Thursday, August 22, 2013

Mhe. Membe apokea Magari ya msaada ya kubebea wagonjwa kutoka Korea Kusini

Magari ya wagonjwa yalitolewa na Korea Kusini kwa ajili ya majimbo ya vituo vya afya vinne vya majimbo ya Ruangwa na Nchinga Mkoani Lindi.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) akionyesha funguo ya moja ya magari ya msaada mara baada ya kukabidhiwa rasmi na Balozi wa Korea Kusini nchini Tanzania, Mhe. Chung IL.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) akipungia mkono watu waliohudhuria hafla ya makabidhiano huku akiendesha moja ya magari ya msaada kutoka Korea Kusini. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa pili kutoka kushoto akimpa funguo Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Serikali za Mitaa na Tawala za Mikoa), Mhe. Kassim Majaliwa (Mb) ambaye jimbo lake la Ruangwa limepatiwa magari mawili.
Mhe. Kassim Majaliwa akifungua mlango wa  moja ya magari aliyokabidhiwa kwa ajili ya jimbo lake ili alijaribu.


Mbunge wa Nchinga, Mhe. Said Mtanda naye akijaribu moja ya magari aliyokabidhiwa kwa ajili ya wananchi wa jimbo lake la Nchinga.


Mhe. Membe kushoto akiwa katika mazungumzo na Balozi wa Korea Kusini kabla ya shughuli ya kukabidhiana magari ya msaada.


Mhe. Naibu Waziri wa TAMISEMI wa kwanza kushoto, Mbunge wa Nchinga wa pili kutoka kushoto pamoja na Diwani wa moja ya Kata ya jimbo la Ruangwa wakifuatilia mazungumzo kati ya Mhe. Membe na Balozi wa Korea Kusini. (hawapo pichani)


picha ya pamoja



Balozi wa Korea Kusini wa kwanza kulia akibadilishana mawazo na Bw. Khatibu Makenga wa kwanza kushoto Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje wakati wa hafla hiyo.
 

 

 

     
 
 
Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Mutinda Mutiso akitembea sambamba na Bibi Zuhura Bundala. Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje wakati alipokuwa anaingia kwenye Hoteli ya Hyatt Regency, Kilimanjaro kwa ajili ya hafla ya kumuaga.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) kushoto akisalimiana na Balozi wa Kenya kabla ya kuanza kwa hafla ya kumuaga.


Mhe. Waziri akiwa katika mazungumzo na Balozi wa Kenya wakati wa hafla ya kumuaga iliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency.


Bibi Bundala akitoa neno kwa ajili ya kumkaribisha Mhe. Waziri kutoa hotuba ya kumuaga Balozi wa Kenya.


Mhe. Membe akitoa hotuba ambayo ilisisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na biashara kati ya Tanzania na Kenya.


Balozi wa Kenya anayemaliza muda wake akitoa hotuba ambapo alishukuru kwa ushirikiano aliopata kutoka Serikali ya Tanzania uliomwezesha kutekeleza majukumu yake kwa wepesi.


picha ya pamoja.
Picha na Reginald Kisaka

No comments: