Thursday, June 30, 2016

Mwenyekiti wa CCM Shinyanga Awafuturisha Waislam Mkoa Wa Shinyanga,Sheikh Mkuu Apongeza,Askofu Atoa Neno Kwa Magufuli

Tukio hilo limefanyika leo  kuanzia  katika Ukumbi wa NSSF mjini Shinyanga na kuhudhuriwa na waumini na viongozi wa dini ya mbalimbali  wakiongozwa na Sheikh Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Ismail Habibu Makusanya.
Wengine waliohudhuria ni viongozi wa vyama vya siasa na serikali,viongozi wa madhehebu mengine ya dini wakiongozwa na Askofu wa Kanisa la Africa Inland Church Tanzania (AICT) Dayosisi ya Shinyanga, Askofu Dr. John Nkola na watu mbalimbali wenye mapenzi mema.
Akizungumza wakati wa kula chakula cha pamoja “Futari” mwandaaji wa chakula hicho ambaye ni mwenyekiti wa CCM mkoa wa Shinyanga Erasto Kwilasa alisema aliwashukuru waumini wa dini ya kiislamu kukubali kushiriki na kudai kuwa ameamua kufanya hivyo ili kuonesha kwa vitendo kuwa anawapenda watu wa Shinyanga bila kujali makabila,dini wala rangi zao.
“Nawashukuruni sana tumekusanyika hapa,tupo hapa katika kushirikiana pamoja kwa kupata futari ya pamoja,mimi binafsi naamini katika ibada hii tutakuwa tumetenda jambo jema mbele ya mwenyezi mungu hasa katika kutekeleza nguzo muhimu miongoni mwa nguzo tano za kiislamu,funga ya mwezi mtukufu”,alisema Kwilasa.
“Ndugu zangu mlikuwa na nfasi ya kutoa udhuru kwamba mimi ni kiongozi wa chama,lakini kwa upendo mlionionesha leo hii,mmedhihirisha ule usemi wa serikali na chama havina dini bali wanachama wake wana dini zao na hii ndiyo maana mmekuja kwa wingi na mpaka sasa tupo pamoja hapa bila ubaguzi wa aina yoyote”,aliongeza Kwilasa.
Kwilasa alitumia fursa hiyo kuwataka wanasiasa kuacha kubaguana kwani binadamu wote ni wa mwenyezi mungu huku akimuomba mungu kupokea funga za waumini wote wa mkoa wa Shinyanga na taifa kwa ujumla.
“Kwa kutambua kazi nzuri zinazofanywa na rais John Pombe Magufuli na timu yake yote,naomba tuendelee kumuombea sana kwa mungu ili aweze kufanikisha malengo yake aliyowaahidi wananchi”,alisema Kwilasa.
Katika hatua nyingine Kwilasa aliwaomba viongozi wote wa madhehebu ya dini kusaidiana na viongozi wa serikali mkoa wa Shinyanga kupiga vita vitendo vya mauaji dhidi ya vikongwe,ubakaji na ulawiti kwa watoto,utumiaji wa madawa ya kulevya na ukatili wa kijinsia.
Kwa upande wake Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Sheikh Ismail Habibu Makusanya alimpongeza mwenyekiti huyo wa CCM kuandaa chakula cha pamoja kwa ajili ya waumini wa dini ya kiislamu na kusema kuwa kitendo alichokifanya kina dhawabu kubwa kwa mwenyezi mungu.
“Ukimuona mja anashughulika kuwalisha watu, wa kweli na wasio wakweli,wacha mungu na wasio wacha mungu huyu ameshika kazi ya mungu..sasa mwenyeji wetu ulichokifanya hapa sisi hatuwezi kukulipa lakini hiki ulichofanya ni kafara kubwa sana katika maisha yako ,ni hifadhi kubwa sana katika maisha yako,ni sadaka kubwa sana,kuwaita na kuwalisha waliofunga ni kazi kubwa,mungu akuzidishie pale ulipotoa”,aliongeza Sheikh Makusanya.
Naye Askofu wa Kanisa la Africa Inland Church Tanzania (AICT) Dayosisi ya Shinyanga, Askofu Dr. John Nkola alisema ni mara kwanza yake ya kwanza kukaribishwa kwenye futari kubwa kama hiyo na kuwashukuru waislamu kukusanyika pamoja kushiriki pamoja kwa futari na kwamba mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani ni kwa ajili ya utukufu wa mungu.
Askofu Nkola alitumia fursa hiyo kuwataka watanzania kujenga mshikamano na umoja uliopo kwani umoja wa madhehebu ya dini ndiyo uzima na amani ya taifa la Tanzania.
“Tukishikamana na kumhubiri mwenyezi mungu ambaye ni wa amani,nchi yetu itaendelea kuwa na amani sana,tuendelee kushikamana,na tuendelee kumuombea rais Magufuli anafanya mambo makubwa ambayo siyo kila mtanzania atayapenda hata kidogo”,alisema Askofu Nkola
“Sasa sisi kazi yetu siyo siasa lakini maandiko na misahafu inatuagiza kuwaombea wale ambao mwenyezi mungu amewapa madaraka ya kutawala,tumuombee sana rais wetu,pamoja na serikali yetu na nchi yote kwa ujumla tuendelee kutulia kwa amani,tuendelee kuwa kimbilio la wanyonge wanaonyanyaswa katika nchi zao”,aliongeza askofu Nkola.

Malunde1 blog huwa haipitwi na matukio,Mwandishi mkuu wa mtandao huu,Kadama Malunde alikuwepo eneo la tukio,ametusogezea picha 85..Shuhudia mwenyewe hapa chini

Juni 29,2016 kumefanyika tukio muhimu mjini Shinyanga ambapo Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Shinyanga ndugu Erasto Kwilasa (pichani) amewaandalia chakula cha pamoja “futari” waumini wa dini ya kiislamu mkoa wa Shinyanga ikiwa ni sehemu ya kuutukuza mwezi mtukufu wa Ramadhani.

PBZ YAADHIMISHA SHEREHE ZA MIAKA 50 KWA KUSAIDIA JAMII NA KUTEMBELEA HOSPITALI YA KIDONGOCHEKUNDU.


Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ Ndg Juma Ameir akimkabidhi msaada wa magodoro 100 Kamishna Msaidizi wa Chuo cha Mafunzo Zanzibar Omar Salum Mgaza. hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya Mafunzo Kilimani Zanzibar.
Baadhi ya magodoro 100 yaliotolewa msaada na PBZ kwa ajili ya matumishi ya Wanafunzi wa Chuo cha Mafunzo Zanzibar, ikiwa ni kusherehekea miaka 50 ya PBZ Zanzibar. hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya Chuo cha Mafunzo Kilimani Zanzibar.  

Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ akizungumza na Maofisa wa Chuo cha Mafunzo Zanzibar wakati wa kikabidhi msaada wa magodoro kwa ajili ya Wanafunzi wa Chuo cha Mafunzo Zanzibar, hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya Mafunzo Kilimani Zanzibar.
Kamishna Msaidizi wa Chuo cha Mafunzo Zanzibar Omar Salum Mgaza akitowa shukrani kwa PBZ  kwa msaada wao huo wa magodoro umeletwa wakati muafaka na kuwata taasisin nyengine kujitokeza kutoa misaada.
Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ Ndg.Juma Ameir akisalimiana na Muuguzi Dhamana wa Hospitali ya Kidongochekundu Zanzibar Ndg. Haji Vuai Hilal, wakati walipofika katika hospitali hiyo ya Mental kutowa misaada ya mashuka 200 kwa ajili ya hospitali hiyo. katikatika Afisa Masoko wa PBZ Ndg. Mohammed Nuhu. 
Afisa Masoko wa PBZ Ndg Mohammed Nuhu akisalimiana na Muuguzi Dhamana wa Hospitali ya Mental Kidongochekundu Zanzibar Haji Vuai Hilal. 
Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ Juma Ameir akizungumza na Uongozi wa Hospital ya Mental Kidongochekundu Zanzibar wakati wa kutembelea hospitali hiyo na kutoa msaada wa mashuka 200 ikiwa ni kusherehekea miaka 50 ya PBZ Zanzibar hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya hospitali hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ Ndg Juma Ameir akikabodhi msaada wa mashuka kwa ajili ya hospitali ya Mental Kidogochekundu Zanzibar akipokea msaada huo Muuguzi Dhamani wa hospitali hiyo Ndg Haji Vuai Hilal. ikiwa ni kusherehekea miaka 50 ya PBZ kushaidia jamii Zanzibar.
Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ Ndg Juma Ameir akikabodhi msaada wa mashuka kwa ajili ya hospitali ya Mental Kidogochekundu Zanzibar akipokea msaada huo Muuguzi Dhamani wa hospitali hiyo Ndg Haji Vuai Hilal. ikiwa ni kusherehekea miaka 50 ya PBZ kushaidia jamii Zanzibar.
Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ Ndg. Juma Ameir akimkabidhi mmoja wa mgonjwa katika hospitali hiyo Bi Amina Mwinyi msaada wa tende kwa ajili yao katika kipindi hichi cha mfungo wa mwezi wa ramadhani.
Mmmoja wa mgonjwa katika hospitali Bi Amina Mwinyi, hiyo akitowa shukrani kwa niaba ya wezake kwa uongozi wa PBZ kwa msaada wao huo kwao na kuuthamini na kuwataka na Wananchi wengi kujitokeza kuwasaidia kwa vitu mbalimbali.  
Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ Ndg. Juma Ameir akikabidhi msaada wa tenda mmoja wa wagonjwa wa hospitali hiyo Ndg. Mrisho Idrisa Hussein.

Muuguzi Dhamana wa Hospitali ya Mental Kidongochekundu Zanzibar Ndg Omar Vuai Hilal akitowa shukrani kwa Uongozi wa PBZ na Wafanyakazi wao kwa msaada wao huo katika hospitali hiyo.
Wafanyakazi wa PBZ wakijumuika na Mkurugenzi Mtenda wa PBZ Ndg Juma Ameir katika kutoa huduma kwa wateja ikiwa ni shamrashamra za kuadhimisha miaka 50 ya PBZ tangu kuazishwa kwa benki hiyo wakiwa katika Tawi la Malindi Zanzibar. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar Ndg Juma Ameir akitowa huduma kwa Wateja wa PBZ katika tawi la PBZ Malindi, Pbz imetimisha miaka 50 tangu kuazishwa kwa kwake Zanzibar. 
Wateja wa PBZ wakipita huduma za Kibenki katika Tawi la PBZ Malindi Zanzibar. 
Meneja wa Benki ya Watu wa Zanzibar Tawi la Malindi akitowa huduma kwa wateja wao akiwa na Afisi wa PBZ wakati wa shamrashamra za kusherehekea miaka 50 ya PBZ Zanzibar.
Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ Ndg Juma Ameir akitowa zawadi kwa Wateja wa PBZ ikiwa ni shamrashamra za kusherehekea miaka 50 ya PBZ kuazisha kutowa huduma za Kibenki Zanzibar.
Wateja wa PBZ wakiwa katika Tawi la Malindi Zanzibar wakisubiri kupata huduma za Kibenki katika tawi hilo.  
Wateja wakipatya huduma katika Benki hiyo Tawi la Malindi Zanzibar.
Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ akitowa zawadi kwa wateja wa PBZ Tawi la Malindi Zanzibar.
Mteja wa PBZ Zanzibar akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na huduma za Kibenki, wakati wa shamrashamra hizo za kusherehekea miaka 50 ya PBZ na kuwataka kuboresha zaidi huduma zao kwa wateja.

Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ akizungumza na waandishi wa habari malengo na changamoto za PBZ kwa wateja wake na malengo yao kutowa huduma kwa Wateja wao na kuboresha zaidi huduma zao. 
Afisa wa PBZ Tawi la Mwanakwerekwe Zanzibar Ndg Jaha akitowa huduma za kibenki kwa Wateja wao katika tawi hilo PBZ inatimiza miaka 50 tangu kuazishwa kwake. 
Afisa Manunuzi wa PBZ  Bi Mwanaidi Ramadhani akitowa huduma za Kibenki kwa Wateja wa PBZ Tawi la Mwanakwerekwe Zanzibar, Maofisa wa PBZ wameungana na wafanyakazi wa Matawi la PBZ kutowa Huduma za Kibenki kuadhimisha miaka 50 ya PBZ tangu kuazishwa kwake.  
Meneja wa PBZ Tawi la Mwanakwerekwe Zanzibar akitowa huduma za Kibenki kwa Wateja wa PBZ ikiwa ni shamrashamra za kusherehekea miaka 50 ya PBZ Zanzibar.
Meneja wa PBZ Tawi la Mwanakwerekwe Zanzibar akizungumza na waandishi wa habari wakati wa shamrashamra za kutimia miaka 50 ya PBZ Zanzibar.
Afisa manunuzi wa PBZ Bi Mwanaidi Ramadhani akitoa zawadi kwa Wateja wa PBZ Tawi la Mwanakwerekwe Zanzibar ikiwa ni kuadhimisha miaka 50 ya PBZ tangu kuazishwa kwake mwaka 1966-2016
Mteja wa PBZ akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na huduma za PBZ ni nzuri na kuwataka kuziboresha zaidi katika kipindi kijacho kwa wateja wao na kuwataka kuongeza huduma na ATM na kuziboresha zaidi huduma hizo kuwafikia hadi wananchi wa vijiji kupata huduma hii ya ATM huko mashamba.

Imetayarishwa na OthmanMapara. 
Zanzinews.com

Wednesday, June 29, 2016

SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA (NHC) LAANZA KUTOA HUDUMA KATIKA MAONESHO YA 40 YA KIMATAIFA ya SABASABA

1 2
Banda la Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) likiwa katika Maonesho ya 40 ya Kimataifa ya Biashara, yanayofanyika kila mwaka katika viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba jijini Dar es salaam tayari limeanza rasmi kutoa huduma zake katika viwanja hivyo.
3
Afisa Mawasiliano na Huduma kwa Jamii wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC),Bi Edith Nguruwe akiwapa maelezo wananchi waliotembelea banda la (NHC) kuhusina na huduma zinazotolewa na Shirika hilo.
4
Afisa Mauzo Mwandamizi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Emmanuel Limo (kushoto), akimuelezea Wananchi Kuhusiana na mradi wa SAFARI CITY uliopo Arusha alipotembelea banda hilo katika maonesho ya Sabasaba.
5
Afisa biashara (NHC), Clara Lubanga akitoa ufafanuzi kwa mmoja wa Wananchi aliotembelea banda hilo kuhusiana uzwaji wa nyumba (katikati), Afisa Mauzo wa (NHC), Joseph Haule.
6
Afisa Mauzo (NHC), Jasson Ipyana akimuelezea mwananchi kuhusina na miradi ya nyumba ya bei nafuu ilioko nchini.
7
Bw: Klison Sanane (kushoto), akifafanua miradi mbalimbali ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).
8
Aika Swai (kushoto), akielezea kuhusiana na utaratibu wa unaoutumika katika ununuzi wa nyumba za (NHC) huku baadhi ya wadau kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) wakimsikiliza kwa umakini.
PICHA ZOTE NA PHILEMON SOLOMON-FULLSHANGWEBLOG.

SIMU TV: HABARI KUTOKA TELEVISHENI

SIMU.TV: Jeshi la polisi mkoani Tanga limewahakikishia wakazi wa mji huo kuwa eneo la mapango ya Amboni baada ya kuwaua watuhumiwa watatu wa ujambazi;https://youtu.be/67G7vZVQXX4

SIMU.TV: Hali ya amani katika soko kuu la samaki Mwanza imetoweka baada ya wafanyabiashara kuamua kuwatembezea kipigo viongozi wa soko hilo baada ya kuchoshwa na manyanyaso; https://youtu.be/9EXF6odECko

SIMU.TV: Manispaa ya Lindi imeziokoa kaya 320 baada ya mfuko wa uwezeshaji vijijini TASAF kusaidia malipo ya awali ya afya kwa kutumia kadi; https://youtu.be/wTIfPYzb2kE

SIMU.TV: Wafanyabiashara katika soko la Kwa Doto lililoko Kigamboni jijini Dar es salaam wako hatarini kuugua magonjwa ya mlipuko baada ya kukosa sehemu za kutupa taka zao;https://youtu.be/AwkTCL2uTEA

SIMU.TV: Mtoto Wilson Jackson anahitaji wa matibabu baada ya kupata ajali ya pikipiki nyumbani kwao Mpiji Magohe jijini Dar es salaam; https://youtu.be/caj0EIqpkZo  

SIMU.TV: Viongozi wa halmashauri zote nchini wametakiwa kupeleka elimu ya ujasiliamali kwa wakulima ili kuepukana na utegemezi wa kilimo cha mvua pekee;https://youtu.be/cOUg2-TMUF0

SIMU.TV: Wadau mbalimbali wameanza kuunga mkono jitihada za kujenga Tanzania ya viwanda baada ya kuanza kuanzisha viwanda vidogo vidogo vya kuzalisha bidhaa za kilimo; https://youtu.be/g-fZWBocQS8

SIMU.TV: Shirkisho la mpira nchini TFF linaendelea kufanya tathimini juu ya uharibifu wa uwanja uliofanywa na mashabiki katika mchezo wake wa jana dhidi ya TP Mazembe;https://youtu.be/Io412qdPpco

SIMU.TVSIMU.TV: Timu ya soka ya vijana Serengeti boys inatarajia kuondoka nchini kuelekea Shelisheli kwenye mchezo wa marudiano na timu ya vijana nchini humo;https://youtu.be/ytEB-D502FA

SIMU.TV: Jeshi la polisi mkoani Tanga limewaua watu watatu wanaosadikiwa kuhusika na mauwaji ya watu nane katika tarafa ya Chumbageni usiku wa kuamkia Mei 31.https://youtu.be/woVOPz0YZ_o

SIMU.TV: Mahakama kuu kanda ya Arusha imetengua ubunge wa Onesmo Ole Nangole wa jimbo la Longido kwa tiketi ya CHADEMA baada ya kubaini kasoro zilizojitokeza kwenye uchaguzi mkuu mwaka jana. https://youtu.be/n8bMcWXoxZM

SIMU.TV: Rais Dr John Magufuli amewaapisha wakuu wa mikoa watatu na kutoa wito kwa wakuu hao wa mikoa na wakuu wa wilaya kufanya kazi ya kuwatumikia watanzania kwa uadilifu. https://youtu.be/vzqSianIY6Y

SIMU.TV: Rais Dr John Magufuli amefanya mazungumzo na mwenyekiti wa taasisi ya BILL AND MELINDA GATES na kumuahidi serikali ya awamu ya tano itaendeleza uhusiano na taasisi hiyo. https://youtu.be/U2GqZlXoYQ8

SIMU.TV: Wafanyakazi wa kiwanda cha kuchapisha vitabu kilichopo Bagamoyo mkoani Pwani wamemuomba rais kuingilia mgogoro ulipo kati yao na mwajiri wao kwa kutolipwa stahiki zao. https://youtu.be/i6Q7Jk6_Z9Y

SIMU.TV: Mkuu wa mkoa wa Tabora amewapa siku 30 watu waliovamia eneo la shule ya sekondari Tabora girls kuondoka mara moja. https://youtu.be/Mw50xtA5zEA

SIMU.TV: Baadhi ya wabunge wamesema kupitishwa kwa sheria ya manunuzi ya umma kutasaidia kupungua ubadhirifu unaotokana na manunuzi ya umma.https://youtu.be/QkerdhM5slQ

SIMU.TV: Wakala wa taifa wa utafiti wa vifaa vya ujenzi vya gharama nafuu wameiomba serikali kuwaunganisha na wananchi ili kuwapa elimu ya kutengeneza matofali ya gharama nafuu. https://youtu.be/9HpHtixL0NE

SIMU.TV: Wateja milioni moja kati ya wateja milioni moja na laki sita waliojiunga na huduma ya kibenki kwa njia ya simu za mkononi katika benki ya CRDB hawatumii huduma hiyo. https://youtu.be/YZjjDW-l1Xg

SIMU.TV: Mfuko wa hifadhi ya jamii nchini LAPF unatarajia kukamilisha ujenzi wa kituo cha mabasi cha Msavu mkoani Morogoro. https://youtu.be/PojkGovs_CM

SIMU.TV: Timu ya Serengeti boys inaondoka nchini usiku huu kuelekea nchini Shelisheli kucheza mchezo wa marudiano na timu ya vijana ya nchi hiyo.https://youtu.be/2pKbzAfPvq0

SIMU.TV: Shirikisho la soka nchini TFF limesema klabu ya Yanga itawajibika kulipa gharama za mchezo na uharibifu uliofanywa na mashabiki kwenye mchezo wake dhidi ya Tp Mazembe. https://youtu.be/HlF7rTqhOJk

SIMU.TV: Timu ya taifa ya tenisi ya wachezaji wenye ulemavu imeibuka mshindi kwenye mashindano yaliyofanyika nchini Kenya. https://youtu.be/dxBJbRt1qrA

SIMU.TV: Mashabiki wa masumbwi wa mikoa ya Morogoro na Iringa wataanza kufurahia mchezo huo baada ya mfungo mtukufu kwenye pambano la kusaka wachezaji kutoka mikoa hiyo. https://youtu.be/xZIowtxFksU  

SIMU.TV: Chama cha soka nchini Uingereza kinatarajia kumtangaza Gareth Southgates kuwa kocha wa muda wa timu ya taifa kabla ya kuanza mchakato wa kumtafuta kocha wa timu hiyo. https://youtu.be/KTaYLJSEPaM

BANDA LA NSSF LAVUTIA WENGI KATIKA MAONYESHO YA SABASABA

 Tuzo ya Ubora wa Huduma ya ISO 9001-2008 inayotoa mwongozo wa huduma bora kwa wanachama ikiwa katika Banda la NSSF Sabasaba.  NSSF ni Mfuko wa kwanza kupata tuzo hii mwaka 2014. 
 Tuzo ilizopata NSSF katika Maonyesho ya 39 ya Biashara ya Kimataifa. 

 Baadhi ya maofisa wa NSSF wakiwa katika picha ya pamoja.
 Ofisa Masoko Mwandamizi, Amina Mmbaga akimsiliza mmoja wa wanachama wa NSSF.
 Ofisa Mauzo wa NSSF,Abbas Ramadhani (kushoto), akitoa maelezo kwa mmoja wa wanachama waliofika katika banda la NSSF.
 Ofisa Uwekezaji wa Shirika la Taifa la hifadhi ya Jamii (NSSF), Moringe Nyerere (kushoto) akiwaonyesha watu waliofika katika banda la NSSF leo, ramani ya mradi wa viwanja vya Kiluvya vinavyouzwa  na shirika hilo, wakati wa Maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa yanayofanyika katika viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam.
 Meneja Kiongozi Masoko na Uhusiano wa Shirikala Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Eunice Chiume (wa pili kushoto) akigawa vibeberushi vyenye taarifa za shirika hilo kwawatu waliofika katika banda lao, wakati Maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea katika viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam. 
Meneja Kiongozi Masoko na Uhusiano wa Shirikala Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Eunice Chiume (kushoto) akiwakaribisha wageni katika banda la NSSF.
Meneja Kiongozi Masoko na Uhusiano wa Shirikala Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Eunice Chiume (kulia) akitoa elimu juu ya ulipaji wa michango kwa wanachama wa hiari kwa watu waliofika katika banda lao, wakati Maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea katika viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam. 
Meneja Kiongozi Masoko na Uhusiano wa Shirikala Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Eunice Chiume (katikati) akiwa katika picha ya pamoja pamoja na maofisa wa NSSF.