Saturday, December 29, 2018

NAMAINGO YAZINDUA MRADI WA ASALI MIZINGA 55000 KIBITI

Baadhi ya Wanachama wa Taasisi ya Namaingo wakiangalia moja kati ya mabanda ya ufugaji nyuki wa asali wakati wa uzinduzi Mradi wa Mizinga 55000 katika Kijiji cha Kikale, wilayani Kibiti, Mkoa wa Pwani.PICHA NA RICHARD MWAIKENDA.
Mwenyekiti wa Kamati ya Nidhamu ya Namaingo, Ignus Augustino, akiwaongoza wanachama kuangalia mizinga.


Na Richard Mwaikenda, Kibiti.

TAASISI ya Namaingo, imezindua uwekezaji wa Mradi wa Mizinga ya nyuki wa asali 55000 wa wanachama wake katika Kijiji cha Kikale, wilyani Kibiti, Mkoa wa Pwani.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi huo uliofanyika jana kijiji hapo, Mwenyekiti wa Kamati ya Nidhamu ya Namaingo, Ignus Augustino, alisema mipango yao ni kila mwanachama kuwa atamiliki mizinga 50.

Uzinduzi huo ulifanywa mbele ya wananchama waliotoka Dar es Salaam pamoja na wanakijiji wa Kikale katika mabanda matatu yenye mizinga 200 ya kuanzia. Mizinga hiyo ipo ndani ya msitu wa miti ya mikoko inayoaminiwa kutoa daraja la kwanza la asali yenye kiwango cha kimataifa.

Augustino alisema kuwa wamejiandaa vilivyo kuutekeleza mradi huo mkubwa ambapo hivi sasa tayari watalaamu wa kutengeneza malkia wapo eneo la mradi. Urinaji ukianza baada ya miezi sita Kila mzinga utakuwa unatoa kilo 20 za asali. Naye Mwenyekiti Msaidizi wa Namaingo, Elesia Mkuru, alisema baadhi ya wanachamama walikuwa 

hawaamini kuwa mradi huo utandinduliwa, lakini sasa wameshaona ukweli wa mambo.Aliipoongeza Serikali kupitia Wakala wa Misitu Tanzania (TFS), kwa kuwaruhusu kuwekeza mradi huo katika misitu iiyopo mikoa ya Pwani, Iringa, Njombe, Dar es Salaam na Morogoro. Mwanachama wa Namaingo, Queen Ryoba, alisema kuwa wamefurahi sana kuona mradi huo umeanza 

kwani walikuwa wanausubiri kwa muda mrefu. Aliimpongeza sana Mkurugenzi wa Namaingo Bi Ubwa Ibrahim kwa kufanikisha mradi huo. Pia aliutaka uongozi wa taasisi hiyo kuendeleza kwa njia ya kisasa miradi mingine ikiwemo kilimo cha kisasa cha mazao mbalimbali wanayoisimamia ii wapate mavuno mazuri hivyo kuwapunguzia umaskini.

Mmoja wa wanakijiji wa Kikale ambapo mradi huo upo, Khamis Ngwaya, alifurahia kuwepo kwa mradi huo ambao anaamini utawaletea maendeleo katika kijiji chao kwani nao wameshirikishwa. Pia kwa niaba ya wenzie aliahidi kutoa ushirikiano kuulinda mradi huo na kuwasihi wanaoupinga mradi huo waachane kabisa na mlengo huo bali wajiunge kwani mradi huo ni faida kwa wananchi wa kijiji hicho, kwa baadhi kupata ajira na kipato pia.

Baada ya wanachama hao waliokuwa kwenye msafara wa mabasi madogo 6 (Coaster) kushiriki katika uzinduzi huo, waliondoka kwenda katika Kijiji cha Mbawa wilayano humo kukagua mipaka ya mashamba yao waliyogawiwa na Namaingo kwa ajili ya kuendesha kilimo cha kisasa na ufugaji pamoja na mabwa ya samaki. 
Mwenyekiti Msaidizi wa Namaingo, Elesia Mkuru, akizungumza na wanachama wakati wa uzinduzi huo ambapo, alisema baadhi ya wanachamama walikuwa hawaamini kuwa mradi huo utandinduliwa, lakini sasa wameshaona ukweli wa mambo.
Wanachama wakiangalia baadhi ya mizinga
Baadhi ya wanachama wa Namaingo wakijiandaa kupanda magari kuelekea Kijiji cha Mbawa kukagua mipaka ya mashamba yao
Wanachama wakiwa mbele ya moja ya majengo ya Namaingo wlipofika kukagua mikuza ya mashamba yao katika Kijiji cha Mbawa kwa ajili Kilimo cha Kisasa na ufugaji
Katapila lialotumika kuweka mipaka katika shamba la Wanachama la Mbawa.
Wanchama wakikagua moja ya mipaka ya mashamba yao

No comments: