Friday, April 3, 2015

CHEF ISSA KIPANDE AFUNGUA MGAHAWA WAKE SWEDEN

IMG_1562
Mgeni rasmi Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mh. Dora Msechu (wa tatu kushoto) akiwa na mwenyeji wake Meya wa Trollhattan, Paul Akerlund (wa tatu kulia), Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa nchini Tanzania, Tagie Daisy Mwakawago (kulia), Mmiliki wa mgahawa unaotoa huduma za chakula cha kitanzania unaofahamika kama "Lunch by Chef Issa" (The house of Tanzanian food) uliopo katika mji wa Trollhattan, Sweden unaomilikiwa na mtanzania Chef Issa Kapande (wa pili kulia) katika picha ya pamoja na wadau mara baada ya kuwasili kwenye mnuso wa uzinduzi wa mgahawa huo.(Picha zote na Zainul Mzige wa modewjiblog).

Na Mwandishi Maalumu, Trollhattan-Sweden

MGAHAWA mkubwa unaotoa huduma za chakula cha Kitanzania unaomilikiwa na mpishi maarufu duniani, Issa Kapande `Chef Issa’, umefunguliwa nchini Sweden na kuvunja rekodi ya dunia.

Mgahawa huo ulizinduliwa na balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mh. Dora Msechu.
Balozi Msechu alimpongeza Issa Kapande na mkewe kwa kufanikisha kuwapo kwa mgahawa huo ambao umeweka rekodi kuwa mgahawa mkubwa kuliko yote ya Kiafrika katika nchi za Ulaya.

Aidha, alimshukuru Torvald Brahm mwenyeji wa mji huo kwa kumuunga mkono Issa hadi kufanikisha ndoto yake ya kuwa na mgahawa wa kwanza wa Kiafrika katika mji wa Trollhattan utakatoa huduma ya chakula cha kitanzania.

Katika uzinduzi huo ambapo wenyeji wa manispaa hiyo akiwemo Meya na mwenyekiti wa Trollhattan, Paul Akerlund na msaidizi wake Peter Eriksson walikuwepo, balozi ambaye ndio kwanza ameanza kazi alielezea kufurahishwa na juhudi za Kapande.
IMG_1477
Wadau wakiwa nje ya ukumbi tayari kuhudhuria hafla ya uzinduzi wa mgahawa huo.
IMG_1567
Mgeni rasmi Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mh. Dora Msechu akiwa na mwenyeji wake Meya wa Trollhattan, Paul Akerlund (kushoto) pamoja na Chef Issa Kapande (kulia) wakielekea kwenye eneo la tukio.

Alisema Issa ameonesha njia kwamba inawezekana kwa watu waliopo Ughaibuni sio tu kuajiriwa, bali kujiajiri katika nyanja mbalimbali.
Alisema hilo linawezekana kutokana na kufuatilia kwa karibu taratibu za wenyeji na kisha kutumia mafunzo yaliyopo kukamilisha ndoto.
"Ni dhahiri kuwa, Chef Issa kwa kupitia taaluma yake ya upishi amewezeshwa kumiliki mgahawa huu hapa Trollhattan,S weden kwa hilo, napenda tuishangilie na kuipigia makofi Sweden na Trollhattan."
Alisema akimpongeza kijana huyo ambaye pia amewekeza mkoani Mtwara.
Katika mahojiano, Mpishi Mkuu Issa Kapande alisema mafanikio yake yanatokana na juhudi kubwa na nia aliyoiweka katika kujifunza na kufundisha wengine katika mitandao ya wapishi wakuu.
IMG_1577
Mgeni rasmi Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mh. Dora Msechu na Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa nchini Tanzania, Tagie Daisy Mwakawago (kulia) wakielekea eneo la tukio.
Kapande ambaye mwaka jana alitwaa tuzo ya dhahabu katika upishi akiwa na timu ya Sweden magharibi alisema kuna umuhimu mkubwa kwa wapishi wa nyumbani kukubali kubadilika na kufanya kazi kwa pamoja kwa lengo la kujifunza na kufunza ili kuwa na aina nyingine ya mapishi katika kuendeleza sekta.
Alisema akiwa amefanyakazi katika nchi 17 na tayari akiwa na vitega uchumi nchini alianzia nia ya kuwekeza Sweden mwaka 2009 wakati alipohamia nchini humo akitokea Uswisi. Alisema alianza kwa kuomba vibali, lakini mchakato kamili ulianza mwaka 2013.
"Tulilazimika kufanya utafiti kidogo" alisema na kuongeza kuwa katika utafiti huo walihoji watu 300 na kujua mwelekeo hasa wa shughuli yao unastahili kuwaje.
Kapande ambaye ni mhitimu wa chuo kikuu cha Manchester Metropolitan na Chuo kikuu cha kimataifa cha menejimenti ya hoteli cha Uswis amesema amepambana vikali na mkewe hadi kufikia hatua ya kuanzisha mgahawa huo ambao upo katika eneo la ukubwa wa skwea mita 810.
IMG_1587
Mgeni rasmi Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mh. Dora Msechu (wa pili kushoto) akikata utepe kuzindua rasmi mgahawa unaotoa huduma za chakula cha kitanzania unaofahamika kama "Lunch by Chef Issa" (The house of Tanzanian food) uliopo katika mji wa Trollhattan, Sweden unaomilikiwa na mtanzania Chef Issa Kapande (wa pili kulia). Wanaoshuhudia tukio hilo ni Meya wa Trollhattan, Paul Akerlund (kushoto), Makamu mwenyekiti wa kamati ya elimu wa Halmashauri ya Manispaa ya Trollhattans Stad, Fahime Nordborg (katikati).
Ndani ya mgahawa huo pia watu mbalimbali watapatiwa taarifa za utalii Tanzania.
Katika kazi yake ya upishi, amebahatika kuwapikia watu mashuhuri duniani, baadhi wakiwa Andrew Young, Mchungaji Jesse Jackson, Robert Mugabe (Rais wa Zimbabwe), Paul Kagame (Rais wa Rwanda), Benjamini Mkapa (Rais mstaafu wa Tanzania), Raila Odinga (Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya), Daniel Arap Moi (Rais Mstaafu wa Kenya), Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Bi. Hillary Clinton na mumewe Bill Clinton, Mke wa Rais wa zamani wa Marekani Laura Bush.
Wengine ni Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein, mwigizaji Chris Tucker, Rais wa zamani wa Afrika Kusini hayati Mzee Nelson Mandela, Koffie Olomide, Youssour ndour, Arsene Wenger (Kocha wa Arsenal ya England), Gianluca Vialli (nyota wa zamani wa Italia aliyewahi kuichezea na kuinoa Chelsea ya England), Rais wa Congo DRC, Joseph Kabila, Billy Gates na wengine wengi.
IMG_1590
IMG_1592
IMG_1598
Mgeni rasmi Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mh. Dora Msechu akiongozana na Mmiliki wa mgahawa unaotoa huduma za chakula cha kitanzania unaofahamika kama "Lunch by Chef Issa" (The house of Tanzanian food) uliopo katika mji wa Trollhattan, Sweden unaomilikiwa na mtanzania Chef Issa Kapande kwenye sehemu maalum aliyoandaliwa.
IMG_1484
Pichani juu na chini ni wadau kutoka kila kona ya dunia waishio nchini Sweden walihudhuria.
IMG_1551
IMG_1487
IMG_1538
IMG_1495
IMG_1512
IMG_1625
Bw. Per R. Bostrom akisalimiana na Meya wa Trollhattan, Paul Akerlund (aliyeketi). Kulia ni Mgeni rasmi Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mh. Dora Msechu.
IMG_1627
Mgeni rasmi Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mh. Dora Msechu na mwenyeji wake Meya wa Trollhattan, Paul Akerlund wakiwa meza kuu.
IMG_1875
Meza kuu.
IMG_1629
Mwenyekiti wa awali wa Chama cha Watanzania waishio Sweden (TANRIKS), Tengo Kilumanga (katikati) akisalimiana na baadhi ya wageni waalikwa kwenye uzinduzi wa mgahawa huo.
IMG_1647
Mmiliki wa mgahawa unaotoa huduma za chakula cha kitanzania unaofahamika kama "Lunch by Chef Issa" (The house of Tanzanian food) uliopo katika mji wa Trollhattan, Sweden unaomilikiwa na mtanzania Chef Issa Kapande akizungumza machache na wageni waalikwa kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kutoa risala ya ufunguzi.
IMG_1656
IMG_1926
Meza kuu wakifuatilia historia ya Chef Issa Kapande (hayupo pichani) wakati akizungumza na wageni waalikwa.
IMG_1980
Mgeni rasmi Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mh. Dora Msechu akisoma risala mara baada ya kuzindua mgahawa unaotoa huduma za chakula cha kitanzania unaofahamika kama "Lunch by Chef Issa" (The house of Tanzanian food) uliopo katika mji wa Trollhattan, Sweden unaomilikiwa na mtanzania Chef Issa Kapande.
IMG_1951
Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa nchini Tanzania, Tagie Daisy Mwakawago akitambulishwa kwa wageni waalikwa.
IMG_1650
Baadhi wageni waalikwa wakisikiliza historia ya Chef Issa Kapande kabla ya mgeni rasmi kusoma risala ya ufunguzi.
IMG_1669
Ukumbi mzima ulionekana kuvutiwa na historia ya maisha na mafanikio ya Mtanzania Chef Issa Kapande (hayupo pichani).
IMG_1685
Meya wa Trollhattan, Paul Akerlund (kushoto) akimkabidhi zawadi ya picha Chef Issa Kapande ambapo alimuomba aitafutie nafasi ndani ya mgahawa wake kama kumbukumbu.
IMG_1699
Mgeni rasmi Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mh. Dora Msechu (kushoto) na mwenyeji wake Meya na mwenyekiti wa Trollhattan, Paul Akerlund pamoja na Makamu mwenyekiti wa kamati ya elimu wa Halmashauri ya Manispaa ya Trollhattans Stad, Fahime Nordborg (kulia) wakiongoza wageni waalikwa 300 kushiriki chakula cha jioni kilichoandaliwa na Mmiliki wa mgahawa huo Chef, Issa Kapande.
IMG_1700
IMG_1708
Chef Issa Kapande akikata nyama ya Mbuzi kwa ajili ya mgeni rasmi, Mh, Balozi Dora Msechu.
IMG_1712
Mgeni rasmi Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mh. Dora Msechu akifurahi jambo na Meneja Mwendeshaji wa Kampuni ya Shamy Tours and Travel Agent Zanzibar, Khamis Mwinjuma Simba (kushoto).
IMG_1715
Meya wa Trollhattan, Paul Akerlund akijisevia minofu ya nyama ya Mbuzi wakati wa uzinduzi wa mgahawa huo.
IMG_1742
Wageni wakiendelea kupakua chakula.
IMG_1769
IMG_1775
IMG_1798
IMG_1816
IMG_1821
IMG_1756
Mwenyekiti wa awali wa Chama cha Watanzania waishio Sweden (TANRIKS), Tengo Kilumanga (kulia) na mkewe wakishiriki chakula cha jioni kwenye mgahawa wa Mtanzania mwezao.
IMG_1824
Viongozi wa  Chama cha Watanzania Sweden (TANRIKS),  ni miongoni kati ya wageni waalikwa 300 waliohudhuria uzinduzi huo.
IMG_1835
IMG_1838
Viongozi wa Chama cha Watanzania Sweden (TANRIKS),  wakijichana msosi uliondaliwa na Chef Issa Kapande.
IMG_1866
Wageni waalikwa wakiendelea kupiga msosi uliofurahiwa na wengi ambao utakuwa unapatikana kwa chakula cha mchana kwa kipindi cha mwezi mmoja na hapo baadae itakuwa mpaka chakula cha usiku ndani ya mgahawa wa "Lunch by Chef Issa" (The house of Tanzanian food).
IMG_1869
Mh. Balozi Dora Msechu na mwenyeji wake Meya wa Trollhattan, Paul Akerlund.
IMG_2028
Mgeni rasmi Mh. Balozi Dora Msechu kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wageni waalikwa.
IMG_2080
Mgeni rasmi Balozi wa Sweden nchini Tanzania, Mh. Dora Msechu (wa pili kushoto) katika picha ya pamoja na wanachama cha Watanzania waishio Sweden (TANRIKS) pamoja na Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa nchini Tanzania, Tagie Daisy Mwakawago.
IMG_2265
Mgeni rasmi Balozi wa Sweden nchini Tanzania, Mh. Dora Msechu (wa pili kulia) na Mtanzania ambaye ni mmiliki wa mgahawa unaotoa huduma za chakula cha kitanzania unaofahamika kama "Lunch by Chef Issa" (The house of Tanzanian food) uliopo katika mji wa Trollhattan, Sweden, Chef Issa Kapande katika picha ya pamoja kikundi cha burudani.........
IMG_2216
Mtanzania ambaye ni mmiliki wa mgahawa unaotoa huduma za chakula cha kitanzania unaofahamika kama "Lunch by Chef Issa" (The house of Tanzanian food) uliopo katika mji wa Trollhattan, Sweden, Chef Issa Kapande katika picha ya kumbukumbu na Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa nchini Tanzania, Tagie Daisy Mwakawago.
IMG_2237
Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa nchini Tanzania, Tagie Daisy Mwakawago, Chef Issa Kapande katika picha ya pamoja na timu yake kwenye mgahawa huo.
IMG_2041
Mdau Abraham Juma Ndwatta wa Ubalozi wa Tanzania nchini Sweden akiwa na Grace Saulli kwenye hafla ya uzinduzi wa mgahawa huo.
IMG_2074
Wadau wakiendelea kupiga picha na Mh. Balozi Dora Msechu.
IMG_2125
Mh. Balozi Dora Msechu akisakata rhumba kwenye uzinduzi huo.
IMG_2093
Chef Issa Kapande akicheza muziki na wageni waalikwa.
IMG_2119
IMG_2106

MADEREVA WAFUNDWA NA TANROADS KUHUSU MZANI WA KISASA WA VIGWAZA

Eng. Japhet Kivuyo kutoka kitengo cha mzani wa Vigwaza mkoani Pwani akifafanua jambo kwa waandishi wa habari waliotembelea mzani huo jana jijini Dar es salaam.
Taa ya mzani wa Vigwaza ikielekeza gari lililobeba mzigo mzito kupinda kushoto kwa ajili ya ukaguzi wa kina. Changamoto kubwa iliyopo madereva hawafati taratibu za taa na wengine hawazielewi.
Kamera zilizounganishwa na Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) eneo la mzani wa Vigwaza zikirekodi matukio mbalimbali yanayotokea katika eneo hilo ili kutambua magari yanayotii na kuvunja sheria.
Meneja wa Wakala wa Barabara mkoani Pwani Eng. Tumaini Sarakikya akielezea ufanisi wa mzani wa vigwaza kwa waandishi wa habari (pichani) ambao unapunguza foleni pamoja na rushwa kwa watumiaji wa mzani huo.
Msimamizi wa Mzani wa Vigwaza, Godo Biwi akionesha jinsi mzani huo unavyofanya kazi kwa njia ya teknolojia kwa uwazi na uharaka.
Baadhi ya magari yaliyozidisha uzito yakiwa yameegeshwa ndani ya mzani wa Vigwaza mkoani Pwani, ambapo gari litakaloegeshwa kwa kushindwa kulipa fidia baada ya siku tatu litalipa faini ya dola 20 kwa siku ambazo zitabadilishwa kwa fedha za kitanzania.
Gari lenye mtambo wa kukagua madaraja makubwa linalomilikiwa na Wakala wa Barabara mkoani Pwani kwa ajili ya kupima umadhubuti wa madaraja na kuona ubora na mapungufu yake.


Imeelezwa kuwa ufanisi wa kutumia mzani wa kisasa wa Vigwaza utafikiwa endapo madereva na watumiaji wa barabara watajielimisha taratibu za kutumia mizani hiyo ili kwenda na kasi ya upimaji, kuokoa muda na kuondoa msongamano katika barabara kuu ya Chalinze-Kibaha.

Hayo yamesemwa na Meneja wa Wakala wa Barabara mkoa wa Pwani Eng. Tumaini Sarakikya, wakati akikagua namna mzani huo unavyofanyakazi na kusisitiza umuhimu wa madereva kufuata maelekezo ya alama za barabarani katika eneo hilo ili kujiepusha na uvunjaji wa sheria.

“Mzani huu una urefu wa mita 22 hivyo utasaidia kuondoa msongamano eneo hili kwani unauwezo wa kupima gari lote mara moja na kwa dakika moja tofauti na mizani nyingine zinazopima gari kwa awamu ambazo hutumia dakika 3”, amesisitiza Eng. Sarrakikya.

Eng. Sarakikya amesema  teknolojia inayotumika katika mzani huo itasaidia kuepuka majadiliano yanayoweza kuleta hisia za  rushwa na upendeleo ambavyo ni changamoto katika utendaji kazi wa mizani hapa nchini. 

Akizungumzia utendaji kazi wa mzani huo Eng. Japhet Kivuyo, amesema takriban magari 1800 hupimwa katika mizani ya awali (weigh in motion sensor) ambapo asilimia 60 ya magari hayo hupimwa katika mizani kuu na asilimia 40 huruhusiwa kupita bila kupimwa baada ya kuonekana yamekidhi vigezo.

Naye Mkuu wa mzani wa Vigwaza Eng. Simfukwe Sylvester, amezungumzia umuhimu wa wasafirishaji kupanga vizuri na kubeba mizigo inayowiana na magari yao ili kuepusha usumbufu na uharibifu wa barabara.

Amesema gari litakalokaidi kupima katika mzani huo litaadhibiwa kwa kulipa faini ya dola za kimarekani elfu 2, na pia gari litakaloegeshwa kwa kushindwa kulipa fidia baada ya siku tatu litalipa faini ya dola 20 kwa siku ambazo zitabadilishwa kwa fedha za kitanzania. 

Katika hatua nyingine Eng. Sarakikya amesema ujenzi wa barabara kati ya Mlandizi -Vigwaza na Vigwaza –Chalinze utaanza hivi karibuni baada ya wakandarasi wa kujenga eneo hilo kupatikana. 


IMETAYARISHWA NA KITENGO CHA HABARI NA MAWASILIANO SERIKALINI, WIZARA YA UJENZI.

MKUTANO WA TAKWIMU WA NCHI WANACHAMA WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI WAFANYIKA JIJINI DAR ES SALAAM

Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS),kutokaTanzania Dkt. Albina Chuwa akifungua mkutano wa Wakurugenzi na Watalaam wa Takwimu kutoka nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kujadili mausuala mbalimbali ya Takwimu leo jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Takwimu Uganda Bw. Ben Mungyereza akizungumza jambo wakati wa mkutano wa Wakurugenzi wa Takwi mu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashari kikuhusu utayari wa nchi yake katika matumizi ya Takwimu mbalimbali.
Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Takwimu Rwanda Bw. Yusuf Murangwa akitoa mchango wake kuhusu umuhimu wa ushirikiano wa matumizi ya Takwimu baina ya nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki leo jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Ofisiya Takwimu Kenya Bw.Zachary Mwangi akizungumza na washiriki wa mkutano wa Wakurugenzi wa Takwimu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuhusu utayari wa nchi yake katika matumizi ya Takwimu mbalimbali.
Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Takwimu ya Burundi Bi. Jeanine Niyukuri akichangia wakati wa mkutano wa Wakurugenzi wa Takwimu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afriki Mashariki uliofanyika leo jijini Dar es salaam.
Baadhi yaWashiriki wa Mkutano waWataalam wa Takwimu wanchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashari ki wakifuatilia mausuala mbalimbali wakati wa Mkutano huo leo jijini Dar es salaam. 

Na. Veronica Kazimoto,

Wakurugenzi Wakuu wa Ofisi za Takwimu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kutoka Rwanda, Uganda, Kenya, Burundi na Tanzania wamekutana leo  jijini Dar es salaam kujadili mchango wa matumizi ya Takwimu sahihi katika kuleta maendeleo na kukuza ushirikiano baina ya Nchi Wanachama wa Jumuiya hiyo.

Akifungua Mkutano huo Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu kutoka Tanzania Dkt. Albina Chuwa amesema kuwa mkutano huo pamoja na mambo mengine unazileta pamoja Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kujadili na kubadilishana uzoefu kuhusu masuala mbalimbali ya Takwimu na mchango wake katika kukuza uchumi na kuleta maendeleo ya nchi hizo.

Amesema kuwa mkutano huo umelenga kuongeza na kuimarisha ushirikiano baina ya Nchi Wananchama wa Jumuiya hiyo katika matumizi ya Takwimu pamoja na kupitia mabadiliko ya sheria mbalimbali zinazosimamia masuala ya Takwimu kwa Nchi Wanachama.

Kwa upande wao wakurugenzi hao kutoka Rwanda, Uganda, Kenya, na Burundi wakizungumza kwa nyakati tofauti wamesema kufanyika kwa mkutano huo nchini Tanzania kunatoa matumaini ya mwendelezo wa ushirikiano katika matumizi ya takwimu sahihi kutokana na mchango wake katika maendeleo ya nchi zao na Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa ujumla.

Wamesema kuwa nchi zao zitaendelea kushirikiana kikamilifu katika kuhakikisha kuwa kunakuwa na usimamizi mzuri wa takwimu mbalimbali zikiwemo za kilimo, Viwanda, Biashara, uchumi  na takwimu nyingine kwa manufaa ya wananchi wa Jumuiya hiyo.


Kufanyika kwa mkutano huo nchini Tanzania ambao umehusisha wakurugenzi wakuu, wakurugenzi na maafisa wandamizi wa takwimu ni mwendelezo wa mikutano mbalimbali inayofanyika katika Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa ajili ya kujadili mchango wa matumizi ya Takwimu sahihi katika kuleta maendeleo na kukuza ushirikiano baina ya Nchi Wanachama wa Jumuiya hiyo.

Thursday, April 2, 2015

EFM YASHEREHEKEA KUTIMIZA MWAKA KWA KISHINDO

Jikekizz la nguvu la kusherehekea siku ya kuzaliwa ya Radio 93.7 EFM.
Mstahiki Meya wa Kinondoni, Yussuf Mwenda akibadilishana mawazo na Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kusini, David Kafulila walipo kutana katika ofisi za EFM asubuhi ya leo.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Mtangazaji wa kipindi cha Joto la Asubuhi, Dennis Ssebo akiwa na Mkurugrnzi Mkuu wa Radio 93.7 EFM, Francis Ciza.
Mmoja wa wageni waliotembelea ofisi hiyo, Sukhwinder Bajwa ambaye ni Mkuu wa Masoko kutoka Kampuni ya Zantel, akizungumza wakati wa kuipongeza EFM siku ya leo.
Samira Kiango ambae ni Mhariri Msaidizi pamoja akiwa na Mkurugenzi Mkuu wa EFM, Francis Ciza.
Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kusini, David Kafulila alipokua akiongea moja kwa moja kutoka katika kituo cha 93.7 EFM siku ya leo.
Ukafika wakati wa kukata keki kwa pamoja.
Meneja Mkuu wa EFM, Geofrey Ndaula, alikipiga stori mbili tatu na Reuben Ndege (Ncha kali) pamoja Sostenas Ambakisye (Rdj-Kamokali).
Picha ya familia yetu.
Keki tayari kwa kuliwa.
Samira Kiango pamoja Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kusini, David Kafulila.

MKOA WA KAGERA WAADHIMISHA SIKU YA KUPANDA MITI KITAIFA WILAYANI ‘MISSENYI MISITU NI MALI PANDA MITI'

Aprili Mosi kila mwaka huwa ni siku ya kupanda miti kitaifa na mwaka huu 2015 mkoa wa Kagera ulipewa heshima ya kuadhimisha siku hiyo ambapo iliadhimishwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Missenyi na kushirikisha wadau mbalimbali pamoja na wananchi wanaojihusisha na kupanda miti na kutunza misitu.

Maadhimisho hayo yaliyoongozwa na mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Celestine Gesimba kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii ambapo maadhimisho hayo yalianzia katika Kijiji cha Bugolola eneo la Omukajunguti kwa kupanda miti 2100 kwa kushirikisha washiriki wote na wananchi wa kijiji hicho.

Kauli mbiu ya siku hiyo ilikuwa ni “Misitu ni Mali Panda Miti.” Katika Hotuba yake Naibu Katibu Mkuu Bw. Gesimba alisema wizara yake siyo kwamba inahamasisha wananchi kupanda miti ili kulinda mazingira tu bali wananchi wapande miti ili kunufaika nayo kwani ni mali inayoingiza kipato kikubwa kwa mwananchi mmoja mmoja.

Bw. Gesimba alisema wananchi wanatakiwa kupanda miti kwa wingi kwani miti isipopandwa itasababisha maafa makubwa hapo mbeleni kama inavyoanza kuonekana kwa sasa mfano, ukosefu wa mvua au mvua kutonyesha kwa wakati, joto jingi, kuyeyuka kwa theruji mlima Kilimanjaro.

Bw. Gesimba alimalizia hotuba yake kwa kusema kuwa kutotunza misitu kumesababisha baadhi ya sehemu kuwa jangwa au kusababisha ugonjwa wa malaria mfano Lushoto mkoani Tanga ambako hakukuwa na ugojwa huo miaka ya 1970 na 1990. Aidha alitahadhalisha misitu kutoweka kabisa kwani kila baada ya dakika sita (6) nusu kiolmeta ya misitu hutoweka duniani.

Bwana Jaffari Omary Afisa Misitu katika Ofisi ya Mkuu wa mkoa akitoa salaamu za mkoa wa Kagera alisema mkoa wa Kagera una jumla ya misitu 17 yenye hekta 341,756.35 pia eneo la misitu na vichaka ni kilometa za mraba 10,148 sawa na asilimia 35 ya nchi kavu ya mkoa mzima.

Mkoa wa Kagera una misimu miwili ya upandaji miti, msimu wa vuli ambapo wananchi hupanda miti kwa wingi kutokana na msimu huo kuwa na mvua za kutosha pia na msimu wa masika ambapo nao hutumika kupanda miti kwa wingi, alifafanua Bw. Jaffari Omary .

Meneja wa Wakala wa Huduma za Misitu Kanda ya ziwa Bw. Haji Khatibu akitoa salaam za Kanda ya Ziwa alisema kuwa kutokana na utafiti uliofanyika mwaka 2003 Kanda ya Ziwa ilionekana kuwa misitu imebakia mapori tu kutokana na uchomaji moto ovyo, mifugo mingi na wananchi kutoshiriki kuitunza misitu, uchomaji mkaa, kilimo na uvunaji wa mbao usiozingatia kanuni na taratibu.

Aidha Bw. Khatibu alisema uharibifu wa miti unachangiwa pia na sera mbalimbali kuingiliana na alitoa mfano katika halmashauri za Wilaya kutoa maeneo ya hifadhi za misitu kwa wananchi kama viwanja vya kuishi na kuendesha kilimo jambo ambalo linapelekea uharibifu mkubwa katika maeneo hayo ya hifadhi.

Ili kukabiliana na changamoto hizo na kuzipatia ufumbuzi Wizara ya Maliasili na Utalii inaendelea kuwahasisha wananchi kushiriki katika kuilinda na kuitunza misitu kupita serikali zao za vijiji na vitongoji pamoja na mwananchi mmoja mmoja kutoshiriki katika vitendo ovu vya kuharibu misitu.

Aidha serikali imekuwa ikiendesha doria katika maeneo ya hafadhi za taifa ili kukabiliana na uvamizi wa maeneo hayo pia kukamata mazao ya misitu ambayo yanavunwa bila kuzingatia sheria, taratibu na kanuni za uvunaji na kuwachukulia hatua kali wahusika wanaokamatwa.

Mwenyekiti wa halmashauri ya Wilaya ya Missenyi William Katunzi akitoa shukrani zake kwa Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kuadhimisha siku ya kupanda miti kitaifa Wilayani missenyi alisema tayari kwa mkoa wa Kagera wananchi wanajua nini maana ya kupanda miti kwa sasa, wapanda miti kibiashara ili kujipatia kipato pia kulinda mazingira.

Takwimu za upandaji na utunzaji wa miti katika mkoa wa Kagera kwa miaka minne mfululizo; mwaka 2011/2012 lengo la kupanda lilikuwa miti 12,500,000 Miti iliyopandwa ni 13,100,875 sawa na asilimia 105, Miti iliyopona ni 11,220,328 sawa na asilimia 89.7. Mwaka 2012/2013 lengo la kupanda lilikuwa miti 12,500,000 Miti iliyopandwa ni 12,755,042 sawa na asilimia 102, Miti iliyopona ni 11,081,519 sawa na asilimia 88.

Aidha mwaka 2013/2014 lengo la kupanda lilikuwa miti 13,000,000 Miti iliyopandwa ni 13,767,022 sawa na asilimia 85, Miti iliyopona ni 11,248,933 sawa na asilimia 88.4. Na mwaka 2014/2015 lengo la kupanda lilikuwa miti 13,000,000 Miti iliyopandwa ni 12,278,125 sawa na asilimia 98.4, Miti iliyopona ni 11,153,627 sawa na asilimia 90.8

IPU impressed by Parliament of Tanzania partnership with the United Agencies

A Panel discussant from Parliament of Tanzania Hon. Suzan Lyimo makes her points during the IPU committee on UN Affairs at the 132 Inte- Parliamentary Union in Hanoi, Vietnam yesterday.
A Panel discussant from Parliament of Tanzania Hon. Suzan Lyimo (left) makes her points during the IPU committee on UN Affairs at the 132 Inte- Parliamentary Union in Hanoi, Vietnam yesterday.
The Special Invited Guest during the discussion on “The Convention on the Rights of the Child 25 Years on: Are Children’s Lives Better? Organized by the IPU Standing Committee on Democracy and Human Rights during the 132 Assembly, Hon. Lediana Mafuru Mng’ong’o (MP) from Tanzania noting some comments from the delegates after presenting her paper on Right to Nutrition in Hanoi, Vietnam, yesterday.
Delegates of the 132 Assembly of the IPU in Hanoi VietNam. Photo By Owen Mwandumbya

By, Owen Mwandumbya,
Hanoi, VietNam

Members of the Inter-Parliamentary Union (IPU) have expressed their satisfaction on the committed done by the Parliament of Tanzania on taking the necessary action to cooperate with the United Nation Agencies for building a strong and committed Parliament through capacity building programs coordinated by the UN.

The comments was made by the Parliamentarians during the discussion on report of the field visit of the Advisory Group to the IPU Committee on United Nations Affairs to Tanzania conducted in 2008 to gather first-hand information about the progress made in the One United Nations reform and, more generally, to gain a better understanding of the complexities of UN field operations during the 132 IPU Assembly, in  Hanoi, Vetnam.


Sharing the Parliament of Tanzania experience on cooperation with the UN Agencies, the panel discussant during the IPU committee on UN Affairs, Hon. Suzan Lyimo (Mp) from Parliament of Tanzania said today, in response to the capacity development needs, the Tanzania National Assembly have signed a five years project called Legislatures Support Project with the UNDP aiming at helping to strengthen Members legislative, oversight and representative capacities and assisting the Secretariats of legislatures to deliver upgraded services to Members.

She said the project has managed to enhance the capacity of MPs and their   committees   to better   exercise their interrelated functions of law making, executive oversight including national budget approval and oversight, and representation of constituents/citizens


Impressed by the achievements of Tanzania Parliament, delegates of the IPU have called for more active partnership from other Parliament citing Tanzania’s achievements and invest more in  keeping with both the core mandate of all Parliaments to scrutinize the disbursement and use of public monies,   in a challenging Sustainable Development Goals and improve the Peoples lives.


In order to better respond to the growing partnership between the Inter-Parliamentary Union and the United Nations, a dedicated IPU Committee on United Nations Affairs was established in the and its first session in October 2007 adopted an IPU Policy Paper on the nature of the relationships between the UN and the World Parliaments and circulated in the United Nations General Assembly.

To date, field missions have been conducted to pilot countries implementing the "Delivering as One" reform of UN operations at the national level and Parliament commitments to cooperate with the UN Agencies. These missions have sought to evaluate progress in ensuring greater system-wide coherence, including in terms of greater involvement by parliament in the elaboration of national development plans and the monitoring of aid effectiveness.

Meanwhile, the Special Invited Guest during the discussion on “The Convention on the Rights of the Child 25 Years on: Are Children’s Lives Better? Organized by the IPU Standing Committee on Democracy and Human Rights during the 132 Assembly here in Hanoi, Vietnam, Hon. Lediana Mafuru Mng’ong’o  (MP) from Tanzania has called for parliaments in the world to deliver an interventions for nutritional deficiencies for the childrens beacuse poor nutrition during the first two years of their life can have multiple life-long consequences.

“We need political commitment and actions, not business as usual but business unusual to safeguard the Children’s and the Mother to fight Malnutrition”

She added that,  Parliamentarians has a duty to conduct public education and promote support groups on nutrition because as representatives of people Parliamentarians can become nutrition champions in advocating and promoting child nutrition including exclusive breast feeding for six months, food fortification and universal health care systems.


The delegates of the 132 has all agreed that Members of Parliaments can enact laws and put in place policies which aim at Increasing health budget to 15% as stipulated in Abuja Declarations, and have nutrition budget line.


The 132 Assembly of the Inter-Parliamentary Union ends yesterday here in Hanoi, Vietnam with the adoption of different resolution on the Warfare on Cyber, New System of Water Governance and Sanitation, International laws related to National Sovereignty, and Access to Health as a basic right.