Tuesday, October 2, 2018

Rais Magufuli atekeleza ahadi ya kutoka Milioni 20 kwa wavuvi na Mama Janeth Magufuli Milioni 5 za mama ntilie eneo la feri jijini Dar es salaam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 02 Oktoba, 2018 ametekeleza ahadi yake ya kutoa shilingi Milioni 20 kwa ajili ujenzi wa ofisi ya Umoja wa Wavuvi Wadogo Wadogo (UWAWAKI) waliopo katika eneo la Feri, Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam.
Mhe. Rais Magufuli alitoa ahadi hiyo jana alipokutana na wajasiriamali hao wakati akifanya mazoezi ya jioni pamoja na Mkewe Mhe. Mama Janeth Magufuli ambaye pia ametekeleza ahadi yake ya kutoa shilingi Milioni 5 kwa akina Mama wajasiriamali wanaofanya biashara ndogondogo hasa ya Mamalishe katika eneo hilo.
Fedha hizo zimekabidhiwa na Katibu wa Rais Bw. Ngusa Samike kwa Makamu Mwenyekiti wa UWAWAKI Bw. Amir Amani na kiongozi wa akina Mama wajasiariamali Bi. Ashura Seif Nanjonga, na kushuhudiwa na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bi. Sofia Mjema na Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala Bw. Tulusubisya Kamalama.
Kabla ya kukabidhi fedha hizo Bw. Ngusa amesema pamoja na kutoa fedha hizo Mhe. Rais Magufuli ameagiza Manispaa ya Ilala impelekee taarifa ya mapato na matumizi ya soko la samaki la Feri haraka iwezekanavyo na amemuagiza Mkuu wa Wilaya na Manispaa ya Ilala kushughulikia kero za wavuvi na wajasiriamali wa eneo hilo ikiwemo ushuru wenye kero na tatizo la vyoo.
Makamu Mwenyekiti wa UWAWAKI Bw. Amir Amani na kiongozi wa akina mama wajasiriamali wa Feri Bi. Bi Ashura Seif Nanjonga wamemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kuwasaidia fedha hizo na kwa kuwajali wao pamoja na Watanzania wengine hasa wanyonge.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bi. Sofia Mjema amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kutembelea soko la Feri na kuwasaidia wajasiriamali wa soko hilo na amesema yeye na timu yake ya viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ilala wataanza mara moja kushughulikia kero za wajasiriamali hao.

.
  Katibu wa Rais Bw. Ngusa Samike (tai Nyekundu) akikaribishwa kwenye  ofisi ya muda ya Umoja Wavuvi Wadogo Wadogo (UWAWAKI) waliopo katika eneo la Feri, Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam
Katibu wa Rais Bw. Ngusa Samike (tai Nyekundu) akiongea na Wajasiriamali waliojikusanya kushuhudia utekelezaji wa ahadi ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya kutoa shilingi milioni 20 kwa ajili ujenzi wa ofisi ya Umoja Wavuvi Wadogo Wadogo (UWAWAKI) waliopo katika eneo la Feri, Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam
 Katibu wa Rais Bw. Ngusa Samike akimsikiliza Bw. Amiri Amani, Mwenyekiti wa Umoja wa Wavuvi Wadogo Wadogo (UWAWAKI) waliopo katika eneo la Feri, Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam kabla ya kumkabidhi shilingi Milioni 20 kutoka kwa Rais Dkt. Magufuli alizowaahidi kwa ajili ujenzi wa ofisi ya Umoja huo
 Wajasiriamali wakishuhudia utekelezaji wa ahadi ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya kutoa shilingi milioni 20 kwa ajili ujenzi wa ofisi ya Wavuvi Wadogo Wadogo (UWAWAKI) waliopo katika eneo la Feri, Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam, pamoja na na mkewe Mama Janeth Magufuli aliyeahidi kutoa shilingi Milioni 5 kwa akina Mama wajasiriamali wanaofanya biashara ndogondogo hasa ya Mamalishe katika eneo hilo.
 Wajasiriamali wakishuhudia utekelezaji wa ahadi ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya kutoa shilingi milioni 20 kwa ajili ujenzi wa ofisi ya Wavuvi Wadogo Wadogo (UWAWAKI) waliopo katika eneo la Feri, Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam
 Katibu wa Rais Bw. Ngusa Samike (tai Nyekundu) akimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Sophia Mjema akiongea na Wajasiriamali waliojikusanya kushuhudia utekelezaji wa ahadi ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya kutoa shilingi milioni 20 kwa ajili ujenzi wa ofisi ya Umoja Wavuvi Wadogo Wadogo (UWAWAKI) waliopo katika eneo la Feri, Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam
 Katibu wa Rais Bw. Ngusa Samike akiongozwa kuangalia sehemu itapojengwa ofisi  na Wajasiriamali waliojikusanya kushuhudia utekelezaji wa ahadi ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya kutoa shilingi milioni 20 kwa ajili ujenzi wa ofisi ya Wavuvi Wadogo Wadogo (UWAWAKI) waliopo katika eneo la Feri, Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam
  Katibu wa Rais Bw. Ngusa Samike akiwa na  Mwenyekiti wa UWAWAKI Bw. Amir Amani   wakielekea sehemu itapojengwa ofisi zao katika utekelezaji wa ahadi ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya kutoa shilingi milioni 20 kwa ajili ujenzi wa ofisi ya Wavuvi Wadogo Wadogo (UWAWAKI) waliopo katika eneo la Feri, Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam
 Katibu wa Rais Bw. Ngusa Samike akiwa na  Mwenyekiti wa UWAWAKI Bw. Amir Amani   sehemu itapojengwa ofisi  na Wajasiriamali waliojikusanya kushuhudia utekelezaji wa ahadi ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya kutoa shilingi milioni 20 kwa ajili ujenzi wa ofisi ya Wavuvi Wadogo Wadogo (UWAWAKI) waliopo katika eneo la Feri, Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam
  Katibu wa Rais Bw. Ngusa Samike akiwaangalia Makamu Mwenyekiti wa UWAWAKI Bw. Amir Amani na kiongozi wa akina Mama wajasiariamali Bi. Ashura Seif Nanjonga wakiweka sahihi katika hati za makabidhiano ya fedha taslimu kutoka kwa Rais Dkt. Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli huku wakishuhudiwa pia na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bi. Sofia Mjema, Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala Bw. Tulusubisya Kamalama na mshauri wa Rais Masuala ya sheria Bw. Dunstan Kiobya (kushoto)
 Katibu wa Rais Bw. Ngusa Samike akimkabidhi shilingi milioni 5 kiongozi wa akina Mama wajasiariamali Bi. Ashura Seif Nanjonga kutoka kwa mke wa Rais Mama Janeth Magufuli alizoahidi kuwasaidia Mama wajasiriamali wanaofanya biashara ndogondogo hasa ya Mamalishe katika eneo hilo.
 Katibu wa Rais Bw. Ngusa Samike akimkabidhi shilingi milioni 20 Bw. Amiri Amani, Mwenyekiti wa Umoja wa Wavuvi Wadogo Wadogo (UWAWAKI) waliopo katika eneo la Feri, Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam shilingi Milioni 20 kutoka kwa Rais Dkt. Magufuli alizowaahidi kwa ajili ujenzi wa ofisi ya Umoja huo
 Wajasiriamali wakishangilia kwa furaha utekelezaji wa ahadi ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya kutoa shilingi milioni 20 kwa ajili ujenzi wa ofisi ya Wavuvi Wadogo Wadogo (UWAWAKI) na ya Mama Janeth Magufuli ya kutoa msaada wa shilingi milioni 5 kwa kia na mama waliopo katika eneo la Feri, Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam
 Wajasiriamali wakishangilia kwa furaha utekelezaji wa ahadi ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya kutoa shilingi milioni 20 kwa ajili ujenzi wa ofisi ya Wavuvi Wadogo Wadogo (UWAWAKI) na ya Mama Janeth Magufuli ya kutoa msaada wa shilingi milioni 5 kwa kia na mama waliopo katika eneo la Feri, Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam
 Wajasiriamali wakishangilia kwa furaha utekelezaji wa ahadi ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya kutoa shilingi milioni 20 kwa ajili ujenzi wa ofisi ya Wavuvi Wadogo Wadogo (UWAWAKI) na ya Mama Janeth Magufuli ya kutoa msaada wa shilingi milioni 5 kwa kia na mama waliopo katika eneo la Feri, Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam
 Wajasiriamali wakishangilia kwa furaha utekelezaji wa ahadi ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya kutoa shilingi milioni 20 kwa ajili ujenzi wa ofisi ya Wavuvi Wadogo Wadogo (UWAWAKI) na ya Mama Janeth Magufuli ya kutoa msaada wa shilingi milioni 5 kwa kia na mama waliopo katika eneo la Feri, Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam

  Katibu wa Rais Bw. Ngusa Samike kiongozi wa akimsikiliza kiongozi wa Mama wajasiariamali Bi. Ashura Seif Nanjonga akishukuru baaada ya kupokea shilingi milioni 5 kutoka kwa mke wa Rais Mama Janeth Magufuli alizoahidi kuwasaidia Mama wajasiriamali wanaofanya biashara ndogondogo hasa ya Mamalishe katika eneo hilo.
 Katibu wa Rais Bw. Ngusa Samike akimsikiliza Bw. Amiri Amani, Mwenyekiti wa Umoja wa Wavuvi Wadogo Wadogo (UWAWAKI) waliopo katika eneo la Feri, Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam akishukuru kwa msaada wa shilingi Milioni 20 kutoka kwa Rais Dkt. Magufuli alizowaahidi kwa ajili ujenzi wa ofisi ya Umoja huo
 Wajasiriamali wakishuhudia utekelezaji wa ahadi ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya kutoa shilingi milioni 20 kwa ajili ujenzi wa ofisi ya Wavuvi Wadogo Wadogo (UWAWAKI) waliopo katika eneo la Feri, Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam, pamoja na na mkewe Mama Janeth Magufuli aliyeahidi kutoa shilingi Milioni 5 kwa akina Mama wajasiriamali wanaofanya biashara ndogondogo hasa ya Mamalishe katika eneo hilo.
 Katibu wa Rais Bw. Ngusa Samike akipewa mikoni na wajasiriamali wenye furaha baada ya  kukabidhi shilingi milioni 20 kwa ajili ujenzi wa ofisi ya Wavuvi Wadogo Wadogo (UWAWAKI) na shilingi milioni 5 toka kwa Mama Janeth Magufuli kwa kinamama waliopo katika eneo la Feri, Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam

No comments: