Sunday, December 9, 2018

MAHOJIANO YA MSEMAJI MKUU WA SERIKALI DKT.ABBAS NA KITUO CHA REDIO JIJINI ARUSHA




Dr. Hassan Abbas mkurugenzi wa idara ya habari maelezo Tanzania picha kutoka Maktaba


Na. Vero Ignarus, Arusha

Msenaji wa Serikali Dkt Abbas amesema serikaki inaendelea na ukarabati na ujenzi wa Zahanati na Vituo vya afya kwa nchi nzima kwani Mpango wa serikali ni kuhakikisha kila Wilaya ina hospitali

Amesema upatikanaji wa dawa umeongezeka kwa rikali kuongeza bajeti ya madawa kutoka bill.31 hadi bil. 280,ambapo Serikali inanunua madawa moja kwa moja kutoka viwandani na sio kwa madalali tena. Tiba za kibingwa zimeimarishwa sana katika nchi yetu hasa magonjwa ya Moyo,kupandikiza figo na matatizo yakutosikia hii imepelekea kupungua kwa idadi ya wagonjwa wakutibiwa nje ya nchi.

Kwa upande wa sejta ya Elimu Dkt Abbas anesema Serikali inatoa fedha kiasi cha bil.29 kila mwezi kuwezesha elimu bure katika nchi yetu.Dkt.Abbas.Amesisitiza kuwa Migomo ya elimu ya juu imeshaisha katika awamu hii ya tano kwani fedha zinapelekwa kwenye vyuo kwa wakati ambapo kwa mwaka huu kiasi cha bil 137 kimeshapelekwa kwenye vyuo mbalimbali nchini.

Amesema kuwa kwenye sekta ya Kilimo Serikali imeanzisha mamlaka ya udhibiti wa masoko kwa bidhaa za Tanzania, hii itawasaidia wakulima, wafanyabiashara kupata masoko yenye uhakika.June mwaka huu Serikali lizindua mpango mpya wa kilimo cha kisasa cha umwagiliaji ili kumuwezesha mkulima kutotegemea mvua

'' Mabalozi wetu katika nchi mbalimbali wanakazi kubwa yakuhakikisha wanaitafutia nchi masoko ya bidhaa zetu za ndani".alisema.Katika Sekta ya Utalii amesema kuwa Serikali inatarajia kupata watalii wengi kutoka China- Hii ni juhudi ya serikali katika kukuza utalii na kuongeza pato la serikali. '' Katika miaka 3 ya serikali ya awamu ya Tano watalii wameongezeka zaidi"alisema Dkt Abbas

Amewataka Wananchi wasiogope kupisha miradi ya maendeleo kwani kwa faida yao na nchi pia'' Viongozi waendelee kutatua migogoro ya ardhi katika maeneo yao".Dkt. Abbas.Amesema viwanda vingi vimeanzishwa vikiwemo vya matrekta,juisi na tiles, hivyo bidhaa hizi zinapatika hapa hapa nchini sio zakuagiza nje tena.

Amesema Sekta ya Viwanda imechangia kwa kiasi kikubwa kuongeza ajira kwa wananchi wa Tanzania.'' Watumishi wanatakiwa kutekeleza majukumu yao kwa nafasi zao''alisema.Serikali ya awamu ya Tano imerudisha nidhamu na weledi kwa watumishi kwa kiasi kikubwa ambapo awamu ya Tano inaheshimu Uhuru na Demokrasia. Amesema kuwa Wananchi watumia Uhuru, demokrasia, utaratibu wa sheria za nchi walionao ila kwa kuzingatia mipaka yake

No comments: