Friday, December 7, 2018

SERIKALI YAIAGIZA BODI YA WATAALAM WA UNUNUZI NA UGAVI KUDHIBITI MAADILI YA WATAALAM WA UNUNUZI NA UGAVI

Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Mipango wa Wizara hiyo, Bw. Richard Mkumbo, akifunga Kongamano la Tisa la Bodi ya Wataalam wa ununuzi na ugavi (PSPTB), kwa niaba ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bi. Susana Benard Mkapa, ukumbi wa DCC, Dodoma.
Baadhi ya Washiriki wa Kongamano la Tisa la Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPSTB), wakiimba wimbo wa Taifa wakati wa hafla ya kufunga kongamano hilo la siku tatu lililofanyika Jijini Dodoma na kuwashirikisha wataalam 650 kutoka Tanzania Bara.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi Sr. Dkt. Hellen Bandiho, akisoma hotuba ya ukaribisho kwa mgeni rasmi Kaimu Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Richard Mkumbo (hayupo pichani), wakati wa hafla ya kufunga Kongamano la Tisa la Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), iliyofanyika katika ukumbi wa DCC, Jijini Dodoma
Kamishana wa Idara ya Sera ya Ununuzi wa Umma wa Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Frederick Mwakibinga (kushoto), na mjumbe wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) Dr. Laurent Shirima, wakifuatilia kwa makini hotuba ya mgeni rasmi, Kaimu Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Richard Mkumbo, wakati akifunga kongamano la Tisa la Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), katika ukumbi wa DCC, Jijini Dodoma.
Baadhi ya Washiriki wa Kongamano la Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPSTB), wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi, Kaimu Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Richard Mkumbo, wakati akifunga Kongamano la Tisa la Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), katika ukumbi wa DCC, Jijini Dodoma.
Waandaji na waratibu wa Kongamano la Tisa la Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi (waliosimama nyuma) wakiwa katika picha ya pamoja na meza kuu baada ya kufungwa kwa Kongamano hilo katika ukumbi wa mikutano wa DCC, Jijini Dodoma.


Na Josephine Majura, WFM, Dodoma


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Susana Mkapa, ameiagiza Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi nchini (PSPTB), kuhakikisha kuwa inadhibiti maadili ya wafanyakazi wa sekta ya ununuzi na ugavi ili fedha za serikali zinazotumika kwenye ununuzi ziwe na tija kwa wananchi.

Bi. Mkapa ametoa maagizo hayo Jijini Dodoma, katika hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Kaimu Naibu Katibu Mkuu ambaye pia ni Mkurugenzi wa Mipango wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Richard Mkumbo, wakati akifunga kongamano la tisa la wataalam wa ununuzi na ugavi kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara.

Bw. Mkumbo amebainisha kuwa licha ya vitengo vya matumizi mabaya ya fedha za umma kupitia sekta ya ununuzi na ugavi, ikiwemo rushwa kuendelea kupungua, Bodi inatakiwa kuhakikisha kuwa vitendo vya rushwa vinadhibitiwa ipasavyo.

Amesema asilimia 75 ya fedha za umma zinatumika kupitia mchakato wa manunuzi ambao taarifa ya mdhibiti na mkaguzi wa hesabu za serikali (CAG) na Mamlaka ya Ununuzi nchini PPRA, umebaini kuwepo kwa viashiria vya rushwa katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya wananchi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi, Sister Dkt. Hellen Bandiho, amesema kuwa Bodi yake itahakikisha inasimamia kikamilifu maadili ya watumishi wa sekta ya ununuzi ili iweze kushiriki katika kukuza uchumi wa viwanda.

Kongamano hilo limewashirikisha wataalam wa ununuzi na ugavi wapatao 650 kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara

1 comment:

Tiba asili said...

UTAJIRI AU FEDHA ZA NDAGU AU MAJINI KWA MUDA MFUPI

(Kwanza kabisa nataka kukwambia kwamba hakika utajili ni azina kutoka kwa mwenyezi mungu na pia kuna viumbe alio wapa mamlaka na nguvu ya kumiliki mali)


MPAKA MASAA 72(SIKU3) PAPO HAPO KWA MASHARTI MAALUM KIKUBWA UWE MWAMINIFU, JASILI NA UWE NA UTAYARI WA KUPOKEA MASHARTI YA KUTUNZA SIRI HII SIO MZAHA......

KUMBUKA MALIPO NI BAADA YA KUFANIKIWA

kwa maelezo kamili piga namba +255742162843

(KWANINI USUMBUKE,HACHA KUTANGATANGA, NA MAISHA NI MAFUPI PUUZA UONGOFU WA KUWA MTU KUWA TAJIRI NI DHAMBI WAKATI AKUAMBIAE YEYE NI TAJIRI (Tumia ufahamu kujinasuaUTAJIRI WA NDAGU(MASHARTI) NDANI YA MASAA 72(SIKU TATU) PAPO HAPO KIKUBWA UWE MWAMINIFU, JASILI NA UWE NA UTAYARI WA KUPOKEA MASHARTI YA KUTUNZA SIRI HII SIO MZAHA......

NAITWA DR, MDIRO piga 0742162843. KAMA UNAITAJI PESA ZA MAJINI AU NDAGU YA MALI AU ULINZI KWA MALI YAKO
(HUSITUME SMS PIGA SIMU KUHEPUKA MATAPELI)
MATIBABU MENGINEYO NI KAMA UTULIVU KATIKA NDOA, AU KUMVUTA UMPENDAE, KUONDOA MIKOSI, MABALAA, KUOSHA NYOTA, KUITAMBUA NYOTA YAKO NA ASILI YA KAZI YAKE, KAMA UNASUMBULIWA NA MAJINI MAHABA NA SHIDA YA UZAZI.

NIPIGIE 0742162843. KIKUBWA NI KUSIKILIZA NA KUFATA MASHARTI. ANGALIZO USITUME SMS PIGA NA UWE NA NIA.

(kuhusu utajiri au pesa) KABLA YA KUPIGA SIMU ZINGATIA YAFUATAYO
1. uwe una umri wa miaka 18+
2. uwe tayari kupokea masharti yote
3.uwe na uwezo wa kutunza siri
4. uwe jasiri wa kupokea taarifa yoyote
KARIBU SANA KWA SHIDA NYINGINE PIA ULIYONAYO AMBAYO SIJATAJA INSHAALAH ITATATULIWA IKIWA NDANI YA UWEZO WANGU.