Wednesday, November 28, 2018

WAZIRI JENISTA AWAFUNDA WATAALAM WA MAENDELEO YA JAMII




Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe. Jenista Mhagama akiangali moja ya vitabu vya Sera mbalimbali zilizo chini ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kabla ya kuzindua Kongamano la wataalam wa Maendeleo ya Jamii unaofanyika mkoani Arusha. 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe. Jenista Mhagama akiangali moja ya vitu mbalimbali inavyotengezwa na Vyuo vya Maendeleo ya Jamii vilivyo chini ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kabla ya kuzindua Kongamano la wataalam wa Maendeleo ya Jamii unaofanyika mkoani Arusha. 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na wataalam wa Maendeleo ya Jamii kutoka Taasisi za serikali Sekta Binafsi,  Mashirika yasiyo ya Kiserikali waliojumuika katika uzinduzi wa Kongamano la Wataalam wa Maendeleo ya Jamii linaloendela Mkoani Arusha. 
Katibu Mkuu Idara Kuu Maendeleo ya Jamii Dkt. John Jingu akielezea jinsia umuhimu wa wataalam wa Maendeleo ya Jamii unavyoweza kuleta mabadiliko katika jamii wakati wa uzinduzi wa Kongamano la Wataalam wa Maendeleo ya Jamii linaloendela Mkoani Arusha. 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe. Jenista Mhagamakiwa katika picha ya pamoja na wataalam wa Maendeleo ya Jamii mara baada ya kuzindua Kongamano la Wataalam wa Maendeleo ya Jamii linaloendela Mkoani Arusha. 
Picha na kitengo cha Mawasiliano WAMJW 

…………………… 

Na Mwandishi Wetu Arusha 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe. Jenista Mhagama amewapa somo Wataalam wa Maendeleo ya Jamii nchini kuwa mfano katika kuanzisha viwanda vidogo vidogo na kuwapa mwanga wananchi kuona mfano na kuiga na kuanzisha viwanda vidogo vidogo vitakavyowezesha kufikia azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kufikia Uchumi wa Kati ifikapo mwaka 2025. 

Ameyasema hayo leo mkoani Arusha alipokuwa akizindua Kongamano la Mwaka liliwakutanisha Wataalam wa Maendeleo kutoka Wizara husika, Taasisi za Serikali, Sekretarieti za Mikoa, Halmashauri, Sekta Binafsi na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali. 

Waziri Jenista amesema kuwa katika maendeleo ya nchi yoyote Wataalam wa Maendeleo ya Jamii ni watu muhimu katika kuamsha ari ya wananchi katika kujiletea maendeleo yao na taifa kwa ujumla katika kulueta uchechembuzi katika utekelezaji wa miradi ya kimaendeleo katika maeneo yao. 

Ameongeza kuwa Serikali imeweka mazingira wezeshi katika kuwawezesha wananchi kuchumi na kusema kuwa katika Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi kuna jumla ya mifuko.. inayotoa mikopo kwa waananchi ili kujikwamua kiuchumi kwa kufanya biashara na kauanzisha viwanda vidogo vidogo katika maeneno yao na kuwataka Wataalam wa Maendeleo ya Jamii kuchukua mikopo hiyo na kuanzisha viwanda vidogo vidogo ili kuwa mfano kwa jamii. 

“ Nataka mkutano wa mwaka 2019 kusiwe na mabanda ya maonesho tu bali kuwe na viwanda vidogo vidogo 350 zaidi katika maeneo mnayotoka ili tuiishi kauli mbiu ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kufikia Uchumi wa Kati na wa Viwanda ifikapo mwaka 2025” alisisitiza Mhe. Jenista 

Aidha amempongeza Katibu Mkuu Idara Kuu Maendeleo ya Jamii Dkt. John Jingu kwa kusimamia Sekta ya Maendeleo ya Jamii kwa ukaribu zaidi kwani ana uzoefu katika Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi kwa muda aliokuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Baraza hilo hivyo kama atatumia uzoefu huo ataipeleka Sekta ya Maendeleo ya Jamii mbele ili iweze kuwezesha wananchi kujikwamua kiuchumi hasa wananchi waliopo vijijini. 

Kwa upande wake Katibu Mkuu Idara Kuu Maendeleo ya Jamii Dkt. John Jingu amesema lengo la Kongamano la Wataalam wa Maendeleo ya Jamii ni kuwakutanisha Wataalam hao kujadiliana mambo mablimbali yahusuyo Taaluma hiyo ili kuja na njia na mbinu mpya za kuiwezesha Taaluma hiyo kuendelea kuwa chachu ya mabadiliko ya kiuchumi kwa wananchi na Taifa la Tanzania kwa ujumla. 

“Mhe. Mgeni rasmi Kongamano ni muhimu sana kwa ajili ya uhai wa Taalaum ya Maendeleo ya Jamii ambayo ni Njini ya Maendeleo yoyote”alisisitiza Dkt. Jingu 

Naye Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Jerry Muro amesema kuwa Maafisa na Wataalam wa Maendeleo ya Jamii ni nguzi muhimu katika maendeleo na anashangaa kwanini mpaka sasa bado tupo nyuma katika taifa kwani kuna baadhi ya watu bado wanajivuta katika kujiletea maendeleo katika maeneo yao. 

“Mwalimu Nyerere alisema Maendeleo yanahitaji Siasa safi tunayo, Ardhi tunayo, Watu tuano,na Uongozi bora tuonao chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Joseph Magufuli na kwanini mpaka sasa tuko nyuma” alisisitiza Mhe. Muro. 

Pia Rais wa Mpito wa Chama cha Maendeleo ya Jamii (CODEPATA) Bw. Sunday Wambura amemuahidi mgeni rasmi kuyatekeleza yale yote ambayo amewaagiza na kuhakikisha wanatumia fursa zilizopo katika kuiwezesha jamii kuamka na kuanza kuona umuhimu wa kushiriki katika shughuli za maendeleo yao wenyewe. 

Kongamano la Wataalam wa Maendeleo Jamii kwa mwaka 2018 lina kauli Mbiu inayosema “ Wataalam wa Maendeleo ya Jamii ni chachu katika kufikia Uchumi wa Kati 2025” na linafanyika kwa siku nne mfululizo Mkoani Arusha.

No comments: