Monday, December 2, 2013
KINANA AKUTANA NA JAMII YA WAFUGAJI WILAYANI CHUNYA LEO
Kinana akiwa na jamii ya wafugaji kabila la wasukuma alipowasili katika kitongoji hicho kukagua mradi wa maji wakati ziara ya kuimarisha uhuai wa CCM na kukagua miradi ya maendeleo katika wilaya zote za Mkoa wa Mbeya.
Kinana akimtwisha maji mmoja wa akina mama wa jamii ya wafugaji, baada ya kuyateka kwenye bomba lililojengwa katika kitongoji hicho kilichotengwa kwa ajili ya jamii hiyo.
Kinana akiangalia sehemu ya bomba iliyotengwa kwa ajili ya maji ya kunyweshea mifugo katika Kijiji cha Mteka, wilayani cChunya leo.
Katibu wa NEC wa Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha Rose Migiro, (katikati), akisaidia kazi ya ujenzi katika jengo la Soko la Mulugo la Mwambani, wakati wa ziara ya kuimarisha uhai wa chama na kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa kuata Ilani ya Uchaguzi ya CCM, wilayani Chunya, Mbeya. Kushoto ni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye abaye naye anasaidia kazi hiyo.
Kinana akikagua bweni la wasichana la Shul ya Sekondari ya Maweni wilayani Chunya leo.
Kinana akifitisha mlngo katika nyumba ya kuishi watumishi wa wa Hospitali na walimu katika Kijiji cha Saza, wilayani Chunya leo.
Mbunge wa Jimbo la Songwe, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo (kushoto) akiahidi mbele ya Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (katikati)kuwasaidia wasaidia wachimbaji madini wadogo wadoko katika machimbo ya Saza, wilayani Chunya juzi. Pia Kianana amewaahidi wachimbaji hao Serikali kuwapatia vifaa vya kuchimbia madini hayo.Kulia ni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye.
Nape akila chakula cha aina ya kipologwa kinachotengezwa kwa kutumia viazi vitamu.
Wasanii wa kabila la wabungu wakitumbuiza kwa ngoma mbele ya Katibu Mkuu wa CCM, Kinana, wakati wa kikao kwa balozi wa shina eneo katika Kata ya Udinde, wilayani Chunya leo.
Mbunge wa Jimbo la Songwe, Phillip Mulugo 9kulia) akimkabidhi Mwenyekiti wa Kikundi cha Vijana wakulima cha St. Marcus, msaada wa sh. 800,000. kwa ajili ya kuendeleza kilimo.
Dk. Migiro akihutubia katika mkutano wa hadhara katika Kata ya Udinde leo.
Kinana akiwa na mtumbwi mdogoo alipewa zawadi na wazee wa kimila wa kabila la wabungu, kwa ajili ya kuvulia wanachama wapya. katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kata ya Udinde, wilayani Chunya leo.PICHA ZOTE NA KAMANDA RICHARD MWAIKENDA
Sunday, December 1, 2013
ASAS NA MSOWOYA WAKEMEA SIASA ZA MAKUNDI NDANI YA UVCCM MKOA WA IRINGA
makada wa CCM wakiwa wamembeba juu mwenyekiti mpya wa chipukizi mkoa wa Iringa
kamanda wa UVCCM mkoa wa Iringa Salim Asas kushoto akimkaribisha mwenyekiti wa chipukizi mkoa Enock Luhala mara baada ya kutangazwa mshindi katika uchaguzi mkuu wa Chipukizi mkoa
Kamanda wa UV CCM ambae alikuwa mgeni rasmi katika uchaguzi wa Chipukizi mkoa wa Iringa Salim Asas akiwa na viongozi wa UVCCM mkoa Tumain Msowoya mwenyekiti wa umoja huo kushoto na mwenyekiti mpya wa chipukizi mkoa Enock Luhala kulia
Kamanda wa UVCCM mkoa wa Iringa Salim Asas kushoto na mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Iringa Tumain Msowoya wakiwa wamewapakata wajumbe wa mkutano mkuu wa Chipukizi mkoa wa Iringa mara baada ya uchaguzi
NA FRANCIS GODWIN BLOG
KAMANDA wa umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi (UVCCM) mkoa wa Iringa Salim Asas amewataka UVCCM mkoa wa Iringa kujipanga vema kujenga chama katika jimbo la Iringa mjini na kuepuka siasa za makundi .
Asas alisema kuwa ili kuwa na chama imara ni vema jumuiya hiyo ya vijana na jumuiya nyingine ndani ya CCM mkoa wa Iringa kufanya kazi kama timu moja ya ushindi na kuepuka kuendesha siasa za makundi ambazo hazina faida ndani ya CCM.
Asas ambae alikuwa mgeni rasmi katika uchaguzi wa chipukizi mkoa wa Iringa alitoa kauli hiyo juzi wakati wa mkutano uliofanyika katika ukumbi wa CCM wilaya ya Iringa mjini
Alisema kuwa kila jumuiya ndani ya CCM kuna makundi isipo kuwa Chipukizi ambao wao wameendelea kuungana kwa kuwa kundi mmoja bila ya kujigawa kama zilizo jumuiya nyingine.
Katika hatua nyingine Asas alitaka kuanzia sasa UVCCM mkoa wa Iringa kuhakikisha inafanya kazi kwa kushirikiana na Chipukizi badala ya kuendelea kuwabagua .
Alisema mara baada ya uchaguzi huo sasa mkoa kuandaa mpango wa kuwatembeza Chipukizi bungeni , katika hifadhi mbali mbali za Taifa na maeneo mengine kwa ajili ya kujifunza kwa gharama za UVCCM mkoa .
"Hivi jumuiya ya wazazi tuna makundi , vijana tuna makundi , UWT tuna makundi ila chipukizi wao hawana makundi...sasa ombi langu vijana tuige mfano wa chipukizi kwa kuepuka makundi na badala yake tuungane pamoja kuwa kundi moja la CCM kwa ajili ya kuimarisha chama"
Alisema hivi sasa chama hasa vijana wanapaswa kuungana pamoja ili kukijenga zaidi chama katika jimbo la Iringa mjini na kuwa iwapo chama kitakuwa imara zaidi muda ukifika wa kumtafuta mgombea hata kama atawekwa nani atashinda kwa kishindo badala ya kuendesha siasa za makundi ambazo zinakigawa chama.
Awali mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Iringa Tumain Msowoya akimkaribisha kamanda huyo wa UVCCM kuzungumza katika mkutano huo alisema kuwa mwaka kuna uchaguzi wa serikali za mitaa hivyo anachoomba vijana kujiepusha na makundi ya kisiasa .
Kwani alisema kuwa vijana kama kisima cha kutoa viongozi baadhi ya wagombea wamekuwa na tabia ya kugawana vijana ili kuwasaidia katika kampeni na mwisho wa siku wamekuwa wakikigawa chama jambo ambalo ni hatari zaidi katika uimarishaji wa chama .
Pia Msowoya aliwataka vijana kujiandaa kugombea nafasi mbali mbali za uongozi ndani ya serikali za mitaa ili ikiwezekana mitaa mingi zaidi mwakani katika mkoa wa Iringa kuongozwa na vijana .
Aliwaagiza viongozi wa UVCCM kwa ngazo zote kutoa taarifa ya kuwepo kwa baadhi ya watu wenye nia ya kuwania nafasi za uongozi, ambao wanataka kuitumia jumuiya yao kama njia ya mafanikio yao kiuongozi.
“UVCCM ya sasa haitakubali kuyumbishwa wala kugawanywa na mtu yeyote mwenye nia ya kuomba madaraka, itafanya kazi kwa mujibu wa kanuni, taratibu na sheria zilizowekwa,” alisema Msowoya.
Akizungumzia uchaguzi wa chipukizi mkoani humo, Katibu wa UVCCM mkoani humo Alawi Haidar alisema umefanyika kwa amani na utulivu na kwamba, watoto hao wameweza kuwapata viongozi bora walioona wanawafaa.
Mwenyekiti mpya wa chipukizi mkoa Enock Meshack Luhala mbali ya kuwashukuru wajumbe waliomchagua bado alisema kuwa ataendelea kutoa ushirikiano mkubwa kwa chama ili kuhakikisha chama kinapata ushindi wa kishindo katika mkoa wa Iringa .
Akitangaza matokeo hayo, Haidar alisema Mwenyekiti mpya wa chipukizi mkoani humo, Enock Luhala alifanikiwa kushindwa kwa kura 18 kati ya 33 zilizopigwa na kuwashinda wenzake, Ashraf Mpogole aliyepata kura 12 na Magreth Lusingo kura nne.
Katika nafasi ya mkutano mkuu wa chipukizi taifa, Junior Mlelwa alishinda kwa kura 26 na kuwabwaga wenzake, Halid Aziz na Christopher Dalu.
Wengine walioshinda ni Tausi Mgambo, Rukia Kimweli na Amina Kimweli kuwa wajumbe wa kamati ya uendeshaji mkoa.
DK.Shein mgeni Rasmi Kilele cha Siku ya Ukimwi, Paje.
Baadhi ya wananchi walioalikwa katika hafla ya maadhimisho ya siku ya Ukimwi,wakisoma majarida yaliyotolewa katika maadhimisho hayo yaliyofanyika Paje Wilaya ya Kusini,Mkoa wa Kusini Unguja,mgeni rasmi akiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
Wananchi wa Vijiji mbali mbali vya Wilaya ya Kusini Unguja,wakiwa katika hafla ya maadhimisho ya siku ya Ukimwi Duniani ambapo kwa mwaka,ambapo kwa mwaka huu Kijiji cha Paje,Wilaya ya Kusini Mkoa wa Kusini Unguja,yamefanyika Maadhimisho hayo na mgeni rasmi akiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
Baadhi ya Viongozi wa Serikali wakiwa katika maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani yaliyofanyika Kijiji cha
Paje,Wilaya ya Kusini Mkoa wa Kusini Unguja, akiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
Vijana wa Zapha+ ni Watu wanaoishi na Virusi vinavyosababisha Ukumwi, wakifanya igozo mbele ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(hayupo pichani) pamoja na Wananchi waliohudhuria katika maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani yaliyofanyika Kijiji cha Paje,Wilaya ya Kusini Mkoa
wa Kusini Unguja
Bibi Fauziat Ismail Aboud, kutoka Shirika la PSI Tanzania,akisoma risala wakati wa maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani yaliyofanyika Kijiji cha Paje,Wilaya ya Kusini Mkoa wa Kusini Unguja, akiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(hayupo pichani)
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Fatma Abdulhabib Fereji,alipokuwa akimkaribisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(wa pili kushoto),kuzungumza na wananchi wakati wa maadhimisho ya siku ya ukimwi Duniani yaliyoafnyika leo katika Kijiji cha Paje,Wilaya ya Kusini,Mkoa wa Kusini Unguja,
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(katikati) alipokuwa akizungumza na wananchi wakati wa maadhimisho ya siku ya ukimwi Duniani yaliyoafnyika leo katika Kijiji cha Paje,Wilaya ya Kusini,Mkoa wa Kusini Unguja,(kushoto) Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Fatma Abdulhabib Fereji, na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja,Dk.Idrisa Muslim Hija,(kulia)
Wasoma Utenzi kutoka Makunduchi,Asia Bukheti,(kulia) na Amina haji Simai,wakitoa burudani hiyo leo wakati wa maadhimisho ya siku ya ukimwi Duniani yaliyoafnyika leo katika Kijiji cha Paje,Wilaya ya Kusini,Mkoa wa Kusini Unguja,mbele ya mgeni rasmi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(wa pili kulia) akiiangalia picha yake wakati alipokuwa Meneja wa Mradi wa Kitengo cha Ukimwi kutoka Nov 1997- Julai 1998, wakati wa maonesho katika banda la kitengo cha Ukimwi,cha Wizara ya Afya,wakati wa maadhimisho ya siku ya ukimwi Duniani yaliyoafnyika leo katika Kijiji cha Paje,Wilaya ya Kusini,Mkoa wa Kusini
Unguja,(kulia) ni Dk.Ahmed Khatib,Kitengo cha Ukimwi
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(wa pili kulia) akiiangalia vifaa mbali mbali wakati alipotembelea banda la kitengo cha Ukimwi la Wizara ya Afya,wakati wa maadhimisho ya siku ya ukimwi Duniani yaliyoafnyika leo katika Kijiji cha Paje,Wilaya ya Kusini,Mkoa wa Kusini Unguja,(kulia) ni Dk.Ahmed Mohamed Khatib,Meneja Kitengo cha Ukimw
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(kulia) akipata maelezo kutoka kwa Dk.Farhat Khalid,kitengo cha Ukimwi,wakati alipotembelea maonesho katika banda la kitengo cha Ukimwi la Wizara ya Afya,wakati wa maadhimisho ya siku ya ukimwi Duniani yaliyoafnyika leo katika Kijiji cha Paje,Wilaya ya
Kusini,Mkoa wa Kusini Unguja,(katikati) ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Fatma Abdulhabib Fereji
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi na jumuiya ya Zayedesa,wakati alipotembelea mabanda mbali mbali ya maonesho yanayojishuhulisha na kutoa elimu ya Ukimwi wakati wa Maadhimisho ya siku ya Ukimwi Duniani,Kitaifa maadhimisho hayo yamefanyika leo katika Kijiji cha Paje, Wilaya ya Kusini,Mkoa wa Kusini Unguja. Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.
Subscribe to:
Posts (Atom)

.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)