Tuesday, December 4, 2018

WAKILI MWAE AHUKUMIWA KWENDA JELA MIAKA 5 AU KULIPA FAINI YA SHILINGI MILIONI 200

NaVero Ignatus ,Arusha

Hukumu ya kesi ya utakatishaji fedha haramu iliyokuwa inamkabili wakili maafuru Jijini Arusha Mediam Mwale imetolewa desema 3 na Jaji Isa Maige wa Mahakama kuu kanda ya Arusha ambapo amemuhukumu kwenda jela miaka mitano au kulipa faini ya shilingi milioni 200

Mshtakiwa analazimika kulipa faini na kama akishindwa atatumikia kifungo cha miaka mitano na kwa kipindi ambapo atakuwa hajakidhi matakwa ya adhabu hiyo atabaki kizuizini

Jaji Isa ameiambia mahakama kuwa mshitakiwa Mediam Mwale amekiri makosa kwa hiari yake mwenyewe na kwamba hiyo ni dalili tosha ya kuwa ameungama na anajutia makosa na kukiri kwake kuna faida mbili katika mfumo mzima wa haki jinai mshtakiwa ameokoa muda na rasilimali za mahakama

Ameiambia mahakama kuwa kukiri kwa mshtakiwa wakwanza kumeondoa uwezekano kukwepa kwa njia za kiufundi hayo ameyazingatia kwani mshtakiwa ni kosa lake la kwanza siyo mkosaji sugu asiyeweza kurekebishika, kuungama kwake kunaonyesha kuwa yupo tayari kujirekebisha

''kwa minajili hiyo muelekeo wa wa kujirekebisha ni hatua stahiki katika kutoa adhabu hiyo''''Mshtakiwa amekuwa kizuizini kwa zaidi ya miaka saba tangia alipokamatwa kama mambo yote yangeenda katika hali ya kawaida si ajabu kwamba mshtakiwa wa kwanza angelikuwa ameshahukumiwa na kutuikia kifungo cha zaidi ya miaka saba'' alisema Jaji Maiga

Akisoma hukumu hiyo Jaji Issa Maige Mahakama kuu kanda ya Arusha adhabu makosa 30 yanaomkabili mshatakiwa wa kwanza ambayo ni makosa ya kughushi kinyume na kifungu namba 337 kwa ambapo adhabu yake kifungo cha miaka 5 kwa kila kosa ,kughushi kinyume na kifungu namba 338 adhabu yake miaka 7

Makosa mengine ni kuandaa nyaraka za kughushi adhabu miaka 2 kwa kila kosa,kukutwa na vitu vilivyopatikana kwa njia isiyosahihi miaka 2 kosa la 2,na 29 la utakatishaji fedha faini yake ni shilingi milioni 100 kwa kila kosa ,kosa la kula njama miaka 5 kwa kuzingatia ya kwamba takwa la kisheria

Jaji Maige ameiambia mahakama kabla ya kutoa hukumu amezingatia hoja za upande zote mbili na maombi ya mawakili upande wa utetezi kuwa mshtakiwa ni mgonjwa, anawategemezi, mzazi wa miaka 78 na mtoto wa miaka 8, kukaa kizuizini zaidi ya miaka saba

''Kama alivyosema Omari wakili wautetezi mshtakiwa ameokoa muda wa mahakama kama kesi ingesikilizwa upande wa jamhuri walipanga kuleta mashahidi 59 na vielelezo 64 baadhi ya mashahidi walitakiwa kutoka nje ya nchi bila shaka hili lingepelekea shauri hili kuchukua muda mrefu na kutumia gharama kubwa sana "alisema Jaji Maiga

Aidha Jaji Maiga ametoa ufafanuzi kuhusiana na amri ya kukamatwa kwa mali ziizopatikana kinyume cha sheria ameiambia mahakama wakili wa serikali aliiomba mahakama ifanye hivyo lakini wakili msomi kwa upande wa utetezi aona swala hilo ni busara likasubiri hadi maombi maalumu yatakapo fanyika

Jaji amesema kwa msingi wa sheria namba 351 cha sheria husika kinaruhusu  mahakama kuweza kutoa kama hiyo lakini kifungu kidogo cha (3)kwamba mahakama inatakiwa izingatie taratibu nyingine maalum ambazo zimewekwa kuhusiana na adhabu husika

Katika makosa haya haswa la utakatishaji fedha sheria husika inazungumza katika kifungu kidogo cha 28 zinatoa utaratibu katika kifungu cha( 9)kwamba mwanasheria mkuu wa serikali anaweza akafanya maombi kwaajili ya kuhakikisha mali hizo zinakamatwa matakwa ya kisheria yanaonyesha wanaweza wahakusika watu wengine zaidi

''Kwakuwa zile mali hazijaainishwa bayana naona ni busara kama maombi haya yakifanyika kwa utaratibu wa kisheria ili yaweze kusikilizwa kwa umakini na kujua ni mali gani zinzpaswa kukamatwa''alisema

Kuhusiana na kughushi chini ya kifungu cha sheria namba 338 ambapo sheria imeruhusu moja kwamoja kutoa amri ya kukamatwa au kuteketeza nyaraka ambazo zimeghushiwa hivyo ametoa amri ya kamba nyaraka zote ambazo zimeghushiwa chini ya kifungu cha sheria namba 338 zikamatwe zote na ziteketezwe baada ya kuisha muda wa kukata rufaa

Amefafanua adhabu stahiki inayomsatahili mshtakiwa wa kwanza kwa kosa la kwanza ni njama ya kufanya kosa kinyume na kifungu namba 384 cha kanuni ya adhabu,ambapo adhabu ya juu kabisa ya kosa hilo adahabu ya miaka 7 au adabu inayoendana sawa na adahabu ya juu ya kosa husika,adhabu ya chini ni miaka 5

'' Mbali ya makosa yote ni miaka saba kwasasa mshtakiwa anatakiwa alipe faini ya kutakatisha fedha ambapo kila kosa atatakiwa kulipa shilingi milioni 100 akishindwa kulipa atakwenda kutumikia jela miaka mitano makosa yote aliyohukumiwa mahakama imezingatia muda wa kukaa kwake mahakamani akishindwa ''alisema

Wakili Mwale na wenzake wanatete watatu wanatetewa na Mawakili Omary Omary, Innocent Mwanga, Bukheri Ngoseki na Mosses Mahuna ,

Kwa upande wa Jamhuri unaongozwa na wakili mkuu wa serikali serikali wapo Osward Tibabyemkomamya,wakili mwandamizi Hashimu Ngole.

No comments: