Saturday, September 29, 2018

MAPINDUZI MAKUBWA SEKTA YA MADINI YAZIDI KUONGEZA MAPATO


Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi.



Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi.



Na Mwandishi wetu, Geita.

Mageuzi makubwa katika sekta ya madini nchini yameifanya sekta hiyo kuendelea kuongeza mapato ya Serikali kutoka bilioni 194.6 ilizopanga kukusanya mwaka 2017/18 hadi kufikia shilingi bilioni 301.6 ikiwa ni ongezeko la zaidi ya asilimia 55.

Hayo yameelezwa leo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi mkoani Geita wakati akiongea na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa Serikali.

Dkt. Abbasi ameeleza kuwa ongezeko hilo la mapato katika sekta ya madini limechagizwa na mabadilikomkatika sheria za madini, kujengwa kwa ukuta wa Mirerani na kuzuia kwa usafirishaji wa mabaki (kaboni) ya dhahabu nje ya mkoa yanapochimbwa madini.

“Mheshimiwa Rais aliagiza kujengwa ukuta eneo la wachimbaji wadogo la Mirerani na April mwaka huu ukuta huo ulikamilika na kuwezesha kuongezeka kutoka kilo 164.6 za madini ya Tanzanite yenye thamani yas milioni 71.8 mwaka 2016 hadi kufikia kilo 449.6 zenye thamani ya shilingi milioni 893.8 kwa kipindi cha Januari hadi Juni 2018”, ameeleza Msemaji Mkuu wa Serikali.

Ameeleza kuwa kutokana na usimamizi mzuri, makampuni ya uchimbaji madini yameendelea kutoa mchango wake kwa jamii ambapo Geita Gold Mine imetoa shilingi bilioni 9.2 kwa mkoa wa Geita kama mchango wa kampuni hiyo kwa maendeleo ya mkoa huo.

Aidha, Msemaji Mkuu wa Serikali ameongeza kuwa zuio la kaboni zenye dhahabu kusafirishwa na kuchakatwa nje ya mkoa zinakozalishwa limesaidia kuongeza pato kwa Serikali kufikia shilingi milioni 850 kwa mwezi Agosti mwaka huu kutoka shilingi milioni 400 kwa mwezi April.

Kwa mujibu wa Msemaji wa Serikali, Wizara ya Nishati na Madini imeendelea kufanya mageuzi mbalimbali ikiwemo kujenga vituo saba vya umahiri vitakavyokamilika Disemba mwaka huu kwa thamani ya shikingi 11.9 kuwapatia wachimbaji wadogo mafunzo na utaalamu zaidi wa uchimbaji. Aidha, vituo vinne vya mfano pia vitajengwa kwa thamani ya shilingi tono kuwasaidia wachimbaji kupata teknolojia rahisi ya uchenjuaji wa madini na kuyaongezea thamani.

Kwa upande wa sekta ya afya, Dkt. Abbasi ameeleza kuwa uwekezaji mkubwa wa vifaa, wataalamu na majengo umefanyika katika hospitali za Muhimbili, Mloganzila, MOI, Bugando, Benjamin Mkapa na ambapo hivi sasa Tanzania inapokea wagonjwa kutoka Komoro, Kenya, Uganda, Burundi, Rwanda, Malawi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Zambia kwa ajili ya kupata matibabu ya kibingwa ya moyo, figo, mifupa na kuongeza uwezo wa kusikia.

“Serikali imeendelea kusogeza huduma za afya karibu kwa wananchi kwa kujenga hospitali za rufaa katika mikoa saba, hospitali za Wilaya 67 zinajengwa mwaka huu kwa gharama ya shilingi bilioni 105 na tayari vituo vya afya 210 pamoja na nyumba za wahudumu wa afya vimejengwa” amesisitiza Dkt. Abbasi.

Katika hatua nyingine, Dkt Abbasi ameeleza kuwa hali ya uchumi wa Tanzania umeendelea kuwa imara ukikua kwa takribani asilimia 7.0 mpaka 7.1 kwa mwaka na kwamba kwa mujibu wa ripoti mbalimbali ikiwemo ya World Economic Forum, Tanzania ni ya tisa duniani kwa ukuaji wa uchumi na kwa Afrika inashika nafasi ya tano kwa nchi zenye uchumi unaokua kwa kasi.

Ameeleza kuwa hali nzuri ya ukuaji wa uchumi unaifanya Serikali kuendeleza mageuzi makubwa katika sekta mbalimbali zikiwemo elimu, miundombinu, afya na nishati ili kuifanya Tanzania kufikia uchumi wa kati wa viwanda ifikapo mwaka 2025.

Miongoni mwa mageuzi makubwa yanayoendelea nchini ni pamoja na uchezi wa miundombunu kama reli ya kisasa ya Standard Gauge, ujenzi wa bwala kubwa la kuzalisha umeme wa megawati 2100 kutoka bonde la mto Rufiji na hivi karibuni ambapo Rais alizindua barabara ya Juu (Flyover) iliyopo TAZARA jijini Dar es Salaam.

No comments: