Wednesday, December 12, 2018

WAZIRI MHAGAMA AITAKA MENEJIMENTI YA OFISI YA WAZIRI MKUU KUZINGATIA HAKI NA USAWA KATIKA KUTATUA KERO ZA WATUMISHI




 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama akiongoza kikao cha pamoja na Watumishi wa Ofisi hiyo walipokutana akujadili masuala yao ikiwa ni sehemu ya kufahamiana na kuendelea kufanya kazi kwa umoja, mkutano huo ulifanyika Desemba 10, 2018 katika Ukumbi Mikutano wa LAPF Dodoma.
P2-min
Katibu Mkuu Ofisi yaWaziri Mkuu (Bunge na Waziri Mkuu) Bi.Maimuna Tarishi akichangia jambo wakati wa mkutano huo.
P3-min P4-min P5-min
Baadhi ya Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia maelekezo ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama  (hayupo pichani) wakati wa mkutano huo.
P6-min
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe.Anthony Mavunde akichangia jambo wakati wa mkutano huo.
P7-min
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Irene Isaka, akifafanua masuala ya malipo ya Pensheni kwa watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu (hawapo pichani) wakati wa mkutano huo.
P8-min
Mkaguzi wa Ndani Ofisi ya Waziri Mkuu Bw.Omari Mpayage akiuliza swali wakati wa mkutano huo.
P9-min
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu) Bw. Peter Kalonga akifafanua masuala ya utawala kwa watumishi wa Ofisi hiyo wakati wa kikao hicho.
P10-min
Msaidizi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Bw.Richard Kalinga akiuliza swali wakati wa mkutano huo.(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu Mhe.Jenista Mhagama ameitaka Menejimenti ya Ofisi yake kushughulikia kero za watumishi kwa haki na usawa ili kumaliza kero zilizopo.

Ameyasema hayo wakati wa Mkutano na Watumishi wa ofisi ya Waziri Mkuu walipokutana kujadili masula yanayowakabili wawapo kazini uliofanyika Desemba 10, 2018 katika Ukumbi wa LAPF Dodoma.

Waziri aliwataka Watendaji wa ofisi yake kuendelea kutatua changamoto zinazowakabili watumishi kuhusu madai mbalimbali ikiwemo; kupanda madaraja, uhamisho, usalama mahali pa kazi na masuala ya kuzingatia afya wawapo kazini ili kuhakikisha wanatekeeleza majukumu yao katika mazingira rafiki.

“Kama kuna motisha kubwa kwa mtumishi ni kumsaidia kutatua kero yake inayohusiana na utumishi wake kwa uzito unaolingana na tatizo au uhitaji wake ili kusaidia kuongeza morali yake katika kufanya kazi.”Alisema Mhagama.
Sambamba na hilo waziri aliwaasa watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu kutumia mabaraza ya Wafanyakazi katika kujadili na kutatua kero wanazokabiliana nazo wawapo kazini.

“Ni vyema watumishi kuendelea kuyatumia mabaraza ya wafanyakazi yaliyopo kisheria katika ofisi ili kabla masuala hayajafika ngazi za juu yawe yamekwishwa sikilishwa na kutafutiwa ufumbuzi pale inapowezekana”.Alisistiza Waziri
Aliongezea kuwa, ni wajibu wa Makatibu wakuu kuendelea kusimamia na kuhakikisha haki na usawa vinazingatiwa katika Ofisi ili kuwa na weredi na ufanisi katika kutekeleza majukumu ya kila siku.

Naye Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Bunge na Waziri Mkuu, Maimuna Tarishi aliahidi kuchugua maagizo ya waziri na kuahidi kuyatekeleza kama ilivyoelekezwa katika mkutano huo.

“Tutaendelea kusimamia shughuli za Ofisi kwa kuzingatia sheria, kanuni na miongozo iliyopo ili kuhakikisha haki na usawa vinazingatiwa mahali pa kazi ili kuweza kufikia malengo na kuendelea kuiletea nchi maendeleo”.Alisema Tarishi

No comments: