Friday, September 21, 2018

CASSIUS MDAMI KWELI UMEENDA; ILA UMEBAKI KWENYE NYOYO ZETU

Cassius O. Mdami ni miaka miwili sasa tangu umetuacha familia yako; mke wako Rose Mdami; na watoto wako Martina, Grace, Gideon, Gonsalver na Gibson. 
Kila uchao hatuachi kuisikia sauti yako na kukumbuka ucheshi wako kila mara ulipokuwa nasi. Kifo kimetutenganisha nawe. 
 Mungu anajua maumivu yote na machungu tuliyopitia familia yako na tunayoendelea kuyapitia kwa kutokuwepo kwako. Machozi yanatudondoka na hakuna wa kuyafuta; ila tumaini tunalo ya kwamba iko siku moja tutaonana nawe katika makao ya Baba Mbinguni.
Mungu endelea kutufariji kama maneno yako yasemavyo katika kitabu cha Kumbukumbu la Torati 31:8 “ Naye Bwana ndiye atakayekutangulia, atakuwa pamoja nawe, hatakupungukia wala kukuacha; usiogope wala usifadhaike ”
 Pumzika kwa Amani Baba G4

No comments: