamoja na usimamizi wa sekta nyingine.
Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Mhe. Abdallah Hamis Ulega akizungumza na waandishi wa habari jinsi wananchi wa Thailand walivyonufaika na rasilimali ya gesi.

No comments: