Saturday, December 15, 2018

Biteko afungua Ofisi ya Madini Mahenge mkoani Morogoro

Wachimbaji madini Mahenge mkoani Morogoro watakiwa kulipa madeni yao


Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko akikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa Ofisi ya Afisa Migodi Mkazi Mahenge-Ulanga mkoani Morogoro, jana Disemba 14, 2018. Wanaoshuhudia ni viongozi mbalimbali wa Serikali, Tume ya Madini pamoja na wachimbaji madini.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko akisaini kitabu cha wageni baada ya kufungua ofisi ya Afisa Migodi Mkazi Wilaya ya Ulanga mkoani Morogoro. Aliyesimama ni mbunge wa Jimbo la Ulanga, Goodluck Mlinga.
Mkuu wa Wilaya Ulanga, Ngolo Malenya akisaini kitabu cha wageni katika Ofisi ya Afisa Migodi Mkazi wilayani humo.
Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko (wa tatu), Mkuu wa Wilaya Ulanga, Ngolo Malenya (wa pili kulia),  Kamishna wa Madini kutoka Tume ya Madini, Dkt. Athanas Macheyeke (wa kwanza kushoto), Mbunge Jimbo la Ulanga, Goodluck Mlinga (wa pili kushoto) pamoja na Afisa Migodi Mkazi Wilaya ya Ulanga, Tandu Jilabi (wa kwanza kulia) wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya ufunguzi wa ofisi hiyo.
Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wakiwemo wa Serikali, Tume ya Madini pamoja na wachimbaji madini wilayani Ulanga.
Jengo la Ofisi ya Afisa Migodi Mkazi Mahenge-Ulanga mkoani Morogoro.
Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko akizungumza na wachimbaji madini katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Mahenge wilayani Ulanga.
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye mkutano huo.
Viongozi mbalimbali wa Chama cha Mapinduzi CCM pamoja na Serikali.
Viongozi mbalimbali wakiwemo wa CCM pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Ulanga.
Wananchi na wachimbaji madini Mahenge wilayani Ulanga wakifuatilia mkutano huo.
Tazama BMG Online TV hapa chini

No comments: