Saturday, September 5, 2015

UZINDUZI WA BODI YA WADHAMINI YA MFUKO WA FIDIA KWA WAFANYAKAZI

 TAREHE 04 – 09 – 2015
 UKUMBI WA MIKUTANO WIZARA YA KAZI NA AJIRA

WCF ni Taasisi ya Serikali  chini ya Wizara ya Kazi na Ajira iliyoundwa kwa Mujibu wa Kifungu cha 5 cha Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi Na. 20 ya mwaka 2008 ili kushughulikia masuala ya fidia kwa Wafanyakazi waliopo katika Sekta ya Umma na Binafsi Tanzania Bara ambao wataumia, kuugua au kufariki dunia wakiwa katika utekelezaji wa majukumu ya Mwajiri.

Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) umeanzishwa kwa Madhumuni makuu yafuatayo;
·        Kutekeleza matakwa ya Sera ya Taifa ya Hifadhi ya Jamii ya mwaka 2003 katika kukabiliana na majanga mbalimbali yanayoikumba jamii ikiwamo ajali, magonjwa au vifo vinavyotokana na kazi;
·        Kutekeleza matakwa ya Kifungu cha 5 cha Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi Na. 20 ya Mwaka 2008;
·        Kulipa fidia stahiki pale mfanyakazi anapoumia, kuugua au kufariki kutokana na kazi;
·        Kuwasaidia wafanyakazi watakaoumia au kuugua kutokana na kazi ili waweze kurudi kazini au kushiriki katika shughuli nyingine zitakazowapatia kipato (ukarabati na ushauri nasaha);
·        Kuweka utaratibu utakaowezesha kuharakisha malipo ya fidia kwa wafanyakazi au wategemezi wao;
·        Kuweka utaratibu utakaowezesha Mfuko kupokea michango kutoka kwa waajiri na kufanya malipo;
·        Kukidhi matakwa ya mikataba ya kimataifa kuhusu fidia kwa wafanyakazi; na 
·        Kukuza mbinu za kuzuia ajali, magonjwa au vifo  katika maeneo ya kazi.

Majukumu ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi yatakuwa ni pamoja na;
·        Kusajili waajiri na waajiriwa;
·        kufanya tathmini ya mazingira hatarishi katika sehemu za kazi;
·        kukusanya michango kutoka kwa waajiri;
·        kuwekeza michango iliyokusanywa;
·        kulipa fidia pale mfanyakazi anapoumia, kuugua au kufariki kutokana na kazi wanazofanya;
·        kutunza kumbukumbu za matukio ya ajali, magonjwa na vifo kutokana na kazi.;
·        kukuza mbinu za kuzuia ajali, magonjwa au vifo kutokana na kazi na kuelimisha umma kuhusu kazi za Mfuko.

HAFLA YA UZINDUZI WA BODI
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi na Ajira Bw. Eric Shitindi akitoa hotuba ya utangulizi juu ya Sheria Na. 20 ya Mwaka 2008 pamoja na uanzishwaji wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) kulia kwake ni Waziri wa Kazi na Ajira Mhe. Gaudentia Kabaka

Waziri wa Kazi na Ajira Mhe. Gaudentia Kabaka akitoa hotuba kwa Wajumbe wa Bodi ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) pamoja na wageni waalikwa kabla ya kuzindua Bodi hiyo Rasmi.

Mwenyekiti wa Bodi Bw. Emmanuel Humba akitoa neno fupi na kueleza namna Bodi ilivyojipanga kuhakikisha malengo na madhumuni makuu ya uanzishwaji wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi yanafikiwa ikiwa na kuwahakikishia Fidia Stahiki Wafanyakazi Wote.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi Bw. Masha Mshomba akipokea vitendea kazi pamoja na Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi Na. 20 ya Mwaka 2008 kutoka kwa Wazi wa Kazi na Ajira Mhe. Gaudentia Kabaka.

Mwenyelkiti wa Bodi ya Wadhamini Bw. Emmanuel Humba akipokea chati cha usajili wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi Kutoka kwa Waziri wa Kazi na Ajira Mhe. Gaudentia Kabaka (Cheti cha Usajili kimetolewa na Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii Nchini SSRA)
Katibu Mkuu Wizara ya Kazi na Ajira Bw. Eric Shitindi wa pili kushoto, Mhe. Gaudentia Kabaka wakiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi

No comments: